CV ya Freeman Mbowe hii hapa

Status
Not open for further replies.
Wahenga wanasema kuoa ni moyo na wala si utajiri. Mimi sikufanikiwa kusoma ila napenda wasomi na nimewasaidia wengi waliotaka kusoma

Sasa napenda nitoe Fursa kwa msemaji Wa chama kama atakuwa tayari kufanya mitihani ya marudio ya kidato cha sita ili kuweka sawa maeneo Fulani Fulani ya elimu yake, nitagaramia garama zoteeeeee.

Nawasilisha: kwa mawadiliano piga namba +12255884489
 
hahahaha! changamkie Fursa. hizi elimu za hapa na pale hazina nafasi kwenye serikali ya magufuli
 
Mi nakushauri bora u mdhamini yule Mwenyekiti ambaye cheti chake cha kidato cha nne anacho lakini kimepotea akalipie 'lost report' polisi ili atangaze kupotelewa na cheti. Kwani hata matokeo ya hicho cheti hakumbuki.Huyo aliyepata ziro achana nae huyo, hana uwezo wa kusoma.
 
Mi nakushauri bora u mdhamini yule Mwenyekiti ambaye cheti chake cha kidato cha nne anacho lakini kimepotea akalipie 'lost report' polisi ili atangaze kupotelewa na cheti. Kwani hata matokeo ya hicho cheti hakumbuki.Huyo aliyepata ziro achana nae huyo, hana uwezo wa kusoma.

mmhh! wewe haumtakii mema msemaji wetu! au unataka atumbuliwe uchukue hiyo nafasi?
 
Freeman Aikael Mbowe alisoma elimu ya msingi katika shule ya Msingi Lambo na kufanikiwa kufaulu.Alifaulia kwenda shule ya Sekondari Kibaha mkoa wa Pwani.

Alipohitimu kidato cha nne Kibaha Sekondari, alifanikiwa kujiunga na kidato cha tano IHUNGO Sekondari Manispaa ya Bukoba. Baadaye alielekea nchini Uingereza kwa masomo zaidi.

Uingereza alisoma programu inaitwa PPE (Politics, Philosophy, and Economics). Ni programu ambayo ilianzishwa na Uingereza (Waingereza) kwa ajili ya watumishi serikalini. Baadaye nchi nyingine kama US na SA zimeshaanzisha programu hiyo. Kwa UK inatolewa kama first degree tu.

Sasa hivi Mbowe anamalizia MBA in Leadership and Sustainability kutoka Chuo Kikuu cha Cumbria.

SOURCE :Ansbert Ngurumo classmate wake Freeman Aikael Mbowe Uingereza.
 
Hehehehe eti alisoma program wakati huo hiyo program walikuwa wanahitimu kwa level ipi ?
Na ni chuo gani kilikuwa kinatoa hiyo program
 
Our next original professor
Amesoma mpaka raha na English yake ni ya BBC London world service.

Sio Ile ya actuaree on behalf of sheiself
 
Magoiga SN-Mwanza

Kwa takribani wiki mbili sasa nimekuwa nikihoji kuhusu giza lililotanda katika historia ya safari ya kielimu ya Freeman. Nimefanya hivyo kwa makusudi kabisa ili kuweka uwazi wa historia yake maana ni kiongozi mkubwa wa kitaifa ambaye wengi wangependa kujifunza mengi kutoka kwake au hata kuandika vitabu vya harakati za kisiasa nchini kwa kumtukama nguzo (case study) ya siasa za upinzani nchini. Baada ya kufanikiwa kuijua historia ya safari ya kielimu ya huyu Mh, nitamuandalia taarifa ya historia yake kielimu itakayosaidia watu kumjua vyema zaidi.

Katika kukazia nia yangu niliainisha maswali kafhaa ambayo yalitumika kama mwongozo wa hoja yangu ya kuhoji safari ya kielimu ya kiongozi huyu. Maswali yenyewe ni;

Alisoma wapi kwa maana ya shule? Alisoma Mwaka Gani mpaka gani? Alikua akitumia majina gani? Alisoma na Nani? Baba Mkwe alitumia kigezo gani kumuajiri BOT?

Katika orodha hii ya maswali yangu ambayo nimeyatumia kama hadidu rejea ktk hii hoja ya kuhoji uwazi ktk SAFARI ya kielimu ya Freeman kuna mtu mmoja amejaribu kutengeneza majibu mepesi na kuyasambaza kama majibu kamili ya hoja yangu. Nimeyasoma hayo majibu na kugundua kuwa mwandishi amejaribu kujibu maswali ya Mtihani wa hesabu kwa kutumia majibu ya Mtihani wa Kiingereza. Yote ni majibu lakini miyihani tofauti, uwezekano wa kupata ziro ni mkubwa sana LABDA aombe mtihani uwe wa majibu ya kuchagua (multiple choice) A, B, C, D nk Anaweza kubahatisha
Yasome Haya Majibu Yao Kisha Nitaendelea ¶¦¶ ️NANUKUU
2935.png
⤵️

"MBOWE NCHINI DENMARK ALIYASEMA HAYA ENZI HIZO
Freeman Aikael Mbowe alisoma elimu ya msingi katika shule ya Msingi Lambo na kufanikiwa kufaulu.Alifaulia kwenda shule ya Sekondari Kibaha mkoa wa Pwani.

