Dr Slaa: Chadema kujenga Mfumo Mpya wa Elimu Mwaka 2015

matasha

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
378
400
Katibu Mkuu cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amesema Chadema imejipanga kuufumua mfumo wa elimu Tanzania ulioshindwa na kuunda upya pindi watakapounda serikali mpya mwaka 2015. Hayo aliyasema katika mahali ya darasa la saba ya shule ya Queen's English Medium Schools iliyopo Ukonga katika hotuba iliyosisimua wengi iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Kitivo cha Elimu(DUCE) na Mshauri wa masuala ya elimu wa Chadema Dr Kitila Mkumbo.


Ifuatayo ni summary ya hotuba hiyo;

Kwanza alitoa udhuru kwamba Dr Slaa amemtuma amwakilishe kwani yupo kwenye kampeni za uchaguzi wa madiwani. Aliupongeza uongozi wa shule hiyo kuweza kumwalika Katibu Mkuu wa Chadema kuwa mgeni rasmi na wamedhihirisha kuwa viongozi wote ni sawa bila kujali ni CCM au upinzani. Shule hiyo ilizinduliwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa DSM John Guninita na mahali ya mwaka jana mgeni rasmi alikuwa naibu Waziri Mh Mahanga.


Pia aliupongeza uongozi wa shule hiyo kwa elimu nzuri wanayotoa kwani mwaka jana walipata cheti cha ushindi na manispaa ya Ilala kwa kufaulisha wanafunzi wote. Na pia alisema ubora wa shule hiyo unathibitishwa na hotuba, mihadhara na maigizo kwa lugha ya kiingereza yaliyotolewa na wanafunzi wa shule hiyo. Watoto wadogo wa darasa la tano walitoa hotuba nzuri sana kuelezea sababu za umaskini Tanzania na pia watoto wengine waliweza kutoa mhadhara kwa ufasaha kuhusu digestive system na pragnancy.


Akielezea sera ya elimu ya Chadema Dr Mkumbo alisema mfumo wa elimu uliopo sasa si mzuri sana na idadi ya watoto wanaopata elimu bora hasa kupitia shule binafsi ni chini ya asilimia moja. Alisema mfumo wa elimu katika shule za umma una matatizo makubwa sana na nchi imegawanywa katika matabaka mawili ya wale wanaomudu elimu nzuri katika shule binafsi na wale wanaosoma shule za umma ambapo elimu inayotolewa huko ni duni sana na walimu wamekata tamaa. Alisema Chadema imejipanga kuurekebisha mfumo wa elimu na pia kuhakikisha elimu katika shule za umma inakuwa bora. Alielezea mambo yafuatayo kuwa ni baadhi ya mambo ya kwanza Chadema kuyarekebisha mara tu watakapochukua dola.


(i) watoto wataanza shule mapema zaidi kwani kwa sasa watoto wanakuwa haraka zaidi. Alisema kwa sasa watoto wanaingia shule wakiwa wamechelewa na hivyo wanachelewa pia kuanza kazi pindi wanapomaliza masomo yao. Moja ya sera za Chadema ni kuhakikisha watoto wanaanza shule wakiwa na miaka mitano na nusu hadi sita. Pia alisema sera ya Chadema ni kuwa na miaka minane kwa elimu ya shule ya msingi ambapo watoto watakuwa wamesoma hadi masoma ya kidato cha pili yanayotolewa sasa. Pia elimu ya sekondari itakuwa kwa miaka minne yaani itakuwa ni kuanzia kidato cha tatu cha sasa hadi kidato cha sita. Baada ya hapo watoto watajiunga vyuo vikuu na ufundi na itawezekana vijana kumaliza vyuo wakiwa na miaka 21 na kuanza kazi mapema kuliko ilivyo sasa.


(ii) Sera ya Chadema ni kuweka mkazo katika elimu ya kujitegemea na stadi za ufundi. Alisema elimu ya nadharia itapewa minofu na elimu ya vitendo na pia elimu ya kujitegemea ili vijana wanaomaliza shule wawe wabunifu zaidi kuliko ilivyo sasa.

(iii) Chadema imepania kuirudisha heshima ya mwalimu iliyopotea. Alisema mwalimu aliyekata tamaa hawezi kutoa elimu bora bali atawafundisha watoto kukata tamaa. Alisema Chadema itawalipa walimu vizuri, itawapatia nyumba na vitendea kazi ili kurudisha heshima ya walimu. Alisema heshima ya mwalimu ni heshima ya taifa.


(iv) Chadema itaimarisha lugha ya Kiingereza kwani kwa sasa watoto wengi wa Kitanzania wametengwa na lugha hiyo. Alisema watoto wanaosoma shule za mfumo wa kiingereza wanaweza kuizungumza lugha hiyo vizuri huku maelfu ya watoto wanaosoma shule za umma wakiwa wametengwa na kuachwa yatima. Alisema kwa sasa hata Wanyaruanda wanawazidi watoto wa kitanzania kwa kuzungumza kiingereza na kusema tutakuwa tunajidanganya kuwa kiingereza sio muhimu wakati sasa ndio imekuwa lugha kubwa ya mawasiliano hasa kwenye makampuni makubwa na kwenye nyanja ya kimataifa. Alisema sera ya Chadema ni kuhakikisha watoto wanazungumza kiswahili vizuri lakini pia kuhakikisha wanamudu lugha ya kiingereza. Alishangaa imekuwaje Rwanda iliyotoka kwenye vita muda mfupi uliopita kutuzidi katika nyanja za elimu, afya na huduma za jamii katika takwimu za hivi karibuni.


(v) Chadema imepania kuvunja matabaka ya elimu ambayo ni tishio kwa umoja wa taifa na kuhakikisha mtoto anayesoma shule ya serikali hatakuwa na tofauti na yule anayesoma shule binafsi.


Alimaliza hotuba yake kwa kuupongeza tena uongozi wa shule hiyo na kuahidi kiasi cha shilingi laki tano katika kusaidia maendeleo ya shule hiyo ambayo inasaidia pia kusomesha bure watoto yatima.


Kwa mawasiliano wa uongozi wa shule hiyo piga no 0719 604156
 
Ahsante mkuu... hiyo ya (V) hapo juu nimeipenda sana..nadhani ndiyo sababu kuu ya watoto wetu wengi kumaliza darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika...
Halafu ningeshauri kabla ya wanasiasa kuahidi mambo yanayohusu mifumo mbalimbali iliyopo ni vema wakawahusisha wataalam kwenye nyanja husika...ili kupata taarifa sahihi...inaendeshwa vipi? kwanini ilibadilishwa? nini mawazo yao ili kuboresha mifumo hiyo.. nk ...ili waje na suluhisho zilizo sahihi....cha mwisho sisi tunaendelea kuhesabu pamoja na kuweka kumbukumbu ya hizi ahadi ......
 
Hii sera imanikamata vilivyo. Hii ndiyo nchi ninayoitaka na haiwezekani chini ya CCM
 
Sera ya elimu bure imefia wapi tena...sasa hiyo namba ya simu ya shule inahusiano gani na hotuba ya Dr Slaa.
 
Ahsante mkuu... hiyo ya (V) hapo juu nimeipenda sana..nadhani ndiyo sababu kuu ya watoto wetu wengi kumaliza darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika...
Halafu ningeshauri kabla ya wanasiasa kuahidi mambo yanayohusu mifumo mbalimbali iliyopo ni vema wakawahusisha wataalam kwenye nyanja husika...ili kupata taarifa sahihi...inaendeshwa vipi? kwanini ilibadilishwa? nini mawazo yao ili kuboresha mifumo hiyo.. nk ...ili waje na suluhisho zilizo sahihi....cha mwisho sisi tunaendelea kuhesabu pamoja na kuweka kumbukumbu ya hizi ahadi ......

Sera hiyo ya elimu ina nafasi nzuri sana katika uchumi wa taifa kuliko mkumbatio wa mfumo wa elimu tuliyo nayo sasa.
Nilisikia karibuni CCM walikuwa na mipango ya kupunguza kutoka miaka 7 hadi 6 ya elimu ya msingi, hapo niliachwa hoi kabisa.

Mpango huo wa Dr. Slaa maana yake unaturudishwa kwenye elimu ya zamani ambao wengi wa viongozi watu walifaidika nao, ndo maana uliona waliohitimu darasa la nane miaka hiyo ilm yao karibu inashabihiana na kidato cha sita siku hizi.

Msingi wa elimu ni elimu ya msingi kwani ukichelea hapo hata huku vyuoni hakuna kitu.

Marekani kwa mfano wana 8 grades na baada ya hapo high school miaka 4 ambayo kwa tanzania tunaiinda secondary school. Hapo mtu akishahitimu anaweza kuajiriwa po pote isipokuwa inapodaiwa kiwango cha juu cha elimu. Hata hivyo inapotajwa kiwango cha juu cha elimu utaona kuna kipengire kinachotaja kama kuna mwenye kiwango cha elimu cha highschool mwenye uzoefu anapewa nafasi kuliko mwenye kusotea degrees kwa kukosa uzoefu.

Kenya wanaonekana elimu yao iko juu zaidi ya elimu ya Tanzania ni kwa sababu tu hawakuvuruga mfumo wa elimu ya kikoloni waliyoikuta. Leo kwa uzembe wetu tunalazimika kutazama nyuma na kurudia tulichokidharau kwa misingi ya kisiasa badala ya kuangalia ubora.

Vijana wengi wanahitimu vyuo wameshakuwa wakubwa mno kwani wali wengi wanahitimu wamefikisha miaka zaidi ya 25, lakini kwa mapendekezo ya Dr. Slaa kuna uwezekana wa vijana wahitimu chuo kikuu umri kuwa chini zaidi ya ilivyo sasa.
 
Sera ya elimu bure imefia wapi tena...sasa hiyo namba ya simu ya shule inahusiano gani na hotuba ya Dr Slaa.

Achana na mipasho bana, Ritz ulipata elimu wakati mambo hayajawa ovyo kama watoto wako au wadogo zako leo. Ukimwuliza swali mwanafunzi anaanza kuchekacheka badala ya kukutazama usoni na kukusoma unachomwuliza. Wanafunzi hata hawajajengeka kisaikologia. Hapa kwenye elimu Ritz tuungane.
 
ritz vipi zile ahadi 500 za jk MWAKA 2010, 2 year to go vp?? na nchi wahisani kama uholanzi wamekata mafungu, na wanataka kuhamisha mambo muhimu katika ubalozi wao waupeleke kenya, umewaona wale vijana wa uvccm wakiwa na mabango na wengine wakipigana na kuibiana mifuko ya nyuma, polesana, vip wewe rejao, chama, gongo la mboto na nepi manazungumziaje rushwa ya wazi ambayo hata mwenyekiti wenu dk rushwa(jk) ameillamikia katika chaguzi zenu hvivi karibuni,,,, rushwa bila shaka ndio sera yenu???hivi unapata picha gani baba wa nyumba naye anapolalamika kama watoto wake.. poleni sana,,,, mwisho wenu umekaribia, mjiandae kisaikolojia na kukimbia nchi tutawanyonga wote na kuwapiga shaba hadharani woote mliotuibia tukianza na dk rushwa (jk)..... R.IP NYINYIEMU YOOTE COZ SHeTANI AMEWAPENDA ZAIDI
 
Hivi Dr Slaa bado anawaza kweli kuwa rais wa Tanzania tufike wakati tuwe wakweli Dr Slaa, ataendelea kuwa rais kivuli wa Tanzania miaka yote.
 
Achana na mipasho bana, Ritz ulipata elimu wakati mambo hayajawa ovyo kama watoto wako au wadogo zako leo. Ukimwuliza swali mwanafunzi anaanza kuchekacheka badala ya kukutazama usoni na kukusoma unachomwuliza. Wanafunzi hata hawajajengeka kisaikologia. Hapa kwenye elimu Ritz tuungane.

Hii dhana mtu akipingana na mitazamo ya Chadema mnasema mipasho mie nimehoji sera ya Chadema kutoa elimu bure kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu imefia wapi.
 
Pole ritz mmemaliza kumpiga makofi shigela???, naona hata wewe unanuka rushwa kama dk rushwa (jk)
 
Hii dhana mtu akipingana na mitazamo ya Chadema mnasema mipasho mie nimehoji sera ya Chadema kutoa elimu bure kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu imefia wapi.

Uzi huu unaelezea mabadiliko ya mfumo wa elimu tulio nao sasa, kama unataka hayo unayoeleza yalishafafanuliwa katika ilani yao ya uchaguzi na hawajatoa tamko la kukanusha au kubadilisha.
 
hivi dr slaa bado anawaza kweli kuwa rais wa tanzania tufike wakati tuwe wakweli dr slaa, ataendelea kuwa rais kivuli wa tanzania miaka yote.

jk ndio anawafundisha mpigane kisa ubwabwa, kofia na kanga?? Poleni miaka 51 ya uhuru bado mnagombania kofia??
 
Hivi Dr Slaa bado anawaza kweli kuwa rais wa Tanzania tufike wakati tuwe wakweli Dr Slaa, ataendelea kuwa rais kivuli wa Tanzania miaka yote.
Ritz kwa ndoto za alinacha, hivi una imani bado ccm itashinda...
 
Sera ya elimu bure imefia wapi tena...sasa hiyo namba ya simu ya shule inahusiano gani na hotuba ya Dr Slaa.
Hiyo sera imefia CCM na iliuawa na CCM. Chadema wataifufua pindi watakapopata uongozi wa taifa hili.
 
Upunguani kitu kibaya sana; ukikosa la kufanya utadanganya mpaka watoto wadogo

Chama
Gongo la mboto DSM
Unewaza kusema hivyo kumbe we unayesema hivyo ndo punguani kwa sababu ya ufahamu mdogo wa kuelewa mambo na hii inatokana na ushabiki wa chama ulichopo.
 
Hii dhana mtu akipingana na mitazamo ya Chadema mnasema mipasho mie nimehoji sera ya Chadema kutoa elimu bure kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu imefia wapi.

usiwe kama mp....vu!sera uwenda ikaendelea kuwepo na kuhusu swala la elimu kutolewa bure walisema itatolewa bure kwanzia elimu ya msingi mbaka elimu ya kidato cha 6. Ila tusubiri uwenda wakaboresha zaidi juu ya sera ya elimu,kwani ninaifahamu cdm si wa2 wa kukurupuka zen wapo makini tofaut na ccm wala ndugu na chukua chako mapema{ccm~cuf,tlp,nccr n.k}
 
Achana na mipasho bana, Ritz ulipata elimu wakati mambo hayajawa ovyo kama watoto wako au wadogo zako leo. Ukimwuliza swali mwanafunzi anaanza kuchekacheka badala ya kukutazama usoni na kukusoma unachomwuliza. Wanafunzi hata hawajajengeka kisaikologia. Hapa kwenye elimu Ritz tuungane.
ni kweli lazima tuungane katika hili lakini ni kweli kwamba sera ya elimu ya1995 ni mbovu kiasi hiki ama usimamizi na utekelezaji ndio mbovu?
hapa hata kwa sera nyingine yoyote itakayoletwa kwa usimamizi na utekelezaji huu sioni elimu bora tanzania!
 
usiwe kama mp....vu!sera uwenda ikaendelea kuwepo na kuhusu swala la elimu kutolewa bure walisema itatolewa bure kwanzia elimu ya msingi mbaka elimu ya kidato cha 6. Ila tusubiri uwenda wakaboresha zaidi juu ya sera ya elimu,kwani ninaifahamu cdm si wa2 wa kukurupuka zen wapo makini tofaut na ccm wala ndugu na chukua chako mapema{ccm~cuf,tlp,nccr n.k}
cdm wapo makini kimfumo ama kikarama?
suala la elimu tanzania liko hovyo kushinda linavyozungumzwa na ingekuwa kwenye nchi za wenzetu wazazi wenye watoto mashuleni pamoja na watu wazima wanafunzi tayari wangeisha ingia mtaani kupinga elimu mbovu itolewayo tanzania.
 
Back
Top Bottom