Diversity in Tanzania: Where are the Asian, Arab, European-Tanzanians?

Ku generalize "Asians" na kuwaweka kundi moja nadhani si busara. Kwani mada inafananisha na wa Tanzania. Ikiwa tu tutafananisha "Africans" basi hapo ndio tufananishe Asians au Europeans na kadhalika. Si vyema kuifananisha au kufananisha wa Tanzania na watu wa Bara zima la Asia au Europe, haina mantiki.

Ikiwa nchi tu kama Tanzania, ina makabila na tabia, mila na hulka tofauti kwa karibu kila kabila, inakuwaje ufananishe na wa Asia? Ambao, kwa mfano mdogo tu, kuna wa China, wa Turuki, wa Hindi, wa Arabu, wa, wa, wa... Na kati ya hao kuna makabila tofauti, ambao wao kwa wao wanatofauti kubwa za kimila ki itikadi ki jamii na kadhalika.

Naona mtowa mada angetumia busara japo kidogo na kuanza kufananisha ki nchi na nchi na si kikontinenti na nchi.

Kwa ufupi tu, tumeshawahi kuona wa Tanzania wengi tu wenye asili ya kiarabu katika nyanja tofauti hapa Tanzania, na wengine ni maarufu sana. Na hali kadhalika kwa wa Tanzania wenye asili ya ki Hindi na ki Pakistan. Wenye asili ya ki Ingereza nao wapo lakini ni wachache sana, hali kadhalika kwa wenye asili za kigiriki, kijerumani.

Kwa hawa wa Tanzania wenye asili za nje ya bara la Afrika, utakuta ni wengi walioshika nyannja na nyadhifa mbali mbali katika Serikali kuliko wa Tanzania wenye asili za ki Afrika nje ya Tanzania.

Wengi wa waTanzania wenye asili ya ki Afrika nje ya Tanzania wako lakini, labda kwa kuogopa kubaguliwa hujichanganya na kujibandika makabila ya ki Tanzania na inakuwa vigumu kuwang'amuwa kwa urahisi kwa kuwa wengi wa waTanzania ni wenye asili ya kiAfrika.
 
wapenzi wa chadema wameanza kuitenga cuf kwa eneo walilotoka, dini, nchi, na mafanikio yao ya kisiasa, yaani chadema wamefika mahali wao ni superior, halafu then unataka waingie waasia, wazungu, na waarabu kwenye siasa zetu au serikalini!!! watadumu kweli na akili hizi kama za wanachadema?? nimetoa mfano tu!


Waberoya acha kuchemka janvini, unajua mgombea wa kiti cha ubunge wa chadema Kigoma kusini ni asili ya wapi? Fuatilia kaka na si ukurupuke.
 
People are still missing a point.. kwanini hadi hivi sasa hakuna mteuliwa yeyote (yawezekana yupo sijajua) wa Rais tangu wakati wa Mkapa na sasa Kikwete ambaye ni racial minority aliyeshika a high profile position katika serikali? Kuna aliyewahi kuteuliwa na Rais au Waziri akakataa nafasi yake kwa sababu yeye ni Mhindi au Muarabu au kwa sababu ya kidini yake?
 
Waasia walalahoi nimewaona sana nikiwa nasoma shule ya msingi miaka 1980s maeneo ya Upanga Dsm nyuma ya chuo cha CBE na Maktaba kuu ya Taifa, vibanda vyao vilikuwa kama vya Kibera Nairobi Slums, wakiwa hawana umeme wanapikia kuni na mkaa hapo jijini DSM.

Pia ktk shule za sekondari kuna waalimu wengi tu wa kihindi wenye asili ya Tanzania, mafundi makenika, mafundi umeme na airconditions, pia wanaendesha migahawa midogo ambayo naweza sema haina tofauti na biashara za 'mama ntilie'.

Miaka ya sasa tunaona wameshaanza kuhamia kama maeneo ya Msasani Mikoroshini DSM n.k , hii yote ni kwa kwenda na wakati, pia bongo flava muziki wanashiriki, wanauza au kuazimisha second hand comics books za Dennis the Menace, Beano, TinTin n.k Waliojenga ukuta mpya wa ngome wa Ikulu hapo DSM ni Nadhra Co. kampuni wa Watanzania wenye asili ya kiasia, madaktari, wanasheria, manesi Watanzania wenye asili ya kiasia wapo wengi tu hapo Bongo.

