Nyoka mwenye makengeza
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 870
- 770
Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha, wananchi kijiji cha misufini wilaya ya kibaha wamezuiwa na RUWASA kutumia maji ya kisima walichochimba kwa nguvu zao wenyewe kisa RUWASA kutaka kuingiza kisima hicho kwenye mradi wa maji vijijini.
Kisima hicho ambacho kilishaanza kuwanufaisha wanakijiji hao kwa zaidi ya miezi 6 kilikuwa pia kinahudumia wanafunzi wa shule ya msingi misufini pamoja na zahanati mpya iliyoanza kazi mwishoni mwa mwaka jana.
Kwa sasa kisima hicho kimefungwa zaidi ya miezi miwili na hatma ya lini kitawanufaisha wanakijini ipo chini ya maamuzi binafsi ya RUWASA japokuwa hawajahusika kutoa ata senti moja kugharamikia uchimbaji wa kisima hicho. Jambo kama hili utaliona Tanzania tuu .
Wakati mama Samia anahangaika kupambana wanachi wapate huduma, kuna viongozi wanakwamisha makusudi maendeleo.
@dawasco
Wizara Maendeleo ya Jamii
======
UPDATES: 23 Februari 2024
=======
Moderator: Baada ya Jamiiforums kufuatilia, tumegundua haya Malalamiko SI SAHIHI. Hali haipo Kama Mleta mada alivyo yasema.
Madai ya "Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha, wananchi kijiji cha misufini wilaya ya kibaha wamezuiwa na RUWASA kutumia maji ya kisima walichochimba kwa nguvu zao wenyewe kisa RUWASA kutaka kuingiza kisima hicho kwenye mradi wa maji vijijini." Si ya kweli.
Andrea Cosmas Mwenyekiti wa Kijiji cha Msufini amekana Madai haya. Pia Wakala wa Maji Ruwasa Kibaha, Engineer Deborah amesema RUWASA haijawahi kuwasimamia Wanakiji hao zaidi ya kupeleka Mafundi kuwasiadia Miundombinu inapoleta tatizo tena bila malipo.
Ni kweli Maji hayapo, ila kutokuwepo Maji hakuhusiani na RUWASA bali kumetokana na Pampu ya kusukuma Maji kuharibika. Pia Maji yamekatika Wiki mbili sasa sio miezi Miwili.
Hicho Kisima cha Maji cha Msufini, kilijengwa na aliyekuwa Mbunge wa Kibaha Vijijini ndugu Hamoud Abuu Jumaa na Wafadhiri wake 2018-2019. Baada ya Ujenzi Kikakabidhiwa kwa Kijiji. Kuanzia Mwaka huo hadi 2022 mwishoni wananchi Walikuwa wanachota maji bure.
Tatizo likaja, Pampu ikiharibika wanakosa hela za kutengeneza, hivyo Kijiji kikaazimia wawe wanauza Maji ili hela isaidie pale Kunapotokea tatizo. Na Makubaliano yalikuwa ndoo moja iuzwe Shilingi mia moja(tsh 100)
Wakawaomba RUWASA wawafungie Mita ambapo Mwezi Desemba Mwaka jana 2023 Walifunga Mita nne katika Vituo Vinne(Walisaidiwa bure na RUWASA). Wakaanza kuuza maji na hela zikihifadhiwa na Mtendaji wa Kijiji Bi. Happiness.
Wiki moja iliyopita Pump iliharibika ambapo Mafundi kutoka RUWASA Jumatatu ya Wiki hii walienda kuangalia kwanini Pump inaharibika mara kwa mara? Wakakuta kisima kina Mchanga hivyo kinatakiwa kisafishwe.
Pump imeshatengenezwa Kinachosubiriwa na Mafundi kuja kusafisha hicho kisima kabla hawajaweka Pampu kwani wakiweka bila kusafisha, itaharibika tena.
Hivyo kinachosubiriwa ni kusafishwa kwa kisima. Wanaweza kuwaomba Ruwasa wawasaidie au Kampuni Binafsi.
Maji yapo Chini ya Kijiji wao ndo wanasimamia. Hawajawahi kuzuilowa kutumia hayo maji na RUWASA wala kuwatoza Gharama yoyote.
Serikali ya Kijiji bado wanatafuta wa kusafisha kisima kwa bei nafuu. Pia wana mpango wa Kiwashirikisha RUWASA pale watakapoona inafaa.
Kisima hicho ambacho kilishaanza kuwanufaisha wanakijiji hao kwa zaidi ya miezi 6 kilikuwa pia kinahudumia wanafunzi wa shule ya msingi misufini pamoja na zahanati mpya iliyoanza kazi mwishoni mwa mwaka jana.
Kwa sasa kisima hicho kimefungwa zaidi ya miezi miwili na hatma ya lini kitawanufaisha wanakijini ipo chini ya maamuzi binafsi ya RUWASA japokuwa hawajahusika kutoa ata senti moja kugharamikia uchimbaji wa kisima hicho. Jambo kama hili utaliona Tanzania tuu .
Wakati mama Samia anahangaika kupambana wanachi wapate huduma, kuna viongozi wanakwamisha makusudi maendeleo.
@dawasco
Wizara Maendeleo ya Jamii
======
UPDATES: 23 Februari 2024
=======
Moderator: Baada ya Jamiiforums kufuatilia, tumegundua haya Malalamiko SI SAHIHI. Hali haipo Kama Mleta mada alivyo yasema.
Madai ya "Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha, wananchi kijiji cha misufini wilaya ya kibaha wamezuiwa na RUWASA kutumia maji ya kisima walichochimba kwa nguvu zao wenyewe kisa RUWASA kutaka kuingiza kisima hicho kwenye mradi wa maji vijijini." Si ya kweli.
Andrea Cosmas Mwenyekiti wa Kijiji cha Msufini amekana Madai haya. Pia Wakala wa Maji Ruwasa Kibaha, Engineer Deborah amesema RUWASA haijawahi kuwasimamia Wanakiji hao zaidi ya kupeleka Mafundi kuwasiadia Miundombinu inapoleta tatizo tena bila malipo.
Ni kweli Maji hayapo, ila kutokuwepo Maji hakuhusiani na RUWASA bali kumetokana na Pampu ya kusukuma Maji kuharibika. Pia Maji yamekatika Wiki mbili sasa sio miezi Miwili.
Hicho Kisima cha Maji cha Msufini, kilijengwa na aliyekuwa Mbunge wa Kibaha Vijijini ndugu Hamoud Abuu Jumaa na Wafadhiri wake 2018-2019. Baada ya Ujenzi Kikakabidhiwa kwa Kijiji. Kuanzia Mwaka huo hadi 2022 mwishoni wananchi Walikuwa wanachota maji bure.
Tatizo likaja, Pampu ikiharibika wanakosa hela za kutengeneza, hivyo Kijiji kikaazimia wawe wanauza Maji ili hela isaidie pale Kunapotokea tatizo. Na Makubaliano yalikuwa ndoo moja iuzwe Shilingi mia moja(tsh 100)
Wakawaomba RUWASA wawafungie Mita ambapo Mwezi Desemba Mwaka jana 2023 Walifunga Mita nne katika Vituo Vinne(Walisaidiwa bure na RUWASA). Wakaanza kuuza maji na hela zikihifadhiwa na Mtendaji wa Kijiji Bi. Happiness.
Wiki moja iliyopita Pump iliharibika ambapo Mafundi kutoka RUWASA Jumatatu ya Wiki hii walienda kuangalia kwanini Pump inaharibika mara kwa mara? Wakakuta kisima kina Mchanga hivyo kinatakiwa kisafishwe.
Pump imeshatengenezwa Kinachosubiriwa na Mafundi kuja kusafisha hicho kisima kabla hawajaweka Pampu kwani wakiweka bila kusafisha, itaharibika tena.
Hivyo kinachosubiriwa ni kusafishwa kwa kisima. Wanaweza kuwaomba Ruwasa wawasaidie au Kampuni Binafsi.
Maji yapo Chini ya Kijiji wao ndo wanasimamia. Hawajawahi kuzuilowa kutumia hayo maji na RUWASA wala kuwatoza Gharama yoyote.
Serikali ya Kijiji bado wanatafuta wa kusafisha kisima kwa bei nafuu. Pia wana mpango wa Kiwashirikisha RUWASA pale watakapoona inafaa.