Huyu aligombea Urais mwaka jana na kama sikosei alipata kura 0.00000001%. Nani anamjua? Sana sana ni kibaraka wa CCM anayetumiwa na Riz wakishirikiana na baba yake Kiwete!
Mgombea wa Uraisi wa Tanzania kwa tiketi ya United People's Democratic Party, UPDP, Fahmi Nasoro Dovutwa amejiondoa katika kinyang'anyiro hicho na kusema kuwa kura yake atampa mgombea wa kiti hicho kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, CCM, Jakaya Mrisho Kikwete.
Fahmi Nasoro Dovutwa/UPDP
Dovutwa amesema uamuzi huo unatokana na kukosewa kwa jina lake katika fomu za uteuzi zilizowakilishwa katika tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania, NEC, ambapo amesema zinaweza kusababisha utata wakati wa kuapishwa ikiwa atashinda uchaguzi huo, hivyo badala ya kuharibu kura hizo, ameamua kumuunga mkono Kikwete.
Amesema amemuunga mkono Kikwete kwa kuwa ndiye mgombea asiye na udini, ukabila wala kutishia kumwaga damu ili kushinda katika uchaguzi huo. Akasema kwa sasa hataki kuleta vurugu za kufuatilia suala hilo la kukosewa jina lake, bali ataendelea kufuatilia suala hilo NEC baada ya uchaguzi kumalizika.
Dovutwa amesema anaungwa mkono na vyama vya SAU, Jahazi Asilia, UMD, NLD na Demokrasia Makini.
Makucha gani mbabaishaji huyu,wakiitwa wa kuonesha makucha yao na Dovutwa atajitokeza??Hawa ndio fisi maji waliojivika ngozi ya kitoweo pweza.Hakuna lolote pale.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.