MtazamoWangu
JF-Expert Member
- Apr 25, 2009
- 313
- 7
Zitto nimependa sana flexibility uliioonyesha hapo mwisho, "only fools never change their minds.." huu ni wakati ambao watawala wameonekana wameshindwa nchi na kila mtu ameona, kuna kipindi jana kilirushwa ITV kuhusu wananchi waliobomolewa nyumba zao Dodoma...wanvyoongea unapata hisia kama watu wameamka...wanaona udhalimu, ufisadi, uonevu, kiburi na jeuri ya walioko madarakani...uongozi mbadala ni muhimu sana...na chadem imekuwa katika nafasi nzuri..let us use it...nimeshaihakikishia chadema jimbo moja 2005...kwahiyo mchango wako kwa wakati kama huu ni muhimu sana..kama uliamua kuitumikia nchi yako, wananchi wamekupokea kwa mikono 2...kuondoka ni sawa na kuwacheza shere....i will suport u if you change your mind and everyone else will do....1. Nilijiunga CHADEMA kabla ya Kabourou. Mimi nilijiunga mwaka 1993, nikiwa kidato cha Tatu Shule ya Sekondari Kigoma. Yeye alikuja mwaka 1994 kugombea Ubunge kuziba nafasi ya Marehemu Rajabu Omar Mbano.
2. Sijawahi kuwa mwanachama wa CCM na hivyo hakuna kitu kurudi nyumbani. Toka nimekuwa na umri wa kujiunga siasa nimekuwa mwanachama wa chama kimoja tu CHADEMA na ninamwomba sana Mungu uhai wangu uishie katika chama hicho tu. Inshaallah
3. Kutangaza kwangu kutogombea hakuhusiani na hata kidogo na uzushi wako hapo juu. Nimeshasema ni kwa nini niliamua kutoomba kipindi kingine cha Ubunge. Hata hivyo, kwa kuwa ni maamuzi yangu ninaweza kubadili msimamo wangu huo na kugombea tena na kushinda. Nipo huru kuamua ninachoona inafaa!