Hadithi: Roho ya paka. (Ben R. Mtobwa)

14

Mamia ya watu walioduwaa nje ya jengo hilo walishangaa kuona mlango ukifunguka taratibu na kumruhusu kijana mmoja mkakamavu na msichana kuanza kuondoka. Mvulana akiwa katika suti yake nyeusi, isipokuwa kwa vumbi kidogo, katika mavazi yake alionekana mtanashati kama ambaye anatoka katika jumba la starehe kinyume na watu waliokuwa nje walivyoamini. Lakini msichana alikuwa taabani, kachakaa mwili na mavazi kama aliyetoroka kuzimu. Alitembea kwa kujikongoja huku akipata msaada wa mkono wa mvulana uliomshika kiuno.

Sura za vijana hawa zilikuwa maarufu nchini kama zilivyomashuhuri kote duniani. Haukupita muda kabla ya watu waliokuwa hapo nje hawajaanza kunong’ona, “Ni joram Kiango!”

“Ndiyo. Na Nuru”

Polisi ambao walianza kuziweka silaha zao sawa kuwaelekea, walipowafahamu walizirudisha makwapani na kusimama kwa utulivu. Mmoja wao saluti ilimtoka, na Joram akapokea kwa kutabasamu kidogo. Kabla askari hao hawajajua wafanye nini na Joram, bosi wao, Inspekta Kombora, alitokea, na askari wote wakamkimbilia.

Yeye pia alikuwa taabani kama Nuru. Nguo zake zilichakaa na kuchafuka, mwili wake ulijaa marejaha, macho yake yalilegea kana kwamba alikuwa amekesha akinywa pombe kali. Akiushikilia ukuta alitembea taratibu na kuzipuuza saluti ambazo zilielekewa kwake.

“Pole sana mzee.”

“Nipelekeni ofisini… hapana nyumbani,” alisema kwa udhaifu

“Tukupeleke hospitali afande?”

“Nimesema nyumbani.”

Dereva mmoja alimsogezea gari. Kabla hajalipanda alitoa maelekezo kwa askari hao, akiwataka wahakikishe jengo hilo linalindwa kwa makini usiku na mchana hadi atakapokuwa tayari kukamilisha suala hilo ambalo alidai limekwisha!

Joram alitumia fursa hiyo kuutoroka umati wa watu. Alimfuata mtu mmoja aliyekuwa ameketi ndani ya gari lake, Toyota Saloon, na kumwomba lifti. Mtu huyo, kwa furaha, aliwafungulia milango na kuwakaribisha ndani. Joram akamwingiza mgonjwa wake kisha yeye akaingia na kumtaka awapeleke hotel ya Mawenzi.

“Nina bahati sana leo” msamaria alisema.

“Bahati gani?” Joram alimwuliza

“Kukutana ana kwa ana na wewe. Ni jambo ambalo sikulitegemea kabisa. Nimekuwa nikikusoma katika vitabu na magazeti tu. Hivi huko ndani kulikuwa na nini?”

“Ngoja gazeti la kesho utaelewa, ni hadithi ndefu sana”

“Hivi haya wanayoyaandika juu yako ni ya kweli? Sio kwamba waandishi wanatia chumvi sana ili magazeti na vitabu vyao vinunuliwe?”

Joram, akiwa hana hamu na magazeti, alijikuta akimwambia, “Hayo unayoyasikia yazidishe mara nne, utoe nane na kuongeza mbili ndipo utapata ukweli wenyewe”

Akiwa amechanganyikiwa, dereva huyo aliendesha gari bila maongezi zaidi mpaka alipowafikisha mbele ya hoteli yao.

Joram alimshukuru kwa ukarimu wake, akamzoa Nuru ambaye alianza kulala na kumwingiza hotelini. Watu waliokuwa mapokezi walitokwa na macho ya mshangao, hasa kutokana na hali ya Nuru, lakini Joram hakuwapa nafasi ya maswali. Badala yake alichukua ufunguo wake na kwenda chumbani kwake, akiwa bado amemshikilia Nuru kiuno. Hakuhitaji funguo huo, chumba kilikuwa wazi, kinyume na alivyokiacha. Jicho lake moja chumbani humo lilimfanya afahamu kuwa alikuwa ametembelewa. Ingawa karibu kila kitu kilikuwa kama alivyokiacha, lakini bado dalili zilimwonyesha kuwa kila kitu kilikuwa kimekaguliwa na kuvurugwa kwa uangalifu mkubwa.

Joram akamtua Nuru kwenye kitanda na kumlaza taratibu. Alipovuta mto ili amweke vizuri, aligutuka kuona mto huo ulikuwa umetumiwa kuficha maiti ya paka mnene, aliyenawiri, ambayo yalilazwa kitandani hapo. Kando ya mzoga huo, Joram aliona maandishi mekundu yalioandikwa juu ya shuka kwa lugha ya kiingereza ‘you’re next’ yakimaanisha kuwa ni yeye Joram atakayefuatia.

Alipomgeukia Nuru kuona kama naye pia alikuwa ameuona mzoga huo, alifurahi kumwona tayari kalala kwa utulivu, akikoroma taratibu. Akainama na kumchunguza paka huyo kwa makini zaidi. Akabaini kuwa aliuawa kwa kunyongwa kwa kwa mkono muda mfupi uliopita kwani alikuwa bado ana joto. Lakini Joram alipozidi kumchunguza aligundua kuwa bado alikuwa akipumua taratibu. Badala ya kumtupa dirishani kama alivyokusudia, Joram alimwinua polepole na kumweka nje ya chumba, upande wa mapumziko.

Baada ya kuduwaa kwa mara ya pili, Joram alimnusisha paka huyo dawa ya kulevya, jambo ambalo lilimfanya mnyama huyo mdogo apige chafya na dakika chache baadaye ainuke na kujikongoja taratibu kuelekea nje.

Joram hakuhitaji kuambiwa paka huyo ameletwa na nani chumbani humo. Adrian!... Ni yeye pia aliyekipekua chumba chake ambamo dalili zilimwonyesha Joram kuwa alikaa muda mrefu akimsubiri.

Kitendo cha kupata uhai kwa paka huyo, ambaye Joram alijua fika aliwekwa hapa kwa njia ya kumtisha huku adui huyo akiamini kuwa ni mzoga, kilimdhihirishia Joram kuwa mapambano bado yalikuwa yanaendelea. Hata hivyo, ilimtia matumaini makubwa ya kuibuka mshindi akizingatia uhai wa paka huyo ulivyorejea baada ya muuaji kuamini kuwa ametimiza kazi yake.

Akifahamu fika jinsi roho ya Adrian ilivyolemaa kwa chuki na fikra zake zilivyomezwa na kiasi Joram alijua kuwa alikuwa na wajibu mkubwa kumteketeza kiumbe huyo kabla hajafanya madhara zaidi. “Ni yeye, au mimi!” aliwaza akiondoka kurudi kitandani ambako Nuru alilala kwa utulivu.

Joram alimtazama msichana huyu alivyolala na mavazi yake yote. Aliitazama sura yake nzuri na umbo lake la kuvutia lilivyopendeza katika mavazi hayo yaliyochakaa na kuchafuka.

***

Pamoja na hasira zake, Adrian alichukua wasaa wa kujilaumu kimoyomoyo. Kwa kiasi kikubwa alihisi alishiriki kuwaangusha waajiri wake ambao alikwisha amua kuwa wana aina fulani ya kichaa. Kitendo chake cha kupenya toka katika eneo hilo la ofisi hadi katika hoteli ya Joram Kiango ili akammalize hukohuko, badala ya kumsubiri, kama wenyeji wake walivyomwelekeza, kwa kila hali kimechangia kumfanya awe hai hadi sasa na awaokoe mateka wake.

Jambo hili, limezifanya jitihada zake zote, za kupenya katika uchochoro wa hoteli hiyo, hadi nyuma ambako alitumia kamba kupanda hadi juu na kisha kwa kutumia tundu la moshi kujipenyeza hadi ndani ziwe za bure.

Chumbani mwa Joram, Adrian alipekua kila sehemu bila kujua anatafuta nini. Hakupata chochote. Hata hivyo, ili asiondoke bila zawadi yoyote, ndipo alipochukua mkufu wa dhahabu uliokuwa kama umesahauliwa katika begi mojawapo.

Adrian alijua ingemchukua muda Joram kugundua upotevu huo, lakini kwake ingekuwa fahari kubaki na kumbukumbu ya kumfuta duniani.

Ni wakati alipokuwa akitoka nje ya chumba hicho alipokutana na paka yule ambaye alipita akinusa huko na huko. Adrian hakuchelewa kumdaka na kumminya koo kwa vidole viwili hadi paka alipokata roho, kisha akamlaza juu ya kitanda cha Joram kama salamu ambazo alijua zitamsisimua zaidi ya kupotea kwa mkufu mdogo wa dhahabu.

Adrian akaamua kurudi kwa waajiri wake. Akiwa nje ya jengo hilo la Paul na Philip, alimwona inspekta Kombora, pamoja na uchovu wake mwingi, akitoa maelekezo juu ya ulinzi wa jengo hilo. Akiwa na hakika kuwa mambo yalikuwa yamewaendea kombo waajiri wake, Adrian alitazama kwa makini jengo hilo huku rohoni akijua wazi kuwa japo jeshi zima la polisi liletwe kulinda usiku huo lazima angeingia katika jengo hilo na kuchukua kila kilicho chake.

Hakukuwa na mtu yeyote, duniani na mbinguni, ambaye angemzuia.

Kwa miji yote mikubwa ilivyo kote duniani, jiji la Dar es Salaam pia halijui usiku. Mara tu jua linapozama na kiza kutanda, wako baadhiya watu ambao huona kana kwamba ndio kwanza kumepambazuka. Hivyo, wakati wenzao wakijiandaa kulala wenzao hujiandaa kutoka tayari kwa shughuli zao mbalimbali, baadhi wakiwa wafanyakazi wa zamu za usiku, baadhi watumiaji tu wa pesa zao, hali wengine wakiwa waviziaji tu, wezi na Malaya wa bandarini.

Usiku wa leo Joram alikuwa mmoja wao. aliporejea toka muhimbili akiwa na aina mbalimbali za dawa ambazo alielekezwa jinsi ya kumpa Nuru, alimwamsha na kumshurutisha kuzinywa.

Kama alivyokuwa ameambiwa na daktari yule, mara tu baada ya kuzinywa, Nuru alichukuliwa tena na usingizi, usingizi mzito ambao ungempumzisha kwa saa ishirini na nne wakati dawa zikifanya kazi.

Baada ya kuhakikisha Nuru amelala kwa utulivu, ndipo Joram pia alipolala kando yake na usingizi mnono, usio na ndoto, kumchukua. Alizinduka saa moja usiku. Akafanya haraka kuoga, kisha kuvaa suti yake.

Baada ya hapo aliichukua bastola yake, bomu moja la mkono, kisu na silaha zake nyingine akazitokomeza katika mifuko yake ya siri. Alipojitazama katika kioo na kuridhika kuwa hata askari mdadisi kiasi gani asingemshuku kuwa anakwenda vitani badala ya kwenda kufanya matumizi, ndipo alipombusu Nuru, akamfunika vizuri na kisha kuondoka baada ya kuufunga mlango vyema nyuma yake.

Hakuwa na haraka. Alipita katika chumba cha maakuli ambako aliagiza ugali kwa kuku wa kuokwa. Wakati akisubiri chakula hicho alijipongeza kwa bia mbili za stella. Chakula chake kilipofika alikula kwa utulivu, huku akiteremsha kwa kopo la tatu la stella. Alipomaliza aliwasha sigara na kuivuta taratibu huku kopo la nne lilkikoza moshi. Saa yake ilipomwashiria kuwa imetimia nne kasorobo za usiku ndipo alipolipa bili yake na kuingia mitaani.

Kwa mwendo ule ule wa taratibu, alivuta hatua moja baada ya nyingine kuziendea ofisi za Kangaroo. Alijua fika kuwa watakuwepo na silaha zao mikononi. Hata hivyo, akiwa amedhamiria kuingia alikwishajiandaa kwa njia moja au nyingine ambayo ingemwezesha kuingia. Hivyo, hilo hakulitilia wasiwasi. Ambalo lilimtia wasiwasi na kumwongezea shahuku ya kufika aendako ni Adrian. Alikuwa na hakika kuwa Adrian, alivo kichwa maji, lazima pia angebuni kuingia katika jengo hilo. Na ni hilo lililomfanya awahi. Alitaka awe wa kwanza kufika katika jengo hilo ili amsubiri na kumpokea. Alijua fika kuwa mkutano wao wa ana kwa ana ulikuwa na maana moja tu, ya kumwacha mmoja hai, mwingine maiti. Joram alikuwa na uhakika kuwa huyo maiti asingekuwa yeye.

Wakati akikaribia ofisi hiyo, Joram aliichomoa tai yake nyeupe na kuisokomeza mfukoni. Kuondolewa kwa tai hiyo, kulimfanya abadilike ghafla na kuwa kama kivuli au sehemu ya kiza. Aliubadili pia mwendo wake na kuanza kunyata kwa uangalifu, toka ukuta hadi ukuta; kichaka hadi kichaka. Wapita njia waliomtazama kwa macho ya udadisi aliwapumbaza kwa kujifanya ama anajisaidia haja ndogo au anafunga kamba za viatu vyake, ama amelewa na hivyo, anakwenda bila mpangilio wowote.

Alipofika mbele ya Kangaroo, kama ivyotegemea, alimwona askari mmoja mwenye silaha na magwanda akiwa amesimama kuuegemea ukuta, bunduki yake kaishika mkono mmoja, wa pili ukiwa mfukoni. Joram alimtazama kwa makini. Akashangazwa na utulivu wa askari huyo. Alipotupa macho kutazama huko na huko hakumwona askari mwingine.

Akaitazama saa yake ambayo ilimuashiria saa nne na dakika kumi. Alihitaji kuwa katika jengo hilo mapema. Hivyo, alipoona askari huyo hatoki hapo aliposimama, aliamua kumfuata. Aliiwasha sigara yake na kuipachika mdomoni, akakohoa, kisha akaanza kumsogelea. Alitegemea kuambiwa simama au kupewa amri yoyote ile. Haikutoka. Joram alizidi kumsogelea hadi alipomfikia na kumsalimu. Hakuitikia.

“Hujambo, brother?” Joram alisalimu tena.

Bado hakuitikiwa, jambo ambalo aliona halikuwa la kawaida. Alimtazama askari huyo kwa makini zaidi na kubaini kuwa alikuwa hatingishiki, haoni wala hasikii. Alipojaribu kumtikisa aliporomoka na silaha yake na kuanguka sakafuni.

Ndio kwanza Joram akabaini kuwa alikuwa anaongea na maiti. Akainama na kumshika kifuani ambako alimkuta kapoa kitambo. Kiasi Joram alitahayari. Alitegemea ukatili. Lakini hakutegemea ukatili wa kiasi hicho. Kwa ujumla, aliondokea kuamini kuwa kipindi cha mauaji ya kinyama kilikuwa kimepita, wazo ambalo sasa alilijutia.

Hakuhitaji kuambiwa kuwa mauaji hayo yamefanywa na nani. Wala hakuiona haja ya kujiuliza kwanini yamefanyika. Adrian alikuwa amemtangulia. Akamwua askari huyo, bila shaka kwa hila, ili asiwe kipingamizi cha kumfanya ashindwe kuingia ndani. Hivyo, ama alikuwa ndani ama ametoka.

Wakati akiyafikiri hayo Joram Kiango tayari alikuwa ameusimamisha mzoga huo wa askari kama alivyoukuta na kuirejesha bunduki mkononi mwake na kuanza kunyata akielekea mlangoni. Kando ya mlango huo, kwenye kibanda kidogo cha mapokezi, Joram aliikuta maiti ya askari wa pili. Huyu alikuwa ameketishwa juu ya kiti na kuiinamia meza, bunduki mkononi. Joram hakuitaji kumgusa kujua kuwa amekufa.

Aidha, hakuwa na haja ya kumshika shingo ili kubaini kuwa lilikuwa limevunjwa kwa pigo kali la judo. Alichofanya ni kukimbilia ndani, ambako aliukuta mlango ukiwa wazi, kama unaomsubiri. Harakaharaka bastola yake ikiwa mkononi, alinyata toka chumba hadi chumba. Akitumia tochi yake yenye ukubwa wa kalamu, alichungulia kila kona, kila uvungu wa meza, kila kabati, kila uvungu wa friji, bila mafanikio. Kila dalili ilimwonyesha kuwa Adrian amekuja na kuondoka.

Joram akaziacha ofisi za kawaida na kuzifuata zile za siri ambako waliwazika hai Paul na Philip. Huko pia Adrian alikuwa amemtangulia na alichokifanya hakikustahili kutazamwa. Mateka hao wawili ambao yeye na Kombora waliamua kuwafungia hai, Adrian alikuwa amewachoropoa toka shimoni humo na kuwachinja kama kuku, mmoja baada ya mwingine. Miili yao, aliitupa juu ya sakafu na kuwafanya walale wakiwa wamekumbatiana ndani ya dimbwi la damu yao wenyewe.

Joram alikiacha chumba hicho na kukimbilia kile ambacho kilihifadhi mamilioni ya pesa za kigeni. Alisogeza sefu ambalo liliwekwa kwa geresha na kulifikia lile la siri ambalo liliunganishwa na ukuta kwa hila. Alipojaribu kulifungua alishangaa kulikuta likiwa wazi. Pale ambapo palikuwa na vitita vya noti za ndani na nje sasa hapakuwa na kitu chochote. Hapana, palikuwa na kitu fulani, kitu kidogo, cheusi. Joram aliisogeza tochi yake na kutazama. Kama macho yake yalichelewa kumwashiria yanatazama nini, pua yake haikuchelea kufanya hivyo. Kitu hicho kilikuwa kinyesi. Baada ya kuchukua pesa hizo, kwa kuonyesha dharau, Adrian, akijua mtu yeyote angetamani kuzipata pesa hizo ndipo alipoamua kufanya hivyo.

Mara ya kwanza maishani mwake hasira hizo zilimfanya atetemeke mwili mzima. “Mshenzi” aliropoka kwa mara ya pili. “Haendi popote! Kamwe haondoki nje ya nchi hii akiwa hai,” alinguruma akigeuka kuanza kutoka nje ya chumba hicho taratibu kwa mwendo wa sismba aliyejeruhiwa mwili na roho.




MWISHO MSIJE MKANIAMBIA TENA NIENDELEE. NIKIENDELEA NITAKUA NAWADANGANYA SASA.....
 
ivo vitabu ni series... adrian yuko mbeleni huko
naomba unitajie seasoni ya kwanza ni ipi mpk kufikia hii roho ya paka na kutoka hapa kinafuata kipi na kipi
yaan nipe mtiririko wa huo seriez nianze kununua kipi araf kifuate kipi ili nifaidi uhondo vizuri

unajua kipindi kile wakati chalii nilipokuwa nasoma vitabu vya FATHER anavyonunua nikawa nadhani JORAM KIANGO yupo kweri arafu MZEE naye alikuwa MAGUMASHI nikimuuliza JORAMU na NURU wanakaa wapi ananiambia eti wanakaa tabata basi ikitojea safari ya tabata naangaza macho kumtafuta JORAM nimuone lkn wapi simuoni nilipopata akili nikasema dah MZEE kweli aliniweza nikawa namuuliza kwann ulikuwa unaniongopea akajibu nilikuwa na maswari sana mpk yanamchosha
teh !
 
naomba unitajie seasoni ya kwanza ni ipi mpk kufikia hii roho ya paka na kutoka hapa kinafuata kipi na kipi
yaan nipe mtiririko wa huo seriez nianze kununua kipi araf kifuate kipi ili nifaidi uhondo vizuri

unajua kipindi kile wakati chalii nilipokuwa nasoma vitabu vya FATHER anavyonunua nikawa nadhani JORAM KIANGO yupo kweri arafu MZEE naye alikuwa MAGUMASHI nikimuuliza JORAMU na NURU wanakaa wapi ananiambia eti wanakaa tabata basi ikitojea safari ya tabata naangaza macho kumtafuta JORAM nimuone lkn wapi simuoni nilipopata akili nikasema dah MZEE kweli aliniweza nikawa namuuliza kwann ulikuwa unaniongopea akajibu nilikuwa na maswari sana mpk yanamchosha
teh !
hahahaaaaaa
Nitafanya hivyo mkuu...
 
14

Mamia ya watu walioduwaa nje ya jengo hilo walishangaa kuona mlango ukifunguka taratibu na kumruhusu kijana mmoja mkakamavu na msichana kuanza kuondoka. Mvulana akiwa katika suti yake nyeusi, isipokuwa kwa vumbi kidogo, katika mavazi yake alionekana mtanashati kama ambaye anatoka katika jumba la starehe kinyume na watu waliokuwa nje walivyoamini. Lakini msichana alikuwa taabani, kachakaa mwili na mavazi kama aliyetoroka kuzimu. Alitembea kwa kujikongoja huku akipata msaada wa mkono wa mvulana uliomshika kiuno.

Sura za vijana hawa zilikuwa maarufu nchini kama zilivyomashuhuri kote duniani. Haukupita muda kabla ya watu waliokuwa hapo nje hawajaanza kunong’ona, “Ni joram Kiango!”

“Ndiyo. Na Nuru”

Polisi ambao walianza kuziweka silaha zao sawa kuwaelekea, walipowafahamu walizirudisha makwapani na kusimama kwa utulivu. Mmoja wao saluti ilimtoka, na Joram akapokea kwa kutabasamu kidogo. Kabla askari hao hawajajua wafanye nini na Joram, bosi wao, Inspekta Kombora, alitokea, na askari wote wakamkimbilia.

Yeye pia alikuwa taabani kama Nuru. Nguo zake zilichakaa na kuchafuka, mwili wake ulijaa marejaha, macho yake yalilegea kana kwamba alikuwa amekesha akinywa pombe kali. Akiushikilia ukuta alitembea taratibu na kuzipuuza saluti ambazo zilielekewa kwake.

“Pole sana mzee.”

“Nipelekeni ofisini… hapana nyumbani,” alisema kwa udhaifu

“Tukupeleke hospitali afande?”

“Nimesema nyumbani.”

Dereva mmoja alimsogezea gari. Kabla hajalipanda alitoa maelekezo kwa askari hao, akiwataka wahakikishe jengo hilo linalindwa kwa makini usiku na mchana hadi atakapokuwa tayari kukamilisha suala hilo ambalo alidai limekwisha!

Joram alitumia fursa hiyo kuutoroka umati wa watu. Alimfuata mtu mmoja aliyekuwa ameketi ndani ya gari lake, Toyota Saloon, na kumwomba lifti. Mtu huyo, kwa furaha, aliwafungulia milango na kuwakaribisha ndani. Joram akamwingiza mgonjwa wake kisha yeye akaingia na kumtaka awapeleke hotel ya Mawenzi.

“Nina bahati sana leo” msamaria alisema.

“Bahati gani?” Joram alimwuliza

“Kukutana ana kwa ana na wewe. Ni jambo ambalo sikulitegemea kabisa. Nimekuwa nikikusoma katika vitabu na magazeti tu. Hivi huko ndani kulikuwa na nini?”

“Ngoja gazeti la kesho utaelewa, ni hadithi ndefu sana”

“Hivi haya wanayoyaandika juu yako ni ya kweli? Sio kwamba waandishi wanatia chumvi sana ili magazeti na vitabu vyao vinunuliwe?”

Joram, akiwa hana hamu na magazeti, alijikuta akimwambia, “Hayo unayoyasikia yazidishe mara nne, utoe nane na kuongeza mbili ndipo utapata ukweli wenyewe”

Akiwa amechanganyikiwa, dereva huyo aliendesha gari bila maongezi zaidi mpaka alipowafikisha mbele ya hoteli yao.

Joram alimshukuru kwa ukarimu wake, akamzoa Nuru ambaye alianza kulala na kumwingiza hotelini. Watu waliokuwa mapokezi walitokwa na macho ya mshangao, hasa kutokana na hali ya Nuru, lakini Joram hakuwapa nafasi ya maswali. Badala yake alichukua ufunguo wake na kwenda chumbani kwake, akiwa bado amemshikilia Nuru kiuno. Hakuhitaji funguo huo, chumba kilikuwa wazi, kinyume na alivyokiacha. Jicho lake moja chumbani humo lilimfanya afahamu kuwa alikuwa ametembelewa. Ingawa karibu kila kitu kilikuwa kama alivyokiacha, lakini bado dalili zilimwonyesha kuwa kila kitu kilikuwa kimekaguliwa na kuvurugwa kwa uangalifu mkubwa.

Joram akamtua Nuru kwenye kitanda na kumlaza taratibu. Alipovuta mto ili amweke vizuri, aligutuka kuona mto huo ulikuwa umetumiwa kuficha maiti ya paka mnene, aliyenawiri, ambayo yalilazwa kitandani hapo. Kando ya mzoga huo, Joram aliona maandishi mekundu yalioandikwa juu ya shuka kwa lugha ya kiingereza ‘you’re next’ yakimaanisha kuwa ni yeye Joram atakayefuatia.

Alipomgeukia Nuru kuona kama naye pia alikuwa ameuona mzoga huo, alifurahi kumwona tayari kalala kwa utulivu, akikoroma taratibu. Akainama na kumchunguza paka huyo kwa makini zaidi. Akabaini kuwa aliuawa kwa kunyongwa kwa kwa mkono muda mfupi uliopita kwani alikuwa bado ana joto. Lakini Joram alipozidi kumchunguza aligundua kuwa bado alikuwa akipumua taratibu. Badala ya kumtupa dirishani kama alivyokusudia, Joram alimwinua polepole na kumweka nje ya chumba, upande wa mapumziko.

Baada ya kuduwaa kwa mara ya pili, Joram alimnusisha paka huyo dawa ya kulevya, jambo ambalo lilimfanya mnyama huyo mdogo apige chafya na dakika chache baadaye ainuke na kujikongoja taratibu kuelekea nje.

Joram hakuhitaji kuambiwa paka huyo ameletwa na nani chumbani humo. Adrian!... Ni yeye pia aliyekipekua chumba chake ambamo dalili zilimwonyesha Joram kuwa alikaa muda mrefu akimsubiri.

Kitendo cha kupata uhai kwa paka huyo, ambaye Joram alijua fika aliwekwa hapa kwa njia ya kumtisha huku adui huyo akiamini kuwa ni mzoga, kilimdhihirishia Joram kuwa mapambano bado yalikuwa yanaendelea. Hata hivyo, ilimtia matumaini makubwa ya kuibuka mshindi akizingatia uhai wa paka huyo ulivyorejea baada ya muuaji kuamini kuwa ametimiza kazi yake.

Akifahamu fika jinsi roho ya Adrian ilivyolemaa kwa chuki na fikra zake zilivyomezwa na kiasi Joram alijua kuwa alikuwa na wajibu mkubwa kumteketeza kiumbe huyo kabla hajafanya madhara zaidi. “Ni yeye, au mimi!” aliwaza akiondoka kurudi kitandani ambako Nuru alilala kwa utulivu.

Joram alimtazama msichana huyu alivyolala na mavazi yake yote. Aliitazama sura yake nzuri na umbo lake la kuvutia lilivyopendeza katika mavazi hayo yaliyochakaa na kuchafuka.

***

Pamoja na hasira zake, Adrian alichukua wasaa wa kujilaumu kimoyomoyo. Kwa kiasi kikubwa alihisi alishiriki kuwaangusha waajiri wake ambao alikwisha amua kuwa wana aina fulani ya kichaa. Kitendo chake cha kupenya toka katika eneo hilo la ofisi hadi katika hoteli ya Joram Kiango ili akammalize hukohuko, badala ya kumsubiri, kama wenyeji wake walivyomwelekeza, kwa kila hali kimechangia kumfanya awe hai hadi sasa na awaokoe mateka wake.

Jambo hili, limezifanya jitihada zake zote, za kupenya katika uchochoro wa hoteli hiyo, hadi nyuma ambako alitumia kamba kupanda hadi juu na kisha kwa kutumia tundu la moshi kujipenyeza hadi ndani ziwe za bure.

Chumbani mwa Joram, Adrian alipekua kila sehemu bila kujua anatafuta nini. Hakupata chochote. Hata hivyo, ili asiondoke bila zawadi yoyote, ndipo alipochukua mkufu wa dhahabu uliokuwa kama umesahauliwa katika begi mojawapo.

Adrian alijua ingemchukua muda Joram kugundua upotevu huo, lakini kwake ingekuwa fahari kubaki na kumbukumbu ya kumfuta duniani.

