Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,413
- 31,403
- Thread starter
- #141
SIASA ZA MAREKANI
Rais Obama ameapishwa kwa muhula wake wa mwisho. Obama ameapishwa mara mbili kwasababu kikatiba siku ya uapishaji wa Rais ni tarehe 20 na kwa vile ilikuwa Jumapili basi ilirudiwa tena Jumatatu.
Ni kipindi cha pili chenye changamoto nyingi ikiwemo uchumi. Kwa kuanzia tu Obama alikabiliwa na tatizo la fiscal clif ambalo limepatiwa ufumbuzi. Ufumbuzi si wa kudumu bali kuweza kuepusha kudorora kwa uchumi wa dunia kwa mara nyingine, bado linarindima ingawa si kwa kiwngo kile kilichotishia uchumi wa dunia.
Kuna tatizo la deni la taifa na kiwango chake ''debt ceiling'' hili nalo linaonekana kupewa afueni ili bajeti ya serikali iendelee n.k.
Lipo suala la uhamiaji ambalo halikuwahi kuguswa hapo awali. Kutokana na matokeo ya uchaguzi, Obama ana nafasi nzuri ya kulipatia ufumbuzi kwasababu kura za Walatino zimeiumiza sana Republican na watafanya kila wawezalo ili kuepuka hasira za Walatino waliompigia kura G.Bush kwa asilimia 44 na Mitt Romney asilimia 20
Nafasi aliyo nayo Obama ni ile hali ya kuwa hana chochote cha kupoteza tena na wakati huo huo Republican wakiwa wameshindwa jaribio la kumfanya rais wa muhula mmoja kama ilivyokuwa kwa Jimmy Carter.
Hata hivyo bado Obama hawezi kufanya lolote alitakalo kwasababu kuna uchaguzi wa senate na Congress katika ya muhula, hivyo anaweza kukabiliana na upinzani hata ndani ya chama chake.
Katika usalama wa taifa, Obama atatakiwa ahakikishe kuwa vita ya Afghan inaisha na askari wanarejea.
Baada ya kufaulu kule Iraq changamoto nyingine ya mageuzi ya mashariki ya kati ilizuka.
Mashariki ya kati Marekani ilifaulu kumuondoa Ghadafi lakini yametokea mengine kule Syria na Egypt ambako hali bado si shwari.
Mashariki ya kati imezaa tatizo lingine la Mali. Tatizo hilo halikuanzia Mali bali Ageria na sasa nchi za Magaharibi zinafanya jitihada kukabiliana na wapiganaji wa kiislam.
MZOZO WA MALI
Mali imekuwa katika ramani kwa muda mrefu kama sehemu ya kufundishia wanamgambo wa Alqaeeda na inajulikana kwa nchi za magharibi kama Alqaeeda in Magreb Region. Magreb region ni pamoja na Algeria na Morocco.
Tunakumbuka jinsi uchaguzi wa Algeria pale chama cha FIS kiliposhinda lakini ulikataliwa na mataifa ya magharibi.
FIS ni waislam wenye msimamo mkali sana na washirika wazuri sana wa Alqaeeda.
Mahusiano yao na nchi za kiarabu ni makubwa na lengo lao ni kuigeza Algeria kuwa nchi ya Kiislam.
Ingawa hilo lingeweza kutokea kwa taabu lakini kuwapa serikali ilikuwa ndio mwanzo wa kufungua kituo cha ugaidi.
Baada ya kuangushwa kwa Ghadafi silaha nyingi na baadhi ya wapiganaji wamekimbilia katika nchi kama Mali.
Mali ni nchi kubwa sana kuliko Afganistan au Pakistan.
Eneo la vita vya sasa ni kubwa kuliko Afghan kwa kusema kwa uchache tu.
Itaendelea......
Rais Obama ameapishwa kwa muhula wake wa mwisho. Obama ameapishwa mara mbili kwasababu kikatiba siku ya uapishaji wa Rais ni tarehe 20 na kwa vile ilikuwa Jumapili basi ilirudiwa tena Jumatatu.
Ni kipindi cha pili chenye changamoto nyingi ikiwemo uchumi. Kwa kuanzia tu Obama alikabiliwa na tatizo la fiscal clif ambalo limepatiwa ufumbuzi. Ufumbuzi si wa kudumu bali kuweza kuepusha kudorora kwa uchumi wa dunia kwa mara nyingine, bado linarindima ingawa si kwa kiwngo kile kilichotishia uchumi wa dunia.
Kuna tatizo la deni la taifa na kiwango chake ''debt ceiling'' hili nalo linaonekana kupewa afueni ili bajeti ya serikali iendelee n.k.
Lipo suala la uhamiaji ambalo halikuwahi kuguswa hapo awali. Kutokana na matokeo ya uchaguzi, Obama ana nafasi nzuri ya kulipatia ufumbuzi kwasababu kura za Walatino zimeiumiza sana Republican na watafanya kila wawezalo ili kuepuka hasira za Walatino waliompigia kura G.Bush kwa asilimia 44 na Mitt Romney asilimia 20
Nafasi aliyo nayo Obama ni ile hali ya kuwa hana chochote cha kupoteza tena na wakati huo huo Republican wakiwa wameshindwa jaribio la kumfanya rais wa muhula mmoja kama ilivyokuwa kwa Jimmy Carter.
Hata hivyo bado Obama hawezi kufanya lolote alitakalo kwasababu kuna uchaguzi wa senate na Congress katika ya muhula, hivyo anaweza kukabiliana na upinzani hata ndani ya chama chake.
Katika usalama wa taifa, Obama atatakiwa ahakikishe kuwa vita ya Afghan inaisha na askari wanarejea.
Baada ya kufaulu kule Iraq changamoto nyingine ya mageuzi ya mashariki ya kati ilizuka.
Mashariki ya kati Marekani ilifaulu kumuondoa Ghadafi lakini yametokea mengine kule Syria na Egypt ambako hali bado si shwari.
Mashariki ya kati imezaa tatizo lingine la Mali. Tatizo hilo halikuanzia Mali bali Ageria na sasa nchi za Magaharibi zinafanya jitihada kukabiliana na wapiganaji wa kiislam.
MZOZO WA MALI
Mali imekuwa katika ramani kwa muda mrefu kama sehemu ya kufundishia wanamgambo wa Alqaeeda na inajulikana kwa nchi za magharibi kama Alqaeeda in Magreb Region. Magreb region ni pamoja na Algeria na Morocco.
Tunakumbuka jinsi uchaguzi wa Algeria pale chama cha FIS kiliposhinda lakini ulikataliwa na mataifa ya magharibi.
FIS ni waislam wenye msimamo mkali sana na washirika wazuri sana wa Alqaeeda.
Mahusiano yao na nchi za kiarabu ni makubwa na lengo lao ni kuigeza Algeria kuwa nchi ya Kiislam.
Ingawa hilo lingeweza kutokea kwa taabu lakini kuwapa serikali ilikuwa ndio mwanzo wa kufungua kituo cha ugaidi.
Baada ya kuangushwa kwa Ghadafi silaha nyingi na baadhi ya wapiganaji wamekimbilia katika nchi kama Mali.
Mali ni nchi kubwa sana kuliko Afganistan au Pakistan.
Eneo la vita vya sasa ni kubwa kuliko Afghan kwa kusema kwa uchache tu.
Itaendelea......