Enzi hizo kuogeshwa

hii imenikumbusha mbali sana.....tulikuwa na housegirl mnoko sana....alikuwa ananisugua miguu na jiwe basi ananikwangua huyo......nilimchukia sana.......

Alitaka upendeze tangu utotoni sema tu hukulijua hilo, sasa unatakiwa umsamehe, umpende, umshukuru kwa maana anao mchango wake kwako kufika hapo ulipo na ulivyo pia.
 
Nilikua naogeshwa kwa maji baridi na nikilia kuwa maji ni ya baridi mama alikua ananiuliza kwani vumbi nililochezea lilikua la moto?

Nakala kwa mama yeyoo.(Mama mzazi yumo humu jf)

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Hapo kwenye red nimecheka sana
 
1. Halafu unanyweshwa kidogo maji ya kuogea.......sijui maana yake
2.Mguuni unaguliwa na jiwe "laini" (siyaoni siku hizi)
3. Ole wako uwe na michubuko kwenye miguu kutokana na kucheza mpira halafu unakumbana na mama kauzu utakoma
4. Ukimaliza kuoga unakaushwa juani na kupakwa mafuta ya mamis na kuvishwa nguo ya mtumba

Dah, ukilia sabuni imeingia machoni unaambiwa eti ndio inayasafisha.
 
Umenikumbusha mbali duh! Enzi zetu nakumbuka sabuni tulizokua tunatumia Lexona na Kwanga sikumbuki aina nyingine,mafuta ni mamis,jua kali,yolanda ya kwenye mkebe! Tumeona mengi hadi mambo ya vipi kukaba watu vifuani!

Mkuu hapo kwenye red kuna siku niliumbuka sana, sitasahau
 
mmenikumbusha mbali sana yaani usiombe kuogeshwa ukiwa na vidonda na ukafanya siri lazima kelele ikutoke
 
Umenikumbusha mbali duh! Enzi zetu nakumbuka sabuni tulizokua tunatumia Lexona na Kwanga sikumbuki aina nyingine,mafuta ni mamis,jua kali,yolanda ya kwenye mkebe! Tumeona mengi hadi mambo ya vipi kukaba watu vifuani!
Kama hii?
20181123_140336.jpeg
 
mimi nilikuwa nikisuguliwa tumboni ni kama unanitekenya nacheka mpaka basi lakini ukimaliza tumboni ukihamia miguuni ukunga kama kawa.
ukimaliza unatumia mafuta ya rays au ashers kwa waliokuwa na vipato ahueni.
We jana sana. Ashers mbona hadi sahizi iko dukani. Enzi hizo ni rays ndo fashion
 
Unamkumbuka MAUMBA wewe na mafuta hayo. Unakumbuka matumizi yake wakati huo?


Ndimi Bazazi!
Maumba wa Dsm enzi hizo. Ukimtukana mtu kwa kumwambia maumba lazima zipigwe. Akina mama ikifika giza ukisema maumba huyu, watakimbia hadi wapumue kwa mlango wa tatu. Nilisahau sana hii.
 
kali ni pale baada ya kuoga unavalishwa kaptula ya kushona kwa mkono, kiunoni unafungwa manati aisee yanabana hayoo usiombe!! na nyuma kuna matundu mawili kila tundu lina saburi (kalio) kama taa za starlet
Heheheh
 
Umenikumbusha mwaka 92 nipo chekechea maza sister aliniuliza hivyo afu akasahau akasugua palepale nililia sana na nikagoma kabisa kumalizia kuogeshwa
 
Nina mengi ya kusimulia, nimekumbuka mbali sana ila moja ni pale ambapo unakuta una vidonda si mnajua mambo ya utoto vidonda miguuni ilikuwa ni lazima, unaulizwa kwanza na mwogeshaji vidonda viko sehemu gani, unamtajia ili achukuwe tahadhari.Ila duh! akikosea, balaa lake, unanisikia umesugua kwenye kidonda(kilio).Hahahahaha!
Umenikumbusha mbali sana mwaka 1992 Niko chekechea sister aliniuliza vilipo vidonda afu akasahau akasugua kidonda niligoma kuoga mpaka kesho yake
 
wangapi waliogeshwa kwa mtindo huu utotoni?mana unaambiwa fumba macho ukifumbua sabuni yake machoni utakoma!!!!!!!! !mana unasuguliwa na dodoki,jiwe au chupi yako na usipokuwa na balanceutakoma mana unasimama na mguummojaa uone hiki nn!!!!!
Daah nilikuwa mbishi sana Pia na baridi la kwetu,kila wakati wa kuoga lazima nipate fimbo
 
wangapi waliogeshwa kwa mtindo huu utotoni?mana unaambiwa fumba macho ukifumbua sabuni yake machoni utakoma!!!!!!!! !mana unasuguliwa na dodoki,jiwe au chupi yako na usipokuwa na balanceutakoma mana unasimama na mguummojaa uone hiki nn!!!!!
Mtoa post unafikir sana,umenikumbusha nikiwa darasa la pili 1998,leo nimecheka sana leo baada ya kukumbuka nilivyokuwa miaka hyo na leo hii nimtu mashughuli sana ,asante mungu na mtoa post pia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom