Dkt. Sebi kielelezo cha Waafrika kukataliwa Tiba zao. Alikufa kifo chenye utata baada ya ugunduzi wa Dawa ya UKIMWI

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
WanaJF,

Mfahamu Dr. Sebi: Mwafrika Aliyetibu Ukimwi Wazungu Wakamla Kichwa!

Alfredo Bowman maarufu kama Dr. Sebi, hakutibu ukimwi tu, alitibu hadi kansa na kisukari biashara za watu, wakamfugulia jumla ya kesi 2,781 akashinda zote, akaja kubambikiziwa zengwe la utakatishaji fedha, akatupwa jela na kufia huko, tukaambiwa alikufa kwa nimonia, Nipsey Hussle, muimbaji rappa akaanza kuandaa makala kuhusu Dr. Sebi, kabla hajamaliza naye wakamla kichwa, nikayakumbuka yale maneno ya Mzee Nyerere, “ UBEPARI NI UNYAMA”!

Dr. Sebi alianza kazi ya utabibu kwa kutumia mitishamba baada ya wazungu kushindwa kumtibu kisukari, ugumba, athma na overweight, akaja kutibiwa kwa mitishamba huko Mexico, mgumba akavunja rekodi ya kuzaa watoto 17. Waafrika wote tungeelewa kwamba sisi ndo wafalme wa tiba hapa duniani tusingepoteza pesa kwenye tiba za kizungu, badala yake tungemshukuru Mungu kwa zawadi hii ya utabibu aliyotupa bure na kisha tuingia kuwatibu wagonjwa wote duniani maana imeandikwa ukishukuru Mungu anatenda usiposhukuru shetani anatenda!

Dr. Sebi alizama kwenye tafiti za mitishamba na matunda akagundua asidi ndo chanzo cha magonjwa yote na tiba yake ni kuacha kula vyakula vyenye acid kama vile ugali nyama choma na kula vyakula vyenye alkaline kwa wingi. Hapa kwenye acid na alkaline najua umebaki njia panda maana uliyasoma shuleni ukatoka kapa! Acid kwa Kiswahili ni tindikali!

Dr. Sebi anasema tindikali huongeza sumu mwilini na kusababisha kansa pamoja na figo na ini kufail, magonjwa yanayotukimbiza sana majira haya. Figo ikifail, inabidi uchague kuitoa au kusafisha damu kwa kutumia mashine ya dialysis machine. Gharama yake shilingi laki tatu kila masaa kadhaa unayosafishwa. Unatakiwa usafishwe walau mara nne kwa wiki,hapo unazungumzia milioni moja na ushehe.

Sasa kama panado ya mia mbili inakutoa jasho, hiyo milioni si ndo msiba wa ukoo? Nani anakula hizo pesa? Ni wale waliomuua Dr. Sebi kwa sababu ndo wenye hizo mashine! Hiyo ni figo, bado sijazungumzia biashara, biashara inayowaingizia mabepari zaidi ya dola bilioni 150 kwa mwaka sawa na bajeti ya Tanzania kwa miaka 10. Nani anakula pesa hiyo? Mabepari waliomuua Dr. Sebi! Hii maana yake nini? Maana yake ni kwamba tiba ya Dr. Sebi ingeingia sokoni, mabepari wangepoteza bilioni 150 kwa kila mwaka.

Katika ulimwengu wa kibepari kuugua ni faida, kufa ni hasara, ndo màana watafanya juu chini wagonjwa wanaendelea kusogeza siku kwa kununua dawa, kununua ARV, kupiga mionzi, kumeza panado na action ili kutuliza kichwa na si kuponya kichwa! Kuna watu wanadhani ARV zinatolewa bure, thubutu. Unadhani hili deni la Afrika linalokuwa kila siku linatoka wapi? Uliishaambiwa no free lunch in Marica lakini bado huelewi siasa za misaada. Chukua mudu ukamsome Dambisa Moyo ili uniache niendelee na habari za huyu mwamba!

Dr. Sebi alitaja orodha ndefu ya vyakula vyenye acid uvikimbie na vile vyenye alkaline uvimbilie. Nyama zote ukitoa kuku wa kienyeji na kitimoto ni acid tupu, kimbia haraka sana. Hata kitimoto Dr. Sebi anashauri usile kwa sababu kina minyoo mingi ambayo ikiingia mwilini inakimbilia kula ubongo na kuathiri uwezo wa kufikiri. Hapa nadhani Daktari anatafuta ugomvi aisee! Unamwabiaje Mh. Sugu aache kula kitimoto yenye mafuta?

Vyakula vingine vyenye acid ni maharagwe, sukari, miwa, mafuta ya kupikia, mahindi makavu, soda, maziwa, pombe zote, ngano, maji ya viwandani, mayai, mtindi, mlonge. Dr. Sebi bwana, mbona hivi ndo vyakula vya kila siku kwa watanzania toka enzi hizo? Jamaa mmoja aliposikia masomo ya Sebi alisema "Mnataka tushinde njaa sasa!" Mwingine akasema, “Nakunywa maji ya Betri sembuse kutafuna Miwa!”

Unajua hakuna kitu kigumu kama kubadilisha tabia. Imagine burudani yako ni nyama choma nusu kilo yenye mafutafuta, ugali, kachumbari na bia baridi unamwambia chakula hicho ni sumu atakuelewa? Hawezi kukuelewa kabisa hadi akipata tezi dume. Dr. Sebi anasema ugali wa dona haufai kabisa usile. Niliwahi kusoma pahali kwamba ugali haufai kwa sababu waulao hudumaza akilo zao. Au ndo maana panya anakula mbegu tu?Dr. Sebi anasema ugali unapoingia mwilini hugeuka na kuwa sukari ambayo baadaye huweza kusababisha ugonjwa wa kisukari.

Unaanza kumwambia mama Rehema pilau nyama ni sumu kwa sababu huzalisha acidi atakuelewa? Huyu hawezi kukuelewa hadi apate kansa ya shingo ya uzazi.Umwambie Masai nyama nyekundu ni sumu atakuacha salama? Hasira zake sizitakuishia? Marastafarian wanasema nyama inasabaisha hasira ndo maana jamii zenye wala nyama wana hasira za haraka.Dr. Sebi anasema hata huu mlonge tunaojidaia haufai kabisa kwa sababu ni acid tu.

Dr. Sebi anasema ulaji wa vyakula hivyo vyenye tindikali hutengeneza vikamasi flani hivi vyenye sumu wazungu wanaviita toxic mucus, sasa hivyo vidude vikizidi kwenye broanchits tubes huzalisha ugonjwa wa bronchitis; vikizidi kwenye mapafu hupelekea nimonia, vikiwa kwenye pancreatic duct hupelekea kisukari, vikizidi kwenye mapingili ya mwili husabaisha mgongo kuuma, vikizidi kwenye retina retina husababisha upofu, vikizidi kwenye thyroid gland husababisha kansa ya koo, yaani vikizidi sehemu yoyote ya mwilini husababisha magonjwa.

Habari njema za utabibu wa Dr. Sebi zikaanza kuwafikia watu wengi duniani. Daktari akaamua kuhamishia huduma yake Marekani, huko akawatibu hadi mastaa wakubwa duniani kama Lisa Lopes, Steven Seagal, John Travolta, Eddie Murphy na Michael Jackson, shuhuda za uponyaji zikazidi kupasua mawimbi, Sebi akaamua kutangaza kabisa huduma yake kwenye gazeti, mwaka 1987 akashitakiwa kwa kuendesha biashara ya tiba bila leseni ya udaktari, wakamtaka kuthibitisha kwa kuonyesha mtu mmoja aliyepona kwa kila ungonjwa, Sebi akaleta watu 77, akashinda kesi, ikawa ni sawa na kumpiga teke chura, maana ilimpa umaarufu na kesi hiyo ndo ikawa ushuhuda wa kuvuna wateja wengi zaidi.

Dr. Sebi akaendelea kung’ara katika tiba za kibabe, kutibu ngoma, kansa, kisukari na uchizi siyo utaalamu wa kitoto. Sebi anakwambia hata ukimwi ni zengwe tu, anasema kwa akili ya kawaida virusi vya ukimwi haviwezi kusababisha ukimwi, hoja ambayo Rais Thambo Mbeki wa Afrika Kusini aliishikilia bango na kupiga marufuku matumizi ya ARV nchini kwake, mataifa ya magharibi yakamuandama hadi kupoteza urais wake.

Mbeki aliwataangazia wananchi wake kutumia malimao, magimbi, vitunguu saumu na mafuta ya mzeituni kutibu UKIMWI. Mbeki alisema ARV ni ‘sumu’ na ni bidhaa zilizokubaliwa na makampuni ya madawa kutika nchi za Magharibi. Mbeki anakwambia virusi haviwezi kusababisha upungufu wa kinga. Mbeki akalaumiwa kusababisha takribani vifo 365,000 vya wagonjwa wa UKIMWI. Mbeki akasema hizo ni hila za wazungu kutugeuza soko la ARV, wanashupaliaje ukimwi ati unaua sana na wakati ni ugonjwa wa tisa kuua? Mbona hatusikii chochote kuhusu kifua kikuu kinachoongoza kwa kuua?

