Hekima inapoita: Mauaji ya Barlow yanahitaji kulaaniwa, kukataliwa na yanalia "haki"

Kila jambo lina chanzo. Katika mfumo wa nchi kama hivi ni rahisi sana kwa hekima kuanzia juu kushuka chini. Lakini ni rahisi pia kwa ukosevu wa uvumilivu kuanzia chini kwenda juu. Tunachoshuhudia sasa ni kukosekana kwa uvumilivu, na hivyo kusababisha moto kuelekea juu. Nini chanzo cha ukosefu wa uvumilivu? Mfumo unajua. Hata wananchi wanajua. Sasa kipi rahisi au ghali kati ya mfumo wa kushuka au wa kupanda? Ni nani kati ya makundi haya mawili atakayepoteza? Upumbavu wa mfumo (unaounda safu ya uongozi wa Dola) ndio chanzo cha hii furaha ya wananchi pale mmojawapo wa wanamfumo anapodhalilika, au hasira na chuki za wananchi pale mmojawao anapodhurika.
 
Hakika umenena MM, Si vyema kushangilia kifo cha mwanadamu mwenzako, cha msingi ni kufahamu kuwa Taifa liko kwenye hatari kubwa,tunapitia kwenye pepeto watanzania, hakika tumuombe MUNGU atuvushe salama kwenye haya mapito.

MUNGU IBARIKI TANZANIA,MUNGU IBARIKI AFRIKA.
 
Polisi walimuua mtu wa kwanza,wananchi kimya,serikali ikatangaza kuwa lazima tuilinde amani yetu,Tukailinda!akafa mtu wa pili mikononi mwa polisi,agenda ikawa kuilinda amani,tukatulia,wakafa wafanya biashara wa mahenge,tukaambiwa kuwa sheria imeshinda hoja,tukatulia,akafa mwingine na mwingine na wengine!!!!sasa wananchi tukajiuliza uhusiano wa ukimya wetu, mauaji yanayoendelea,na amani tunayohubiriwa,kumbuka kuwa polisi kama jeshi lina msemaji,lina amiri jeshi na zaidi ya yote lina sheria zao,wananchi kama umma wana mhamasishaji/wahamasishaji,wanaoelekeza vichwa vyao kule upepo unapoelekea,hao ndio wa kwanza watakaojiuliza how long should we go on greaving over these actions? Sisi kama umma tutajiuliza pia! Na jumla ya majibu yatakayopatikana yaweza kuwa jawabu,mheshimiwa MMK usijifanye kushangaa ilipotokea risasi wakati shooter ulishamwona!what goes around comes around!it is the rule of the game,anayeku kaba mkabe!!hali itaendelea kuwa mbaya zaidi kama wahusika wakuu wataendelea kuukalia mfuniko wa majawabu,tutaendelea kuumizana kila mmoja kwa nafasi yake hadi hapo mwenye funguo za suluhu atakapokuwa tayari kuzisalimisha funguo.
 
  • Thanks
Reactions: ral
Sio wewe uliesema humu 'umetafuna' wake za watu saba?
sasa unashangilia nini hapa?
wewe ufanywaje na wenye wake?

Mkuu nilipoona wanawake wana post picha za ajabu kwenye facebook niliamua kufanya research,nilianza na wale wanaodai wameolewa ili nione nia yao ni nini hasa,baada ya miezi minne ya majaribio nilijikuta nimelala na wanawake saba ambao ni wake za watu kutoka facebook,wanawake niliotongoza walikuwa 13 nikapata saba,sababu iliyonifanye nipate saba kati ya kumi na tatu nilijiondoa na ku delete account yangu manake wale saba walikuwa wakituma message kila wakati,baada ya hapo ndio nikaja jf kuwaletea matokeo ya research yangu,hukufurahia mkuu??manake ile inaitwa reality!
 
Mkuu nilipoona wanawake wana post picha za ajabu kwenye facebook niliamua kufanya research,nilianza na wale wanaodai wameolewa ili nione nia yao ni nini hasa,baada ya miezi minne ya majaribio nilijikuta nimelala na wanawake saba ambao ni wake za watu kutoka facebook,wanawake niliotongoza walikuwa 13 nikapata saba,sababu iliyonifanye nipate saba kati ya kumi na tatu nilijiondoa na ku delete account yangu manake wale saba walikuwa wakituma message kila wakati,baada ya hapo ndio nikaja jf kuwaletea matokeo ya research yangu,hukufurahia mkuu??manake ile inaitwa reality!

Wewe umesema ni halali mtu kupigwa risasi kwa kutembea na mke wa mtu
ndo nakuuliza.....unaonaje na wake za uliotembea nao wangefanya hivyo kwako?
 
Nimesema juzi kuwa ukosefu wa hekima ni janga kubwa la kitaifa kwa kweli nilimaanisha hilo. Tangu habari za mauaji ya Kamanda Barlow yalipotokea mwitikio wa watu wengi umekuwa ni kutokujali, kuhalalisha na hata kushangilia ni kama mtu kusema "akome". Wengi wanahalalisha hili kwa sababu wanaamini ujumbe umetumwa kwa polisi na kuwa polisi 'wanaua watu na sasa kimewarudia'. Kauli hizi ndizo zinazothibitisha ukosefu wa hii hekima.Tumeshuhudia kosa la mtoto mmoja kwenda kuhukumiwa makanisa na wakristu; leo kosa la Kamuhanda anahukumiwa Barlow? Leo hii kosa la askari mmoja wanalaumiwa jeshi zima kiasi kwamba leo chochote kitakachompata polisi tunafurahia?

Ni lazima tujifunze kuwa na hekima ya kutofautisha kitu kinachoitwa "collective punishment" kwamba tunaadhibu wote kwa kosa la mmoja. Labda ni kwa sababu tunaamini (bila kufikiria sana) kuwa "samaki mmoja akioza wameoza wote". Ukweli ni kuwa samaki mmoja akioza siyo wote wameoza!

Kamanda Barlow ahukumiwe kwa matendo yake mwenyewe na si matendo ya wengine. Je alikuwa ni kamanda mzuri kwa polisi, je alisimamia haki na utawala wa kisheria kwa kadiri ya uwezo wake (yaani pamoja na mapungufu yake kama alivyoshughulikia hili la koswakoswa la afisa)? Je kuwa dhaifu kiutendaji adhabu yake ni mauti?

Tuna tofauti gani basi na wale ambao wanaona mtu anapigwa na watu kwa sababu kadaiwa ni 'kibaka' na wao bila kuuliza wanachukua jiwe na kurusha au wanauliza "lete petroli" halafu wanaondoka zao huku nyuma mtu anatiwa kiberiti? Tuna tofauti gani na jamii isiyoerevuka ambayo haitaki kutafuta ukweli inaishi kwa imani na hisia tu?

Mauaji ya Barlow kama yalaivyokuwa mauaji ya Mwangosi na ya wananchi wengine wengi yanapaswa kulaaniwa na siyo kuhalalishwa, yanastahili kupingwa na siyo kutetewa na yanahitaji kukataliwa na siyo kuzoeleka.

Ni wazi kuna mapungufu ya kiutendaji na mambo mengi ambayo hayajibu maswali yetu ndio maana wengine tulitaka maafisa wa juu wa jeshi hilo wang'olewe kwa sababu wameligeuza kuwa ni jeshi la kisiasa sasa. Inapofika watu wanaona jeshi la polisi ni la CCM au lisilo na ule ukaribu wa zamani na wananchi basi ni hatari kwa sababu hawatalipa ushirikiano na wakipata nafasi ya kuwatendea polisi wanawatendea! Mwema, Chagonja na wengine wajuu wanapaswa kuondolewa ili mabadiliko ya kweli ya jeshi yaletwe na watu wenye uwezo. Inapofika watu hawaoni huruma ya mtu kupoteza maisha yake tumefika pabaya.

Hivi mauaji haya yana tofauti gani ya Pro. Mwaikusa? yana tofauti gani na mauaji ya yule Mwanasheria miaka michache iliyopita pale Dar; yana tofauti gani na mauaji wananchi kule Arusha, au Songea? Well.. tofauti ni namna tu lakini ni kuwa wote wamepoteza maisha katika mazingira ambayo hayakupaswa kutokea; ni mazingira ambayo yanahitaji kuchunguzwa na kuondolewa ili isije ikafika mahali huko mbeleni tukasikia Waziri auawa, Mwenyekiti wa Chama cha siasa apigwa risasi au Mbunge auawa au hata iwe yale yale ya Afisa auawa au mwananchii auawa akidhwaniwa ni jambazi!

