Fikra za Mwalimu: Hizi hapa.. mzikubali au mzipinge!

Wakuu wachangia mada,

MKJJ,FMES,KM,na wengine wote,

Mi nadhani kwamba mjadala kuhusu Nyerere na destiny ya Tanzania ni sawa na ule wa mwanzo wa ulimwengu (dunia) kati ya divinity and science,yaani nani wako sahihi divinti or science.Vivyo hivyo kwa Nyerere kuna makundi mawili mabayo yako opposed to each other,sasa inategemea kila mtu anaargue kutoka angle ipi.Kwa wale wanaopenda utafutaji na utumiaji (kwa maana ya a material life) Nyerere sio mfano wa kuigwa na ni karibu na shetani kabisa,hawa ndo watapinga siku zote mazuri yale aliyoyafanya au aliyojaribu kuyafanya (mf. kutoa elimu bure,matibabu,ujamaa,kutenganisha siasa/uongozi na biashara,njia za uchumi kuwa chini ya serikali,etc)kundi hili litajaribu siku zote kuhighlite failure za Nyerere katika mambo haya (ingawa katika ulimwengu halisi kila attempt lazima iwe na upande wa pili,yaani kufail),watataka kudiscredit yote aliyoyafanya Nyerere.Pia watu hawa wanajifanya kwa makusudi kuignore kabisa falsafa binafsi ya Nyerere ambayo ni kutopenda maisha ya juu na/au kufaidika kupitia mali ya umma.Kundi la pili ni lile ambalo linamuunga mkono Nyerere,watu hawa ni wale wanaopenda maisha kwa maana ya usawa (kwa maana yoyote ile) kwa binadamu wote,watu ambao huumia wanapoona mwenzao mmoja kashndwa kulipia dawa hospitali,watu ambao siku zote utawakuta hawana raha na maisha wanapoona injustice inayoendelea hapa duniani.Hawa siku zote watapingana na wale wanaojilimbikizia (sina neno zuri zaidi) mali kwa kisingizio cha utafutaji (rejea Mkapa na mtaji wa masikini au Sumaye:Ukitaka mfanyabiashara mambo yako yakinyookee),kundi hili siku zote litaonesha ubaya wa watu binafsi kumiliki njia kuu za uchumi (hata kama kuna faida kwa jamii nzima).Huku ndiko utakuta watu kama kina Shivji na wenzake wengi.

Hivyo basi mjadala huu kuhusu legacy ya Nyerere hautakwisha kamwe kwa sababu unareflect hali halisi ua ukinzani wa falsafa mbili kuu katika maisha ya mwandamu ambao kina Karl Marx na wenzake walikiwsha kuyaona na kuyajadili almost two centuries ago.Matabaka katika jamii ndo mjadala husika,Nyerere is just being used as a battle ground katika swala hili.

Kwangu mimi ndo naona mjadala huu umesimama hapa.Ni jukumu la kila mwanabodi kujiangalia yeye yuko upande gani ndo ataweza kuchangia mjadala huu kwa ukweli wake.

Mimi niko upande wa Nyerere kwa maana ya usawa wa maisha kwa binadamu wote (ambayo kimsingi ndiyo mafundisho ya karibu dini zote hapa chini ya jua).

Naomba kuwasilisha mada.
 
Hivi kuna faida gani kuchapisha maandishi ambayo huyaamni na wala hutaki kuyatekeleza? Na kuna umuhimu gani wa kujaribu kukiendeleza kitu ambacho unajua fika hakitekelezeki katika mazingira uliyo nayo kama sio kujipotezea muda na tija? Biblia na Quran ni vitabu vizuri sana na ukisoma vinafariji na kuhamasisha, lakini ni mangapi yaliyomo humo yanatekelezeka?
 
Hivi kuna faida gani kuchapisha maandishi ambayo huyaamni na wala hutaki kuyatekeleza? Na kuna umuhimu gani wa kujaribu kukiendeleza kitu ambacho unajua fika hakitekelezeki katika mazingira uliyo nayo kama sio kujipotezea muda na tija? Biblia na Quran ni vitabu vizuri sana na ukisoma vinafariji na kuhamasisha, lakini ni mangapi yaliyomo humo yanatekelezeka?

Hivi unadhani utaweza vipi kujustify unyonyaji na dhuluma dhidi ya watu wale unaowakandamiza?

Tumeona pia vituko vya wahubiri/wachungaji/mapadre matapeli kwa kutumia biblia/kurani.

Kitila unasahau mara hii falsafa ya Machiavelli?

"The End justifies the means."

Tafuta kitabu pia kitabu cha Maciavelli "The Prince" ndo utapata majibu ya maswali yako hapo juu.
 
