Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Mara kadhaa tumeshuhudia makundi mbalimbali ya watumishi wa umma yakiingia mgogoro ma Serkali kubwa likiwa ni maslahi.
Nitumie nafasi hii kuongelea MADAKTARI na WALIMU. migoggo ya makundi haya mawili dhidi ya Serikali mara kadhaa imekuwa na sura tofauti husani hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa na makundi haya. Nina miaka mingi sana sijashuhudia Walimu wakifikia hatua ya kugoma toauti ya Madaktari ambao mara kadhaa wameamini kuwa migomo ndiyo suluhisho la madai yao. Hii tafsiri yake ni nini? Je Madaktari ni muhimu zaidi ya walimu?. Inawezekana ni kweli kwa vile pamoja na kwamba wamefundishwa na walimu bado Mwalimu hurudi kwa Daktari huyo huyo ili kulinda afya yake. Je ulinzi wa uhai wa watu ni kigezo tosha cha Daktari kuwa nguvu zaidi ya mtumishi mwingine wa umma? Mbona inaonekana kama ilikuwa ni lazima Daktari azaliwe, ila asiye Daktari alizaliwa kwa makosa? Madaktari mkae chini na Serikali mpate suluhisho badala ya kutumia ubabe kwa vile mnajua mmebeba uhai wa watu. Hizo talanta kawapa Mungu. Muwe kama walimu, mtambue kuwa ninyi ni watoa huduma mliotumwa na mwenyezi Mungu kufanya kazi hiyo kwa alijua watakuwepo watu wana matatizo na suluhisho ni ninyi.
Nitumie nafasi hii kuongelea MADAKTARI na WALIMU. migoggo ya makundi haya mawili dhidi ya Serikali mara kadhaa imekuwa na sura tofauti husani hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa na makundi haya. Nina miaka mingi sana sijashuhudia Walimu wakifikia hatua ya kugoma toauti ya Madaktari ambao mara kadhaa wameamini kuwa migomo ndiyo suluhisho la madai yao. Hii tafsiri yake ni nini? Je Madaktari ni muhimu zaidi ya walimu?. Inawezekana ni kweli kwa vile pamoja na kwamba wamefundishwa na walimu bado Mwalimu hurudi kwa Daktari huyo huyo ili kulinda afya yake. Je ulinzi wa uhai wa watu ni kigezo tosha cha Daktari kuwa nguvu zaidi ya mtumishi mwingine wa umma? Mbona inaonekana kama ilikuwa ni lazima Daktari azaliwe, ila asiye Daktari alizaliwa kwa makosa? Madaktari mkae chini na Serikali mpate suluhisho badala ya kutumia ubabe kwa vile mnajua mmebeba uhai wa watu. Hizo talanta kawapa Mungu. Muwe kama walimu, mtambue kuwa ninyi ni watoa huduma mliotumwa na mwenyezi Mungu kufanya kazi hiyo kwa alijua watakuwepo watu wana matatizo na suluhisho ni ninyi.