Mbeki anasema ili mtu asipate huo upungufu wa kinga mwilini inabidi ale vizuri, afanye mazoezi na atibiwe ugonjwa wowote alionao hadi upone kabisa, iwe T.B, iwe kuhara, iwe infection au chochote kile; lakini makampuni yalimwambia watu wasifanye hivyo, wapewe ARV,na ukishazitumia, ukiacha utaumwa hadi kufa.

Lakini ukimsikiliza Thambo na Sebi kuna hoja! Toka lini upungufu wa kinga mwilini ukaambukizwa? Sasa kama kinga imeshuka siule vyakula vya kupandisha? Kwa nini ule dawa maisha? Hivi mimi niwe na upungufu wangu wa kinga ya mwili kwa kuwa nazembea kula vizuri nikamwambukize mpenzi wangu ambaye anayekula vizuri na kufuata taratibu zote za afya? Utapiamlo wangu unaambukizwaje kwako? Huoni kama huo siyo ukimwi ila una jina lingine ambalo limefichwa ili waendelee kupiga pesa?

Magonjwa mengi virus wake huonekana maabara huyu kirusi gani hajawahi kuonekana? Hapo ndo huwa nasema bado tuna kibarua cha kufikiri sana ili kwenda sambamba na mabeberu. Tukizama kwenye tafiti, majibu yake yanaweza kutushangaza! Wakati tukiendelea kutumia ARV serikali zote za Afrika zielekeze pesa kwenye tafiti!

Dr. Sebi alianza na tafiti akapata majibu ya tatizo akayafanyia kazi, huku kwetu, wasomi wanafanya tafiti, wanapata majibu na kuyafungia makabatini! Tembelea vyuo vikuu vyetu uone, huko kuna hadi tafiti za kutengeneza ndege, zinakula vumbi! Kituo chake cha utafiti alikiita USHA Research Institute, kilikuwa katika kijiji cha Usha.

Mei 28, 2006 alikamatwa na kosa la utakatishaji pesa baada ya kumkamata na dola 37,000 mkononi bila maelezo kazipata wapi huku wakijua kabisa alikuwa anaingiza dola 3,000 kwa siku. Alikuwa anasafirisha mapesa hayo kutoka Marekani kwenda Honduras kwa private jet. Wakati familia yake ikifanya harakati za kumtoa, Dr. Sebi alifia huko jela, wakasema amekufa kwa nimonia wakiwa njia kwenda hospitali. Alikufa 6 August 2016!

Dr Sebi anakwambia chakula ndo tiba, vingine ni usanii tu! Anasema Mungu alipotuleta hapa duniani alituwekea na vyakula vyote vinavyotibu magonjwa yetu. Ni aina ya ulaji wetu ndiyo unafanya sisi kuandamwa na magonjwa.

“Eat to live or eat to die!” Dr Sebi anashauri unywaji wa galoni moja ya maji kwa siku kama njia nzuri ya kutoa takata taka zilizomo mwilini. Chai na kahawa ni sumu kubwa katika mwili, kama vipi piga zako mchaichai au maji tu inatosha! Halafu jitahidi pia kula matunda kulingana na msimu, Mungu hakuwa mjinga kukuletea maembe disemba na zabibu kiangazi. Kula tunda nje ya msimu wake kuna changamoto pia. Tikiti linalopatikana mwaka mzima linaweza kuwa hatari kwa afya!

Anashauri mfungo wa maji, “water fasting”. Yeye anasema alifunga kwa miezi mitatu akinywa maji tu, akapona mazima. Dr. Sebi pamoja na uzee wake wote, amewahi kufanya interview kwa masaa mawili bila kukohoa wala kusafisha koo kwa kutoa sauti flani hivi kama tufanyavyo wengi, ule ni ugonjwa brother, kuna mwingine kila akicheka lazima akohoe! Mfungo ni tiba ndo maana dini zote zinasisitiza maombi ya kufunga na kuomba!

Lengo siyo kwenda mbinguni, lengo ni kuendelea kuwa na afya ya kumtumikia Mungu. Mwenzangu unakula mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka hilo tumbo linapumzika lini? Linapumzishwa gari sembuse tumbo? Pumzisha tumbo lako brother hata mara moja kwa wiki.Water fasting inaondoa sumu mwilini! Chupa mbili za maji kwa siku haziwezi kukushinda hata kama unatumia choo cha kulipia, piga maji, osha uchafu uliokotumboni, kutokunywa maji ni sawa na kulia kwenye vyombo vichafu.

Hata Hippocrates wa Kos, mtaalamu wa tiba kutoka Ugiriki aliwahi kusema “Your food your medicine and your medicine your food” Sebi alikuwa anawaamsha watu watumie vyakula na matunda kama tiba badala ya kutumia vidonge vya sumu kama chakula. Kevin Trudeau ni moja kati ya wazungu waliomuelewa sana Dr. Sebi na kuandika kitabu kiitwacho, “Natural Cures "They" Don't Want You to Know About” kuonyesha jinsi mabeberu wanavyofaidika kutokana na magonjwa yetu. Mwandishi anasema chuo kikuu cha Calgary kiligundua tiba ya kisukali kwa kutumia mitishamba lakini wakaficha data kuogopa mkono wa pharmaceutical industry.

