Hekima inapoita: Mauaji ya Barlow yanahitaji kulaaniwa, kukataliwa na yanalia "haki"

Si vyema kufurahia kifa lakini kwa Polisi wa Tanzania tena wakubwa wacha wafe labda watapata adabu ya kuheshimu kazi yao na kuacha kufuata maajizo ya Kisiasa. Rest in Hell Kamanda
 
Watu hawashangilii mtu kufa, bali Kifo cha polisi maana polisi ni polisi tu they are never good to people na kwa hiari yao wameamua kujitenga na raia, hawaaminiki kabisa kuwa wao ni sehemu ya jamii hii waliyoapa kuilinda, wanajidhani wapo katika next stage of evolution...yaani uraia then u-polisi. Hawana nidhamu ya utu wa mtu, wala uhai wa mtu.
Si vizuri kulipa jino kwa jino lakini wamezichosha akili za watu, wame paralyze akili na mioyo ya watu kwa matendo yao ya kinyama.
Matendo yao yanaanza kuleta athari ndani ya jamii, ni athari mbaya kabisa, athari ambayo Mzee Mwanakijiji anaona tishio lake na kutishika kiasi cha kuamua kushika kalamu kuiasa jamii.....hajachelewa bado, ni mapema sana...ila tu itambulike kuwa hali hii isiyo ya kawaida ni matokeo ya jitihada za hao Polisi (hata kama ni wachache), jitihada hizo zinaumba hisia mpya mioyoni na akilini mwa watu.
Naomba nimalize kwa kusema:
WATU HAWAFURAHII KIFO CHA MTU, BALI WANAFURAHIA KIFO CHA POLISI.
 
Tangu police wamuue mwangosi kwa kumsambaratisha tumbo lake policcm wamenitoka kama matapishi sijui kama nitakuja kuwapenda tena
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu nakuomba sana ufahamu tabia na hulka za binadamu kabla hujahukumu na kitu gani kinatakiwa kufanywa kwanza ili kuondoa nafasi ya mambo yanayoweza kutokea. wazungu wanasema mahala popote ambapo diplomacy imeshindikana basi fahamu ya kwamba upo uwezekano mkubwa wa vita hata kama swala limeanzishwa na mtu mmoja. Iraq ilishambuliwa kwa sababu ya mtu mmoja tu Saadam na walokufa ktk mashambuliszi hayo wameitwa nani Collateral damage. Mtu mmoja anaweza kabisa kuimaliza jamii nzima, hivyo hekima huanza na watu wenyewe kutofundishana shari.

Binafsi yangu husema kama kuna uwezekano wa kuepusha shari Je, kuna sababu gani ya kupuuza UPENDO lakini tuwe wepesi wa kulaani matokeo wakati mbegu tulizopanda ndizo chanzo na sababu ya matokeo hayo?. Kwa nini tusijifunze kutopanda mbegu chafu ambazo matokeo yake ndio haya..Hivi kweli wewe na wengineo mlitegemea Polisi wanaweza kuua na tukawalaani kwa maneno lakini wananchi wataendelea kuvumilia kuona mauaji yakiendelea na jeshi letu likijenga Chuki na uadui baina yake na wananchi?..

Kosa la kamuhanda linaweza kabisa kuchukua sura mpya ni lazima tujifunze haya, na hivyo kosa la mtoto alokojolea Msahafu linaweza kabisa kuzua vita baina ya Waislaam na Wakristu, kosa la Chadema linaweza kuzua vurugu kubwa baina ya wanachama wa CCM ana Chadema na kosa la Chadema linaweza kuzua vifo vya raia wengine wengi..

La muhimu kwetu sisi ni kujiuliza kama kuna umuhimu wa kuendeleza vitendo vyovyote kwa gharama hizi kubwa ambazo zinajenga chuki baina yetu. Kuna tatizo gani kwa serikali yetu, viongozi wa vyama na serikali na dini kufundisha UPENDO?.. kwa nini kila unapokwenda nchini siasa ni za CHUKI tu.. aidha viongozi kutupiwa mawe, makanisani na misikitini hakuna mafundisho ya upendo isipokuwa upande wa pili ni watu gani. Ukienda Msikitini Hotuba hazizungumzii hadithi za mtume isipokuwa SIASA za chuki, Ukienda makanisani vile vile, Ofisi za CCM na Vijana ni jinsi ya kuwasambaratisha Chadema. CUF ni Uzanzibar dhidi ya bara, JF ni waislaam against wakristu, CCM against Chadema, CUF agaisnt Chadema tena kwa matusi mazito mazito. Hi kweli ndio demokraisa au tunafanya madudu mengine?..Kweli mnategemea kuwepo na AMANI?..

Leo hii katika vyama vyetu wachungaji ndio wanagombea Ubunge, I mean mkuu wangu unategemea nini kutoka kwa mchungaji anayekwenda kanisani kufundisha dini wakati ni mwanasiasa mgombea Ubunge wa jimbo lake?.. halafu tunasema nchi yetu haina dini! huyu ni mbunge ambaye kuna uwezekano mkubwa akawa Waziri kama chama chake kitaingia madarakani..Kwa nini asiache kwanza Uchungaji kama alivyofanya Dr.Slaa na kujishughulisha na siasa lakini unakuta mtu anagombea Uongoz huku akifundisha Gospel makanisani na hata ktk majukwaa ya siasa. jamani tunatafuta nini kama sio kuitaka shari sisi wenyewe?..

mambo mengine jamani sina haja ya kuyazungumza sana lakini ukweli unabakia kwamba sisi wenyewe tunafundisha a chuki, sisi wenyewe ndio tunaochochea hizi CHUKI na HuSUDA ktk mfumo mzima wa siasa zetu na Utawala. Maana sioni tatizo kabisa kwa Polisi nchini kuwalinda wananchi kama walivyoapa badala yake wananchi ndio wanakuwa maadui zao kwa makosa yalofanywa na viongozi wao halafu tutegemee watu watakaa kimya tu....


Natamani kukuunga mkono Mkuu Mkandara, kwa matumaini kuwa ulitaka kusema tumefikishwa mahali pa kuchoka.

Nyongeza yangu ni hii: kwamba katika mazingira tuliyonayo sasa, pengine ni busara kuanza kujianda kwa vita ya wao kwa wao, kwa sababu vita si mbaya katika kila maana. Vita inaweza kuwa mapito ya jamii kuboresha nchi. Historia ya mataifa mengi inaonesha vita inao uwezo wa kuboresha nchi. Vita itaboresha Iraq, vita iliboresha Ujerumani, Vita iliboresha ufaransa. Vita iliboresha Marekani. Vita imeboresha Afrika ya Kusini.

Mawazo yaliyosababisha wewe kutoa mchango huu ninaoupatia nyongeza, kwangu yanafanana na mawazo ya mtu mwoga.

Now uwoga unayo nafasi katika kumlinda mtu, lakini mimi nionavyo, amani inayotokana na uwoga wa mmojawapo katika jamii si amani ya haki. Tunahitaji amani ambayo chimbuko lake ni heshima, na heshima katika jamii nyingi imejengwa kwa vita.
 
MMK Wao police ndiyo wamewafikisha hapo watz,

Hapana Isaya, soma tena hii mada iliyopikwa na kuiva sawa sawa. Kwa vyovyote vile, hatuwezi tukachukua ushenzi wa mtu au kikundi cha watu tukawahukumu wananchi au jamii yote. Ile sera ya kuvua gamba ya CCM ilionekana kama kushadidia haya tunayozungumza hapa, na aliyoyaweka kwa ufasaha mkubwa Mzee Mwanakijiji. Lakini CCM kama jamii imezidiwa na hao wachache, na wamebaki kuwa gamba. Leo Barlow mdogo wangu, kesho mimi au wewe. Kwa mantiki hio kwa kuwa mimi ni Mkristo na ikatokea mwenye imani yangu akawaudhi wenzetu, na mimi nikauawa basi utakuwa na haki gani kunihukumu kwa kiasi hivho Isaya?
 
Binafsi sikufurahishwa na mauaji ya huyo polisi kule Mwanza,lakini pia sikuhuzunishwa! Polisi wetu wameamua kutumiwa vibaya na watawala,matokeo yake wamejitenga na sisi kwa hiyo jambo lolote baya linalowatokea ni sawa tu! Liwalo na liwe!
 
Kwenye hili MM sikubaliani na wewe!
Kamanda anajitwalia mke mtu ki ubabe, mwenye mke anamlalamikia bila mafanikio, hata kama hana nguvu ulitaka afanyeje?
 
NI dhambi lakini tulipofikia si pazuri........... next awe Kamuhanda tu, aliua songea kaua iringa na sasa anakejeli ripoti za uchunguzi
 
Be it or not, Barlow anabaki kuwa binadamu aliyekuwa na haki ya kuishi kama mimi na wewe tunavyoendelea kupumua. Kimsingi kufurahia jambo baya hata kama umewahi kutendwa au kuathirika kwa ubaya wowote wa dunia hii au wa kimfumo wa serrikali, hupaswi kushangilia kifo cha mtu mwenzako, hata kama angekuwa mnyama kiasi gani. Jamani mbona tunakuwa kama hatuna dini? tusiruhusu nafsi na akili zetu zitekwe na fikra za kipuuzi kiasi hicho maana tutaanza kujijengea mazingira ya kinafsi ya unyama. Barlow kafa kinyama kabisa hata kama tukio hilo lina maswali mengi na kimsingi hakupaswa kuuawa kishenzi kiasi hicho.
 
tunaweza kulaumiana lkn naomba niwaambie kuwa kila mwanadamu ana kiwango chake cha uvumilivu na huruma ndani yake. huruma/ubinadamu na uvumilivu wake huweza kuondoka hususani pale panapokuwepo uonevu wa makusudi, mauaji ya raia wasio na hatia, kubambikiwa kesi zisizo na kichwa wala miguu, kunyangánywa haki yake isiyohitaji msomi kumpatia n.k.

mm naomba niwambie mauaji yote ya wananchi wsio na hatia, watu walijenga matumaini kuwa ccm na serikali yake watachukua hatua madhubuti kuwawajibisha polisi na viongozi waliohusika. cha kusikitisha baadhi ya polisi walipandishwa vyeo na wengine kuhamishwa, hili liliwapa picha wananchi kuwa hivi polisi akimuua mwananchi asiye na hatia ni halali kwake na anapandishwa cheo kwa hilo. pili kifo cha mwandishi Daudi Mwangosi, kilichukiza watu sana hususani jinsi ccm na serikali yake walivyojitahidi kupotosha ukweli wakati zipo picha(video) zinazoonesha tukio zima ambalo halikuhitaji tume kuchunguza. wameunda tume kibao wameleta taarifa za uongo na mkanganyiko kitu ambacho kimeongeza hasira ya jamii,

kifupi mm niwaambie sasa hivi watu hata risasi hawaogopi kama zamani, siku hizi kila mtanzania akimwona polisi anamuhesabu adui yake na nadhani wengine wanatamani waanze kuwaua polisi kabla hawajauliwa.


unajua kwann binadamu anaitwa mnyama, ni kwa sababu pale anapoonewa vya kutosha na kukosa njia mbadala ya kupata haki yake hujenga uadui na kuwa tayari kufanya tukio lolote baya. mtu wa aina hii ni mbaya kuliko hata simba jike mwenye njaa, maana hutumia akili na ustadi wa kutosha kutekeleza maamuzi yake

sifurahii kufa kwa RPC wa mwanza ila nasikitika kuwa kama amekufa kwasababu ya kuzini na mke wa mtu, ni aibu na fedheha kubwa kwa jeshi, serikali, familia yake na kwamba hataingia mbinguni. atakuwa amekwenda zake motoni ndicho kinachonisikitisha

jamani mke wa mtu ni sumu, acheni uzinzi, ndio maana hata Mungu alisema usimtamani mke wa jirani yako...period. kumbuka dhambi zote kabla ya kutendwa hutangulia tamaa ya kuona jambo hilo ni jema na inafaa kufanywa. ukiona mwenzio ananyolewa wewe tia maji kichwa...""
 
naomba mnikumbushe ile issue ya kutaka kuwaua wale wabunge wa chadema aliishughulikiajee?
alizingatia haki? au alipotezea.
nafikiri tusisubiri tuonewe huruma tukifa, ila inatakiwa tuishi maisha ya haki na kweli, huruma yetu sasa haitamsiadia hata tukikesha kumlilia cha msingi ni
kukumbuka kuwa sisi tu mavumbi na mavumbini tutarudi ; tusiishi kama tutaishi milele
 
View attachment 68063
dada huyu ndiye mwenyewe


Correction kiongozi. Hiyo picha ni ya black american na iko kwenye website inayoongolea mambo ya unene (obesity). Sijui imefikaje Tanzania?

Back to the main point: These are trying times kwa Taifa la Tanzania na tukikosea tutaungukia upande wa pili, upande ambao ni very ugly and it may take generations to correct it. Taratibu tunaanza kubomoa mambo ya msingi yanayotuunganisha kama taifa, tunaanza kuwa na kizazi cha kuviziana na kulipiziana visasi!

Kelele za watu wakati wa mauji ya Ally Zonga, Daudi Mwangosi na wengine si kwa sababu ya taalum zao, bali ni kwa kutambua haki ya msingi ya kila mtu kuishi. It is very regrettable kwamba Tanzania tumefikia mahali tunafurahia kifo cha mtanzania mwingine. Na ndiyo nasema these are trying times.

Kunahitajika juhudi za hali ya juu kuturudisha kwenye mstari. Ni kwa kutambua haki za kila mmoja wetu ndipo mtu utakuwa na moral authority ya kunyoosha kidole pale mtu anapokwenda kinyume. Tofauti na hapo tunakuwa kama taifa la laana.

Sijui kama hili linawezekana. Lakini tungekuwa na wazee (regardless wako affiliated na itikadi,dini, kabila gani) wakae chini na uongozi wa juu wa nchi hii na kuongea kwa uwazi.Tuliona juhudu za Warioba, Dr Salim wakati wa utata wa katiba mpya na walk out ya CHADEMA. Tunaweza kuwa na juhudi za namna hiyo kwa sasa ili walau tuwe na framework ya pamoja.

Sasa hivi ni kama hatuna mwelekeo and no one anaonekana kushtushwa na hii hali. Mwezi ulipita mwandishi wa habari amelipuliwa na bomu, jana watu wazima wanamwinda mtoto mdogo wamuuwe, wengine wanachoma makanisa, leo RPC anapigwa risasi! Something must change.
 
Correction kiongozi. Hiyo picha ni ya black american na iko kwenye website inayoongolea mambo ya unene (obesity). Sijui imefikaje Tanzania?

Back to the main point: These are trying times kwa Taifa la Tanzania na tukikosea tutaungukia upande wa pili, upande ambao ni very ugly and it may take generations to correct it. Taratibu tunaanza kubomoa mambo ya msingi yanayotuunganisha kama taifa, tunaanza kuwa na kizazi cha kuviziana na kulipiziana visasi!

Kelele za watu wakati wa mauji ya Ally Zonga, Daudi Mwangosi na wengine si kwa sababu ya taalum zao, bali ni kwa kutambua haki ya msingi ya kila mtu kuishi. It is very regrettable kwamba Tanzania tumefikia mahali tunafurahia kifo cha mtanzania mwingine. Na ndiyo nasema these are trying times.

Kunahitajika juhudi za hali ya juu kuturudisha kwenye mstari. Ni kwa kutambua haki za kila mmoja wetu ndipo mtu utakuwa na moral authority ya kunyoosha kidole pale mtu anapokwenda kinyume. Tofauti na hapo tunakuwa kama taifa la laana.

Sijui kama hili linawezekana. Lakini tungekuwa na wazee (regardless wako affiliated na itikadi,dini, kabila gani) wakae chini na uongozi wa juu wa nchi hii na kuongea kwa uwazi.Tuliona juhudu za Warioba, Dr Salim wakati wa utata wa katiba mpya na walk out ya CHADEMA. Tunaweza kuwa na juhudi za namna hiyo kwa sasa ili walau tuwe na framework ya pamoja.

Sasa hivi ni kama hatuna mwelekeo and no one anaonekana kushtushwa na hii hali. Mwezi ulipita mwandishi wa habari amelipuliwa na bomu, jana watu wazima wanamwinda mtoto mdogo wamuuwe, wengine wanachoma makanisa, leo RPC anapigwa risasi! Something must change.

Mkuu kumbe nimeingizwa chaka??kuna post inaendelea hapa jamvini inaonyesha huyu mwanamke kuwa ndiye yule aliyekuwa na kamanda!jamani!
 
Barlow alifanya mema yatakuwa yameoneka kama alifanya mabaya vile vile yatakuwa yalioneka lakini yote kwa yote atahukumiwa kutokana na matendo yake
 
viongozi wana wajibu wa kuonesha njia,wanalala na hawaoni hatari hii iliyopo na kwa safari yetu kama nchi,mzee mwanakijiji pamoja na umbali wa ulipo lakini umekuwa ukipaza sauti kwa nguvu pasi kuchoka lakini watawala wametia pamba masikioni na hawataki kusoma ngano zake,madhani ni mazoea na kupuuza kila jambo linalozungumzwa na aina fulani ya watu,binafsi sipendi wanayotukia,sifurahishwi na mlolongo wa upotevu wa amani,unyanyasaji kwa wananchi,na imekuwa ngumu kuelewa wajibu wa viongozi ni nini?wote huapa kwa kusema watatetea na kuinda nchi kwa mujibu wa sheria,sheria zinapokiukwa wao kimya ama kuchukulia kimzaha,kila mtu ana haki ya kuishi na tuna haki ya kulinda haki hiyo,so huu upuuziaji wa vilio vya wananchi kupitia wanahabari muda mfupi ujao tutakuwa pabaya zaidi.napenda kusema ni hekima,busara,uvumilivu,upendo na tupaze sauti kwa pamoja kwa viongozi kuwa hatufurahishwi na namna wanavyochukulia mambo ya usalama wetu.nakubalia na hoja yako mwanakijiji.
 
Mwanakijiji ipitie tena ile kitu inaitwa the great law inayoitwa ''the law of karma ''
 
Last edited by a moderator:
Correction kiongozi. Hiyo picha ni ya black american na iko kwenye website inayoongolea mambo ya unene (obesity). Sijui imefikaje Tanzania?

Back to the main point: These are trying times kwa Taifa la Tanzania na tukikosea tutaungukia upande wa pili, upande ambao ni very ugly and it may take generations to correct it. Taratibu tunaanza kubomoa mambo ya msingi yanayotuunganisha kama taifa, tunaanza kuwa na kizazi cha kuviziana na kulipiziana visasi!

Kelele za watu wakati wa mauji ya Ally Zonga, Daudi Mwangosi na wengine si kwa sababu ya taalum zao, bali ni kwa kutambua haki ya msingi ya kila mtu kuishi. It is very regrettable kwamba Tanzania tumefikia mahali tunafurahia kifo cha mtanzania mwingine. Na ndiyo nasema these are trying times.

Kunahitajika juhudi za hali ya juu kuturudisha kwenye mstari. Ni kwa kutambua haki za kila mmoja wetu ndipo mtu utakuwa na moral authority ya kunyoosha kidole pale mtu anapokwenda kinyume. Tofauti na hapo tunakuwa kama taifa la laana.

Sijui kama hili linawezekana. Lakini tungekuwa na wazee (regardless wako affiliated na itikadi,dini, kabila gani) wakae chini na uongozi wa juu wa nchi hii na kuongea kwa uwazi.Tuliona juhudu za Warioba, Dr Salim wakati wa utata wa katiba mpya na walk out ya CHADEMA. Tunaweza kuwa na juhudi za namna hiyo kwa sasa ili walau tuwe na framework ya pamoja.

Sasa hivi ni kama hatuna mwelekeo and no one anaonekana kushtushwa na hii hali. Mwezi ulipita mwandishi wa habari amelipuliwa na bomu, jana watu wazima wanamwinda mtoto mdogo wamuuwe, wengine wanachoma makanisa, leo RPC anapigwa risasi! Something must change.
very right...wanasema tz kuna amani lakini ukweli halisi ni kwamba hamna amani bali......kwa miaka yote hii watu wamekua wanaishi kwa harmony.....huku wakivumiliana tofauti zao.....lakini sasa imefika mahali tolerance level kwa maovu ya aina yoyote inafikia mwisho wake katika jamii ya tz....na hili limefikishwa hapa kwa kiasi kikubwa na watawala wetu...ambao jeshi la polisi liko chini ya mamlaka yao......Jamii ya mtanzania inaanza kufikia mahali kujichukulia hatua wanavyotaka maana wanaona kuwa watawala hawajali......Labda tukumbuke tu kuwa jamii nyingi zilizowahi kufikwa na machafuko pia zilipitia hatua hii ilipo tz kwasasa...mfano: nchini Kenya kabla ya yale mauaji ya kuchinjana baada ya uchaguzi..polisi wao walikuwa wanalaumiwa sana sana na raia kwa kufumbia macho maovu.....jambo lililochangia sana mauaji yale kutokea Kenya.....kama itakumbukwa katika watu waioshtakiwa kule ICC the Hague alikua mkuu wao wa jeshi la polisi(japo mwishoni aliachiwa).....Hapa kwetu tayari raia wameshapoteza imani na jeshi la polisi na kama watawala wataenddelea kufumbia macho haya mambo basi tunakoendelea only God knows......Kwa kifupi what needs to be done ni kwa jeshi la polisi kubadilika.....pamoja na watawala.......raia watanzania bado ni wapole saana......
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Nao wafe 2mepoteza ndugu ze2 weng hawajali na hata hawaumii,mungu mkubwa kilajambo malipo yake niHAPAHAPA duniani,wanafrahia kifo cha mwangosi kwaku2eleza makapi ya2me walizo unda,arusha,songea,mwanza,mbea.nyamongo,geita.kote huko wanatoa majibu mepesi kisa serikali wameiweka viganjani.hawajali wanadhani wao ndo wanahaki ya kuish.mkumbukeni Mungu wenu.
 
Back
Top Bottom