X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Filam Ya Vikaragosi (Cartoon) Ya Kiswahili Kwa jina la Manzese
Hii ni kazi ya Dr. Boniface Mhella, mjumbe wa Jumuiya ya Watanzania Roma, ambaye tayari amekamilisha filamu yake yenye mandhali ya kikatuni, inayokwenda kwa jina la "Manzese".
Dr. Boniface yupo kwenye harakati za kutafuta wasambazaji wanaoeleweka watakao fanya nae kazi.
Maelezo:
Filamu hii ni ya kutungwa na ni yenye kufurahisha, kusikitisha na vile vile kuleta matumaini. Inamuhusu mwanamume aitwae Kindunde. Kwa kifupi tu ni kwamba, Kindunde baada ya kuchoshwa na hali ya umasikini na ya maisha duni ya Manzese, aliamua kuangalia uwezekano wa kuitengeneza Manzese kuwa mji mpya.
*****
Goofy:
Kwenye filam hii kuna hitirafu ambazo mtengenezaji angeweza kuzirekebisha, na filam yake ikaleta uhalisia. Kwa mfano, ametumia sauti ya mwanaume sehemu ambayo alipaswa kuwekwa mwanamke.
Kitu kingine nilicho kigundua ni kuwa sauti zote zilizomo kwenye filam hii ni za mtu mmoja. Amejaribu kubadilisha badilisha uzungumzaji tu.
Vile vile speed au mwendo kasi wa filam ni mdogo sana, sina uhakika kama waliseti PAL/SECAM 24/25 FPS (frames per second). Hivi ni vitu ambavyo vilipaswa kusetiwa kabla ya kuanza kuchukuwa picha au kutengeneza hivi vigaragosi (Cartoon).
Wasiliana Naye:
Wasiliana naye kwa email hii: bonn-j@hotmail.com ili muweze kushauriana nae.
Last edited by a moderator: