Idimi
JF-Expert Member
- Mar 18, 2007
- 14,970
- 10,462
Wana JF Naomba kama kuna anayefahamu gharama za kuchimba kisima kwa Dar
anipe picha kamili,ikiwa nikuanzia kupima mkondo maji,Site ni Bunju karibu na mpiji
natanguliza shukrani.
Lady,
Gharama zinatofautiana kati ya kampuni na kampuni, lakini kati ya eneo na eneo kutegemeana na umbali wa maji chini ya ardhi. Kwa maeneo ya Kitunda, let say kuanzia Banana hadi ndani ndani kwenda Msongola, maji yapo kati ya meta 60 hadi 150 chini ya ardhi na uchimbaji wake unaweza kukugharimu kuanzia milioni 3 na kuendelea. Hiyo milioni 3 ni gharama za uchimbaji na mabomba ya kuleta maji juu, gharama za pampu, tangi na mabomba ya kusambaza maji ni nje ya hiyo m3. Normally kazi wanaimaliza ndani ya saa 24, kama kila kifaa kimeandaliwa
Kwanza kabisa nawashukuru wote kwa mchango wenu.Mwenzetu wewe uliyechimbiwa na wajasilimali
ullichimbiwa maeneo gani? je unaweza kutuunganisha na hao wajasilimali ?tutawapataje?
Kwa upande wangu, hizo gharama nilizoandika hapo juu ni kisima ambacho kimechimbwa kwa ndugu yangu, Kitunda, mwezi Desemba mwishoni, 2011. Mhusika anaweza kukupa namba za wachimbaji, anapatikana kwa 0764 518 851
Wadau kuna yeyote ambaye amechimba kisima na hao jamaa wa Drilling and Dam Construction Agency (DDCA) wa ubungo? Naomba atupe tathmini yake kama wanafaa (kwa kufanya survey na kisha kuchimba). Watu wamezungumzia diameter ya kisima, kisima kikubwa kabisa (kulingana na mabomba yaliyopo sokoni) ni kipi? Mfano kama nahitaji kisima kwa ajili ya biashara (kama nahitaji maji mengi sana) nahitaji kuchimba kisima cha diameter kiasi gani?
Hawa jamaa wanaaminika, kwa sababu ni taasisi ya serikali. Wana takwimu za kutosha za maji kuhusu maeneo mbalimbali ya Dar, kwa hiyo kwao inakuwa rahisi sana kukujulisha gharama za uchimbaji kwa eneo husika ndani ya muda mfupi. Niliwakuta mahali wanachimba, around mwaka 2009 na nilihojiana nao sana. Wao walianiambi kwamba wanafuata procedure zote za uchimbaji kisima, kabla hawajachimba, i.e. wanafanya survey ya eneo, wanalinganisha na taarifa zilizo ktk ramani zao. Wanachukua sample ya maji wakishachimba kisima, kabla hujaanza kutumia, wanapeleka maabara kwa utafiti wa usalama, kisha wanakuruhusu kutumia iwapo yako poa. Ni lengthy procedure ambayo wengi hatupendi, ila ndo ya kuaminika zaidi.
La kwangu la lita 4000 nimenunua 600,000/- mwezi Januari mwaka huujamani me napenda kufahamu na bei ya matank kuanzia lita 1000 na kuendelea????????