Ni wakati alipokuwa akitoka nje ya chumba hicho alipokutana na paka yule ambaye alipita akinusa huko na huko. Adrian hakuchelewa kumdaka na kumminya koo kwa vidole viwili hadi paka alipokata roho, kisha akamlaza juu ya kitanda cha Joram kama salamu ambazo alijua zitamsisimua zaidi ya kupotea kwa mkufu mdogo wa dhahabu.

Adrian akaamua kurudi kwa waajiri wake. Akiwa nje ya jengo hilo la Paul na Philip, alimwona inspekta Kombora, pamoja na uchovu wake mwingi, akitoa maelekezo juu ya ulinzi wa jengo hilo. Akiwa na hakika kuwa mambo yalikuwa yamewaendea kombo waajiri wake, Adrian alitazama kwa makini jengo hilo huku rohoni akijua wazi kuwa japo jeshi zima la polisi liletwe kulinda usiku huo lazima angeingia katika jengo hilo na kuchukua kila kilicho chake.

Hakukuwa na mtu yeyote, duniani na mbinguni, ambaye angemzuia.

Kwa miji yote mikubwa ilivyo kote duniani, jiji la Dar es Salaam pia halijui usiku. Mara tu jua linapozama na kiza kutanda, wako baadhiya watu ambao huona kana kwamba ndio kwanza kumepambazuka. Hivyo, wakati wenzao wakijiandaa kulala wenzao hujiandaa kutoka tayari kwa shughuli zao mbalimbali, baadhi wakiwa wafanyakazi wa zamu za usiku, baadhi watumiaji tu wa pesa zao, hali wengine wakiwa waviziaji tu, wezi na Malaya wa bandarini.

Usiku wa leo Joram alikuwa mmoja wao. aliporejea toka muhimbili akiwa na aina mbalimbali za dawa ambazo alielekezwa jinsi ya kumpa Nuru, alimwamsha na kumshurutisha kuzinywa.

Kama alivyokuwa ameambiwa na daktari yule, mara tu baada ya kuzinywa, Nuru alichukuliwa tena na usingizi, usingizi mzito ambao ungempumzisha kwa saa ishirini na nne wakati dawa zikifanya kazi.

Baada ya kuhakikisha Nuru amelala kwa utulivu, ndipo Joram pia alipolala kando yake na usingizi mnono, usio na ndoto, kumchukua. Alizinduka saa moja usiku. Akafanya haraka kuoga, kisha kuvaa suti yake.

Baada ya hapo aliichukua bastola yake, bomu moja la mkono, kisu na silaha zake nyingine akazitokomeza katika mifuko yake ya siri. Alipojitazama katika kioo na kuridhika kuwa hata askari mdadisi kiasi gani asingemshuku kuwa anakwenda vitani badala ya kwenda kufanya matumizi, ndipo alipombusu Nuru, akamfunika vizuri na kisha kuondoka baada ya kuufunga mlango vyema nyuma yake.

Hakuwa na haraka. Alipita katika chumba cha maakuli ambako aliagiza ugali kwa kuku wa kuokwa. Wakati akisubiri chakula hicho alijipongeza kwa bia mbili za stella. Chakula chake kilipofika alikula kwa utulivu, huku akiteremsha kwa kopo la tatu la stella. Alipomaliza aliwasha sigara na kuivuta taratibu huku kopo la nne lilkikoza moshi. Saa yake ilipomwashiria kuwa imetimia nne kasorobo za usiku ndipo alipolipa bili yake na kuingia mitaani.

Kwa mwendo ule ule wa taratibu, alivuta hatua moja baada ya nyingine kuziendea ofisi za Kangaroo. Alijua fika kuwa watakuwepo na silaha zao mikononi. Hata hivyo, akiwa amedhamiria kuingia alikwishajiandaa kwa njia moja au nyingine ambayo ingemwezesha kuingia. Hivyo, hilo hakulitilia wasiwasi. Ambalo lilimtia wasiwasi na kumwongezea shahuku ya kufika aendako ni Adrian. Alikuwa na hakika kuwa Adrian, alivo kichwa maji, lazima pia angebuni kuingia katika jengo hilo. Na ni hilo lililomfanya awahi. Alitaka awe wa kwanza kufika katika jengo hilo ili amsubiri na kumpokea. Alijua fika kuwa mkutano wao wa ana kwa ana ulikuwa na maana moja tu, ya kumwacha mmoja hai, mwingine maiti. Joram alikuwa na uhakika kuwa huyo maiti asingekuwa yeye.

Wakati akikaribia ofisi hiyo, Joram aliichomoa tai yake nyeupe na kuisokomeza mfukoni. Kuondolewa kwa tai hiyo, kulimfanya abadilike ghafla na kuwa kama kivuli au sehemu ya kiza. Aliubadili pia mwendo wake na kuanza kunyata kwa uangalifu, toka ukuta hadi ukuta; kichaka hadi kichaka. Wapita njia waliomtazama kwa macho ya udadisi aliwapumbaza kwa kujifanya ama anajisaidia haja ndogo au anafunga kamba za viatu vyake, ama amelewa na hivyo, anakwenda bila mpangilio wowote.

Alipofika mbele ya Kangaroo, kama ivyotegemea, alimwona askari mmoja mwenye silaha na magwanda akiwa amesimama kuuegemea ukuta, bunduki yake kaishika mkono mmoja, wa pili ukiwa mfukoni. Joram alimtazama kwa makini. Akashangazwa na utulivu wa askari huyo. Alipotupa macho kutazama huko na huko hakumwona askari mwingine.

Akaitazama saa yake ambayo ilimuashiria saa nne na dakika kumi. Alihitaji kuwa katika jengo hilo mapema. Hivyo, alipoona askari huyo hatoki hapo aliposimama, aliamua kumfuata. Aliiwasha sigara yake na kuipachika mdomoni, akakohoa, kisha akaanza kumsogelea. Alitegemea kuambiwa simama au kupewa amri yoyote ile. Haikutoka. Joram alizidi kumsogelea hadi alipomfikia na kumsalimu. Hakuitikia.

“Hujambo, brother?” Joram alisalimu tena.

Bado hakuitikiwa, jambo ambalo aliona halikuwa la kawaida. Alimtazama askari huyo kwa makini zaidi na kubaini kuwa alikuwa hatingishiki, haoni wala hasikii. Alipojaribu kumtikisa aliporomoka na silaha yake na kuanguka sakafuni.

Ndio kwanza Joram akabaini kuwa alikuwa anaongea na maiti. Akainama na kumshika kifuani ambako alimkuta kapoa kitambo. Kiasi Joram alitahayari. Alitegemea ukatili. Lakini hakutegemea ukatili wa kiasi hicho. Kwa ujumla, aliondokea kuamini kuwa kipindi cha mauaji ya kinyama kilikuwa kimepita, wazo ambalo sasa alilijutia.

Hakuhitaji kuambiwa kuwa mauaji hayo yamefanywa na nani. Wala hakuiona haja ya kujiuliza kwanini yamefanyika. Adrian alikuwa amemtangulia. Akamwua askari huyo, bila shaka kwa hila, ili asiwe kipingamizi cha kumfanya ashindwe kuingia ndani. Hivyo, ama alikuwa ndani ama ametoka.

