a4afrika
JF-Expert Member
- Apr 13, 2012
- 1,389
- 1,337
Mkuu Nguruvi3 umegusia hoja muhimu sana hasa chama kikuu cha upinzani kutokutoa sera na misimamo yake kueleweka wazi kwa wapiga kura wa kawaida.
Mpaka leo CDM haielezei vizuri na kwa uwazi juu ya sera yake ya majimbo jinsi itakavyomnufaisha mwananchi wa kawaida mijini na vijijini.Kuacha kutoa ufafanuzi mzuri juu ya sera yako kunatoa nafasi nzuri sana kwa CCM kuikosoa na kueleza ubaya wake kwa kutoa mifano jinsi ilivyoshindwa kufanyakazi katika nchi nyingi za kiafrika Nigeria ikiwemo.
Msimamo wa CUF kuhusu muungano unajulikana wazi lakini msimamo wa CDM haujulikani,tunachokifahamu ni misimamo ya baadhi ya viongozi wake kama Tindu Lissu.Mikutano mingi ya M4C imejaa ubabaishaji wa hali ya juu kiasi wananchi wengi badala ya kuchota elimu ya uraia wamekuwa wakikumbana na vijembe na mipasho usiowasaidia na hili limeshaanza kuzoeleka.
Well said Mkuu wangu:
Kuna vitu huwa napenda vitenganishwe katika Harakati za Ukombozi za vyama vyetu nchini! Navyo ni Political Movements na Welfare Movements!
*Political Movement, hujikita zaidi kukisimika chama kwenye HISIA za watu(ni propaganda), focus huwa "UMAARUFU" masikioni na midomoni mwa watu, mikutanoni na kona zote mitaani! Na humo ndimo vyama vyetu vyote vilimojikita, mfano mdogo tu "omba uwe maarufu kidogo tu, then tangaza nia ya kugombea ubunge kupitia chama chochote kile, utapewa support kubwa na uongozi wa juu kabisa! Tunawaona kina Komba, Rwakatale, Sugu, sasa Afande Sele, n.k. Hizo ni Political movements, na ni JANGA la taifa! Huku kauli "mkitupa ridhaa...tupeni ridhaa muone...tupeni kipindi kingine...."n.k hutawala majukwaa. Ni Upumbavu!
*Welfare Movements, hizi huhangaikia AKILI za watu na si HISIA zao, vigezo na hoja hutangulizwa kwanza katika kila jambo! Harakati hizi huwa haziyumbishwi na chochote ila Ustawi wa Raia tu/Maslahi ya Umma. Hapo ndipo akili zinapokubaliana na chama fulani kwa kuendesha harakati hizo, hata kama Hisia zitapinga, lakini Akili ikikubali Inatosha!
Huku tatizo hubainishwa, humeng'enywa, na kufanyiwa maamuzi sahihi na hatua mahususi! Lengo ni kujenga imani kwa watu juu ya chama kupitia AKILI ZAO NA SI HISIA ZAO! Wanachama na mashabiki wapo, hakuna mtaji bora wa kutekeleza hayo kama hiyo!
CDM kama chama kikuu cha Upinzani, kikiundwa na wasomi, kilitakiwa kione tayari fursa nyingi za kuisimika imani kwa watu kupitia akili zao juu ya chama chao! Mfano, ingekuwaje kama Chdm kupitia Bavicha ikaunganisha vijana kwa kila tawi na kubuni miradi na kuifanya kama timu, kesho wameacha wizi mtaani, wazee wao wangeizungumziaje chadema?
Kuna wanasheria wengi Cdm, ingekuwaje kama wangefungua vituo vya msaada wa kisheria kila tarafa hata kwa kusema viwe vinahudumiwa na matawi ya chama, kupitia miradi yao iliyobuniwa! Chama kama Taasisi iliyoamua kujitoa muhanga, kuna atakayedai mshahara mkubwa huko vituoni, kama yupo hafai. Kila mtu ale kiapo cha kukitumikia chama katika mazngra yoyote.
Hiyo ni mifano midogo tu ya Welfare Movements za CHAMA MAKINI.
Ni kujidanganya kwamba akili za watz zitajenga imani kwa Cdm, kwa kuwataja wala rushwa hazarani, kukandia ccm hazarani, n.k atakayejenga imani zake kwasababu ya hayo leo, kesho ataiondoa na kuipeleka ccm tena kwani wamemwambia cdm ni wadini au wakanda! HISIA HAZINAGA MSIMAMO!
Mungu wetu anaita sasa!
Last edited by a moderator: