Haji Manara atafuta wafanyakazi wa ndani wamsaidie Mke wake kupika

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,306
Baada ya kumuoa mchumba wake Zailyssa, Haji Manara ameamua kumtafutia Mke wake huyo Vijakazi wa ndani ili wamsaidie kwenye majukumu ya nyumbani.

Anaandika Haji Manara kwenye ukurasa wake wa Instagram,

TANGAZO TANGAZO TANGAZO 🙌
NAFASI ZA AJIRA MPYA

Kwa Sheria ya Dini yangu, Mila na Desturi za Watu wa Pwani, Utamaduni na Maadili ya Mwanamme wa Kiswahili, ni haraam kumfanya Mkeo Kijakazi au Mtumwa ndani ya nyumba.

Kwetu Sisi Mashomvi Mke ni Pambo, Mke ni Malkia, Mke ni Pozo la tabu zako, Mke yake Hina na Piko, Mke ni kujikwatua kwa ajili ya kumfurahisha Mmewe, Mke wa kikwetu kazi yake kubwa ni kukupa furaha na kukusaidia kutekeleza majukumu ya kifamilia, ni makosa kwetu hata Mke kwenda Sokoni kuhemea , hata ile kufanya kazi ni kwa sababu ya dunia ya kisasa ya kusaidiana maisha, lakini akiwa home hapaswi tena kuwa MTUMWA!!

Basi kwa maneno haya nawaomba wale wote ambao ni Make Up artists au watengeneza kucha na venders wengine wa majumbani,,natangaza ajira nyumbani kwangu, bila kusahau Wapishi.

Na kwenye Wapishi nahitaji Chefs anaejua kuuchezea Mchele kisawa sawa, kuanzia Biriani,Pilau,Mandi na Ubwaba.

Chef’s mwingine ni maalum kwa Madiko madiko kama Rost ,Burger, Pizza, Chips, Nyama Choma na Chefs maalum wa kutengeneza Salads na Mboga nyingine, nisisahau mtengeneza Juice na desert, ila huyu wa mwisho ntamleta kutoka Philippines.

Sihitaji Mke wangu akaungue na moto au kuhangaika na kuni coz si haba naweza kumfanya malkia kwa kumuwekea wasaidizi na yeye kazi yake ibaki kunipa furaha Bugati, kunipikia iwe labda atake mwenyewe tena mwisho iwe coffee yangu ya asubuhi tu.

Nini maoni yako?

Written by Mjanja M1
 
Back
Top Bottom