Dk. Slaa: Si uhaini kumng'oa rais Kikwete kabla ya 2015

palalisote

JF-Expert Member
Aug 4, 2010
8,335
1,455
Daktari (PhD) wa ukweli amemjibu Mukama kuwa wananchi wanauezo kikatiba wa kumuondoa JK madarakani kabla ya 2015. “Ibara ya 146 ya Sheria ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1982, inasema wananchi ndio wenye mamlaka yote ya kumweka mwenyekiti wa serikali ya mtaa au kijiji na ndiyo wenye mamlaka ya kumwondoa wakati wowote kwa kupiga kura ya maoni.

“Wakitaka hata kabla ya kipindi rasmi cha uchaguzi kufika....kwa hiyo kama ni halali kwa ngazi ya kijiji basi ni halali pia kwa ngazi ya urais kama wananchi wenyewe walio wengi wakiamua kufupisha muda wa serikali yao,” alisema Dk. Slaa.

Kauli hiyo ya Dk. Slaa, imekuja siku chache baada ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama, kusema kuwa Rais Kikwete hawezi kung’olewa kabla ya mwaka 2015 na kusisitiza kuwa kufanya hivyo ni uhaini.

CHANZO: GAZETI LA TANZANIA DAIMA
 
Tafsiri aliyotumia Dr nyepesi sana haiendani na hadhi yake
Hata hivyo kuna "kuweza kumtoa" na kuna sheria pia imetamka bayana kuwa ni uhaini
 
Hiyo ndiyo Sheria aliyosoma dr slaa bora akagombee uenyekiti wa kijiji huko kwao Karatu kwa urais anadhihirisha kua hatoshi.ndiyo maana alishindwa kusimamia. canon law akafukuzwa upadri!
 
Hiyo ndiyo Sheria aliyosoma dr slaa bora akagombee uenyekiti wa kijiji huko kwao Karatu kwa urais anadhihirisha kua hatoshi.ndiyo maana alishindwa kusimamia. canon law akafukuzwa upadri!
Na wewe pia unajiona great thinker, eeh?
 
Duh shame on him! Mwenyekiti wa Kijiji anaweza kushtakiwa yaani hana kinga, kwahiyo na rais ni hivyohivyo! Kuongea sn wakati fulani ni kutafuta kuonekana mjinga. Hivi kuna clip ya hii kitu?
 
labda tuanze na maana ya uhaini

Uhaini ni pale mtu anapotenda jambo dhidi ya nchi yake. Kwa mfano, mtu anaweza kuisaidia nchi nyingine ipigane vita dhidi ya nchi yake kwa kuwaambia habari za siri. Uhaini ni neno la kawaida, lakini nchi tofauti zina sheria tofauti na adhabu dhidi ya matendo ya kihaini.
Neno la mtu anayefanya uhaini ni msaliti. Miongoni mwa wasaliti maarufu duniani ni pamoja na Yuda, Benedict Arnold, Pétain na Quisling.

SASA USALITI HUKO WAPI? DR SLAA NI MWANASIASA ANAYETUMIA NGUVU YA WANANCHI KUMTOA RAISI WASIYEMTAKA HUKO WAPI USALITI(UHAINI) HAPO,? Kwa tafusili hii ya usaliti (uhaini) ni kiongozi gani msaliti hapa nchini kwa kuwalaghai wananchi?

kale watu walifungwa kwa kubebeshwa kesi nzito kama hizi lakini sasa ni wakati wa WELEDI mwanasiasa anayetumia majukwaa kamwe awezi kuwa muhaini maana hakuna anachofanya kasiri, sio kila mapinduzi ya serikali ni uhaini kama wamefanywa kwa nguvu ya umma kamwe sio uhaini.

huu ni ujanja wa ccm kudanganya umma wasinge muacha Dr slaa kutembea huru na kesi ya kihaini halafu Arusha wamfungulie kesi ya uchochezi, mimi ni hakika kama kungekuwa na uhaini angekuwa UKONGA aU segere zamani sana kama kuna mtu anatafuli tofauti ya uhaini amwage hapa.
 
