palalisote
JF-Expert Member
- Aug 4, 2010
- 8,335
- 1,455
Daktari (PhD) wa ukweli amemjibu Mukama kuwa wananchi wanauezo kikatiba wa kumuondoa JK madarakani kabla ya 2015. Ibara ya 146 ya Sheria ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1982, inasema wananchi ndio wenye mamlaka yote ya kumweka mwenyekiti wa serikali ya mtaa au kijiji na ndiyo wenye mamlaka ya kumwondoa wakati wowote kwa kupiga kura ya maoni.
Wakitaka hata kabla ya kipindi rasmi cha uchaguzi kufika....kwa hiyo kama ni halali kwa ngazi ya kijiji basi ni halali pia kwa ngazi ya urais kama wananchi wenyewe walio wengi wakiamua kufupisha muda wa serikali yao, alisema Dk. Slaa.
Kauli hiyo ya Dk. Slaa, imekuja siku chache baada ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama, kusema kuwa Rais Kikwete hawezi kungolewa kabla ya mwaka 2015 na kusisitiza kuwa kufanya hivyo ni uhaini.
CHANZO: GAZETI LA TANZANIA DAIMA
Wakitaka hata kabla ya kipindi rasmi cha uchaguzi kufika....kwa hiyo kama ni halali kwa ngazi ya kijiji basi ni halali pia kwa ngazi ya urais kama wananchi wenyewe walio wengi wakiamua kufupisha muda wa serikali yao, alisema Dk. Slaa.
Kauli hiyo ya Dk. Slaa, imekuja siku chache baada ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama, kusema kuwa Rais Kikwete hawezi kungolewa kabla ya mwaka 2015 na kusisitiza kuwa kufanya hivyo ni uhaini.
CHANZO: GAZETI LA TANZANIA DAIMA