Daktari Pekee wa upasuaji wa watoto wachanga Muhimbili aondoka

WaTZ tujitafakari.Wengi wa wangonjwa (hata wanaotibiwa private) huishia kupelekwa hospitali za serikali. Jambo hili ni vizuri turitafakari kwa kina ili tujue nini cha kufanya.Jamii sasa inaishi kwa hofu kwa sababu ya huduma za afya kuzorota hali inayoshusha TIJA na UFANISI katika shughuli za uzalishaji.
 
Amefanya vizuri kuondoka. Ni afadhali aondoke wabaki watu wenye wito na moyo kuliko kubaki kunyanyasa wananchi wenye matatizo.

Kuondoka kwake kutaisaidia serikali kupeleka wasomi zaidi wakasomee hiyo area yake kama ni kweli yupo peke yake.

Ila kwa Tanzania ya leo hatuna eneo ambao tuna mtaalam mmoja.

Sawasawa mkuu, endelea kujipa moyo..kama una uhakika na kitu usichokijua usikimbilie kupost tu, Ulizia Plastic Surgeons, Cardiothoracic Surgeon, Nephrologist, Hematologist n.k(Hizi ni baadhi tu) wako wangapi ndio uje hapa na kupost.
 
Katika kuonyesha kuitika mwito wa Rais kikwete aliyetangaza kuwa Madaktari wasioridhika na malipo kiduchu na mazingira mabaya wanayofanyia kazi hapa nchini waondoke, Daktari pekee bingwa wa upasuaji wa vitoto vichanga (paediatric surgeon) ameondoka muhimbili na kuhamia hospitali moja ya binafsi mikoa ya kaskazini.

Hili ni pigo kubwa sana kwa watoto wachanga na sisi wazazi. Sasa mtoto akiwa na tatizo la upasuaji sasa hana tumaini tena la kuishi maana daktari huyu alikuwa anawafanyaia upasuaji watoto wote kutoka nchi nzima.

Ubinafsi huu wa wanasiasa kujineemesha huku wakitukana na kuadharau wataalamu utatumaliza.

Imagine mwanao anazaliwa bila njia ya haja kubwa halafu anakosa kufanyiwa upasuaji wa kuifungua! Mungu atusaidie!
Naamini kwa dhati kabisa kuwa Kikwete hakufikiria kwa kina madhara ya kauli yake kuwa asiyeridhika na malipo ya serikali aondoke. Naamini aliitoa kauli hii bila kufikiria kuwa kwa muda mrefu madaktari, na wataalamu wengine wengi tu, wamekuwa wakifanya kazi wkamoyo wa kuipenda nchi yao. Ingawa wanakatishwa tamaa na malipo dunui, lakini watu hawa wanatiwa moyo na uzalendo wao ambao hutiwa moyo zaidi na kauli chanya za viongozi wao. Inapotokea kiongozi, tena kiongozi mkuu, kutoa kauli kama hii ya Kikwete, kwa kweli inawakatisha tamaa sana.
Sijiik kama Kikwete alijiuliza iwapo madaktari hao wakiondoka ndio itakuwa suluhisho la kukatishamigomo kutokana na malipo finyu? Au, wakiondoka madaktari hao ndio huduma za afya zonakuwa bora?
 
atapatikana mwingine kwa njia hizo hizo alizopatikana yeye.

Njia ni hizi: S/Msingi 7, Sekondari 6, Shahada ya kwanza 6, kuwa wa watoto 4 na kuwa mpasuaji 4 jumla ni miaka 27 hao watanzania watazaliwa kweli waweje? Tusichukue majibu mepesi kujibu hoja nzito, kumtayarisha daktari bingwa inachukua muda mrefu na bado kumfanya awe mzoefu inachukua muda mrefu zaidi kwa hiyo labda kama wewe umeshamaliza kuzaa na watoto wako ni wazee lakini hata hivyo wajukuu wako watazaa watoto watakaokuwa kama waliolishwa dawa ya 'thalidomide' ukitaka google upate undani wake zaidi maana unashabikia kitu usichokijua naona!
 
kuna madaktari wanaotembeza cv zao wanatafuta kazi,haya sasa mambo hayo.inaitwa bandua,bandika

Qualified dr. from qualified training institute with required credits hawezi kuzunguka kutafuta kazi. Kama ni wale ambao wamesoma vyuo ambavyo not certified na pass za mashaka ni lazima watembeze CV. Hivyo kama ni bandika bandua angalieni isiwe na madhara!!! Badala ya kupasua mguu unapasua kichwa!!! Au unachoma sindano ambayo haikutakiwa na matokeo yake paralysis!!! Udaktari ni fani ambayo inahitaji uangalifu na heshima. Matashi yasiyokuwa na tija kutoka kwa viongozi wetu yataleta madhara sana kwa huduma za afya. I tell you Drs wana hasira sana, wamekatishwa tamaa.
 
Njia ni hizi: S/Msingi 7, Sekondari 6, Shahada ya kwanza 6, kuwa wa watoto 4 na kuwa mpasuaji 4 jumla ni miaka 27 hao watanzania watazaliwa kweli waweje? Tusichukue majibu mepesi kujibu hoja nzito, kumtayarisha daktari bingwa inachukua muda mrefu na bado kumfanya awe mzoefu inachukua muda mrefu zaidi kwa hiyo labda kama wewe umeshamaliza kuzaa na watoto wako ni wazee lakini hata hivyo wajukuu wako watazaa watoto watakaokuwa kama waliolishwa dawa ya 'thalidomide' ukitaka google upate undani wake zaidi maana unashabikia kitu usichokijua naona!

Mkuu pongezi sana. Umeweka data wazi. Nami naendelea kurudia Udaktari si mchezo. Ninawaheshimu watoa huduma ya afya kuliko kitu chochote. Ukiachia utashi wa Mungu wa kukufanya wewe uishi but pia hawa madaktari wanatusaidia sana kuongeza miaka ya kuishi. Kweli kila mfanyakazi ana mchango kwa serikali but wa afya na elimu are over and above.
 
Anaitwa Dr. Mng'ong'o ..hapana, uliowataja mkuu ni Pediatricians ( Pediatric Physicians), na aliyeondoka ni Pediatric Surgeon...so hawawezi fanya upsauaji kwani si speciality yao...ila aliondoka zamani mkuu yapata miezi miwili sasa.
Sure ni paediatric surgeon, ila sina hakika kama yupo pekeyake, ila kuna Dr. Sayi, mara nyingi alikuwa anafanya operation za watoto sina hakika kama ni paediatric surgeon au la.
Huyo mama alikuja muhimbili nadhani kati ya 2006 au 2007 akitoke KCMC. nadhan ameonja machungu ya kufanya kazi na serikali isiyojali na kuthamini michango ya wataalam. Nenda mama kapumzike, uilinde heshima yako dhidi ya kashfa za huyo Dk. ambaye hana sifa za kupewa hizo PhD
 
Sure ni paediatric surgeon, ila sina hakika kama yupo pekeyake, ila kuna Dr. Sayi, mara nyingi alikuwa anafanya operation za watoto sina hakika kama ni paediatric surgeon au la.
Huyo mama alikuja muhimbili nadhani kati ya 2006 au 2007 akitoke KCMC. nadhan ameonja machungu ya kufanya kazi na serikali isiyojali na kuthamini michango ya wataalam. Nenda mama kapumzike, uilinde heshima yako dhidi ya kashfa za huyo Dk. ambaye hana sifa za kupewa hizo PhD

Dr. Sayi is out of Med practise with Hospital G,ment mkuu...and no si Ped. Surgeon.
 
huu ni uongo,KCMC kuna madaktari bingwa wanaopasua watoto kila kukicha

Umeelewa alikuwa anamaanisha nini?
kwani mnavosema watanzania maskini kwani ni wote?Usishambulie kwa maneno makali kama hujui kilimaanishwa!
 
kama aliweza kufuatwa Muhimbili, atafatwa huko huko kaskazini hata kama ni Seriani au KCMC

jamani kwenye maswala muhimu kama afya ya m2, naomba madudu 2weke pembeni!, hili c pigo kwa jk au pinda, au mbowe au slaa, hili ni pigo jwa watz kama mimi ambao ha2wez kumudu matibabu ya private!!
 
wat2 wengene wanadharau, cz hajawakuta...haya mambo sio ya kupuuza..tz kila k2 ni siasa' i wsh madaktar walipwe vizur kuliko wabunge
 
wat2 wengene wanadharau, cz hajawakuta...haya mambo sio ya kupuuza..tz kila k2 ni siasa' i wsh madaktar walipwe vizur kuliko wabunge!!
 
Kama kuna muhusika anasoma thread hii anisikilize kwa makini, Namfahamu vyema Dr Catherine Mng'ong'o alimfanyia oparesheni mtoto wangu.

Sasa nawashauri Serikali kuna daktari wenu huku mtaani anaitwa Dr Kabote mlimdisco KCMC wakati anachukuwa mafunzo yake ili awe daktari Bingwa wa huo upasuaji weni, mimi si mtaalamu wa hayo majina.

Dr Kabote mkamfukuza kazi na kodi zetu tulizomsomesha zimegeuka useless, yuko mtaani anakunywa pombe tu 24/7. pls namfamu huyu Dr Kabote kweli ni mlevi lakini pls hebu mrudisheni huyu mtu afanye kazi, kwani nilimjuwa Dr Catherine kupitia Dr Kabote na Dr Catherine akasema Kabote ni sinior sana kwake kwenye hayo mambo ya upasuaji, na ilibidi Dr Kabote ndio aanze kuwa Daktari Bingwa kabla ya Catherine.

Pls nyinyi serikali dhaifu hebu njooni mumtowe huyu Dr huku mtaani analewa tu wakati tumemsomesha kwa gharama kubwa sana.

Ni majuzi nilikuwa najiuliza alipoishia Dr Kabote. Taarifa hii inasikitisha!
 
Kumbe Tanzania nzima kuna Pediatric Surgeon mmoja tu sasa humu Jamvini kuna kundi linajitapata kuwa ni wasomi kumbe hakuna kitu porojo tu.
 
Back
Top Bottom