Hekima inatuita tulaani mauaji haya, kuyapinga na kutaka juhudi zote za kuwaleta kwenye haki zifanyike pasi ya huruma au upendeleo au husuda. Hii haina maana watu tunaridhika na utendaji wea jeshi la polisi. Ushahidi ni mwingi mno kuwa jeshi letu linahitaji mabadilikko ya mfumo (structural reform) ili kulifanya liwe la kisasa zaidi, likijali watu na likiwa linaelewa tunu ya kanuni za demokrasia. Mahitaji ya mabadiliko hayo hayalalishi unyama dhidi ya polisi au raia. Na pamoja na hilo mabadiliko ya msingi yatokee ndani ya jeshi la polisi ili lionekane kweli linajali raia.

Binafsi ninalaani vikali mauaji ya kinyama ya kamanda wa polisi na kutaka haki itendeke kuhakikishwa wahusika wanakutana na mkkono wa sheria. Huwezi kupinga mauaji ya Mwangosi na kutaka haki itendeke halafu ushangilie mauaji ya Kamanda.

Haki ni haki hata ya adui yako ni haki. Mwangosi alikuwa na haki ya kuishi kama vile Barlow alivyokuwa nayo na kama mamia wengine walivyokuwa nayo na ambayo ilikatishwa kinyama. Tusivumilie mauaji ya aina hii kwani yana chochea visasi. Itakuwaje kama polisi nao katika kujihami wanaanza kuua kama mbwa na wananchi wanarudishia kisasi kama wana wazimu?

Litakuwa ni taifa la damu. Damu ambayo isipokataliwa itaendelea kutiririka kama kijito kisichokoma.

Mkuu MMKJJ, katika posti zako za awali kuhusiana na tukio la kuuwawa Kamanda Barlow uliusia kuwa tungojee ukweli ujitokeze.

Kweli sasa details za ukweli zimeanza kutiririka, na si nzuri sana kwa jamii.

Tunasikitika sana kuuwawa kamanda Barlow kinyama, kwa kosa lolote lile.

Hta hivyo icnachoelekea kutokea ni tatizo la kijamii lenye kuhusiana na wake za watu.
Kwamba suala hili limetokea Mwanza ,TWO EPISODES , IN TWO CONSECUTIVE DAYS inatosha kueleza level of indiscipline katika jeshi hilo.
Juzi kakoswa koswa askari wa immigration, ilikuwa auwawe kwa sababu ya kesi ya askari polisi aliyekuwa anatembea na mke wake.Leo Kamanda Barlow ndo kauwawa kabisa kwa hisia za kuwa na mwanamke ambaye si mke wake, saa za usiku mkubwa.

Namsikitikia sana kamanda Barlow kwa kuingia katika tatizo linaloitwa social vices in society,na yeye ni muathirika.

Kuchukua mwanamke ambaye ni mke wa mtu mwingine , toka historia, ni chanzo cha matatizo makubwa,both kidini na kijamii.
Mimi kwa ukweli nahisi mume wa huyo mwanamke waliyekuwa naye amemtenda.

Lakini tuache yote hayo, kiini cha matatizo ni level of INDSCIPLINE kwenye Police Force, na tatizo hili lililojitokeza ni kielelezo tosha.

Manifestation ya indiscipline ndio tuanaanza kuiona , kuua watu bila sababu, kutembea na wake za watu, kubambika kesi, kushirikiana na majambazi n.k.

