Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 17,796
- 32,150
-BUSU (KISS)-
(Kutoka Ikulu hadi Kumpenda Kiziwi)
Episode one
Hey! Naitwa Jack, ni mtoto wa kitajiri na nina miaka 24. Nimekulia katika familia ya Baba, Mama na mtoto mmoja ambaye ni Mimi. Baba yangu anaitwa Mr Charles kwahiyo moja kwa moja Mama yangu ataitwa Mrs Charles. Binafsi nimekulia katika familia ambayo haina dhiki ya aina yoyote. Baba na Mama yangu ni wafanyakazi wa ofisi ya Rais hivyo kwetu kula, kulala na kufanya matanuzi mengine ni jambo la kawaida sana. Tunatanua utadhani sisi ni watoto wa Rais.
Sio kwamba najigamba lakini ndio maisha ambayo nimelelewa, tangu nimekuwa sikuwahi kuona mwanamke ambaye anatembea peku, hajapaka mekapu, anayenuka vumba la kuni wala amevaa nguo za kuchanika. Mara zote nilikuwa ni mtu wa ndani nikilindwa na ulinzi kisha nikitoka labda nimeenda kwa marafiki zangu ambao wengi ni watoto wa mawaziri pamoja na wabunge. Zaidi ya hapo ningeenda chuo ambapo nilisoma Kampala, Uganda.
Kukua katika malezi haya kidogo kulinifanya niwe ni mtu mwenye dharau, kejeli na sijali mtu mwinhine. Pia nachukulia kila mtu ambaye yupo chini yangu hawezi kunifanya lolote lile. Hii ndio amri ya kwanza ambayo nilifundishwa na Mama pamoja na Baba yangu. Nikaimeza amri hii na kuifanyia kazi lakini nilikuja kuivunja siku moja ambapo nilikutana na msichana mrembo, mwenye kuvutia.
Nakumbuka ilikuwa Alhamis katika mkesha wa Sikukuu ya ya uhuru ambapo kulikuwa na shughuli za kiserikali kwahiyo viongozi mbalimbali na watu wenye hadhi zao walikutana katika uwanja na shughuli zilifanyika hapo. Katika eneo hili ndipo kulikuwa na binti mzuri, mwenye macho ya kuvutia yenye kubeba haiba, msichana ambaye kwa kumtazama kwa mara ya kwanza hakuzidi miaka 20.
Mrembo huyu alikuwa anapiga mbira wakati wenzake wakiendelea kuimba nyimbo mbalimbali ili kuwabururidisha wageni ambao wamefika eneo lile. Upigaji wake wa mbira ulikuwa tofauti na ule ambao nimewahi kuusikia kwa watu wengine. Nilijikuta namtazama sana, nilimtazama kiasi kwamba hadi Baba ambaye alikuwa pembeni yangu aliniuliza.
“Unatazama nini”🤔
“Nothing daddy”😒 nilimkatalia kwa makusudi sababu nilikuwa namjua Baba yangu, tabia ya kutopenda masikini lilikuwa ni jambo ambalo amerithi enzi na enzi kutoka kwenye koo yake. Kwahiyo pale napo nilifanya makusudi kabisa.
“Hakuna kitu wakati nakuona unamtazama yule masikini, unataka akurithishe dhiki si ndio?🙄
“Mmmh! Nimeona anapiga vizuri”🤗
“Ok, achana naye ni masikini. Huwa wanachukuliwa na kuburudisha kwa siku kama hizi”
“Sawa daddy” Niliamua kumaliza mada maana sikupenda marumbano lakini hii haikunifanya kuendelea kumtaza yule binti.
Kiukweli nilitokea kumpenda, nilitamani awe katika maisha yangu lakini namna ya kumuingia, namna ya kumfanya awe karibu na mimi ndio ulikuwa mziki. Basi, shughuli ilimalizika. Nami nilijaribu kumtafuta yule binti lakini sikuweza kumpata.
Nilichanganikiwa mno, nikawaza wapi ambapo ningeweza kumpata lakini ukweli ni kwamba kwa wakati ule ilikuwa ni ngumu sana kumpata yule binti? Siku iliyofuata nilisumbuka maeneo tofauti tofauti lakini sikuweza kumpata.
Nilipatwa na hasira😠kwanini nimeshindwa kumpata sasa? Basi nilirudi Ikulu ambako ndiko kulikuwa na makazi yetu. Jioni Rais aliniita maana alikuwa anapenda sana kuzungumza na mimi, nilienda kumsikiliza.
“Judy anaweza kurudi hapa akitokea marekani kimasomo” 🤗
“Oh! Nahisi itapendeza maana tutakuwa wawili”💏
“Kweli kabisa au ushapata mpenzi maana kila siku anakuulizia?”🤔
“Hapana, mwambie nipo bado kama ikiwezekana basi tutaoana”😎
“Sawa” Niliamua kumkubalia Rais kwakuwa kwanza alikuwa ni kiongozi wangu lakini ukweli ni kwamba huyo mtoto wake ambaye aliitwa Judith sikuwa nampenda hata chembe. Kulikuwa na ushawishi kutoka kwa Baba pamoja na Mama ambao muda wote hawakuacha kumpigia debe na kuamini kwamba kama tukiwa wawili basi tutapendezana na huenda nami ningekaribishwa vizuri Ikulu kama Rais huko mbeleni.
