Mbeya: Zaidi ya Mawakili 100 wamejitokeza kuwatetea Dkt Slaa na Wenzake

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,741
218,329
Taarifa kutoka kwa Phillipo Mwakilima Wakili wa Watuhumiwa wa Uhaini , inaeleza kwamba zaidi ya Mawakili 100 wamejitokeza kumtetea Dkt. Slaa na wenzake kwenye kesi ya uhaini inayowakabili.

Tayari wengine wamekwishaanza kuripoti Mkoani Mbeya kwa ajili hiyo .

---

Zaidi ya mawakili 100 kutoka taasisi mbalimbali ikiwemo TLS wanatarajia kuungana na mawakili watatu kumtetea Balozi Dk Willibrod Slaa na wenzake wawili katika kesi ya uahaini wanayotuhumiwa nayo.

Akizungumza nje ya Mahakama Wakili Philip Mwakilima anayewatetea Wakili Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali amesema mawakili hao wameshaanza kuwasili Jijini Mbeya kwa ajili ya kesi hiyo.

Hata hivyo watuhumiwa hao wanaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya ikiwa ni siku ya nne bila kufikishwa mahakamani kwa kesi ya uhaini wanayotuhumiwa nayo.

Mwakilima amesema kwa mujibu wa sheria watuhumiwa walipaswa kufikishwa mahakamani leo lakini hawajafikishwa na wanakusudia kufungua kesi kwa lengo la kuiomba Mahakama imlazinishe Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwafikisha mahakamani au kuwaachilia endapo watabaki wakiwashikilia.
 
Screenshot_20230816-130532.jpg

Afu uzuri neno lenyewe limetoka huko huko arabuni
 
Taarifa kutoka kwa Phillipo Mwakilima Wakili wa Watuhumiwa wa Uhaini , inaeleza kwamba zaidi ya Mawakili 100 wamejitokeza kumtetea Dr Slaa na wenzake , kwenye kesi ya uongo ya uhaini waliyobambikwa na serikali ya Tanzania , baada ya kujitokeza kupinga mkataba wa milele wa Bandari za Tanganyika .

Tayari wengine wamekwishaanza kuripoti Mkoani Mbeya kwa ajili hiyo .

View attachment 2719051
Great news
 
Taarifa kutoka kwa Phillipo Mwakilima Wakili wa Watuhumiwa wa Uhaini , inaeleza kwamba zaidi ya Mawakili 100 wamejitokeza kumtetea Dr Slaa na wenzake , kwenye kesi ya uongo ya uhaini waliyobambikwa na serikali ya Tanzania , baada ya kujitokeza kupinga mkataba wa milele wa Bandari za Tanganyika .

Tayari wengine wamekwishaanza kuripoti Mkoani Mbeya kwa ajili hiyo .

View attachment 2719051
Copy: TLS

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom