Najua sana kwamba Mnyika anaiweza kazi hiyo lakini ndio kusema hatuna watu wengine?.. Kwa nini hawahawa wabunge ndio tunawapa nafasi za uongozi ndani ya chama?.. Wapo vijana wengi BAVICHA ambao wanaiweza kazi na hawana madaraka mengine na wanaweza weka masaa mengi zaidi kushughulikia hili (kukitangaza chama) maana hapa ndipo kazi kubwa inatakiwa na mtu mwenye muda na nafasi kubwa zaidi ktk vyombo vya habari..Kimsingi mawazo yako ni mazuri sana.Lakini kwa jinsi tunavvyomfahamu Mnyika ni kijana mtulivu,damu inachemka na anaupeo wa hali ya juu kwa siasa za nchi hii.Kwa mahali ambapo chama chao kimefikia kinahitaji mtu kama yeye kwa hiyo nafasi.Naamini atamudu kubeba majukumu yote mawili bila matatizo.Na kuhusu hoja ya ULAJI binafsi sina jibu.
Mkandara nashukuru kwa mawazo yako kuwa viongozi hasa wabunge wanazidi kulundikiwa vyeo, lakini elewa si kila cheo anapewa mtu yeyote almradi terms zake ni nafuu. Cheo hicho cha katibu mwenezi kinatakiwa mtu anayekielewa vyema chama (not an employee) na awe loyal kwa chama na uongozi kwa ujumla. Hicho cheo kinaweza kukiuza chama au kukiua chama kwa muda mfupi sana refer Nape alivyopigwa stop baada ya miezi michache. Kwangu mimi naona Slaa kalamba dume kwa kumuweka Mnyika pale.Chadema sasa mnachosha.... kwa nini mnawalimbikiza wabunge kazi zaidi wakati walizonazo tayari ni mzigo kwa chama?.. Vijana wengine wapo kwa nini hawatumiwi hawa!..Sipingi swala la Mnyika kuteuliwa nafasi hii, bali nadhani wapo vijana wengi sana wenye uwezo ari na wamejikita ktk media wanaweza kuifanya kazi hii kila siku masaa 16 kwa malipo madogo sana kuliko kumshindilia mtu mmoja majukumu kibao.. Mtamzeesha huyu dogo kabla ya wakati wake.
Swali langu ktk uteuzi huu, Je, Hawa viongozi wa chama na ni wabunge pia hawapokei mishahara miwili kwa kutoa huduma hizi?.. mathlan Mnyika leo hii pato lake haliongezeki kwa kupewa jukumu hili zaidi maana twende mbele turudi nyuma. Kupinga posho kepee haitoshi ikiwa chama kinawapa madaraka kundi la watu wale wale tu hii inaashiria zaidi kwetu kama ni ULAJI zaidi kwao..
- Mtanisamehe nawakilisha mawazzo yangu.
Utakuwa ni uteuzi mzuri na makini kwani kurugenzi yetu ya habari na uenezi haikuwa active kiasi kinachotakiwa.
Ili afanye kazi zake vizuri zaidi na kwa uhakika inabidi wampunguzie majukumu ya ukurugenzi wa mambo ya nje.
Na kuanzia sasa wale watunga propaganda dhidi ya chadema wamepata kiboko yao, JJ amekuja kuwashika!
Mkuu kusema hivyo, unataka kunambia hao vijana wengine waliopo na wanachama wa miaka Chadema hawaaminiki?.. mbona unanitisha..basi inakuwa chama hiki kina wenyewe? kuaminiana kupi huko hadi wachache tu ndio wanaaminika..Mkuu tusijenge ukuta maendeleo ya chama vijana wapo na wengi wanaiweza kazi maana hii sio nafasi ya mweka siri wa chama, bali mwenye uwezo wa kukitangaza chama na kujibu tuhuma. Kama tutawaogopa vijana wetu kama Nape, inaashirika kuna kina Lowassa ndani ya chama.. dhana hii ni hatari...Mkandara nashukuru kwa mawazo yako kuwa viongozi hasa wabunge wanazidi kulundikiwa vyeo, lakini elewa si kila cheo anapewa mtu yeyote almradi terms zake ni nafuu. Cheo hicho cha katibu mwenezi kinatakiwa mtu anayekielewa vyema chama (not an employee) na awe loyal kwa chama na uongozi kwa ujumla. Hicho cheo kinaweza kukiuza chama au kukiua chama kwa muda mfupi sana refer Nape alivyopigwa stop baada ya miezi michache. Kwangu mimi naona kwa Mnyika Slaa kalamba dume.
Huku Nape Nnauye huku John Mnyika. We acha tu,
Najua sana kwamba Mnyika anaiweza kazi hiyo lakini ndio kusema hatuna watu wengine?.. Kwa nini hawahawa wabunge ndio tunawapa nafasi za uongozi ndani ya chama?.. Wapo vijana wengi BAVICHA ambao wanaiweza kazi na hawana madaraka mengine na wanaweza weka masaa mengi zaidi kushughulikia hili (kukitangaza chama) maana hapa ndipo kazi kubwa inatakiwa na mtu mwenye muda na nafasi kubwa zaidi ktk vyombo vya habari..
Wapo watu nawasoma kila siku huku wakiandika mambo mazito mazito na wanaelewa siasa za Bongo kwa nini tumwongezee mzigo Mnyika hali tayari kisha elemewa.. Kama unakumbuka kisha kuja hapa Kijiweni na kusema tummuwie radhi ana majukumu mengi sana hataonekana mara kwa mara hapa JF, leo unampa kazi inayohusu swala amblo yeye mwenyewe alishindwa kutokana na majukumu mengine?..
Kama kawaida yangu mimi siku zote msema kweli sina unafiki napoona jambo halikukaa vema hulisema sisubiri kwanza watu walitafune.. Binafsi nadhani Mnyika anatakiwa kupunguziwa kazi ili apate muda mzuri wa kuboresha sehemu alizopo, haya ya kuongezewa majukumu zaidi wakati vijana wapo wanakula, kushinda na kulala JF, Mwananchi, na vijiweni nadhani sii uchaguzi mzuri..
Najua sana kwamba Mnyika anaiweza kazi hiyo lakini ndio kusema hatuna watu wengine?.. Kwa nini hawahawa wabunge ndio tunawapa nafasi za uongozi ndani ya chama?.. Wapo vijana wengi BAVICHA ambao wanaiweza kazi na hawana madaraka mengine na wanaweza weka masaa mengi zaidi kushughulikia hili (kukitangaza chama) maana hapa ndipo kazi kubwa inatakiwa na mtu mwenye muda na nafasi kubwa zaidi ktk vyombo vya habari..
Wapo watu nawasoma kila siku huku wakiandika mambo mazito mazito na wanaelewa siasa za Bongo kwa nini tumwongezee mzigo Mnyika hali tayari kisha elemewa.. Kama unakumbuka kisha kuja hapa Kijiweni na kusema tummuwie radhi ana majukumu mengi sana hataonekana mara kwa mara hapa JF, leo unampa kazi inayohusu swala amblo yeye mwenyewe alishindwa kutokana na majukumu mengine?..
Kama kawaida yangu mimi siku zote msema kweli sina unafiki napoona jambo halikukaa vema hulisema sisubiri kwanza watu walitafune.. Binafsi nadhani Mnyika anatakiwa kupunguziwa kazi ili apate muda mzuri wa kuboresha sehemu alizopo, haya ya kuongezewa majukumu zaidi wakati vijana wapo wanakula, kushinda na kulala JF, Mwananchi, na vijiweni nadhani sii uchaguzi mzuri..
Hapa JF wamejaa tele yaani siwezi hata kuwamaliza... na wameonyesha uwezo mkubwa sana ktk kukitetea chama. Na tuache siasa za makundi wapo kina Ben, Lwakatale, Feedback, Sikonge, Lunyungu, Mwita Maranya na wengine watu wazima wapo ktk media kila kukicha...Unaweza kunitajia hao vijana watano wenye uwezo km wa mnyika?
Na mbali na Ubunge ni waziri kivuli bado ana cheo chake cha kuchaguliwa ndani ya chama, kisha leo anateuliwa jukumu na sii mjumbe tu yaani huyu huyu mtu mmoja....Hii inaleta picha kwamba Chadema haina watu wengi wenye uwezo (viongozi)..Vyema mkuu. Hapo bila kusahau kwamba John ndie mkurugenzi wa mambo ya nje!!
Kwa hii tabia ya kumlundikia mtu mmoja vyeo kibao,napata shida kuona CHADEMA kimejiandaa vipi kua mbadala wa CCM,kama nacho kinafanya madudu ambayo CCM kimekua kikifanya toka enzi na enzi.
Na hiyo tabia imekua ni chanzo cha ufanisi na utendaji husioridhisha kutoka kwa hao wenye vyeo lukuki. Pia tabia hiyo ni chanzo cha matumizi mabaya ya pesa,kwani huyo mtu mwenye vyeo lukuki pia atakua na malipo lukuki!
Hao uliowataja wamekuambia wanaiweza hiyo nafasi? Je wamekumbia hawana majukumu kiasi hawatatingwa kama wangeteuliwa kwenye hiyo nafasi?Hapa JF wamejaa tele yaani siwezi hata kuwamaliza... na wameonyesha uwezo mkubwa sana ktk kukitetea chama. Na tuache siasa za makundi wapo kina Ben, Lwakatale, Feedback, Sikonge, Lunyungu, Mwita Maranya na wengine watu wazima wapo ktk media kila kukicha...