Mimi nafikiri ni suala la life experince ya Mwanakijiji kutofahamu hawa ndugu zetu wenye asili ya Kiasia hapa Tanzania wanaishije kufuatana na wakati na maeneo gani Tanzania, ni kama vile Mkurya wa Buhemba atake kumwona Mmakonde asilia hapo Buhemba ni changamoto kubwa hiyo.

Ila nafikiri ni kweli serikali ya Tanzania ya miaka hii kuna kila sababu ya kuwa angalau na waziri kamili mwenye asili ya kiasia ktk baraza la mawaziri. Mimi katika tembea yangu ulimwenguni nimekutana na Watanzania waasia wakiongea kiswahili baina yao wakiwa ughaibuni hii inadhihirisha Utanzania wao.

Mwisho tutaulizana kwa nini koronikoroni wa sasa mijini ni Wamasai tu au kwa nini Waasia hupendelea biashara, mimi nafikiri ni suala la wakati, maana zamani kama wadau walivyochangia walikuwapo mapolisi, askari, makarani wa kiasia na koronikoroni wa Kimakonde ambao sasa ni Machinga.
 
People are still missing a point.. kwanini hadi hivi sasa hakuna mteuliwa yeyote (yawezekana yupo sijajua) wa Rais tangu wakati wa Mkapa na sasa Kikwete ambaye ni racial minority aliyeshika a high profile position katika serikali? Kuna aliyewahi kuteuliwa na Rais au Waziri akakataa nafasi yake kwa sababu yeye ni Mhindi au Muarabu au kwa sababu ya kidini yake?

Unatuchanganya, sidhani kama Nyerere, Mkapa, Mwinyi na Kikwete wamewahi kuwachagua hao minority kwa rangi kabila au dini zao, ila, nafahamu kuwa Nyerere alikuwa akichaguwa majority kwa Ukatoliki wao.
 
Unatuchanganya, sidhani kama Nyerere, Mkapa, Mwinyi na Kikwete wamewahi kuwachagua hao minority kwa rangi kabila au dini zao, ila, nafahamu kuwa Nyerere alikuwa akichaguwa majority kwa Ukatoliki wao.

Hivi wakina Amir Jamal, Leader Stirling, Al Noor Kassam, Derek Bryceson walikuwa wakatoliki au kwa lugha zenu za siku hizi, wazawa? Nadhani mtu mwenye asili ya bara hindi kuteuliwa kushika uwaziri katika jmt alikuwa yule dada mbunge wa Mororgoro aliyeishia unaibu waziri. Kuna dada mmoja kutoka unguja ambaye alijikita sana kwenye UVCCM lakini sidhani kama nae aliona ndani huko kwenye kuhitaji baraka za mkuu wa nchi.

Hali ya kisiasa sasa imekuwa toxic kiasi sidhani kama mtu mwenye akili yake kutoka hizo jamii atakubali uteuzi wowote maana utakuwa mwanzo wa kumwagia matope na kumuita ghabacholi, fisadi na majina mengine ya ovyo!

Amandla......
 
Hivi wakina Amir Jamal, Leader Stirling, Al Noor Kassam, Derek Bryceson walikuwa wakatoliki au kwa lugha zenu za siku hizi, wazawa? Nadhani mtu mwenye asili ya bara hindi kuteuliwa kushika uwaziri katika jmt alikuwa yule dada mbunge wa Mororgoro aliyeishia unaibu waziri. Kuna dada mmoja kutoka unguja ambaye alijikita sana kwenye UVCCM lakini sidhani kama nae aliona ndani huko kwenye kuhitaji baraka za mkuu wa nchi.

Hali ya kisiasa sasa imekuwa toxic kiasi sidhani kama mtu mwenye akili yake kutoka hizo jamii atakubali uteuzi wowote maana utakuwa mwanzo wa kumwagia matope na kumuita ghabacholi, fisadi na majina mengine ya ovyo!

Amandla......

unajaribu kusaga maji kwenye mashine .. hayageuki unga!
 
Kwa jinsi tunavyowasulubu hao wachache waliojiingiza kwenye siasa, kweli unashangaa kwa nini wengine hawajitokezi?

Kumbukumbu ya kuchagua.

Al Noor Kassim hakuwahi kuwa na shutuma na "hakusulubiwa." Rostam Aziz ana shutumiwa kwa ufisadi kwa sababu kampuni anayomiliki imehusishwa kinyaraka na kampuni zilizobaka nchi. Hakuna anaemshutumu kwa Uhindi. Dewji wa Singida hana kashfa na "hasulubiwi." Zakia Meghji, kama ni Mhindi, na anaonekana ana uhindi uarabu, alisulubiwa kwa sababu alitajwa katika kupitisha ufisadi wa EPA. Iddi Azzan, muarabu arabu wa Kinondoni, hana kashfa na hasulubiwi.

Usichore picha za kibaguzi kutetea jamii ambayo inajulikana siku zote inajitenga kwenye viota Upanga.
 
Pale kituo cha central police mjini dsm kuna wahindi wanafanya kazi hapo 3 hivi sema muda mwingi hunyoa nyele zao so ni ngumu kuwatambua lakini wanavaa uniform kama askari wengine bila shida yoyote - ishu huja kwenye lafudhi tu
 
Je, serikali inafanya juhudi zozote za kuwarecruit hawa minority katika public service? Inaonekana wengi tumekubali tu kuwa "wao wanapenda Biashara" as if kupenda huko kuko kwenye genes zao! Nani hapendi biashara akipata nafasi? Mbona wapo Wachagga wengi wanapenda Biashara na wengi wameingia kwenye utumishi wa serikali vile vile? Wengine wanasema ati wao wako zaidi katika medical fields? Kwani kwenye public service hakuna medical field?
 
Hapa ieleweke kuwa kama unawafutilia vizuri watu kiundani utagundua kuwa kinacholalamikiwa ni kwamba hawa wenzetu wameingia mpaka kwenye ofisi za serikali na kujua baadhi ya siri muhimu za nchi hili ni la hatari sana kwa masuala ya kufanya biashara na kuishi Tanzania mimi sioni kama linashida kama mtu ana sifa zote za kuwa raia au muhamiaji wa halali

Kingine nashindwa kuelewa huu utaratibu wa kuwapa madaraka tumeutoa wapi wakati hakuna mtanzania aliyewahi kuwa mbunge huko kwao.

Tumezidi kujipendekeza tusipopendwa
 
Kingine nashindwa kuelewa huu utaratibu wa kuwapa madaraka tumeutoa wapi wakati hakuna mtanzania aliyewahi kuwa mbunge huko kwao.

Tumezidi kujipendekeza tusipopendwa

Kwao wapi? ndio nyinyi mnaoamini kuwa Richa Adhia siyo Mtanzania japo amezaliwa, kusoma na kukulia Tanzania na kuwa na sifa zote kama mpogoro wa Morogoro isipokuwa rangi? Ndio mnaweza kuwa "huko kwao"..?
 
Mwanakijiji, I tend to agree kuwa ethinc minority are sidelined somehow,.......mimi ni mtanzania mwenye asili ya kiasia.....na nimezaliwa magharibi mwa Tanzania na nimekulia katika shule za serikali za Tanzania.....lakini nakubali sijawahi kuwaona mapolisi waasia na pia nafasi zingine za public sector ambazo ni aghalabu kumuona muasia akiishika........lakini nataka niwaulize wana JF ni asilimia ngapi ya Watanzania ni ethnic Minority.......Mimi sifikiriii hata kama wanaweza wakafika zaidi ya asilimia mbili ya watanzania nchini.........
Kuhusu suala la kutopewa uwaziri ni jambo la kujiuliza......nataka niwaulize wana JF je mnafikiri yule Rakesh Rajani mkurugenzi wa zamani wa asasi ya Haki elimu na Prof Jumanne Maghembe, Waziri wa Elimu katika serikali iliyopita........nani anaweza akaitendea haki zaidi sekta ya elimu........pia wapo Waasia wengi ambao wana uwezo, lakini je mifumo inasaidia kutoa nafasi hizo........Waasia siku zote wanaambiwa wezi....lakini jiulize TANROADS pale kwenye mizani anakaa muasia anayedai Rushwa au pale trafiki Salender Bridge Jumapili wanaovizia magari ni waaasia pia .,.........mifano ni mingi......Tatizo linaweza likawa sisi Watanzania wenyewe bila kujali rangi zetu lakini tuna hulka ya kutafuta kikundi, kabila, rangi za watu kuwashutumu wakati mabadiliko hayaji bila sisi wenyewe kuanza kubadilika.......
 
Nooresh.. haya ndiyo ninataka kuyahoji.. well.. tukiamini takwimu kuwa ni asilimia moja tu ya Watanzania ni racial minority.. basi hii asilimia mia moja iwe reflected basi katika serikali yetu? Hivi utumishi wa umma wa Tanzania una watu wangapi? Je katika kila watanzania kumi wanaopewa nafasi za umma au kuteuliwa, yawezekana mmoja tu akawa ni ethnic minority?
 
tatizo la hapa jm wachangiaji wengi ni makaburu weusi...kama alivowahi kusema mwalimu....kaburu ni kaburu tu hata akiwa mweusi.
Ukweli kabla ya uhuru wafanyakazi wengi walikua wa asia na wazungu, warabu wachache pia walikuwapo lakini sio sana...
Kuanzia trafic, wakagauzi wa magari,watoa licence zote..za driving na biashara...lakini hakuna aliedaiwa kitu kiduchu wakati huo....( fikiria adha ya kubadilisha driving licence sasa hivi ukitowa rushwa basi utapata mapema....au mambo mengine ya trafic kamuulize muro wa tbc..

Wakati tunagombea uhuru waarabu na wa asia wote walikua pamoja na waafrika na walitoa mali zao kusaidia harakati hizo.....uliza karimjee hall alitoa nani kwa serikali..jengo la anatouglou ...nk,

baada ya uhuru waliendelea kufanya kazi serikalini kwa uwaminifu sana...na ukweli huduma zilikuwa bila ya zengwe...driving licence licence ya mzee wangu ilitolewa na jaffer somji.....familia hii ipo bado na wanajishughulisha na bima.....
Masinga singa walikua wengi police force .sasa siasa ya africanazation aliyo ianzisha nyerere kwa nia njema labda ya kuwawezesha waafrika washike nafasi za kazi za jiserikali ilitumika vibaya ....hawa ndugu zetu hawakuajiriwa tena ndani ya serikali...wakabaki madaktari wachache, ma-advocate..na walimu...lakini ubaguzi ulikuwapo ndani kwa ndani pamoja na fitna...kwa hio wengi walivunjika moyo na wakajiona hawatakiwi kufanya kazi ndani serikali.....mpaka sasa serikali yetu ni 100% african....na mweupe yoyote hata akiwa na elimu gani hatakiwi na akijaribu atapata yaliomfika salim ahmed japo uhai wake kaitumikia nchii hii kwa uwaminifu kabisa
tanzania ndio nchi pekee ambayo haijiri tena raia wake ambao sio wa africa ..japo sio official policy ya nchi lakini ni ukweli.....wenzetu mfano kenya tu....hawakufanya ubaguzi huu...ndio maana mkuu wa jeshi wa kati wa kenyata alikua ni msomali ..general mohammed..na ipg wao aliepita pia alikua msomali/mshihiri...mwanasheria wao mkuu aliepita wakati wa moi na ghai ..myahudi..
Hata commissioner wa kubadilisha katiba alikua mwarabu mr hussein..
Tunaenda shule nao hawa na wengi wanafanya uzuri sana ..lakini hatutaku kuwatumia...ni kosa kubwa la ki strategia....
Unafahamu usa..wanatoa visa kwa watu wa mataifa mbali mbali 50,000 kila mwaka...kwani unafikiri raia wao wapatao million 600 hawatoshi.....? Wanajua wazi binadamu wanatafautiana iq zao kutegemeana na asili zao....hivyo iq tofauti zitasaidia kuijenga usa... Na kuwa mbali na wengine....
Sasa hapa tanzania kuwa na raia wenye asili tofauti ni jambo jema kama akili hizi tofauti....tutazitumia bila ya ubaguzi kujenga nchi hii....
Leo tuna ona mashule pale shaaban robert school. Al muntazir schools..agha khan schools, hindu mandal school, burhani schools,istiqama schools,india school..na nyenginezo kama hizo..wanafunzi zaidi 70% ni ndugu zetu..wengi ni very intelingent....lakini hawachaguliwi tena kwenye uni zetu( juzi udsm walitoa picha za wana chuo wa mwanzo na wanafunzi walikua mchanganyiko)
wanao gradute ni wengi...lakini hakuna kazi ardhi, police,jeshini,utalii, anywhere hawastahiki kupata kazi.....
Ningetamani labda tanesco iongozwe na baniani kama sir chande..naamini umeme usingekua wa mgao baada ya miaka 50 ya uhuru....au dawasco akapewa mohamed dewji ..naamini maji yasingekua tatizo....na issa shivji angekuwa mwanasheria mkuu..basi katiba mpya tungeipata...ubaguzi ni dhambi na laana yake huipata kila mtu hasa pale jamiii wana ifurahia..

Juu ya yote hayo kuwa serikali na taasisi zake zina ongozwa na wa africa bado wabaguzi hawajatosheka...wasema bado watu weupe wana kila kitu wao hawana....utafikiri kuna mtu amewazuia kupata....
 
People are still missing a point.. kwanini hadi hivi sasa hakuna mteuliwa yeyote (yawezekana yupo sijajua) wa Rais tangu wakati wa Mkapa na sasa Kikwete ambaye ni racial minority aliyeshika a high profile position katika serikali? Kuna aliyewahi kuteuliwa na Rais au Waziri akakataa nafasi yake kwa sababu yeye ni Mhindi au Muarabu au kwa sababu ya kidini yake?

Do we have qualified people from those minority groups with interest to serve the public without prejudices? Maana wale waliojaa wengi bungeni wanatisha kama ukoma. Watu safi ndio hao wamesukumizwa pembeni ya uongozi na wenye nguvu zao.
Hata hivyo, you have raised a good point if we really want to make the difference for now and in the future, other races should be part of the process.
 
Mwanakijiji,
Ukimalizana na suala hili naomba uingilie suala la makabila ya Tanzania. Tuna makabila zaidi ya 120. Je yote hayo yamewahi kuwakilishwa katika ngazi za juu katika serikali ya Tanzania?
 
Hao jamaa mnaowasema nafikiri wameridhika na na maisha ya kutojichanganya kabsa na African ancestry. Kama zamani walikuwa kwenye system tujiulize kwa nini sasa wameamua kukaa pembeni. Sababu nying zimeishatolewa, lakini mimi nafikiri kuna moja kubwa japokuwa nayo imeishagusiwa UMBAGUZI WA RANGI.
Hawa jamaa hwapendi kabsa kumfaidisha mblack isipokuwa kumtumia tu, ndo maana hata pale walipokuwa wamejichanganya nasi wakakaona wanatufaidisha kwa wao kuserve in the military and civil service wakaamua wasepe na kubaki kuwa wanyonyaji. Hapo na sisi tukajenga chuki zidi yao na kuona kuwa hawa jamaa wapo kimaslahi zaidi, na kwa vile wameshikiria secta mhimu (biashara & uchumi) popote watapojaribu kuingia in the civil servise tunaogopa kuwapokea japokuwa wao ndo wanaoamua mambomengi nchini mwetu.
 
Njooni tuzungumze tu... tutafute sababu kwanini tunahalalisha ubaguzi wa minority groups zetu na kuangalia jinsi gani tunaweza kutengeneza mazingira ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata nafasi iliyo sawa. Jasusi sasa hivi sidhani kama utakosa Mtanzania wa kabila lolote kwenye public service.. hicho ndicho ninachouliza hasa.. hilo la nafasi ya juu ni swali la nyongeza tu..
 
Back
Top Bottom