Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,741
- 218,329
Taarifa kutoka kwa Phillipo Mwakilima Wakili wa Watuhumiwa wa Uhaini , inaeleza kwamba zaidi ya Mawakili 100 wamejitokeza kumtetea Dkt. Slaa na wenzake kwenye kesi ya uhaini inayowakabili.
Tayari wengine wamekwishaanza kuripoti Mkoani Mbeya kwa ajili hiyo .
---
Zaidi ya mawakili 100 kutoka taasisi mbalimbali ikiwemo TLS wanatarajia kuungana na mawakili watatu kumtetea Balozi Dk Willibrod Slaa na wenzake wawili katika kesi ya uahaini wanayotuhumiwa nayo.
Akizungumza nje ya Mahakama Wakili Philip Mwakilima anayewatetea Wakili Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali amesema mawakili hao wameshaanza kuwasili Jijini Mbeya kwa ajili ya kesi hiyo.
Hata hivyo watuhumiwa hao wanaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya ikiwa ni siku ya nne bila kufikishwa mahakamani kwa kesi ya uhaini wanayotuhumiwa nayo.
Mwakilima amesema kwa mujibu wa sheria watuhumiwa walipaswa kufikishwa mahakamani leo lakini hawajafikishwa na wanakusudia kufungua kesi kwa lengo la kuiomba Mahakama imlazinishe Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwafikisha mahakamani au kuwaachilia endapo watabaki wakiwashikilia.
Tayari wengine wamekwishaanza kuripoti Mkoani Mbeya kwa ajili hiyo .
---
Akizungumza nje ya Mahakama Wakili Philip Mwakilima anayewatetea Wakili Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali amesema mawakili hao wameshaanza kuwasili Jijini Mbeya kwa ajili ya kesi hiyo.
Hata hivyo watuhumiwa hao wanaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya ikiwa ni siku ya nne bila kufikishwa mahakamani kwa kesi ya uhaini wanayotuhumiwa nayo.
Mwakilima amesema kwa mujibu wa sheria watuhumiwa walipaswa kufikishwa mahakamani leo lakini hawajafikishwa na wanakusudia kufungua kesi kwa lengo la kuiomba Mahakama imlazinishe Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwafikisha mahakamani au kuwaachilia endapo watabaki wakiwashikilia.