Wakati akiyafikiri hayo Joram Kiango tayari alikuwa ameusimamisha mzoga huo wa askari kama alivyoukuta na kuirejesha bunduki mkononi mwake na kuanza kunyata akielekea mlangoni. Kando ya mlango huo, kwenye kibanda kidogo cha mapokezi, Joram aliikuta maiti ya askari wa pili. Huyu alikuwa ameketishwa juu ya kiti na kuiinamia meza, bunduki mkononi. Joram hakuitaji kumgusa kujua kuwa amekufa.

Aidha, hakuwa na haja ya kumshika shingo ili kubaini kuwa lilikuwa limevunjwa kwa pigo kali la judo. Alichofanya ni kukimbilia ndani, ambako aliukuta mlango ukiwa wazi, kama unaomsubiri. Harakaharaka bastola yake ikiwa mkononi, alinyata toka chumba hadi chumba. Akitumia tochi yake yenye ukubwa wa kalamu, alichungulia kila kona, kila uvungu wa meza, kila kabati, kila uvungu wa friji, bila mafanikio. Kila dalili ilimwonyesha kuwa Adrian amekuja na kuondoka.

Joram akaziacha ofisi za kawaida na kuzifuata zile za siri ambako waliwazika hai Paul na Philip. Huko pia Adrian alikuwa amemtangulia na alichokifanya hakikustahili kutazamwa. Mateka hao wawili ambao yeye na Kombora waliamua kuwafungia hai, Adrian alikuwa amewachoropoa toka shimoni humo na kuwachinja kama kuku, mmoja baada ya mwingine. Miili yao, aliitupa juu ya sakafu na kuwafanya walale wakiwa wamekumbatiana ndani ya dimbwi la damu yao wenyewe.

Joram alikiacha chumba hicho na kukimbilia kile ambacho kilihifadhi mamilioni ya pesa za kigeni. Alisogeza sefu ambalo liliwekwa kwa geresha na kulifikia lile la siri ambalo liliunganishwa na ukuta kwa hila. Alipojaribu kulifungua alishangaa kulikuta likiwa wazi. Pale ambapo palikuwa na vitita vya noti za ndani na nje sasa hapakuwa na kitu chochote. Hapana, palikuwa na kitu fulani, kitu kidogo, cheusi. Joram aliisogeza tochi yake na kutazama. Kama macho yake yalichelewa kumwashiria yanatazama nini, pua yake haikuchelea kufanya hivyo. Kitu hicho kilikuwa kinyesi. Baada ya kuchukua pesa hizo, kwa kuonyesha dharau, Adrian, akijua mtu yeyote angetamani kuzipata pesa hizo ndipo alipoamua kufanya hivyo.

Mara ya kwanza maishani mwake hasira hizo zilimfanya atetemeke mwili mzima. “Mshenzi” aliropoka kwa mara ya pili. “Haendi popote! Kamwe haondoki nje ya nchi hii akiwa hai,” alinguruma akigeuka kuanza kutoka nje ya chumba hicho taratibu kwa mwendo wa sismba aliyejeruhiwa mwili na roho.




MWISHO MSIJE MKANIAMBIA TENA NIENDELEE. NIKIENDELEA NITAKUA NAWADANGANYA SASA.....
natanguliza shukurani za dhati wakati nasubiri nyingine,asante sana
 
14

Mamia ya watu walioduwaa nje ya jengo hilo walishangaa kuona mlango ukifunguka taratibu na kumruhusu kijana mmoja mkakamavu na msichana kuanza kuondoka. Mvulana akiwa katika suti yake nyeusi, isipokuwa kwa vumbi kidogo, katika mavazi yake alionekana mtanashati kama ambaye anatoka katika jumba la starehe kinyume na watu waliokuwa nje walivyoamini. Lakini msichana alikuwa taabani, kachakaa mwili na mavazi kama aliyetoroka kuzimu. Alitembea kwa kujikongoja huku akipata msaada wa mkono wa mvulana uliomshika kiuno.

Sura za vijana hawa zilikuwa maarufu nchini kama zilivyomashuhuri kote duniani. Haukupita muda kabla ya watu waliokuwa hapo nje hawajaanza kunong’ona, “Ni joram Kiango!”

“Ndiyo. Na Nuru”

Polisi ambao walianza kuziweka silaha zao sawa kuwaelekea, walipowafahamu walizirudisha makwapani na kusimama kwa utulivu. Mmoja wao saluti ilimtoka, na Joram akapokea kwa kutabasamu kidogo. Kabla askari hao hawajajua wafanye nini na Joram, bosi wao, Inspekta Kombora, alitokea, na askari wote wakamkimbilia.

Yeye pia alikuwa taabani kama Nuru. Nguo zake zilichakaa na kuchafuka, mwili wake ulijaa marejaha, macho yake yalilegea kana kwamba alikuwa amekesha akinywa pombe kali. Akiushikilia ukuta alitembea taratibu na kuzipuuza saluti ambazo zilielekewa kwake.

“Pole sana mzee.”

“Nipelekeni ofisini… hapana nyumbani,” alisema kwa udhaifu

“Tukupeleke hospitali afande?”

“Nimesema nyumbani.”

Dereva mmoja alimsogezea gari. Kabla hajalipanda alitoa maelekezo kwa askari hao, akiwataka wahakikishe jengo hilo linalindwa kwa makini usiku na mchana hadi atakapokuwa tayari kukamilisha suala hilo ambalo alidai limekwisha!

Joram alitumia fursa hiyo kuutoroka umati wa watu. Alimfuata mtu mmoja aliyekuwa ameketi ndani ya gari lake, Toyota Saloon, na kumwomba lifti. Mtu huyo, kwa furaha, aliwafungulia milango na kuwakaribisha ndani. Joram akamwingiza mgonjwa wake kisha yeye akaingia na kumtaka awapeleke hotel ya Mawenzi.

“Nina bahati sana leo” msamaria alisema.

“Bahati gani?” Joram alimwuliza

“Kukutana ana kwa ana na wewe. Ni jambo ambalo sikulitegemea kabisa. Nimekuwa nikikusoma katika vitabu na magazeti tu. Hivi huko ndani kulikuwa na nini?”

“Ngoja gazeti la kesho utaelewa, ni hadithi ndefu sana”

“Hivi haya wanayoyaandika juu yako ni ya kweli? Sio kwamba waandishi wanatia chumvi sana ili magazeti na vitabu vyao vinunuliwe?”

Joram, akiwa hana hamu na magazeti, alijikuta akimwambia, “Hayo unayoyasikia yazidishe mara nne, utoe nane na kuongeza mbili ndipo utapata ukweli wenyewe”

Akiwa amechanganyikiwa, dereva huyo aliendesha gari bila maongezi zaidi mpaka alipowafikisha mbele ya hoteli yao.

Joram alimshukuru kwa ukarimu wake, akamzoa Nuru ambaye alianza kulala na kumwingiza hotelini. Watu waliokuwa mapokezi walitokwa na macho ya mshangao, hasa kutokana na hali ya Nuru, lakini Joram hakuwapa nafasi ya maswali. Badala yake alichukua ufunguo wake na kwenda chumbani kwake, akiwa bado amemshikilia Nuru kiuno. Hakuhitaji funguo huo, chumba kilikuwa wazi, kinyume na alivyokiacha. Jicho lake moja chumbani humo lilimfanya afahamu kuwa alikuwa ametembelewa. Ingawa karibu kila kitu kilikuwa kama alivyokiacha, lakini bado dalili zilimwonyesha kuwa kila kitu kilikuwa kimekaguliwa na kuvurugwa kwa uangalifu mkubwa.

Joram akamtua Nuru kwenye kitanda na kumlaza taratibu. Alipovuta mto ili amweke vizuri, aligutuka kuona mto huo ulikuwa umetumiwa kuficha maiti ya paka mnene, aliyenawiri, ambayo yalilazwa kitandani hapo. Kando ya mzoga huo, Joram aliona maandishi mekundu yalioandikwa juu ya shuka kwa lugha ya kiingereza ‘you’re next’ yakimaanisha kuwa ni yeye Joram atakayefuatia.

Alipomgeukia Nuru kuona kama naye pia alikuwa ameuona mzoga huo, alifurahi kumwona tayari kalala kwa utulivu, akikoroma taratibu. Akainama na kumchunguza paka huyo kwa makini zaidi. Akabaini kuwa aliuawa kwa kunyongwa kwa kwa mkono muda mfupi uliopita kwani alikuwa bado ana joto. Lakini Joram alipozidi kumchunguza aligundua kuwa bado alikuwa akipumua taratibu. Badala ya kumtupa dirishani kama alivyokusudia, Joram alimwinua polepole na kumweka nje ya chumba, upande wa mapumziko.

Baada ya kuduwaa kwa mara ya pili, Joram alimnusisha paka huyo dawa ya kulevya, jambo ambalo lilimfanya mnyama huyo mdogo apige chafya na dakika chache baadaye ainuke na kujikongoja taratibu kuelekea nje.

Joram hakuhitaji kuambiwa paka huyo ameletwa na nani chumbani humo. Adrian!... Ni yeye pia aliyekipekua chumba chake ambamo dalili zilimwonyesha Joram kuwa alikaa muda mrefu akimsubiri.

Kitendo cha kupata uhai kwa paka huyo, ambaye Joram alijua fika aliwekwa hapa kwa njia ya kumtisha huku adui huyo akiamini kuwa ni mzoga, kilimdhihirishia Joram kuwa mapambano bado yalikuwa yanaendelea. Hata hivyo, ilimtia matumaini makubwa ya kuibuka mshindi akizingatia uhai wa paka huyo ulivyorejea baada ya muuaji kuamini kuwa ametimiza kazi yake.

Akifahamu fika jinsi roho ya Adrian ilivyolemaa kwa chuki na fikra zake zilivyomezwa na kiasi Joram alijua kuwa alikuwa na wajibu mkubwa kumteketeza kiumbe huyo kabla hajafanya madhara zaidi. “Ni yeye, au mimi!” aliwaza akiondoka kurudi kitandani ambako Nuru alilala kwa utulivu.

Joram alimtazama msichana huyu alivyolala na mavazi yake yote. Aliitazama sura yake nzuri na umbo lake la kuvutia lilivyopendeza katika mavazi hayo yaliyochakaa na kuchafuka.

***

Pamoja na hasira zake, Adrian alichukua wasaa wa kujilaumu kimoyomoyo. Kwa kiasi kikubwa alihisi alishiriki kuwaangusha waajiri wake ambao alikwisha amua kuwa wana aina fulani ya kichaa. Kitendo chake cha kupenya toka katika eneo hilo la ofisi hadi katika hoteli ya Joram Kiango ili akammalize hukohuko, badala ya kumsubiri, kama wenyeji wake walivyomwelekeza, kwa kila hali kimechangia kumfanya awe hai hadi sasa na awaokoe mateka wake.

Jambo hili, limezifanya jitihada zake zote, za kupenya katika uchochoro wa hoteli hiyo, hadi nyuma ambako alitumia kamba kupanda hadi juu na kisha kwa kutumia tundu la moshi kujipenyeza hadi ndani ziwe za bure.

Chumbani mwa Joram, Adrian alipekua kila sehemu bila kujua anatafuta nini. Hakupata chochote. Hata hivyo, ili asiondoke bila zawadi yoyote, ndipo alipochukua mkufu wa dhahabu uliokuwa kama umesahauliwa katika begi mojawapo.

Adrian alijua ingemchukua muda Joram kugundua upotevu huo, lakini kwake ingekuwa fahari kubaki na kumbukumbu ya kumfuta duniani.

Ni wakati alipokuwa akitoka nje ya chumba hicho alipokutana na paka yule ambaye alipita akinusa huko na huko. Adrian hakuchelewa kumdaka na kumminya koo kwa vidole viwili hadi paka alipokata roho, kisha akamlaza juu ya kitanda cha Joram kama salamu ambazo alijua zitamsisimua zaidi ya kupotea kwa mkufu mdogo wa dhahabu.

Adrian akaamua kurudi kwa waajiri wake. Akiwa nje ya jengo hilo la Paul na Philip, alimwona inspekta Kombora, pamoja na uchovu wake mwingi, akitoa maelekezo juu ya ulinzi wa jengo hilo. Akiwa na hakika kuwa mambo yalikuwa yamewaendea kombo waajiri wake, Adrian alitazama kwa makini jengo hilo huku rohoni akijua wazi kuwa japo jeshi zima la polisi liletwe kulinda usiku huo lazima angeingia katika jengo hilo na kuchukua kila kilicho chake.

Hakukuwa na mtu yeyote, duniani na mbinguni, ambaye angemzuia.

Kwa miji yote mikubwa ilivyo kote duniani, jiji la Dar es Salaam pia halijui usiku. Mara tu jua linapozama na kiza kutanda, wako baadhiya watu ambao huona kana kwamba ndio kwanza kumepambazuka. Hivyo, wakati wenzao wakijiandaa kulala wenzao hujiandaa kutoka tayari kwa shughuli zao mbalimbali, baadhi wakiwa wafanyakazi wa zamu za usiku, baadhi watumiaji tu wa pesa zao, hali wengine wakiwa waviziaji tu, wezi na Malaya wa bandarini.

Usiku wa leo Joram alikuwa mmoja wao. aliporejea toka muhimbili akiwa na aina mbalimbali za dawa ambazo alielekezwa jinsi ya kumpa Nuru, alimwamsha na kumshurutisha kuzinywa.

Kama alivyokuwa ameambiwa na daktari yule, mara tu baada ya kuzinywa, Nuru alichukuliwa tena na usingizi, usingizi mzito ambao ungempumzisha kwa saa ishirini na nne wakati dawa zikifanya kazi.

Baada ya kuhakikisha Nuru amelala kwa utulivu, ndipo Joram pia alipolala kando yake na usingizi mnono, usio na ndoto, kumchukua. Alizinduka saa moja usiku. Akafanya haraka kuoga, kisha kuvaa suti yake.

Baada ya hapo aliichukua bastola yake, bomu moja la mkono, kisu na silaha zake nyingine akazitokomeza katika mifuko yake ya siri. Alipojitazama katika kioo na kuridhika kuwa hata askari mdadisi kiasi gani asingemshuku kuwa anakwenda vitani badala ya kwenda kufanya matumizi, ndipo alipombusu Nuru, akamfunika vizuri na kisha kuondoka baada ya kuufunga mlango vyema nyuma yake.

Hakuwa na haraka. Alipita katika chumba cha maakuli ambako aliagiza ugali kwa kuku wa kuokwa. Wakati akisubiri chakula hicho alijipongeza kwa bia mbili za stella. Chakula chake kilipofika alikula kwa utulivu, huku akiteremsha kwa kopo la tatu la stella. Alipomaliza aliwasha sigara na kuivuta taratibu huku kopo la nne lilkikoza moshi. Saa yake ilipomwashiria kuwa imetimia nne kasorobo za usiku ndipo alipolipa bili yake na kuingia mitaani.

