Diversity in Tanzania: Where are the Asian, Arab, European-Tanzanians?

Sir Leem, nimeelezea kuhusu wenzetu hawa kuwa ni vibarua tuu kule Dubai wakati hapa kwetu ni waheshimiwa sana!. Pia nemesema hapa kwetu wanachagua kazi zenye hadhi fulani ndizo wanafanya hivyo kwa hapa Tz wao ni watu wa maana sana kufikia hata kiwango ilipojulikana wanahusika EPA, gereza la Ukongo likakarabatiwa na kufungwa AC ili kuwaacomodate waheshimiwa hawa!

Sababu pekee ya kutumika wenzetu hawa ni kuwa wako too cheap, you can pay them the minimum of minimum na kazi ikafanyika. Kwa sasa, ni gharama ndogo zaidi kutengenezea India,tangazo zuri la TV kuliko kutengenezea hapa. Its cheaper kutibiwa India kuliko kutibiwa Ulaya, yaani wazungu sasa wanafiri toka Ulaya kwenda India kufuata matibabu. Hata gharama za uwakili India ni cheaper kuliko ulaya, hivyo wateja wa ulaya, wanawafuata malawyer wa India.

Naomba nikurudishe kidogo kwenye historia, jee unajua ni kwa nini Wahindi ni wengi Afrika ya Mashariki na wamejikita kibiashara zaidi?. Hao unaowaona, wengi wao, haswa mababu zao, walikuja tangu enzi za German East Africa kama makuli wa kutengeneza reli ya kati, mishahara waliolipwa ndio wakajengea maghorofa unayayaona miji yote reli ilikopita. Hivyo mwanzo walikuwa makuli wakati sisi tungali bado tukiishi gizani. Sasa wao ndio wafanya biashara wakubwa hapa kwetu, ukuli wa nini tena?, kibao kimetugeukia sasa sisi wenye nchi ndio makuli wao, ndio watumishi wao na wao ndio mabwana zetu mpaka serikali yetu nasi wenye nchi ndio watwana wao.

Nawaombeni sana sana sana, msije mkanitafsiri mimi kuwa ni racist, no, its about values. Hapa hufanya nguma zao za Bhagra pale Nkurumah Street, ukitaka kuingia kwanza hapo hapo mlangoni, unakataliwa!. Wana baa zao, maja wapo ni pale Odeon, kwenye jengo la DTV, wahuduma wa hizo bar ni waswahili wenzetu, nenda kaingie, huhudumiwi ng'o!. Wao ndio wateja wakubwa wa dada zetu wa usuku kwenye ma night club, nenda kwao uonekana unahangaika na vibinti vyao!. Yule Mtanzania aliyeuwawa Dheli, sababu haukusemwa na haitasemwa, we acha tuu. Mimi nimekaa New Dheli, mambo mengine ya huko kwao kuhusu wenzetu hawa, wee acha tuu! hapa kwetu ndio wafalme wetu!.

Pasco unataka watu wasikuite mbaguzi wakati kwenye post yako kumesheheni alama za ubaguzi huo.

Unatukumbusha historia kuwa mababu zao ndio waliokuja na kuwa makuli, lakini hapo hapo unawatenga kwa kusema 'sisi wenye nchi' ikimaanisha kuwa huamini/huwachukulii kuwa hapa ni kwao.

Baadae kidogo unasema "wao wanachukua wanawake wetu, lakini ukenda kwao..."
Kwao wapi?
 
Most of the minorities mentioned by Mwanakijiji also have intial problem of practicing a 'closed society' which is not open to the native Tanzanians hence mistrust build up amongst these societies.
 
I noticed a funny thing wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu nchini. Ilikuwa ni vigumu sana kuona Watanzania Wahindi ama Wazungu wakija kusikiliza sera za Wagombea Uraisi na Ubunge. Maana yake ni kwamba wao yoyote ambaye angechaguliwa ni sawa tu. Iwapo watu hawa hawajali hata mwenendo wa Kisiasa wa Nchi yao unavyokwenda, Iweje leo tuwatake Viongozi wetu waumize Vichwa vyao kutafuta njia za kuwajumlisha kwenye taasisi za uongozi wa nchi ambao mwingi unaanzia kwa kuwa Muwakilishi wa Watu?

Labda mikutano ya wagombea wa Chadema. Lakini mkutano wa CUF na CCM walikuwapo!

Tena kule Zanzibar kuna Mh. Mohammed Sanya na Mh. Ismail Jussa wote ni Wahindi ni viongozi wa chama cha upinzani. In fact kiongozi wa kwanza wa upinzani ndani ya bunge baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa nchini alikuwa muhindi, Mh. Muhammed Sanya.
 
Pasco unataka watu wasikuite mbaguzi wakati kwenye post yako kumesheheni alama za ubaguzi huo.

Unatukumbusha historia kuwa mababu zao ndio waliokuja na kuwa makuli, lakini hapo hapo unawatenga kwa kusema 'sisi wenye nchi' ikimaanisha kuwa huamini/huwachukulii kuwa hapa ni kwao.

Baadae kidogo unasema "wao wanachukua wanawake wetu, lakini ukenda kwao..."
Kwao wapi?
Gaijin, ukifanya utafiti huo utajiri wanaouvuna hapa nchini kwao Tanzania, wanauwekeza wapi, ndipo utajua kwao haswa wapi, licha ya kuzaliwa, kukulia, kusomea na kuchumia Tanzania!.

Baada ya ule utaifishaji wa majumba yao baada ya Azimio la Arusha, mpaka leo, wameamua kuishi maghorofani, wakilipa kodi Msajili wa Majumba na sasa NHC na hawajengi hata kibanda, sasa huo utajiri wao wote, wanaupeleka wapi?. Huko utajiri wao unakoishia ndio kwao halisi!.

Kwa wale mliobahatika kuisoma ile Ripoti ya Jaji Warioba kuhusu Rushwa, aliorodhesha makampuni makubwa ya wenzetu moja itaturn over ya bilioni moja kila mwezi, ofisi zake ziko jengo la Msajili, inafanya Agriculture bussiness, haina shamba, inanunua mazao ya wakulima toka the big five, haimiliki hata ghala moja, imepangisha maghala Pugu Rd. Inamiliki trasport company ya kusafirisha hayo mazoa, inamiliki insuarance compay ya kuweka bima mali zake, inamiliki freight company ya kuexport hayo mazao, inamiliki shipping company ya kuyasafirisha nje ya nchi, inamiliki import na export company ya kuyasimamia, kwa kifupi inamiliki kila kitu tangu hata moja hadi ya mwisho, inatengeneza faida ya bilioni moja kila mwezi halafu haina fixed asset hata moja, nil!, faida hiyo inawekezwa wapi?. Hawa ndio wenzetu hawa!.
 
Gaijin, ukifanya utafiti huo utajiri wanaouvuna hapa nchini kwao Tanzania, wanauwekeza wapi, ndipo utajua kwao haswa wapi, licha ya kuzaliwa, kukulia, kusomea na kuchumia Tanzania!.

Baada ya ule utaifishaji wa majumba yao baada ya Azimio la Arusha, mpaka leo, wameamua kuishi maghorofani, wakilipa kodi Msajili wa Majumba na sasa NHC na hawajengi hata kibanda, sasa huo utajiri wao wote, wanaupeleka wapi?.

Kwa hiyo wewe umeamua kuuvua uraia wao kwa sababu hujui pesa zao wanaziweka wapi au zinakwenda wapi!


Hivi unataka kunambia hujawasikia mafisadi wanao wekeza nje ya nchi pia? Hawa pia uliwavua uraia wao?

Hivi unataka kunambia kuwa hakuna Watanzania wenye asilia ya India ambao ni masikini?

Kuishi kwenye nyumba za NHC ni kosa kisheria?

Unauliza pesa zao wanawekeza wapi wakati wewe wewe ndo ulokuja na kusema wana makampuni makubwa Tanzania.

Sasa hayo makampuni makubwa yanaendeshwaje?

Hivi uko radhi wewe uhukumiwe kwa makosa ya Chenge?
 
Sir Leem, nimeelezea kuhusu wenzetu hawa kuwa ni vibarua tuu kule Dubai wakati hapa kwetu ni waheshimiwa sana!. Pia nemesema hapa kwetu wanachagua kazi zenye hadhi fulani ndizo wanafanya hivyo kwa hapa Tz wao ni watu wa maana sana kufikia hata kiwango ilipojulikana wanahusika EPA, gereza la Ukongo likakarabatiwa na kufungwa AC ili kuwaacomodate waheshimiwa hawa!

Sababu pekee ya kutumika wenzetu hawa ni kuwa wako too cheap, you can pay them the minimum of minimum na kazi ikafanyika. Kwa sasa, ni gharama ndogo zaidi kutengenezea India,tangazo zuri la TV kuliko kutengenezea hapa. Its cheaper kutibiwa India kuliko kutibiwa Ulaya, yaani wazungu sasa wanafiri toka Ulaya kwenda India kufuata matibabu. Hata gharama za uwakili India ni cheaper kuliko ulaya, hivyo wateja wa ulaya, wanawafuata malawyer wa India.

Naomba nikurudishe kidogo kwenye historia, jee unajua ni kwa nini Wahindi ni wengi Afrika ya Mashariki na wamejikita kibiashara zaidi?. Hao unaowaona, wengi wao, haswa mababu zao, walikuja tangu enzi za German East Africa kama makuli wa kutengeneza reli ya kati, mishahara waliolipwa ndio wakajengea maghorofa unayayaona miji yote reli ilikopita. Hivyo mwanzo walikuwa makuli wakati sisi tungali bado tukiishi gizani. Sasa wao ndio wafanya biashara wakubwa hapa kwetu, ukuli wa nini tena?, kibao kimetugeukia sasa sisi wenye nchi ndio makuli wao, ndio watumishi wao na wao ndio mabwana zetu mpaka serikali yetu nasi wenye nchi ndio watwana wao.

Nawaombeni sana sana sana, msije mkanitafsiri mimi kuwa ni racist, no, its about values. Hapa hufanya nguma zao za Bhagra pale Nkurumah Street, ukitaka kuingia kwanza hapo hapo mlangoni, unakataliwa!. Wana baa zao, maja wapo ni pale Odeon, kwenye jengo la DTV, wahuduma wa hizo bar ni waswahili wenzetu, nenda kaingie, huhudumiwi ng'o!. Wao ndio wateja wakubwa wa dada zetu wa usuku kwenye ma night club, nenda kwao uonekana unahangaika na vibinti vyao!. Yule Mtanzania aliyeuwawa Dheli, sababu haukusemwa na haitasemwa, we acha tuu. Mimi nimekaa New Dheli, mambo mengine ya huko kwao kuhusu wenzetu hawa, wee acha tuu! hapa kwetu ndio wafalme wetu!.

Siyo kweli wahindi walijenga hayo magorofa kwa mshahara wa ukuli. Wahindi waliletwa kutoka India kama makuli lakini baada ya ujenzi wa reli kuisha wengine walilowea na kufungua maduka ya vyakula (siku hizi yanaitwa dukani kwa Mpemba ama kwa Mchaga). Hizi biashara zilikuwa taratibu kama zinavyokuwa biashara zingine na ukizingatia kuwa mafanikio ya biashara ni ku-save na kukuza mtaji badala ya kuongeza mke, vimada na magari kwa ajili ya matanuzi.
 
Kwa hiyo wewe umeamua kuuvua uraia wao kwa sababu hujui pesa zao wanaziweka wapi au zinakwenda wapi!


Hivi unataka kunambia hujawasikia mafisadi wanao wekeza nje ya nchi pia? Hawa pia uliwavua uraia wao?

Hivi unataka kunambia kuwa hakuna Watanzania wenye asilia ya India ambao ni masikini?

Kuishi kwenye nyumba za NHC ni kosa kisheria?

Unauliza pesa zao wanawekeza wapi wakati wewe wewe ndo ulokuja na kusema wana makampuni makubwa Tanzania.

Sasa hayo makampuni makubwa yanaendeshwaje?
Gaijin, sijamvua mtu urai hapa, nimeuliza tuu hiyo faida wanayoivuna hapa, unamfadia nani, at the end of the day?.
Ya makampuni, nilia update posti yangu, lakini kwa faida yako nakuwekea tena.

Kwa wale mliobahatika kuisoma ile Ripoti ya Jaji Warioba kuhusu Rushwa, aliorodhesha makampuni makubwa ya wenzetu moja itaturn over ya bilioni moja kila mwezi, ofisi zake ziko jengo la Msajili, inafanya Agriculture bussiness, haina shamba, inanunua mazao ya wakulima toka the big five, haimiliki hata ghala moja, imepangisha maghala Pugu Rd. Inamiliki trasport company ya kusafirisha hayo mazoa, inamiliki insuarance compay ya kuweka bima mali zake, inamiliki freight company ya kuexport hayo mazao, inamiliki shipping company ya kuyasafirisha nje ya nchi, inamiliki import na export company ya kuyasimamia, kwa kifupi inamiliki kila kitu tangu hata moja hadi ya mwisho, inatengeneza faida ya bilioni moja kila mwezi halafu haina fixed asset hata moja, nil!, faida hiyo inawekezwa wapi?. Hawa ndio wenzetu hawa!.

Sijasema mahali ni kosa kuishi nyumba za NHC, nimeuliza faida wanapeleka wapi, kama hawawezi hata kuwekeza kwa kujenga kibanda hapa. Sisi tunaishi nyumba za kupanga kutokana na umasikini ulikithiri, hatuna uwezo wa kujenga, wenzetu wenye uwezo ndio wamenganganias vile viota mjini ambavyo tungeishi sisi tusio na uwezo, hivyo kujikuta tunalazika kukabwa koo na wenye majumba kwa kupandisha kodi kutokana na demand. Kama wenzetu wote wenye uwezo wa kujenga, wangejenga na kutoa nafasi kwa wasio na uwezo ndio tupange, Tanzania si ingekuwa a bit better off?.

Sijasema hakuna masikini kwa wenzetu hawa, ndio maana nimekuambia nimeishi Dheli, niliyoyaona huko na umasikini wa huo, Matonya ni tajiri!.
 
Pasco mbona unaheshimika lakini unatoa udenda?
Elewa kwanza uislam hauna kabila,tofautisha uarabu na uislam.Jua pia huko mid-east ulikokutaja pia wapo waarabu wakristo.Halafu jua kwamaba wyahudi sio wazungu wala sio wakristo.Hata hivyo hao waarabu uliwataja wana mchango mkubwa katika ustaarabu wa dunia.Mfano mdogo tu ni tarakimu za namba zinazotumika ulimwenguni ni ARABIC NUMERALS.Kabla ya kontact na waarabu, wazungu walikuwa na shida ya kuandika namba.Umeitaja Uturuki umesahau Iran na Pakistan zenye nyuklia.Ni story ndefu sina haja ya kukupa lecture
 
Naombeni tusizame sana kuhusu wenzetu hawa, mada ya Mwanakijiji ikaenda hali jojo, lengo libaki pale pale, hawa ni wenzetu, wamezaliwa hapa, wamekulia hapa, wanaishi hapa na tuko nao japo sio mitaani kwetu, lakini kwa nini hawapatiwi nafasi za ulaji na kuila ile keki ya taifa kwa ulaini?. Kwa nini hawapewi ulaji kwa kushikwa mikono, kubebwa na kulishwa (uteuzi) kama walivyo wengine?.

Naungana mkono na Mzee Mwanakijiji, lazima tuwafikirie, yaani mwenye nacho, anaongezewa, tena namshauri Mzee Mwanakijiji kuwashauri wazee wa chama chake, hili waliweke kwenye ilani yao ya 2015 kwa sababu ni hakika, wanachukua nchi kiulani kama kumsukuma mlevi!
 
nooresh, kwanza karibu jf, uwepo wako humu ni muhimu sana hata kwa divesity ya jf.

Naomba read me in between the lines, hoja ya Mzee Mwanakijiji ameuliza kwa nini minority ya wenzetu hawaonekani serikalini, mawizani au hata nafasi za kuteuliwa?.

Mimi nikamjibu, wenzetu hawa, hawaonekani, hata hao wachache waliongia bungeni, wameingia tuu lakini wana biashara zao, uwaziri hata wa bure, hawautaki!.

Nikasema, japo hao ni minority na haonekani kwa nafasi za uteuzi, lakini ndio hao wenye upprer hand kwenye kazi za maana mashirika ya kimataifa na ubalozini, nikataloe mfano nafahamu graduate fulani mwenye masters yake ya MBA, analipwa M.3 na ofisi hiyo hiyo, mwenzetu mmoja toka kundi la minority analipwa M.5, hivyo sio kweli kuwa hawapo kabisa, bali hawapo kwenye low paying jobs na wamejazana kwenye high paying jobs kama UN na mashirika yake.

Nikamalizia kwa kutolea mfano enzi za Nyerere, wakati huo, kina Amir Jamal, Al Noor Kassum, Dr. Leader Starring, Dereck Bryson, Joan Wickens, kuwa enzi hizo sasa zimepita, sasa tuko katika enzi za hao minority ndio wamekamata kila kitu and infact sisi ni watumishi wao, tangu rais wetu mpaka watoto wetu na watoto wa watoto wetu!.

Sijasema sio Watanzania, ndio maana nawaita wenzetu japo siulizi fedha zote wanazochuma, wanaivest wapi ili hali wanaishi kwenye viota vyao vya NHC?.

Ni kweli, watoa tenda wote ni sisi, ila tenda zote huangukia kwao, mind well, wao n i middle men tuu, huku tukiwa na nafasi ya kununua direct lakini tunawang'ang'ania hawa middle men, najua unajua ni kwanini!.

Mimi wala sijasema wenzetu wanaitafuna nchi, bali wamebahatika kuzaliwa na silver spoon hivyo wanakula top layer na sisi tunaambulia kilichobakia!.

Nilikwenda Dubai, huko nikakuta wenzetu hawa ndio mahouse girls, makuli, wabeba zege na kazi zote za ajabu ajabu, niliporudi hapa, nililisema hili mahali jinsi wenzetu hawa walivyo Dubai, na jinsi wenzetu hawa walivyo Tanzania, nearly ingenicost my job, maana nami nilikuwa natumika kwao.

Ufisadi ni ufisadi tuu, hauna rangi, hauna dini, hauna kabila, kwenye thread za kuwalaani mafisadi, mimi ni mmoja niliowasifu waliofisidi na kuporomosha ma-housing estates kwamba angalau wamefanya kitu cha kuonekanika hata wakiitwa siku ya siku, wataviacha hapa kwetu hivyo walivyofisidi, lakini wenzetu hata wakifisidi, hizo proceed za ufisadi wanaziinvest wapi?.

Divesity ni namna kumanage utofauti wetu, yaani tunakubali tuu tofauti, tufanya kazi ya ujenzi wa taifa letu kwa umoja, pamoja na utofauti wetu, lakini the facts inabaki pale pale, tuko tofauti!.


Unajua kaka mimi nataka ifanyike sensa ili tujue hasa percentage of ethnic minority......mimi nilikuwa nina degree yangu tena nimesoma nje ya nchi.....nikawa nalipwa below half a million........halafu nakutana na mshikaji ambaye analipwa hela zaidi kuliko mimi tena ni form four leaver........eventually niliacha kazi lakini baadaye nikaja kugundua jamaa alikuwa analipwa kwa advantage zake za kupiga mzigo zaidi.......so one example of somebody getting paid high doesnt make sense to generalize it.......kitu cha pili waasia wengi hawapendi kukaa mbali na mji hii imejengeka miongoni mwao kwa sababu sehemu zao za kusalia.....sehemu wanazotembelea mostly zinakuwa mjini so wanajazana huko huko......pesa akiipata utashangaa atasomesha mtoto au ataanzisha biashara, hata asome vipi bado atapenda kufanya biashara, hiyo imejengeka kwao they are not creative but more enterprenuars.......ushasikia wahindi wanachangiana harusi......very rarely kaka......wenyewe michango yao ni kwenye elimu, kuugua, na kadhalika......huo ni utamaduni.....lakini kukaa kwenye nyumba za NHC si vibaya ni comfortability tu.....mimi ninakaa kijitonyama......sijauziwa nyumba za Serikali......sasa mimi siwezi kusema kuwa Watu wote wanaofanya kazi serikalini ni wezi......lakini Serikalini wahindi hawapo wengi na ndipo huduma mbovu, ubadhirifu na mambo mengine yanatokea lakini wachache hao ukilinganisha na population iliyokuwepo nje ya Serikali......mimi nakuambia kuna middle men gani kwa Trafiki........au kuna middle men gani pale TANROADS.....au kuna middle men gani pale Serikali na viongozi wanapojiuzia nyumba wenyewe......Tatizo we are looking for reasons to blame for our failures while its ourselves who are the source........Viongozi wanajisahau.......na kuwaumiza wengi......huyo Middle Men si chochote iwapo Daktari, Trafiki, Mfamasia akitenda wajibu wake kaka.....