Daktari (PhD) wa ukweli amemjibu Mukama kuwa wananchi wanauezo kikatiba wa kumuondoa JK madarakani kabla ya 2015. "Ibara ya 146 ya Sheria ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1982, inasema wananchi ndio wenye mamlaka yote ya kumweka mwenyekiti wa serikali ya mtaa au kijiji na ndiyo wenye mamlaka ya kumwondoa wakati wowote kwa kupiga kura ya maoni.

"Wakitaka hata kabla ya kipindi rasmi cha uchaguzi kufika....kwa hiyo kama ni halali kwa ngazi ya kijiji basi ni halali pia kwa ngazi ya urais kama wananchi wenyewe walio wengi wakiamua kufupisha muda wa serikali yao," alisema Dk. Slaa.

Kauli hiyo ya Dk. Slaa, imekuja siku chache baada ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama, kusema kuwa Rais Kikwete hawezi kung'olewa kabla ya mwaka 2015 na kusisitiza kuwa kufanya hivyo ni uhaini.

CHANZO: GAZETI LA TANZANIA DAIMA

Te hehe he! Mengi tutayaona! Hivi CHADEMA wanalilia serikali za Mitaa?
 
labda tuanze na maana ya uhaini

Uhaini ni pale mtu anapotenda jambo dhidi ya nchi yake. Kwa mfano, mtu anaweza kuisaidia nchi nyingine ipigane vita dhidi ya nchi yake kwa kuwaambia habari za siri. Uhaini ni neno la kawaida, lakini nchi tofauti zina sheria tofauti na adhabu dhidi ya matendo ya kihaini.
Neno la mtu anayefanya uhaini ni msaliti. Miongoni mwa wasaliti maarufu duniani ni pamoja na Yuda, Benedict Arnold, Pétain na Quisling.

SASA USALITI HUKO WAPI? DR SLAA NI MWANASIASA ANAYETUMIA NGUVU YA WANANCHI KUMTOA RAISI WASIYEMTAKA HUKO WAPI USALITI(UHAINI) HAPO,? Kwa tafusili hii ya usaliti (uhaini) ni kiongozi gani msaliti hapa nchini kwa kuwalaghai wananchi?

kale watu walifungwa kwa kubebeshwa kesi nzito kama hizi lakini sasa ni wakati wa WELEDI mwanasiasa anayetumia majukwaa kamwe awezi kuwa muhaini maana hakuna anachofanya kasiri, sio kila mapinduzi ya serikali ni uhaini kama wamefanywa kwa nguvu ya umma kamwe sio uhaini.

huu ni ujanja wa ccm kudanganya umma wasinge muacha Dr slaa kutembea huru na kesi ya kihaini halafu Arusha wamfungulie kesi ya uchochezi, mimi ni hakika kama kungekuwa na uhaini angekuwa UKONGA aU segere zamani sana kama kuna mtu anatafuli tofauti ya uhaini amwage hapa.
Kwako wewe demokrasia ni nini? Na nini maana ya chaguzi? Hizi kelele zinapoteza lengo sasa na hatimaye hata ile maana ya sensitisation inaondoka.

Hivi kwanini kelele hizi zisipigwe kwenye katiba? Au kwanini nafasi hii na hizo rasilimali chache wangewekeza kwenye majimbo? Maana hii ni njia rahisi kujulikana kuwa chama kinataka kufanya nn kuliko sasa hivi msisitizo umekuwa ni vurugu.
 
Kama kweli Dr Slaa kasema hivi,basi atakuwa amechemka na kajishushia hadhi.Mfano wa Rais na Mwnyekiti wa Kijiji wapi na wapi?
 
Hiyo ndiyo Sheria aliyosoma dr slaa bora akagombee uenyekiti wa kijiji huko kwao Karatu kwa urais anadhihirisha kua hatoshi.ndiyo maana alishindwa kusimamia. canon law akafukuzwa upadri!
Walewale wa hoja za kopo la kuchambia.
 
labda tuanze na maana ya uhaini

Uhaini ni pale mtu anapotenda jambo dhidi ya nchi yake. Kwa mfano, mtu anaweza kuisaidia nchi nyingine ipigane vita dhidi ya nchi yake kwa kuwaambia habari za siri. Uhaini ni neno la kawaida, lakini nchi tofauti zina sheria tofauti na adhabu dhidi ya matendo ya kihaini.
Neno la mtu anayefanya uhaini ni msaliti. Miongoni mwa wasaliti maarufu duniani ni pamoja na Yuda, Benedict Arnold, Pétain na Quisling.

SASA USALITI HUKO WAPI? DR SLAA NI MWANASIASA ANAYETUMIA NGUVU YA WANANCHI KUMTOA RAISI WASIYEMTAKA HUKO WAPI USALITI(UHAINI) HAPO,? Kwa tafusili hii ya usaliti (uhaini) ni kiongozi gani msaliti hapa nchini kwa kuwalaghai wananchi?

kale watu walifungwa kwa kubebeshwa kesi nzito kama hizi lakini sasa ni wakati wa WELEDI mwanasiasa anayetumia majukwaa kamwe awezi kuwa muhaini maana hakuna anachofanya kasiri, sio kila mapinduzi ya serikali ni uhaini kama wamefanywa kwa nguvu ya umma kamwe sio uhaini.

huu ni ujanja wa ccm kudanganya umma wasinge muacha Dr slaa kutembea huru na kesi ya kihaini halafu Arusha wamfungulie kesi ya uchochezi, mimi ni hakika kama kungekuwa na uhaini angekuwa UKONGA aU segere zamani sana kama kuna mtu anatafuli tofauti ya uhaini amwage hapa.

Tanzania si kigenge cha wahuni! Wananchi wa Tanzania msiwafanye waovyo! Ni miezi sita tu nyuma walipewa hiyari na kumchaguwa waliemuona anawafaa. Walipofanya hivyo walikuwa wakijuwa kwa hakika kuwa watakuwa nae kwa kipindi cha miaka mitano!

Hivyo hiki kipindi cha miezi sita kimeshatowa jawabu kuwa walikosea? na kipi kilichofanywa na CHADEMA cha kuwafanya wahisi walikosea kutokichagua?
 
Dr. Slaa ametumia mantiki na si ngumu kuelewa; kama Mwenyekiti wa Mtaa amechaguliwa na anaweza kuondolewa na wananchi wake waliomchagua kabla ya muda wake (wakifuata taratibu zilizopo) basi yawezekana kabisa kumuondoa Rais aliyeko madarakani kabla ya muda wake kwa kufuata taratibu zilizopo. Hili haliitaji uanasayansi kulielewa vinginevyo tusingekuwa na vipengele vya impeachment au sheria inayoruhusu mtu akivuliwa uanachama wake anapoteza haki ya kuwa Mbunge au Rais.
 
Duh shame on him! Mwenyekiti wa Kijiji anaweza kushtakiwa yaani hana kinga, kwahiyo na rais ni hivyohivyo! Kuongea sn wakati fulani ni kutafuta kuonekana mjinga. Hivi kuna clip ya hii kitu?

Anfaal, rais anaweza kuondolewa madarakani kabla ya kikomo cha muda wake. Hili haliitaji ugenius wowote kuliona. Kinga ya rais haimzuii kuondolewa na Bunge au kulazimishwa kujiuzulu kabla ya muda wake. Wananchi kwa mfano wakiamua kumshinikiza ajiuzulu Rais atajiuzulu na Makamu wake atachukua nafasi yake. Kama serikali nzima inaonekana imepoteza uhalali wake basi Bunge zima linaweza kujiuzulu na Uchaguzi Mkuu mpya ukaitishwa ndani ya siku 90. Hakuna alichokisema Slaa ambacho ni nje ya uwezekano wa kinadharia au kisheria.

Rais amefanya ile ile syllogism ambayo niliitumia kwenye ile mada nyingine; kama inawezakana wananchi (ambao ndio asili ya madaraka) kumuondoa kiongozi wao waliyemchagua wao wenyewe kwenye mtaa ina maana inawezekana wananchi wa nchi nzima wanaweza kumuondoa Rais wao. Hivi ndivyo ilivyokuwa Tunisia, Misri, Ukraine au hata nchi nyingine ambapo wananchi walitumia madaraka yao ya kutawala kumuondoa mtu waliyemkasimisha madaraka hayo.
 
Back
Top Bottom