Hatimaye yametimia walimu kucheka huu ndiyo waraka mpya.

Hii issue niliipata hata kabla haijaja hapa jukwaani (sijui ihakika wake) ila nasikia ipo halimashauri zote Tusubiri
 
Mkuu walimu ni waajiriwa wa Wakurugenzi, lakini 'MAMLAKA YAO YA AJIRA NA NIDHAMU NI TSD AMBAYO NI SERIKALI KUU' ndio maana hata post zao hazitangazwi na TAMISEMI, wanapandishwa vyeo na TSD Mkurugenzi hawezi kubadili mishahara bila idhini ya UTUMISHI. Mwenye Jukumu la kusimamia MIUNDO NA VIWANGO VYA MISHAHARA YA WATUMISHI WOTE NCHINI NI UTUMISHI, wao wakisema HAPANA hakuna marekebisho yatakayofanyika.
Wewe ni expert sugu ila tu watu hawajakufahamu kwa sababu hawajui mambo haya na wanapenda kujifariji na umbea mwingi. Nimefuatilia maoni yako kwenye post mbili hivi, nimejifunza kitu kikubwa sana toka kwako....... Big up
 
Kwanza sio malengo yangu kupotosha watu, ilikuwa ni katika kushare information kidogo tulizonazo.
Pili ukisoma kipengele cha nne cha barua ile utaona anasisitiza kwamba kwa wale wenye shida kwenye madaraja yao watapandishwa kulingana na waraka mpya na hawataruhusiwa kudai malimbikizo..Swali: Je kulikuwa na haja gani ya kufika kote huko kama swala bado halijakubakiwa na utumishi?

Ni kweli ni kitu kizuri kushare information kidogo tulizonazo lakini si kwa kupotosha bali kwa uhalisia wake!ANGALIA TITLE YAKO ILIVYO NA KITU ULICHOKIWEKA!Umeongelae waraka na haujaweka waraka na unaendelea kusisitiza kuwa ni waraka!Hapo kwenye bold wewe ulitaka waandikaje?Hujui kuwa kila mwaka mpya wa fedha huwa kuna marekebisho ya mishahara ya watumishi wa uma ambayo husapotiwa na waraka?

Na waraka hauwi kama makaratasi haya uliyoyaweka.Huandikwa na katbu mkuu utumishi.Wanaposema "kulingana na waraka mpya" hawamaanishi haya makaratasi uliyoyaweka.Wanamaanisha waraka mpya wa mishahara wa mwaka huu wa fedha ambao haujauweka hapa.

Kwa hiyo tukubaliane kuwa umepotosha kwa kuyaita haya makaratasi ni waraka.Na pia huujui waraka mpya wa mishahara ambao unaongelewa kwenye hiyo barua uliyoiweka.
 
Mi nimeuona huo mnaousema ni waraka. Hayo i mapendekezo tu ambayo wizara ya elimu imeyatoa kwa wizara ya utumishi. Sasa tamisemi wamewaagiza wakurugenzi wapitie waraka wa mwaka 2002 ambao walimu waliulalamikia jambo mojawapo ni kuhusu walimu waliojiendeleza ambao walitaiwa kurudi daraja la chini badala ya kupanda hivyo wakurugenzi wamwagizwa kuwa identify walimu wale na kusema wanastahili madaraja gani sasa ili kama waraa mapendekezo hayo yatakubaliwa na wizara ya utumishi nao hawa wasiachwe tena nyuma. Hata hivyo waraka hua unasema lini utanza kutumika lakini mapendekezo haya hayasemi lini yataanza rasmi. Kwa mtanzamo wangu haya baso ni mapendekezo utumishi waaweza kuyakataa au kuyakubali. Hata hivyo mapendekezo haya yanarusha kila mwalimu ngazi moja ukiyatazama kwa undani utaona kuwa wale woote walofikia kikomo cha kupanda daraja wamepelekwa kwwnye yale madaraja ambayo kama wasingekua kwenye ukomo wangefika huko. Hivyo hayo mapendekezo yapo lakini si waraka,kwakuwa unasema tu madaraja hausemi kiwango na nyongeza kwa kila mwaka kwa kila daraja,pia hauaemi unaanza kutumika lini. Ni mapwndekezo ambayo yakikubaliwa yatafuta waraka wa 2001 na hiyvo kuwa waraka kamili. Swali bajeti si inapita leo haya yapo
 
Mie nilivyoelewa huu walaka wa kubumba ni kuwa ni kwa wale tu walioathirika na waraka wa 2002,na siyo walimu wote.Ni kwa baadhi ya walimu tu.ila uko na mkanganyiko bado,kwani mapendekezo ya muundo mpya wa mshahara unaonyesha kuwa kwa aliye na degree anatakiwa kuanza na TGTS F.kitu ambacho siyo kweli kwani hata walio anza kazi mwaka jana pia wataathirika,hivyo kwa hitimisho langu ni kuwa watakuwa walimu wote,watakao takiwa kubadilishiwa madalaja,kitu ambacho ni IMPOSSIBLE FOR OUR POOR COUNTRY------TZ
 
Wewe ni expert sugu ila tu watu hawajakufahamu kwa sababu hawajui mambo haya na wanapenda kujifariji na umbea mwingi. Nimefuatilia maoni yako kwenye post mbili hivi, nimejifunza kitu kikubwa sana toka kwako....... Big up

Asante Mkuu, Nipo kwenye mfumo unaotoa huduma kwa watumishi wa Serikali na kwenye Idara inayoshughulikia masuala ya walimu. Ni vyema kumwambia mtu ukweli kuliko kumpa Tumaini Hewa.
 
Hichi kilchoandkwa ni huko kwa wenzetu,TZ hakuna ki2 kama hiki,mtapiga makelele lakn hakuna ongezeko kama hili,ETI WALIM
 
Ndg yangu inaelekea hujui kabisa mfumo wa serikali, tofautisha mamlaka ya ajira na upandishwaji wa vyeo na nidhamu na upandishwaji wa mishahara. Mwenye dhamana ya kutangaza nyongeza ya mishahara serikalini ni Waziri wa ofisi ya Rais management ya Utumishi wa Umma, na anayetoa waraka ni katibu wake Mkuu, katika kifuatilia bajeti ya serikali umewahi hata sikia waziri wa elimu au hata Tamisemi katangaza nyongeza ya mshahara? Mifumo wa sasa mapendekezo ya kuongeza mishahara hujadiliwa kisekta na kupeleka mapendekezo kwa Waziri mwenye dhamana ili wajadiliane na Waziri wa fedha kabla ya kutangazwa ili baadae utolewe waraka kwa waajiri. Ukisoma document hii tunayosema ni waraka, ni maelekezo ya mkoa kwa walimu kuandikisha majina wale ambao wanafikiri madaraja yao yamekosewa, hivyo hata mleta uzi ametupotosha wote hapa. Nawasilisha


Hii ni barua toka kwa katibu tawala wa mkoa wa Kilimanjaro kwenda kwa wakurugenzi wa halimashauri kuwajulisha juu ya waraka mpya uliotolewa unaorekebisha waraka wa 2002 kuhusu mishara ya kada ya utumishi wa walimu. Pamoja na mambo mengine, unaelezea malimbikizo ya mishara ya nyuma ya walimu kuwa haitalipwa badala yake wataingizwa moja kwa moja kwenye madaraja mapya kulingana na waraka huo. Sasa la msingi la kujiuliza, ni hii hii serekali sikivu ya SSeM ndio waliotoa waraka huo, na kama ni ndio, ni kweli watautekeleza, au ni yale yale ya kuwatapeli watanzania
kwa kauli za maisha bora kwa kila mtanzania? Kumbuka tunaelekea uchaguzi.
 
Naoana chenga tu hata siwezi kusoma kabisa... Mkuu huwezi summaraize japo kidogo kilicho andikwa hapo ili na wengine tuelewe japo kwa ufupi
 
Hii ni barua toka kwa katibu tawala wa mkoa wa Kilimanjaro kwenda kwa wakurugenzi wa halimashauri kuwajulisha juu ya waraka mpya uliotolewa unaorekebisha waraka wa 2002 kuhusu mishara ya kada ya utumishi wa walimu. Pamoja na mambo mengine, unaelezea malimbikizo ya mishara ya nyuma ya walimu kuwa haitalipwa badala yake wataingizwa moja kwa moja kwenye madaraja mapya kulingana na waraka huo. Sasa la msingi la kujiuliza, ni hii hii serekali sikivu ya SSeM ndio waliotoa waraka huo, na kama ni ndio, ni kweli watautekeleza, au ni yale yale ya kuwatapeli watanzania
kwa kauli za maisha bora kwa kila mtanzania? Kumbuka tunaelekea uchaguzi.

Waraka upi huo unaouzungumzia?
 
Back
Top Bottom