Dubai sio wahindi tu hata wafilipino, wa Indonesia , na Bara zima la Asia linatoa wafanyakazi kwa sababu kuwa hausgeli Dubai inalipa kuliko kuwa hausgeli India au Hausgelli Bongo.......so hata wanaweza wakatuma pesa kwao zaidi..........brother i believe ni kuwa wahindi ni wacchache mno......na wapo waliofulia lakini kwa sababu za community na religious institution kuwapa sapoti wanakuwa hawaonekani trafiki lite.......mimi sio mtu wa dini sana lakini dhehebu letu unaposalia zile pesa zinakusanywa na wale wasioweza kusomesha watoto, hawapati tiba wanasaidiwa kwa pesa za waumini.....wanaita Welfare......wanachoangalia ni kama wewe ni muumini na sio rangi yako becoz wapo waumini wasiokuwa wahindi pia kaka.......hiyo ni Info ambayo ninakupa kuwa ndio sababu unakuta wahindi hawako street kuomba pamoja na matatizo waliyokuwa nayo.........kwa sababu wanasaidiwa na sehemu wanazoenda kuabudu.......wahindi wengi ni aidha Shia Itna Ashiria, Ismaili, Sunni ( ambao sina info za hizo welfare ) Hindu........This system ipo nationally kwa wenzetu Ulaya kwa sababu ya mifumo ya serikali ina allow WElfare allowancess......
 
Gaijin, sijamvua mtu urai hapa, nimeuliza tuu hiyo faida wanayoivuna hapa, unamfadia nani, at the end of the day?.
Ya makampuni, nilia update posti yangu, lakini kwa faida yako nakuwekea tena.

Ushasema si kwao, ni kwenu wewe, wao kwao India. Hapo ni sawa na kuwavua uraia.

Kwa kuwa hawa wana asili ya nchi nyengine imekuwa rahisi kuwanyooshea vidole na kusema si kwao, mbona Chenge husemi kwao ni alikoweka vijisenti vyake? Na si Chenge tu kama ungekuwa mtenda haki ungesema watu wote wa kabila la Chenge kwao ni huko kwenye vijisenti vya mtu mmoja.

Haijalishi umeishi wapi, hata Tanzania wapo Watu wenye asili ya India wenye umaskini wa kutupwa, unamsimamo gani juu ya hawa?

Huwezi kuwa hukumu wote na kusema Tanzania si kwao kwa sababu wenye pesa wanawekeza nje ya nchi. Hiyo inaonekana ni moja ya element ya kibaguzi tu, wala si sababu ya msingi.
 
Pasco......nitakuambia kitu kingine ambacho nimefikiria na nikiweke wazi.....wazazi wetu wengi wamekuwa reluctant kwa sababu moja naamini tofauti na sisi ambao tumeshaamua kuwa nitakufa Tanzania na thats where I call Home........Nationalization iliwakuta wahindi wengi pabaya.......mimi nilizaliwa Kigoma na mji ule ulikuwa na wahidni wengi sana.......sasa hivi wamebaki wachache sana......wengi walihama baada ya Nationalization ......kwa sababu waliamini kuwa wakifanya kazi na baadaye wakapata hiyo wealth itakuja kuchukuliwa na taifa tena......hence ile feeling ya kubaki ikawa haipo......mind you hao ni only second generation Asianms......sasa hivi tushafika kwenye fifth na fourth generation......Baadae Iddi Amin pia akafanya hivyo hivyo......kwa hiyo hao wakaogopa kuinvest kwa kununua majumba kwa sababu wanakuwa waoga......lakini vijana wengi wa Kiasia ambao ni Watanzania utakuta stori zao ni za hapo bongo na investment ni humuhumu.......kwa hiyo lazima tuangalie na matukio ya zamani......kwa hesabu zangu za haraka haraka wahindi actually hawafiki hata laki mbili........Obama once said alipoingia shuleni watu walimzomea kwa sauti za nyani.....na enzi alizoenda Obama shule alisoma gazeti ambapo kijana mmoja mweusi aliunguza ngozi vibaya kwa sababu he hated the color after the abuse........so huyo Obama alikuja akawa Rais wa taifa hilo hilo.....makes me think wacha Asians get called looters, wezi, closed society but I believe wezi wa taifa hilo wapo wengi apart from hao few asians who are tarnishing images of others.....muhimu sote ni WAtanzania na tujenge nchi kwenda mbele.......
 
I noticed a funny thing wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu nchini. Ilikuwa ni vigumu sana kuona Watanzania Wahindi ama Wazungu wakija kusikiliza sera za Wagombea Uraisi na Ubunge. Maana yake ni kwamba wao yoyote ambaye angechaguliwa ni sawa tu. Iwapo watu hawa hawajali hata mwenendo wa Kisiasa wa Nchi yao unavyokwenda, Iweje leo tuwatake Viongozi wetu waumize Vichwa vyao kutafuta njia za kuwajumlisha kwenye taasisi za uongozi wa nchi ambao mwingi unaanzia kwa kuwa Muwakilishi wa Watu?
Hili ni kweli kabisa..mimi nina rafiki mwarabu nilimuuliza " ulipiga kura?"..hakunijibu alibakia kucheka tu na kunishangaa ni kwa vipi naweza hata kuwaza ati angepiga kura!..LAkini pamoja na hilo, haina maana hawastahili kufikiriwa maana wapo wenye kupenda kushiriki kwenye siasa ndio maana tulikuwa na akina Adamjee,Premji, Dewji na wengineo kama wabunge.
"
'"
 
Labda mikutano ya wagombea wa Chadema. Lakini mkutano wa CUF na CCM walikuwapo!

Tena kule Zanzibar kuna Mh. Mohammed Sanya na Mh. Ismail Jussa wote ni Wahindi ni viongozi wa chama cha upinzani. In fact kiongozi wa kwanza wa upinzani ndani ya bunge baada ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa nchini alikuwa muhindi, Mh. Muhammed Sanya.

CHADEMA kuna a young Indian tena anavaa zile combat na kuhudhuria mikutana kama kawa! I was impressed!
 
It's true that Kikwete's cabinet does not reflect racial diversity. And that's wrong, dead wrong.

But people should not get the wrong impression that has been the case since independence. Nyerere's government was most inclusive through the years since independence.

Kuhusu baraza la mawaziri, Nyerere alikuwa na mawaziri ambao hawakuwa weusi tu, ingawa mawaziri weusi walikuwa ni wengi kuliko wengine tangu tulipopata uhuru.

Namkumbuka Derek Bryceson na Amir Jamal kati ya mawaziri wa kwanza. Pia alimchagua Ernest Vasey kuwa waziri wa fedha katika baraza la kwanza la mawaziri. Lakini Vasey alikuwa siyo Mtanganyika na aliondolewa kutoka baraza hilo baada muda mfupi. Alipewa kazi nyingine kama chief financial adviser wa serikali.

Baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Nyerere's cabinet iliendelea ku reflect racial diversity. Pia haikujaa Wakatoliki wenzake kama tunavyo ambiwa na watu fulani hapa Jamii Forums. Kulikuwa na Waislamu, na Wakristo wa madhehebu mbali mbali. As Mobhare Matinyi stated in his article, "Recalling the first Union cabinet of 1964," in The Citizen, Dar es Salaam, Tanzania, 26 November 2010:

"Immediately after Africa's historical proclamation that the Republic of Tanganyika and the Peoples' Republic of Zanzibar shall be united in one Sovereign Republic, the next thing was the new cabinet.

Julius Kambarage Nyerere, then the president of Tanganyika who had just been sworn in as the first president of Tanzania, sat down with his two newly sworn-in vice presidents, Abeid Amani Karume, then the president of Zanzibar, and Rashidi Mfaume Kawawa, then the vice president of Tanganyika, to form the first Union cabinet.

Nyerere, who by then had slowly started pushing for the title 'Mwalimu' against the title 'Doctor' which the Western media like the Times of London preferred, asked his two vice presidents to take two portfolios.

Literally, the title doctor from Latin lexicon, doctoris, means teacher or mwalimu in Kiswahili.

Thus, Sheikh Karume also became the minister responsible for Zanzibar Affairs while Kawawa was the minister of defense and national service. We had no Prime Minister then, and being a deputy minister wasn't such a big deal.

Then Nyerere appointed three ministers in his office to deal with economic planning. These guys were Nsilo Swai, Mohammed Abdulrahman Babu and Amir Jamal, a mixture of an African, an Arab and an Indian, respectively.

Following allegations of taking part in the assassination of Karume, Babu had to leave the country in 1978 after a brief imprisonment. He later became a renowned London-based scholar, and in 1995 NCCR-Mageuzi appointed him the running mate for the presidency of Tanzania together with Augustine Mrema.

Mwalimu then appointed Aboud Jumbe as the minister of state in the first vice president's office while Lawi Sijaona and Bhoke Munanka became ministers of state in the second vice president's office. Jumbe later became the Tanzania vice president after the death of Karume in 1972.

The portfolio dealing with agriculture, forestry and animal husbandry went to Said Maswanya while Jeremiah Kasambala took over the portfolio of commerce and cooperatives. Nyerere appointed his buddy, George Kahama, famous as Sir George, the minister for transport and buildings.

Nyerere set apart an important ministry, finance, from economic planning placing Paul Bomani in charge. Oscar Kambona, another of Nyerere's buddies who rejected the socialism idea in 1967, became the minister for foreign affairs. Kambona later escaped to Britain to avoid treason charges, leaving his colleagues in hot soup.

Nyerere appointed Job Lusinde the minister of internal affairs while lands, settlement and water was placed as one portfolio under Tewa Said Tewa.

Abdullah Kassim Hanga, a vibrant politician from Zanzibar, became the minister for industries and mines. Nyerere also appointed Solomon Nkya Eliufoo the minister for education and a British, Dereck Bryceson, the minister for health.

Labour went to Michael Kamaliza while the development and culture portfolio was placed under Sheikh Amri Abeid, the first mayor of Dar es Salaam after Tanganyika got independence in 1961. The famous stadium in Arusha, Sheikh Amri Abeid, is named after him.

Nyerere appointed Austin Shaba to head the portfolio of housing and local government as Hassan Nassoro Moyo became the minister of law. Information and tourism were charged to Idrissa Abdulwakil.

This merit-based cabinet, as Godfrey Mwakikagile put in his book, Nyerere and Africa, End of an Era, included everybody. Unlike in other newly independent African states, Tanzania's cabinet had every major race that existed in the Tanzanian polity in the 1960s: Africans, Arabs, Asians and whites.

President Nyerere did not include every region for sure as our leaders do today, but included people of all religions. There were, not only Christians and Muslims, but even Hindus.

Nyerere's administration recognized the importance of building one nation and one country, contrary to what some hypocrites proclaim today: that Nyerere forgot a section of our people. What a big lie!

As a matter of fact, Mwalimu stopped discrimination in schools immediately after independence to get education for every child regardless of his parents' religion. Most of our leaders today, including the ones who want to divide Tanzanians for selfish ends, benefited from Nyerere's decision.

Nyerere did not wish to have any division at all, and even after his retirement he still held to his principle, saying: 'I don't want my people to suffer.' This is a feeling our leaders today rarely bother to ponder about.

No wonder that in 2009 the United Nations General Assembly named Nyerere the 'World Hero of Social Justice.'

Nyerere was truly, as Nelson Mandela put it in his 1994 autobiography, Long Walk to Freedom, a man of the people.

Hello politicians, the unity, peace and stability we cherish always in Tanzania did not fall like manna from heaven; somebody worked for it. Visit other African countries and see for yourself.

Our present leaders ought to emulate Nyerere in building one Tanzania that does not divide people for any reason whatsoever. Long live Tanzania!"

Comments:

Kitoto, 2010- 11- 26:

Brilliant piece of history, Matinyi.

Graca Macha, 2010-11-26:

Deserve(s) reading and contemplating. Congrats."

Source: The Citizen, Dar es Salaam, Tanzania.
 
Unajua kaka mimi nataka ifanyike sensa ili tujue hasa percentage of ethnic minority......mimi nilikuwa nina degree yangu tena nimesoma nje ya nchi.....nikawa nalipwa below half a million........halafu nakutana na mshikaji ambaye analipwa hela zaidi kuliko mimi tena ni form four leaver........eventually niliacha kazi lakini baadaye nikaja kugundua jamaa alikuwa analipwa kwa advantage zake za kupiga mzigo zaidi.......so one example of somebody getting paid high doesnt make sense to generalize it.......kitu cha pili waasia wengi hawapendi kukaa mbali na mji hii imejengeka miongoni mwao kwa sababu sehemu zao za kusalia.....sehemu wanazotembelea mostly zinakuwa mjini so wanajazana huko huko......pesa akiipata utashangaa atasomesha mtoto au ataanzisha biashara, hata asome vipi bado atapenda kufanya biashara, hiyo imejengeka kwao they are not creative but more enterprenuars.......ushasikia wahindi wanachangiana harusi......very rarely kaka......wenyewe michango yao ni kwenye elimu, kuugua, na kadhalika......huo ni utamaduni.....lakini kukaa kwenye nyumba za NHC si vibaya ni comfortability tu.....mimi ninakaa kijitonyama......sijauziwa nyumba za Serikali......sasa mimi siwezi kusema kuwa Watu wote wanaofanya kazi serikalini ni wezi......lakini Serikalini wahindi hawapo wengi na ndipo huduma mbovu, ubadhirifu na mambo mengine yanatokea lakini wachache hao ukilinganisha na population iliyokuwepo nje ya Serikali......mimi nakuambia kuna middle men gani kwa Trafiki........au kuna middle men gani pale TANROADS.....au kuna middle men gani pale Serikali na viongozi wanapojiuzia nyumba wenyewe......Tatizo we are looking for reasons to blame for our failures while its ourselves who are the source........Viongozi wanajisahau.......na kuwaumiza wengi......huyo Middle Men si chochote iwapo Daktari, Trafiki, Mfamasia akitenda wajibu wake kaka.....

Dubai sio wahindi tu hata wafilipino, wa Indonesia , na Bara zima la Asia linatoa wafanyakazi kwa sababu kuwa hausgeli Dubai inalipa kuliko kuwa hausgeli India au Hausgelli Bongo.......so hata wanaweza wakatuma pesa kwao zaidi..........brother i believe ni kuwa wahindi ni wacchache mno......na wapo waliofulia lakini kwa sababu za community na religious institution kuwapa sapoti wanakuwa hawaonekani trafiki lite.......mimi sio mtu wa dini sana lakini dhehebu letu unaposalia zile pesa zinakusanywa na wale wasioweza kusomesha watoto, hawapati tiba wanasaidiwa kwa pesa za waumini.....wanaita Welfare......wanachoangalia ni kama wewe ni muumini na sio rangi yako becoz wapo waumini wasiokuwa wahindi pia kaka.......hiyo ni Info ambayo ninakupa kuwa ndio sababu unakuta wahindi hawako street kuomba pamoja na matatizo waliyokuwa nayo.........kwa sababu wanasaidiwa na sehemu wanazoenda kuabudu.......wahindi wengi ni aidha Shia Itna Ashiria, Ismaili, Sunni ( ambao sina info za hizo welfare ) Hindu........This system ipo nationally kwa wenzetu Ulaya kwa sababu ya mifumo ya serikali ina allow WElfare allowancess......

Umetusuta kiaina! Hatuchangiani kwenye elimu. Lakini hodari wa kupanga na kuchangia harusi ambako pesa yote iliyochangwa inateketezwa bila kujali maharusi watakula nini kesho! Hatuchangiani kwenye kuuguza bali tuko mbele kwenye kupeleka maiti nyumbani! Hatuchangiani wala kusaidiana kibiashara. Halafu tunashangaa kuwa katika nchi ambayo sisi tu wengi lakini tumeshika madaraka bado tuko nyuma?

Amandla.......
 
Umetusuta kiaina! Hatuchangiani kwenye elimu. Lakini hodari wa kupanga na kuchangia harusi ambako pesa yote iliyochangwa inateketezwa bila kujali maharusi watakula nini kesho! Hatuchangiani kwenye kuuguza bali tuko mbele kwenye kupeleka maiti nyumbani! Hatuchangiani wala kusaidiana kibiashara. Halafu tunashangaa kuwa katika nchi ambayo sisi tu wengi lakini tumeshika madaraka bado tuko nyuma?

Amandla.......

Fantastic!!!
 
Uzuri wa mada kama hizi ni huwa zinatuonyesha kuwa ni nani ana hisia za ubaguzi katika jamii yetu.
 
Uzuri wa mada kama hizi ni huwa zinatuonyesha kuwa ni nani ana hisia za ubaguzi katika jamii yetu.


Halafu unajua kinachoshangaza ni kuwa we don't even recognize kwamba tuna ubaguzi.. we have these euphemisms ambazo tunatumia kuhalalisha; "wao wanapenda biashara zaidi"; "wao hawachanganyiki na sisi".. this is how it used to be for black folks in US. It is a natural reaction ya jamii yoyote inayoona inatengwa na jamii kubwa kuanza kufanya mambo kivyao vyao.. it happened with the Jews in Europe in the antiquities, it happened and still happens with the Roma people, it has happened with Arabs in Metro Detroit etc.

Lakini wenzetu kama US walikuja na anti-discrimination laws na kubwa zaidi ni ile ya Civil Act ya 1964 ambayo ilikataza ubaguzi kwa namna yoyote. Leo hii ukienda karibu ofisi zote za umma na binafsi wanaposti sehemu ya sheria hiyo ikiweka msingi kwa kile kinachojulikana kama "Equal Opportunity" ambapo inasema hakuna discrimination based on race, color, sex, ethnicity or national origin" wengine wameongeza hadi "sexual orientation".

Walifikia hadi kuwa na kile tunakiita affirmative action..

Sasa sisi hata kuzungumzia suala la minority groups katika jamii yetu inakuwa kama unasaliti watu weusi!
 
Halafu unajua kinachoshangaza ni kuwa we don't even recognize kwamba tuna ubaguzi.. we have these euphemisms ambazo tunatumia kuhalalisha; "wao wanapenda biashara zaidi"; "wao hawachanganyiki na sisi".. this is how it used to be for black folks in US. It is a natural reaction ya jamii yoyote inayoona inatengwa na jamii kubwa kuanza kufanya mambo kivyao vyao.. it happened with the Jews in Europe in the antiquities, it happened and still happens with the Roma people, it has happened with Arabs in Metro Detroit etc.

Lakini wenzetu kama US walikuja na anti-discrimination laws na kubwa zaidi ni ile ya Civil Act ya 1964 ambayo ilikataza ubaguzi kwa namna yoyote. Leo hii ukienda karibu ofisi zote za umma na binafsi wanaposti sehemu ya sheria hiyo ikiweka msingi kwa kile kinachojulikana kama "Equal Opportunity" ambapo inasema hakuna discrimination based on race, color, sex, ethnicity or national origin" wengine wameongeza hadi "sexual orientation".

Walifikia hadi kuwa na kile tunakiita affirmative action..

Sasa sisi hata kuzungumzia suala la minority groups katika jamii yetu inakuwa kama unasaliti watu weusi!

Sidhani kama tunahitaji affirmative action. Nadhani msingi ni kuwa na Anti-Discrimination law ambapo mtu yeyote atakayenyimwa nafasi ya kazi katika taasisi za umma, masomo au starehe ( kukataliwa kuingia sehemu ya starehe au kunyimwa huduma halali) kutokana na rangi, kabila, jinsia au ulemavu aweze kufungua mashtaka!

Kama nakumbuka sawasawa kuna mahali nilimtetea Rostam dhidi ya Mengi nikatupiwa madongo kuwa ninajikomba kwa wahindi! Iko kazi.

Amandla......
 
Back
Top Bottom