Mkuu Ogah,

Heshima mbele mkuu, ninajua kuwa wewe ni kichwa, ila sikutegmea kuwa one day utakuja na hizo very low ideas, hapa tunamjadili Mwalimu, na the good he did kwa taifa letu, na what he did not na impact yake kwa wale tuliobaki,

They can go to hell, tutakula manyasi, na the rest of your story, exactly hizo kauli kama ni kweli zilisemwa ziliuwa wananchi wangapi? As opposed na wananchi waliohamishwa bila ridhaa zao na kuachwa maporini wakiliwa na simba I mean your response ni out of the ishu kabisa mkuu, ndio maana unahitaji kujibiwa out of the ishu pia!

Sikutegemea wewe kuja na kauli kama hizi za personal, knowing a lot of things Mwalimu did using Mkapa, pale Daily News ambavyo they did affect directly your personal life, may be unahitaji kuelimishwa who was on your side of interest against those attacks, kwa sababu I know the whole story bro, ila mnahitaji kuwa makini na hoja zenu hapa,

Ahsante Mkuu!
 
Mkuu Ibambasi,

Heshima mbele, usawa wa maisha kwa binadamu wote sio mafundisho ya dini mkuu, maana kama ninaelewa vizuri Mungu anasema kuwa dunia iko mikononi mwa shetani mpaka siku mungu atakapoamua basi, sasa kama hiyo ni kweli ni lini shetani aliwahi kusimamia hizo ideas mkuu unazosema za usawa?

Halafu, the last thing tunahitaji kwenye siasa zetu za taifa ni kuingiza dini, especially, in the wake of wahubiri kutuambia kuwa muungwana ni chaguo la Mungu, please keep dini out,

Ninaheshimu again kwamba angalau una msimamo, kuliko wengine wanaokurupuka tu bila kuelewa hasa maana ya hii topic, lakini ninasema hivi, kama nia yako ni kuwafanya binadamu wote wawe sawa, as a leader then usingeruhusu kuwepo kwa tabaka, na kama mawazo yako yalikuwa ni realistic then yanakuwa ni muongozo hata wewe usipokuwepo, lakini ukiona kiongozi ameondoka aliowaachia wanahangaika, ina maana moja tu kuwa yule kiongozi aliyeondoka alikuwa na walakini mkubwa sana,

na hili nilijifunza kule City, Keeenja alipopoondoka tu the whole system went down, ina maana moja tu mkuu alikuwa for himself, pamoja na kwamba alikuwa akifanya mengi kwa faida ya wengi, in the end unaweza kuwa ulikuwa ni ujanja ulioenda shule wa kuwafarijisha wengi kwa manufaa ya binafsi, kina Mao, George Washington, na wengineo hawapo tena, lakini tizama system zao zinaendelea kuwaka moto,

Sasa why not us?
 
Kitila,

you are very right, idea ambazo hazitekelezeki hatuzihitaji tena, unyonyaji na dhuluma zilikuwepo hata wakati wa zamani na kwenye vitabu bya dini vinasema wazi ont this, na Mungu mara kwa mara aliwatumia viongozi wabaya kwa ajili ya kuwafundisha adaabu wananchi au mataifa yasiyokuwa matiifu kwa amri zake, au viongozi wake waliokuwa waasi wa amri zake, je Ibambasi una maana sasa Mungu anatu-punish kwa kutokumtii au viongozi wetu?

Kuna wakati Mungu alikuwa radhi kulisamehe taifa lwa sababu tu ya tabia za kiongozi wa lile taifa kufuata amri zake, hata kama amekufa lakini Mungu siku zote alimkubuka na kuwasamehe taifa, sasa unasema nini kuhusu sisi na taifa letu on this idea?

Dini has nothing to do na moto tunaoendelea nao bongo, wala maneno na maandishi ya Mwalimu, tunahitaji kuanza na kuheshimu sheria kwanza za jamhuri, na sio maaadili ya vyama vya siasa, mengine yote yatajipanga!
 
Mimi sijui kama sielewi au nimefikia kikomo cha uelewa wangu au vipi? Hivi kuna uhusiano gani katika ya so called mawazo makubwa na kuishi kwenye nyumba za udongo na kula mizizi wakati kila siku naambiwa eti Tanzania ni nchi iliyojaliwa maliasili za kumwaga. Naomba wajuzi wa mambo humu wanionyeshe uhusiano uliopo kwa lugha rahisi ambayo hata mimi nitaielewa.
 
Mkuu Ibambasi,

Heshima mbele, usawa wa maisha kwa binadamu wote sio mafundisho ya dini mkuu, maana kama ninaelewa vizuri Mungu anasema kuwa dunia iko mikononi mwa shetani mpaka siku mungu atakapoamua basi, sasa kama hiyo ni kweli ni lini shetani aliwahi kusimamia hizo ideas mkuu unazosema za usawa?

