Wazo Kebehi: Wangetaka Kutuua Wangetuacha na HIV/UKIMWI...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,998
Kuna watu wanatembea kwa afya na wameishi maisha marefu sababu ya Wamarekani. Wapo ambao kila mwezi au wiki kadhaa wanaenda kuchukua dawa za ARVs ili kujiongezea Kinga mwilini na kupiga vita magonjwa ambukizi mbalimbali.

Madawa na tiba hizi zimetoka kwa msaada wa watu wa Marekani (na mimi mmojawapo). Ingekuwa wanataka kutupunguza kwa haraka hakuna pazuri kama pale tupapendapo!! Jinsi masikini wetu wanavyopenda kula na kulana, kulala na kulaliana, kutafuna na kutafuniana; maelfu kama siyo mamilioni ya maskini Hawa wangekuwa wamepumzika ahera madukani siku nyingi.

Tuache ufyatu!! Waacheni wazazi au jamii wanaotaka watoto wao wale chakula cha msaada. Tulikula sisi miaka ya themanini na tunashukuru. Wazazi au jamii wasiotaka kula wasilazimishwe. Wazazi wawakataze watoto kula chakula Nicholas. Lakini kuwanyima watoto na wazazi wengine wasio na tatizo na vyakula hivi ni ufyatu . Tukifika mahali kweli tu tunajitegemea kwa chakula tunaweza kukataa kwa sababu ya kutokujiabisha. Sasa hivi msemo wa wahenga "mwenye njaa hana haramu" una ukweli wake.

Nashauri serikali iache hamaki, itulie na kufikiria tena a more balanced approach. Tusiwe wote hamnazo.
 
Kuna watu wanatembea kwa afya na wameishi maisha marefu sababu ya Wamarekani. Wapo ambao kila mwezi au wiki kadhaa wanaenda kuchukua dawa za ARVs ili kujiongezea Kinga mwilini na kupiga vita magonjwa ambukizi mbalimbali....
Tulikula njano iwe leo hii!ni wajinga wachache tu ndio wenye mawazo mgando kama hayo.kwani Marekani akitaka kutumia si ni dakika chache kwa umaskini huu.mbona gaza wanapanga foleni kugombea hicho chakula kwa hiyo wao ni wajinga
 
Kuna watu akili zao wanazijua wenyewe.

Madawa mengi ya Cancer, Kifua kikuu na chanjo zote zinatoka hukp. Hizo ndiyo njia rahisi kudhuru watu .... lakini watu wanakubali ili wapone. Kwenye chakula wanajifanya wazalendo wakati watoto wa watu wanakufa na njaa ... inaelekea kuna watu hawajui hali ya utapia mlo kwa watoto wa Tanzania. The statistics are not good.

For the first time nimemdharau Bashe kwa kupoliticize hii issue.
 
Saa nyingine huwa hata naona aibu baadhi ya mambo, unagomea mchele tani kadhaa. Kisha watoto wa nchi nzima huko mashuleni na hospital wanapewa chanjo kwa hisani uliyekataa mchele wake?
 
Kuna watu akili zao wanazijua wenyewe.

Madawa mengi ya Cancer, Kifua kikuu na chanjo zote zinatoka hukp. Hizo ndiyo njia rahisi kudhuru watu .... lakini watu wanakubali ili wapone. Kwenye chakula wanajifanya wazalendo wakati watoto wa watu wanakufa na njaa ... inaelekea kuna watu hawajui hali ya utapia mlo kwa watoto wa Tanzania. The statistics are not good.

For the first time nimemdharau Bashe kwa kupoliticize hii issue.
Pressure za Mitandaoni zimemchanganya Hadi anajifunga.
 
Kuna watu wanatembea kwa afya na wameishi maisha marefu sababu ya Wamarekani. Wapo ambao kila mwezi au wiki kadhaa wanaenda kuchukua dawa za ARVs ili kujiongezea Kinga mwilini na kupiga vita magonjwa ambukizi mbalimbali.
Kwakweli ni uwendawazimu kabisa ule.