Tuwe makini na pharmaceutical industry kama mgonjwa nayetibiwa na mke wa muuza majeneza. Trudeau anakwambia kuna dawa za asili zinazotibu magonjwa yote lakini mababeru wanatumia nguvu kubwa kuhakikisha watu wanazipuuza ndo maana majina ya dawa na madaktari wa dawa zote za asili ni mabaya, mganga wa kienyeji, wapiga lamri, waganguzi.

Tutumie vyakula vyenye alikaline kwa bidii sana. Limao ni mfano wa vyakula vyenye tindikali nyingi ingawa wengi tunadhani lina acid. Limao ni msada mkubwa kwa ini kwani humsaidia ini kuondoa masumu mwilini, jenga urafiki na limao. Pata kiburudisho cha glass ya limao kila siku asubuhi ufurahie maisha. Tatizo wengi tunakula matunda au mboga za majani ‘kwa bahati mbaya’, siyo chakula muhimu sana.

“When an old man dies, a library burns to the ground.” – African proverb.
 
Mkuu hiyo Mei 28 2026 alikamatwa kwa kutakatisha pesa ni mwaka gani? Huo na wewe unasema alikufa 2016 🤔🤷
 
Kwenye tiba za mitishamba nimekuelewa, na hizo tiba ili zwe tiba, lazima awepo mgonjwa wa kutibiwa

Dr, anafundisha njia za kuepuka kuugua kabisa endapo zikifuatwa, Wakati huohuo anatibu magonjwa!

Halafu njia zake kuzifuata ni ngumu balaa!

Naunga mkono Kwa dawa za tiba Africa Mungu katujalia, ni Nzuri kutumia na hazina madhara na huponyesha kweli, Mzungu hajawahi kutengeneza dawa za kuponyesha zaidi ya kutuliza maumivu na kuzalisha shida nyingine badaye huku akijali zaidi kuvuna pesa
 
Waafrica wenyewe hatujiamini. So sad kuna watu wamekuwa brainwashed anawaona Wazungu watu wa maana hadi kuwatetea watuibie raslimali
Kuna mtu ananiambia kupitia taasisi yetu ya NIMR wamepewa masharti magumu tena kutokea WHO endapo wakitaka kufanya utafiti kuhusu hizi tiba mbadala. Mie kibinafsi nnaziamini sana tatzo lipo kwenye kuzipata zile zenye uhalisia, enzi zetu zile za wamasai zilikua zikisaidia sana lkn skuiz zimechakachuliwa.

Kuna dokta mmoja nlimuona wakat walipotoka Madagascar juzi kuleta chupa moja ya dawa aliongea vizuri sana kuhusu Tiba mbadala na alionekana mjuvi sana wa tiba asilia. Tatzo lipo kwetu wenyewe kwa NIMR na wapigaji binafsi.
 
Siku zote Mzungu haitatokea ampende mtu Mweusi akimpenda ujue wana ajenda nyuma ya pazia

Bahati mbaya tumepumbazwa kwa kudharau vya kwetu na kuamini upumbavu wao
Mtanzania akimuona mtu anauza traditional medicine anamdharau
Kuna mtu ananiambia kupitia taasisi yetu ya NIMR wamepewa masharti magumu tena kutokea WHO endapo wakitaka kufanya utafiti kuhusu hizi tiba mbadala. Mie kibinafsi nnaziamini sana tatzo lipo kwenye kuzipata zile zenye uhalisia, enzi zetu zile za wamasai zilikua zikisaidia sana lkn skuiz zimechakachuliwa. Kuna dokta mmoja nlimuona wakat walipotoka Madagascar juzi kuleta chupa moja ya dawa aliongea vizuri sana kuhusu Tiba mbadala na alionekana mjuvi sana wa tiba asilia. Tatzo lipo kwetu wenyewe kwa NIMR na wapigaji binafsi.
 
Waafrica wenyewe hatujiamini. So sad kuna watu wamekuwa brainwashed anawaona Wazungu watu wa maana hadi kuwatetea watuibie raslimali
Mbona KONDOMU, PEDI na DAWA ZA MALARIA mnapokea???

Kabudi kila siku anashinda kuwapigia magoti ili hata watukopeshe ila hapa unajifanya kichwa ngumu.

Hiyo ELFU SABA unayolipwa na Polepole ili kutetea U.HARO anaofanya mzee Meko ni sehemu ya msaada wa hao mabeberu!
 
Back
Top Bottom