Hii Taarifa ya NHIF kama ni ya kweli basi Tanzania tuna tatizo

... kero ni nyingi sana kwenye huu mfuko. Unakatwa mshahara wako kwa lazima kulipia NHIF ila kama huna mtoto wa kumzaa huruhusiwi kuweka ndugu (mfano unayemlea); nafasi zako 4 (kama ungekuwa na watoto) zinakuwa zimekwenda bure faida kwa mfuko. Ukiuguliwa na huyo ndugu itakubidi kuingia gharama za matibabu yake ilhali kwenye mfuko una nafasi ambazo hutakiwi kumsajili.

Pili, watoto wote uliokuwa umewasajili wameshavuka 18/21; kwanini mwanachama huyu asipate nafuu ya makato? Badala yake makato yake yanabaki yaleyale. Tatu, badhi ya huduma muhimu zimepunguzwa; ukosefu wa baadhi ya dawa hivyo mhusika kulazimika kuingia mfukoni, n.k.
Hivi serikalini huwa wanakata asilimia (%) kwenda NHIF maana bima ya afya kwa watumishi wa serikali inatibu magonjwa mengi kuliko hizi bima za vifurushi kama wanavyoziita na ukute mtu amelipia 600,000 (laki 6), huwa najiuliza serikalini huwa wanalipa zaidi kiasi kwamba hizi za vifurushi zinapewa hadhi ya chini
 
Habari za mchana wapendwa.

Habari za kusikitisha - NHIF wamebadilisha mifumo yao ya matumizi ya card.

1- Tegemezi wengi wameondolewa,

2- Card itumike x 3 tu kwa mwezi.

3- Kama umetibiwa Jana au juzi, ukienda hospitali nyingine utatakiwa uende na Referral toka hiyo hospitali ulikotibiwa mara ya mwisho.

Makorokoro kibao yamebadilika. Tunaendelea kuwasikiliza. Ni shida tupu.


HII SIO HAKI MTU ANACHANGIA AFU HUDUMA ANAPANGIWA ATIBIWE KTK KITUO KIMOJA TU KWA MWEZI NA NA MARA TATU TU KWA MWEZ HII SIO HAKI. BASI WATUMISHI WARUHUSIWE KUJIUNGA NA MIFUKO MINGINE ISIWE LAZIMA NHIF ILI AFUATE HUDUMA SEHEMU ANAYOONA INAFAA
Kingekuwa na vyama huru na kweli vya wafanyakazi, hii kitu ingeondolewa mara moja. Mfanyakazi anakatwa asilimia tatu ya mshahara wake kuchangia NHIF hzlafu unampangia idadi ya siku za kuugua kwa mwezi? Nikatwe maelfu kila mwezi kisha nikalipie matibabu kisa tu kwa,mwezi huo tayari nimeenda hospitali mara tatu! Fikiria mtu ameenda hospitali anaambiwa apime vipimo na kwa kuwa amekula asubuhi basi siku hiyo hawezi kupimwa vipimo fulani hivyo aje kesho; siko inayofuata anakuja na kupimwa anaambiwa aje kuchukua vipimo siku inayofuata, akija siku ya tatu na kuchukua majibu na akimwona daktari anakuwa amemaliza siku tatu anazoruhusiwa kutu.mia bima yake anayokatwa pesa kila mwezi; hivyo kama asipopata nafuu hawezi kurudi tena hospitali baada ya siku chache katika mwezi huo huo upuuzi ulioje? Mtu huyo huyo akisafiri nje ya mji anapoishi kama likio@ kikazi na akaugua huko alikoenda hawezi kutibiwa na bima yake anayokatwa kila mwezi.

Ufumbuzi ni kuwa sheria ya ku.lazimisha mfanyakazi kuchangia NHIF ifutwe na wafanyakazi waruhusiwe kuchagua bima inayowafaa na kujiunga.

NHIF wana.pangia mwanachama siku za kuugua kwa mwezi!
 
Hali ni mbaya sanaa kila kiongozi anamua anachotaka, kule mafuta, pale tozo,huku mitandao na sasa hawa wapuuzi tena, nchi haina kiongozi mkuu inakwenda kwenda tu.
 
Hivi serikalini huwa wanakata asilimia (%) kwenda NHIF maana bima ya afya kwa watumishi wa serikali inatibu magonjwa mengi kuliko hizi bima za vifurushi kama wanavyoziita na ukute mtu amelipia 600,000 (laki 6), huwa najiuliza serikalini huwa wanalipa zaidi kiasi kwamba hizi za vifurushi zinapewa hadhi ya chini
... nadhani kutokana na wigo wa wateja kuwa mdogo ndio maana za vifurushi ni ghali. Ila huenda za serikali zisingekuwa LAZIMA badhi ya wafanyakazi wange-opt za vifurushi hivyo kuongeza wigo hence reduced cost.
 
AAR na STRATEGIES wateja wao huwa hawana tabia za kujirudia rudia kwenye vituo vya afya kupata huduma,, ila NHIF leo yupo hapa, kesho pale, kesho kutwa huku, ndyo maana wameamua kuwadhiti, hata wewe jiulize ndugu yangu, mtu hata dose hii hajamaliza kashahamia kwingine, huko nako hajamaliza dose aliyopewa kaenda kwingine, unakuta mtu mmoja kahudhuria mara 10 au zaidi vituo vya afya kwa mwezi!

NSSF wao huo utaratibu wa kutibiwa kituo kimoja tu na mara 3 wanao muda mrefu Sana, wateja wao hawasumbui washazoea.

Kwa Sasa kinachowafavour AAR na STRATEGIES, wao hawanalimit nyingi hasa upande wa dawa na vipimo, kwa hyo unaweza tibiwa vizur ukakaa Zaid ya miezi 3 hospital hupajui!

Ila Kuna viashiria nmeviona juzi juzi ndyo maana nasema Ni suala la muda huko kwao
Mkuu kumbe nssf ni mara tatu tu kwa mwezi? Nilikuwa sijajua hili, niko nao mwaka wa tatu sasa,20 tu kila mwez
 
Wameamua kusitisha kwa muda
FB_IMG_16595293061203794.jpg

View attachment 2312951
 
Wacha tukachague hospital zenye hadhi basi ili wawe wanapapaswa vizuri hamna kwenda kule kwa wakulima.

Hapa gongo la mboto nafanya utafiti kati ya rugambwa au kitonka nikite kambi wapi.
Kitonka ni ya mtu binafsi nasikia, na halipi vizuri wafanyakazi. Rugambwa ni ya dini, wala huhitaji hata kufaulu chekechea kujua wapi pa kukomaliza for the better future
 
TAARIFA KUHUSU BIMA ZA WAGOJWA KUKATAA KUWA AUTHORISED KWENYE MFUMO

Utaratibu wa mfuko wa NHIF umebadilika ili kuzuia polyvisit za wagonjwa pamoja na polyservices zingine za wagonjwa wetu

Kuanzia sasa mteja atakua na nafasi ya VISIT 3 TU KWA MWEZI kwa kituo husika na mteja hawezi kujiamulia kuhama Kituo cha kutolea huduma(Hosp,H/na disp) moja kwenda nyingine kwa kujiamulia, mfano mgonjwa akianza kutibiwa Kituo X basi atakua wa X tu mpaka pale X tutakapo amua sisi mrefer mgonjwa kwenda sehemu nyingine la sivyo mgonjwa hataweza kwenda sehemu nyingine ,kama kuna emergency kutakua kuna utaratibu kwenye mfumo wa kuruhusu huduma ziendelee

Aidha mfuko utaweka pia utaratibu wa wale wagonjwa ambao ni wa refill ili kama amekuja kwa ajili ya refill asiweze kuchomekea kitu kingine cha kimatibabu

Kwa huduma za physio, meno kutawekwa utaratibu maalumu ili huduma kama hizo ziendelee

Mfuko unataka kubana wale wa watu wanaozunguka kila kituo kufanya vipimo, kuona madaktari na kulinganisha huduma za madaktari

Ni hayo tu ndugu zangu,muwe ka kazi njema.

Watu wa mapokezi mutakua munawaelekeza kwa upole wateja ambao kadi zao zimepata changamoto hizo.

NHIF.
Taarifa kwa umma
Screenshot_20220803-150623_Adobe%20Acrobat.jpg
 
Tayari asali tamu wamejisahau kuwa watu wanakatwa mishahara.asali tamu.wakitimuliwa wakuu kama watatu utaona ufanisi
 
Baada ya taharuki kwa wanachama,wizara ya afya imeweka zuio kwa utaratibu huu mpya uliowekwa na NHIF
 
Mbona NSSF siku zote tuliambiwa kuchagua hospitali moja tu katika eneo unaloishi utakako tibiwa, na tuliendelea hivyo unless unakiwa referred hospitali nyingine na haijawa tatizo?
 
Mbona NSSF siku zote tuliambiwa kuchagua hospitali moja tu katika eneo unaloishi utakako tibiwa, na tuliendelea hivyo unless unakiwa referred hospitali nyingine na haijawa tatizo?
Watu hapa wanaongelea NHIF (mfuko wa taifa wa Bima) unaochangiwa hela kutoka kwenye mishahara ya wafanyakazi na sio NSSF ambayo wameamua kutoa zawadi ya bima ya matibabu kwa wanachama wao (ukipewa zawadi huwezi kuchagua/kudai); ila ukilipia huduma, unahaki ya kushirikishwa
 
Back
Top Bottom