Halafu, the last thing tunahitaji kwenye siasa zetu za taifa ni kuingiza dini, especially, in the wake of wahubiri kutuambia kuwa muungwana ni chaguo la Mungu, please keep dini out,

Ninaheshimu again kwamba angalau una msimamo, kuliko wengine wanaokurupuka tu bila kuelewa hasa maana ya hii topic, lakini ninasema hivi, kama nia yako ni kuwafanya binadamu wote wawe sawa, as a leader then usingeruhusu kuwepo kwa tabaka, na kama mawazo yako yalikuwa ni realistic then yanakuwa ni muongozo hata wewe usipokuwepo, lakini ukiona kiongozi ameondoka aliowaachia wanahangaika, ina maana moja tu kuwa yule kiongozi aliyeondoka alikuwa na walakini mkubwa sana,

na hili nilijifunza kule City, Keeenja alipopoondoka tu the whole system went down, ina maana moja tu mkuu alikuwa for himself, pamoja na kwamba alikuwa akifanya mengi kwa faida ya wengi, in the end unaweza kuwa ulikuwa ni ujanja ulioenda shule wa kuwafarijisha wengi kwa manufaa ya binafsi, kina Mao, George Washington, na wengineo hawapo tena, lakini tizama system zao zinaendelea kuwaka moto,

Sasa why not us?

FMES,

Natanguliza heshima kwako,

kwanza ningependa kutofautiana nawewe kwenye yale maneno niliyobold na kuhighlite.Kwa ninavyofahamu ni kuwa Mwl. Nyerere alijitahidi sana kufuta matabaka katika jamii nadhani ndio moja ya sababu ya kutaifisha shule za makanisa na kuzifanya za serikali ili watanzania WOTE wasome kwa pamoja achilia mbali kutaifisha njia kuu za uchumi.Hizo zilikuwa jitihada zake binafsi kuleta usawa.Kuhusu kushindwa kwa mfumo aliokuwa akiusimamia nakumbuka yeye mwenyewe aliwahi kujiuliza swali hili bila kupata majibu pia FMES lazima uelewe kwamba kubadili mfumo ni kubadili fikra za wanadamu wenzako,sasa kama alikuwa na watu kama kina Kambon ambao nao walikuwa wengi tu (ukiachia Kambona laiyejitokeza hadharani) waliokuwa wakimpinga huoni kuwa Nyerere tried his best at least kuachieve something tangible?Hii nadhani itaelezea kwa nini pia Keenja naye alishindwa ingawa kulikuwa na mafanikio tangible.

As to the rest nabaki na mtazamo wangu kuwa Nyerere was committed to his cause,whether you disagree with him or not.Ni afadhali yake aliyekuwa wazi na Ujamaa wake kuliko hawa kina Mkapa,Kikwete na wenzano ambao hata wao hawajijui wako upande gani.

Kufanikiwa au kutofanikiwa ni swala jingine ambalo hakimhusu Nyerere pekee.Kuhusu kina Mao na Washington nadhani huo ni mjadala tofauti kidogo.

But the bottomline ni kwamba Nyerere is well defined,what about others?
 
Mkuu Ogah,

Heshima mbele mkuu, ninajua kuwa wewe ni kichwa, ila sikutegmea kuwa one day utakuja na hizo very low ideas, hapa tunamjadili Mwalimu, na the good he did kwa taifa letu, na what he did not na impact yake kwa wale tuliobaki,

Hatujadili hayo yote... naomba tustick na substance. Haya ya mafanikio na nini tuendeleze kwenye ile mada nyingine. Please.
 
Duh wewe ndugu uanaishi marekani gani inayotoa elimu bure ?Hakuna kitu cha namna hiyo labda kwa wateule vinginevyo elimu na huduma ya afya marekani ni gharama kubwa ,afya mpaka uwe na insurance ndipo unasikilizia unafuu napo deductable inapanda kila siku.Elimu wanachofanaya cha maana ni mikopo ila gharama ni kubwa ,kama New York Un. inafika $45,000 per yr.Na hiyo ngoma lazima urudishe haina janja.
Afya kwa wastaafu wanatumia sehemu ya pesa zao walizokuwa wanalipa kodi kwenye social ambazo zimewekwa kwenye mfuko wa Madicare kwa wazee above 65 and disiabled.....

Usibishe hili mkuu,

Elimu ya msingi na upili huko marekani ni bure. Wasiopenda public schools ndio wanakwenda hizo za private. Elimu ya juu pia inapewa ruzuku na serikali kwa asilimia zaidi ya 50%
 
Mwafrika, do confuse between social welfare programs and socialism. Socialism does not allow private ownership of means of production. Under Mwalimu, we kept singing that "the commanding heights of the economy" should be publicly owned. As it turned out, the "commanding height" of our economy included things like schools, hospitals and small hotels. Mwalimu nationalized these.

Mwalimu alikataza hata mabasi ya watu binafsi. Ilifika wakati ikawa shida kweli kweli kusafiri toka mji hadi mji. Nikiwa mwanafunzi UDSM nilibidika kutegemea KAMATA peke yake ili kwenda Moshi. Ilikuwa wakati mwingine inalala njiani.

Mwalimu alisema "hageuki kuwa jiwe". He could persevere for he really never had to shoulder the pain. Alianzisha "duka la viongozi", akawa anaponea huko yeye na "wezake".

Kwani tafsiri ya capitalism na socialism ni ipi?

Mwanakijiji tusaidie hapa tafadhali kama unaweza?
 
Nyerere alikuwa Binadamu kama sisi (kama Kikwete) isipokuwa tu aliwahi kutawala wakati asilimia kubwa ya Watanzania wapo kwenye giza nene.
 
Kwani tafsiri ya capitalism na socialism ni ipi?

Mwanakijiji tusaidie hapa tafadhali kama unaweza?

Mgaya,

My kid sis amenitumia hii tafsiri toka kwenye moja ya vitabu maarufu vinavyotumika kwenye matayarisho ya cheti ya uhasibu (CPA) hapa Marekani. Kitabu hicho kinaitwa Business Environment Concept na kimeandikwa na wanasheria wa Bisk.

Katika kitabu hicho kuna tafsiri zifuatazo:

Capitalism - a free-enterprise system where every economic unit is free to act in its own interests; Resources are owned privately and decisions are made individually thus economic questions are answered by the pricing mechanism of free markets

Communism - an economic system where resources are owned by the state and most decisions are made by the state. Individuals make limited choices thus economic questions are answered by government planning.

Socialism - is something of mixture of capitalism and communism


Naendelea kugoogle ili kupata tafsiri zaidi hapa!
 
Mimi sijui kama sielewi au nimefikia kikomo cha uelewa wangu au vipi? Hivi kuna uhusiano gani katika ya so called mawazo makubwa na kuishi kwenye nyumba za udongo na kula mizizi wakati kila siku naambiwa eti Tanzania ni nchi iliyojaliwa maliasili za kumwaga. Naomba wajuzi wa mambo humu wanionyeshe uhusiano uliopo kwa lugha rahisi ambayo hata mimi nitaielewa.

Ngabu,
Norway ilikuwa moja kati ya nchi masikini sana kule Ulaya. Mwaka 1962 makampuni ya kimarekani yaliwafuta na kuwaambia kuwa wana mafuta katika eneo lao la bahari na wakataka(USA) wachimbe, ila Norway ilikataa. Si kwa sababu walikuwa hawataki kuchimba au walikuwa matajiri ila kwa kuwa hawakuwa na ujuzi wa aina yeyote kuhusu mafuta na mikataba,experience na zaidi fedha.Hawakutaka wamarekani pekeyao ndo wafanye uchimbaji huo na wao walipwe mrabaha tu. Kwa kushirikana na UIingereza waliamua kuchimba na kisha ndipo walialika Kampuni zingine za nje. Baada ya hapo Norway iliunda Kampuni ya mafuta iliyochini ya serikali ili ku-control shughuli zote za mafuta na serikali ikaamua kununua shea kutoka kampuni zingine za mafuta.
Kuwa na mali asili tele haina maana ukurupuke tu bila kuweka mikakati ni jinsi gani mali hizo zitaisaidia nchi. Nyerere sio kwamba hakutaka tufaidike na maliasili yetu ila aliona kuwa hatukuwa na uwezo wala uzoefu na wataalamu wa kutosha kusimamia mambo ya madini. Hakutaka yetukute yanayotukuta sasa, viongozi kama Mkapa kuruhusu uchimbaji bila mikakati yeyote ili mradi tu ahakikishe anafaidika katika kipindi chake cha uongozi.Madini yanakwisha bila Watanzania kufaidika.

Nchi za Scandinavia walichukua mambo waliyoona mazuri kutoka katika Ujamaa na baadhi kutoka katika Ubepari na kuyachanganya na ndo maana tunaona hapa walipo.
Nyerere alikuwa na filosofi nzuri sana ila zilitekelezwa vibaya. Alitaka kila mtu awe na maisha bora.Siku zote matajiri huishi kwa gharama watu fulani kuwa masikini.
 
Back
Top Bottom