Tusione aibu, Jeshi la Polisi lazima liundwe upya, miaka ya nyuma Mwalimu aliwahi kulitikisa na kuwaondoa makamanda wengi ili kurudisha discipline.
 
kwa sababu watanzania wamekosa moral of life ndio tunaona haya ya ajabu na bado MUSA! dhambi ya dhuluma imebarikiwa katika nchi hii ,kila kitu kwao kimekuwa ni twende. wewe mwanakijiji unachukuliwa mkeo... eti " ameuawa na majambazi" hapa unadhani utapata haki... na mwanamume mwenzako saa nane usiku, ulitaka mme wa huyu binti amwangukie huyo afande asitishe uroda kama huyo bwana asinge uawa kabla hata ya asubuhi. kama kuna haki katika nchi hii kwanini kila kitu kipindishwesasa hii dharau ilikuwa imevuka kikomo wanzinzi hasa viongozi hutumia madereva kufanya cover sasa huyu jamaa alikuwa amefikia kuwa anamshusha yeye mwenyewe. sasa naanza kujiuliza hekima yako mwanakijiji iko wapi? mtu acheze na ndevu zako lakini asicheze na mkeo.....anahaki ya kufa kama kifo hicho kilivyompata. nadhani sasa kuna haja ya kuwaua hata watuhumiwa wa rushwa mtindo huo....mpaka kieleweke.
 
Ni hekima ya kawaida kuwa mauaji hayanabudi kulaaniwa. Imefika mahali inakuwa kama vile kuna vita kati ya polisi na raia ila kwa bahati mbaya raia hawana silaha wala mamlaka. Kinachowafanya raia wengi washabikie ni pale jeshi la polisi linapotumika kama wakala wa chama cha siasa na kutumia silaha zao kudhuru raia wasio na hatia. Kinachotakiwa kubadilika ni mfumu wa uteuzi ambao utaondoa uteuzi wa kuangalia urafiki au mahusiano binafsi ili taaluma na uwezo wa mtu viwe ndio vigezo pekee. Jeshi la polisi halinabudi kuwa 'neutral' katika kusimamia haki na demokrasia, vinginevyo hali haitatengamaa. Imani kwa jeshi imeshuka sana ingawa wanafanya kazi katika mazingira magumu na wakati mwingine wanafanya mambo mazuri.
 
Mwanakijiji ni kweli Kabisa. Ndg zetu wa Roman Catholic wanawimbo unasema....Bwana Kama wewe ungehesabu maovu yetu, nani angesimama, nani angesimama, nani angesimama mbele yako.... Taifa haliwezi kuendelea hivi, hatujui yatamkuta nani Kesho.

Sio mambo ya kushangilia haya hata kidogo!. Bado naamini TZ ni kisiwa cha AMANI na Mungu atusaidie na kutulinda. Tuliombee Taifa letu, damu zisiendelee kudai damu ktk ardhi, wana maombi mmenielewa naamini.

Queen Esther
Kesho yatamkuta yule anayewindwa kwa sababu fulani,everything happens for a reason!don't be mad.
 
Wewe umesema ni halali mtu kupigwa risasi kwa kutembea na mke wa mtu
ndo nakuuliza.....unaonaje na wake za uliotembea nao wangefanya hivyo kwako?

kuna mahali unamis point mkuu
sitembei na wake za watu nilikuwa nafanya research ili nijue nia ya wanawake hasa maried kumwaga mipicha ya ajabu kwenye facebook
nilijitolea kwa niaba ya mamilioni ya waume wenye wake zao facebook ili wajue mwenendo mzima wa mke wake ndani ya mtandao huo wa kutisha'
nilishafuta account kama nilivyosema pale juu lakini nimekuja na bonge la lesson,FUNGUKA!
 
'VITU VIZITO' vinazidi kuua wananchi. Ilikuwa raia na sasa KITU KIZITO kimemuua RPC...

Kuh hiyo hoja, ni hasira tu za wananchi kuhusiana na wanavyonyanyaswa. RIP Barlow, naye ni binadamu.
Angalizo: Mmeicheki picha ya huyo mwalimu? Ni kisu balaa!
 
Nyoka mmoja akikung'ata hata ukimwona asiye na sumu lazima umkimbie tu, ni kweli kwamba kushangilia kifo kwa binadamu mwenzako ni laana kubwa, lakini tunapaswa kujiuliza nini kimewafikisha watu mpaka wanashangilia kifo cha mtu, angalia matamko ya polisi juu ya vifo vya raia vyenye utata, hata mwenye mtindio wa ubongo huwa anang'amua ni nini kinaendelea, nina uhakika hata kesho wananchi wakisikia kuwa polisi mwingine kauawa wataendelea kushangilia tu na hakuna atakayewakanya, hata wewe MM kwa hili bandiko lako hujafanya chochote.
Ili kuweka mambo sawa jeshi la polisi lenyewe linahitaji kujisafisha kwa kuweka mambo sawa pasipo kutiliwa mashaka, maana wakiendelea hivi itafika kipindi wananchi hawataamini hata wakisema ukweli
 
Mungu atusaidie make kuna kila dalili ya makundi yenye chuki yanakua taratibu kila kukicha, kama mtu anaweza kuchoma jengo la ibada bila hofu au watu kufurahia kifo cha mtu ni dhahiri kuna mahali hapajakaa sawa..
Sitoshangaa tunakoelekea kwamba tunaweza kuanza kuona vipande vya kina boko haram vya kidini na kisiasa vikianza kuibuka, Mungu atuepushie tu
 
......wote wamepoteza maisha katika mazingira ambayo hayakupaswa kutokea; ni mazingira ambayo yanahitaji kuchunguzwa na kuondolewa ili isije ikafika mahali huko mbeleni tukasikia Waziri auawa, Mwenyekiti wa Chama cha siasa apigwa risasi au Mbunge auawa au hata iwe yale yale ya Afisa auawa au mwananchii auawa akidhwaniwa ni jambazi!

kama kawaida, MM ni mwandishi makini mwenye kufikiri sana, lakini hapo tu, kwamba mazingira kama hayo 'yaliyopelekea kifo cha barlow' inabidi yashughuliwe ili tusije kufika mahali huko mbeleni tukasikia waziri flani kauawa, MM mahali hapo tumefika tayari, roho ya mtu awe waziri au raia ina thamani sawa.
 
Mheshimiwa mwanakijiji heshima kwako kwa uchambuzi uliotukuka lakini mzee mwanakiji jamii yetu saizi ndio imefikia hapo anakojolea KORAN mtoto wa dhehebu jingine yanachomwa makanisa ya dhehebu mengine sasa Mzee mwanakijiji labda wewe hujaona picha ya huyo mwl.ambayo alikwa na kamanda mtoto katokelezea kweli kamanda amekufa kishujaaa!!!!!!!!!

Bushman, tunaomba hiyo picha ya huyo mwalimu aliyekuwa na kamanda, je ni mwanmme au mwanamke??? Ni wa CCM au Chadema???? Usichoke na maswali yangu, aulizaye anataka kujua!!!
 
Wengine wanasema ameuawa na majambazi, wengine polisi jamii.

But the point remain kuwa Binadamu ameuawa, amekatishwa maisha yake. Kila mtu ana haki ya kuishi kama wengine. Barlow, Mwangosi, Zona, na wengine wengi walikuwa na haki ya kuishi kama wengine. Tatizo asilimia kubwa ya wana wa nchi hii wameuawa na jeshi la polisi kwa uonevu, ama kwa visa kwa ajili ya kulinda maslahi ya chama tawala.
Tunachotakiwa kupiga vita siyo mauaji ya kutatanisha Mzee Mwanakijiji, bali mfumo mzima unaoweza kujenga heshima na haki kwa kila mwananchi wa nchi hii.
Well; Barlow ameuawa na majambazi, na tukiri tu kuwa ujambazi upo kila mahali, but what about the rest?
Mzee Mwanakijiji umeleta hii hoja wakati ambapo kiongozi anayetegemewa kulinda maisha na mali ya wananchi ameguswa. Juzi huyu huyu Barlow alitoa kauli kuwa kushambuliwa kwa gari la Afisa Uhamiaji was coincidence, lakini Afisa Uhamiaji mwenyewe ameeleza kuwa OCS aliyemshambulia wanafahamiana sana, na kuwa ana mahusiano na mkewe na kesi ipo mahakamani.
Tukubali kuwa there are underlying issues ndani ya jeshi la polisi.
Zingine zote zinaweza kuwa mbwembwe, tukubali kuwa mtu amekatishwa uhai, tukiamini kuwa bado akiwa tegemeo kwa jamii na familia na jamii yake.
 
Last edited by a moderator:
Hakuna hoja hapa!!aliyetenda dhambi A kahukumiwa kwa dhambi B its a lesson,with its answer attached,liwalo na liwe.
 
Back
Top Bottom