(Kutoka Ikulu hadi Kumpenda Kiziwi)
Episode one
Hey! Naitwa Jack, ni mtoto wa kitajiri na nina miaka 24. Nimekulia katika familia ya Baba, Mama na mtoto mmoja ambaye ni Mimi. Baba yangu anaitwa Mr Charles kwahiyo moja kwa moja Mama yangu ataitwa Mrs Charles. Binafsi nimekulia katika familia ambayo haina dhiki ya aina yoyote. Baba na Mama yangu ni wafanyakazi wa ofisi ya Rais hivyo kwetu kula, kulala na kufanya matanuzi mengine ni jambo la kawaida sana. Tunatanua utadhani sisi ni watoto wa Rais.
Sio kwamba najigamba lakini ndio maisha ambayo nimelelewa, tangu nimekuwa sikuwahi kuona mwanamke ambaye anatembea peku, hajapaka mekapu, anayenuka vumba la kuni wala amevaa nguo za kuchanika. Mara zote nilikuwa ni mtu wa ndani nikilindwa na ulinzi kisha nikitoka labda nimeenda kwa marafiki zangu ambao wengi ni watoto wa mawaziri pamoja na wabunge. Zaidi ya hapo ningeenda chuo ambapo nilisoma Kampala, Uganda.
Kukua katika malezi haya kidogo kulinifanya niwe ni mtu mwenye dharau, kejeli na sijali mtu mwinhine. Pia nachukulia kila mtu ambaye yupo chini yangu hawezi kunifanya lolote lile. Hii ndio amri ya kwanza ambayo nilifundishwa na Mama pamoja na Baba yangu. Nikaimeza amri hii na kuifanyia kazi lakini nilikuja kuivunja siku moja ambapo nilikutana na msichana mrembo, mwenye kuvutia.
Nakumbuka ilikuwa Alhamis katika mkesha wa Sikukuu ya ya uhuru ambapo kulikuwa na shughuli za kiserikali kwahiyo viongozi mbalimbali na watu wenye hadhi zao walikutana katika uwanja na shughuli zilifanyika hapo. Katika eneo hili ndipo kulikuwa na binti mzuri, mwenye macho ya kuvutia yenye kubeba haiba, msichana ambaye kwa kumtazama kwa mara ya kwanza hakuzidi miaka 20.
Mrembo huyu alikuwa anapiga mbira wakati wenzake wakiendelea kuimba nyimbo mbalimbali ili kuwabururidisha wageni ambao wamefika eneo lile. Upigaji wake wa mbira ulikuwa tofauti na ule ambao nimewahi kuusikia kwa watu wengine. Nilijikuta namtazama sana, nilimtazama kiasi kwamba hadi Baba ambaye alikuwa pembeni yangu aliniuliza.
“Unatazama nini”🤔
“Nothing daddy”😒 nilimkatalia kwa makusudi sababu nilikuwa namjua Baba yangu, tabia ya kutopenda masikini lilikuwa ni jambo ambalo amerithi enzi na enzi kutoka kwenye koo yake. Kwahiyo pale napo nilifanya makusudi kabisa.
“Hakuna kitu wakati nakuona unamtazama yule masikini, unataka akurithishe dhiki si ndio?🙄
“Mmmh! Nimeona anapiga vizuri”🤗
“Ok, achana naye ni masikini. Huwa wanachukuliwa na kuburudisha kwa siku kama hizi”
“Sawa daddy” Niliamua kumaliza mada maana sikupenda marumbano lakini hii haikunifanya kuendelea kumtaza yule binti.
Kiukweli nilitokea kumpenda, nilitamani awe katika maisha yangu lakini namna ya kumuingia, namna ya kumfanya awe karibu na mimi ndio ulikuwa mziki. Basi, shughuli ilimalizika. Nami nilijaribu kumtafuta yule binti lakini sikuweza kumpata.
Nilichanganikiwa mno, nikawaza wapi ambapo ningeweza kumpata lakini ukweli ni kwamba kwa wakati ule ilikuwa ni ngumu sana kumpata yule binti? Siku iliyofuata nilisumbuka maeneo tofauti tofauti lakini sikuweza kumpata.
Nilipatwa na hasira😠kwanini nimeshindwa kumpata sasa? Basi nilirudi Ikulu ambako ndiko kulikuwa na makazi yetu. Jioni Rais aliniita maana alikuwa anapenda sana kuzungumza na mimi, nilienda kumsikiliza.
“Judy anaweza kurudi hapa akitokea marekani kimasomo” 🤗
“Oh! Nahisi itapendeza maana tutakuwa wawili”💏
“Kweli kabisa au ushapata mpenzi maana kila siku anakuulizia?”🤔
“Hapana, mwambie nipo bado kama ikiwezekana basi tutaoana”😎
“Sawa” Niliamua kumkubalia Rais kwakuwa kwanza alikuwa ni kiongozi wangu lakini ukweli ni kwamba huyo mtoto wake ambaye aliitwa Judith sikuwa nampenda hata chembe. Kulikuwa na ushawishi kutoka kwa Baba pamoja na Mama ambao muda wote hawakuacha kumpigia debe na kuamini kwamba kama tukiwa wawili basi tutapendezana na huenda nami ningekaribishwa vizuri Ikulu kama Rais huko mbeleni.