Wakitutaka ni sekunde tu...hata hizi soda nyingi formula na ingredients zake si zinatoka Merekani jamani?
Sisi tunazihakiki kwa vipimo kutoka Namanyere Sumbawanga?
 
Kuna watu wanatembea kwa afya na wameishi maisha marefu sababu ya Wamarekani. Wapo ambao kila mwezi au wiki kadhaa wanaenda kuchukua dawa za ARVs ili kujiongezea Kinga mwilini na kupiga vita magonjwa ambukizi mbalimbali.

Madawa na tiba hizi zimetoka kwa msaada wa watu wa Marekani (na mimi mmojawapo). Ingekuwa wanataka kutupunguza kwa haraka hakuna pazuri kama pale tupapendapo!! Jinsi masikini wetu wanavyopenda kula na kulana, kulala na kulaliana, kutafuna na kutafuniana; maelfu kama siyo mamilioni ya maskini Hawa wangekuwa wamepumzika ahera madukani siku nyingi.

Tuache ufyatu!! Waacheni wazazi au jamii wanaotaka watoto wao wale chakula cha msaada. Tulikula sisi miaka ya themanini na tunashukuru. Wazazi au jamii wasiotaka kula wasilazimishwe. Wazazi wawakataze watoto kula chakula Nicholas. Lakini kuwanyima watoto na wazazi wengine wasio na tatizo na vyakula hivi ni ufyatu . Tukifika mahali kweli tu tunajitegemea kwa chakula tunaweza kukataa kwa sababu ya kutokujiabisha. Sasa hivi msemo wa wahenga "mwenye njaa hana haramu" una ukweli wake.

Nashauri serikali iache hamaki, itulie na kufikiria tena a more balanced approach. Tusiwe note hamnazo.
Mkuu viongozi wetu wa CCM na Serikali wana matatizo, wanapenda tu misaada ya fedha.
 
Issue ni kuwepo kwake au watu kuyapata ? Yapo sababu hayanunuliwi sababu watu hawana pesa ya kuyanunua kila mtu angenunua basi yasingetosha...

Unaweza kusema kwanini wasitupe pesa.., Jibu ni kwamba kule kuna surplus (wakulima wamepewa ruzuku hivyo kuna ziada..., sasa ziada iende wapi)? Yaani ziada waitupe ili wewe wakupe pesa usiwe na ziada na wenyewe ziada yao itupwe ?

Mwisho kabisa kuna watu kule wana charities ni either watoe pesa zao kwenye charity fulani au hio pesa yao walipe Kodi..., Kwahio kuwa na hizi charities kwao wanapata publicity kwa bei nafuu (hivyo kwa hesabu zao msaada kama huu ambao wana uhakika watu watakula na sio wachache kula pesa) unawasaidia zaidi...

By the way beggars are not choosers.., na sera mbovu za watunga sera zimepelekea watu kutokuwa na pesa ya basic needs..., Hivyo Yes we are Beggars.....
 
mjomba ni bora kufa na ukwimi lkn una sifa ya dume la mbegu kwanza hakuna wakubaki milele kuliko kuletewa michele itakayopelekea vijana kuwa mchelemchele
Kwahio wewe kuna chakula ukila unakuwa Shoga ? Yaani unaamini kabisa hayo kwamba una element za ushoga ambazo zinakuwa triggered na Chakula ?

Kweli tunahitaji msaada zaidi upstairs....
 
Tulikula njano iwe leo hii!ni wajinga wachache tu ndio wenye mawazo mgando kama hayo.kwani Marekani akitaka kutumia si ni dakika chache kwa umaskini huu.mbona gaza wanapanga foleni kugombea hicho chakula kwa hiyo wao ni wajinga
Njano naikumbuka ilikuwa noma sana
 
Back
Top Bottom