Kwa mwendo ule ule wa taratibu, alivuta hatua moja baada ya nyingine kuziendea ofisi za Kangaroo. Alijua fika kuwa watakuwepo na silaha zao mikononi. Hata hivyo, akiwa amedhamiria kuingia alikwishajiandaa kwa njia moja au nyingine ambayo ingemwezesha kuingia. Hivyo, hilo hakulitilia wasiwasi. Ambalo lilimtia wasiwasi na kumwongezea shahuku ya kufika aendako ni Adrian. Alikuwa na hakika kuwa Adrian, alivo kichwa maji, lazima pia angebuni kuingia katika jengo hilo. Na ni hilo lililomfanya awahi. Alitaka awe wa kwanza kufika katika jengo hilo ili amsubiri na kumpokea. Alijua fika kuwa mkutano wao wa ana kwa ana ulikuwa na maana moja tu, ya kumwacha mmoja hai, mwingine maiti. Joram alikuwa na uhakika kuwa huyo maiti asingekuwa yeye.

Wakati akikaribia ofisi hiyo, Joram aliichomoa tai yake nyeupe na kuisokomeza mfukoni. Kuondolewa kwa tai hiyo, kulimfanya abadilike ghafla na kuwa kama kivuli au sehemu ya kiza. Aliubadili pia mwendo wake na kuanza kunyata kwa uangalifu, toka ukuta hadi ukuta; kichaka hadi kichaka. Wapita njia waliomtazama kwa macho ya udadisi aliwapumbaza kwa kujifanya ama anajisaidia haja ndogo au anafunga kamba za viatu vyake, ama amelewa na hivyo, anakwenda bila mpangilio wowote.

Alipofika mbele ya Kangaroo, kama ivyotegemea, alimwona askari mmoja mwenye silaha na magwanda akiwa amesimama kuuegemea ukuta, bunduki yake kaishika mkono mmoja, wa pili ukiwa mfukoni. Joram alimtazama kwa makini. Akashangazwa na utulivu wa askari huyo. Alipotupa macho kutazama huko na huko hakumwona askari mwingine.

Akaitazama saa yake ambayo ilimuashiria saa nne na dakika kumi. Alihitaji kuwa katika jengo hilo mapema. Hivyo, alipoona askari huyo hatoki hapo aliposimama, aliamua kumfuata. Aliiwasha sigara yake na kuipachika mdomoni, akakohoa, kisha akaanza kumsogelea. Alitegemea kuambiwa simama au kupewa amri yoyote ile. Haikutoka. Joram alizidi kumsogelea hadi alipomfikia na kumsalimu. Hakuitikia.

“Hujambo, brother?” Joram alisalimu tena.

Bado hakuitikiwa, jambo ambalo aliona halikuwa la kawaida. Alimtazama askari huyo kwa makini zaidi na kubaini kuwa alikuwa hatingishiki, haoni wala hasikii. Alipojaribu kumtikisa aliporomoka na silaha yake na kuanguka sakafuni.

Ndio kwanza Joram akabaini kuwa alikuwa anaongea na maiti. Akainama na kumshika kifuani ambako alimkuta kapoa kitambo. Kiasi Joram alitahayari. Alitegemea ukatili. Lakini hakutegemea ukatili wa kiasi hicho. Kwa ujumla, aliondokea kuamini kuwa kipindi cha mauaji ya kinyama kilikuwa kimepita, wazo ambalo sasa alilijutia.

Hakuhitaji kuambiwa kuwa mauaji hayo yamefanywa na nani. Wala hakuiona haja ya kujiuliza kwanini yamefanyika. Adrian alikuwa amemtangulia. Akamwua askari huyo, bila shaka kwa hila, ili asiwe kipingamizi cha kumfanya ashindwe kuingia ndani. Hivyo, ama alikuwa ndani ama ametoka.

Wakati akiyafikiri hayo Joram Kiango tayari alikuwa ameusimamisha mzoga huo wa askari kama alivyoukuta na kuirejesha bunduki mkononi mwake na kuanza kunyata akielekea mlangoni. Kando ya mlango huo, kwenye kibanda kidogo cha mapokezi, Joram aliikuta maiti ya askari wa pili. Huyu alikuwa ameketishwa juu ya kiti na kuiinamia meza, bunduki mkononi. Joram hakuitaji kumgusa kujua kuwa amekufa.

Aidha, hakuwa na haja ya kumshika shingo ili kubaini kuwa lilikuwa limevunjwa kwa pigo kali la judo. Alichofanya ni kukimbilia ndani, ambako aliukuta mlango ukiwa wazi, kama unaomsubiri. Harakaharaka bastola yake ikiwa mkononi, alinyata toka chumba hadi chumba. Akitumia tochi yake yenye ukubwa wa kalamu, alichungulia kila kona, kila uvungu wa meza, kila kabati, kila uvungu wa friji, bila mafanikio. Kila dalili ilimwonyesha kuwa Adrian amekuja na kuondoka.

Joram akaziacha ofisi za kawaida na kuzifuata zile za siri ambako waliwazika hai Paul na Philip. Huko pia Adrian alikuwa amemtangulia na alichokifanya hakikustahili kutazamwa. Mateka hao wawili ambao yeye na Kombora waliamua kuwafungia hai, Adrian alikuwa amewachoropoa toka shimoni humo na kuwachinja kama kuku, mmoja baada ya mwingine. Miili yao, aliitupa juu ya sakafu na kuwafanya walale wakiwa wamekumbatiana ndani ya dimbwi la damu yao wenyewe.

Joram alikiacha chumba hicho na kukimbilia kile ambacho kilihifadhi mamilioni ya pesa za kigeni. Alisogeza sefu ambalo liliwekwa kwa geresha na kulifikia lile la siri ambalo liliunganishwa na ukuta kwa hila. Alipojaribu kulifungua alishangaa kulikuta likiwa wazi. Pale ambapo palikuwa na vitita vya noti za ndani na nje sasa hapakuwa na kitu chochote. Hapana, palikuwa na kitu fulani, kitu kidogo, cheusi. Joram aliisogeza tochi yake na kutazama. Kama macho yake yalichelewa kumwashiria yanatazama nini, pua yake haikuchelea kufanya hivyo. Kitu hicho kilikuwa kinyesi. Baada ya kuchukua pesa hizo, kwa kuonyesha dharau, Adrian, akijua mtu yeyote angetamani kuzipata pesa hizo ndipo alipoamua kufanya hivyo.

Mara ya kwanza maishani mwake hasira hizo zilimfanya atetemeke mwili mzima. “Mshenzi” aliropoka kwa mara ya pili. “Haendi popote! Kamwe haondoki nje ya nchi hii akiwa hai,” alinguruma akigeuka kuanza kutoka nje ya chumba hicho taratibu kwa mwendo wa sismba aliyejeruhiwa mwili na roho.




MWISHO MSIJE MKANIAMBIA TENA NIENDELEE. NIKIENDELEA NITAKUA NAWADANGANYA SASA.....
natanguliza shukurani za dhati wakati nasubiri nyingine,asante sana
 
Back
Top Bottom