Alipohitimu kidato cha nne Kibaha Sekondari, alifanikiwa kujiunga na kidato cha tano IHUNGO Sekondari Manispaa ya Bukoba. Baadaye alielekea nchini Uingereza kwa masomo zaidi.

Uingereza alisoma programu inaitwa PPE (Politics, Philosophy, and Economics). Ni programu ambayo ilianzishwa na Uingereza (Waingereza) kwa ajili ya watumishi serikalini. Baadaye nchi nyingine kama US na SA zimeshaanzisha programu hiyo. Kwa UK inatolewa kama first degree tu.

Sasa hivi Mbowe anamalizia MBA in Leadership and Sustainability kutoka Chuo Kikuu cha Cumbria. Kwa taarifa nilizonazo
Source: Ansbert Ngurumo classmate wake Freeman Uingereza" - Mwisho wa Kunukuu

Kwa kifupi majibu hayo yamelenga kujibu maswali yote niliyouliza, lakini ukiyasoma utagundua kiwa yamejibu kipengele kimoja pekee kinachohoji ALISOMA WAPI? Hata hicho kipengele hakijajibiwa ipasavyo, wamekigusa tu.

Kwanza ikumbukwe kuwa haya majibu yametolewa baada ya qiki mbili za kuhoji kuhusu historia ya safari ya kielimu ya huyu Mh. Kwa wiki mbili tumeambulia matusi, dhihaka, na mipasho huku wakikwepa hoja ya msingi na kujaribu kuanzisha hoja tifauti na mipasho isiyo na mwisho.

Lakini ktk vyote kuna kitu nimejifunza kuhusu suala la Historia ya safari ya kielimu ya huyu kiongozi wao. Nimejifunza kuwa wafuasi wengi wa hu msafara wa Kibwetere hawaijui historia ya safari ya kielimu ya kiongozi wao. Hakuna mwenye taarifa ya uhakika, walio wengi wanahisi au hata kufuata mkumbo tu. Ukiwabana huchagua matusi kama majjbu ya hoja iliyo mezani.

Ningewashauri kuwa badala ya kutumia nguvu kubwa kujifanya kutetea ilihali hata wao wenyewe hawana majibu ni bora waungane na sisi tusiojua tulioamua kuhoji ili mwisho wa siku na wao waijue historia ya mmiliki wa akili zao. Ni raha na inakupa nguvu mpya kuijua vyema Historia ya kiongozi wako. Maana unaweza hata kuandika kitabu kuhusu kiongozi huyo.

JE MAJIBU HAYO WALIOYATOA NI SAHIHI KUJARIBU KUJIBU HOJA YANGU NI SAHIHI ??

Hayo majibu yanaweza kuwa sahihi kabisa au yakawa yameongezewa chumvi nyingi ili kujaribu kumuokoa kiongozi wao. Nasema hivyo kutokana na mwongozo wa maswali niliyouliza kama ifuatavyo ;

i) Hakuna sehemu ktk majibu yao walipotaja mwaka hata mmoja ambao Freeman alianza shule ktk ngazi flani ya elimu na kumaliza. Yaani haioneahi alisma hapo Lambo kuanzia mwaka gani mpaka gani, Haionyeshi alisoma Kibaha mwaka gani mpaka gani, haionyeshi alisoma IHUNGO mwaka gani mpala gani, haionyeshi alisoma hiyo degree huko Uingereza mwaka gani mpaka gami, haionyeshi hiyo Master degee aliianza mwaka gani. Kwa ufupi swali la Alisoma Mwaka Gani mpaka Gani limekosa MAJIBU sahihi

ii) Walipoanza kuhusu elimu yake ya msingi wametaja kuwa Freeman alifaulu na kujiunga Kibaha Sekondari, lakini walipofika kidato cha nne hawakusema kuhusu kufaulu, na walipofika kidato cha sita hawakusema kuhusu kufaulu. Kama kufaulu kulikuwa hakuna maana ktk majibu yao kulikuwa hakuna maana kutaja kuhusu ufaulu darasa la saba. Hata hivyo hoja yangu haina shida kujua Ufaulu au Kufeli kwake, bali nimejikita zaidi ktk kijua historia ya safari yake kielimu. Ila kwa kuwa mmeanza kuonyesha kuwa alifaulu darasa la saba, basi ni vyema kila ngazi ya elimu mngesema kama alifaulu au lah

iii) Mwanzo wa maelezo wameweka kichwa cha habari kinachosemeka kuwa 'MBOWE NCHINI DENMARK ALIYASEMA HAYA ENZI HIZO' wakimaanisha kuwa hayo majibu yametokana na maelezo ya huuo kiongozi. Lakini wakasahu mwishoni kabisa mwa maelezo wakataja sehemu ambayo hayo maelezo yametoka. Wakasema 'Source: Ansbert Ngurumo classmate wake Freeman Aikael Mbowe Uingereza'

iv) Haya maelezo wanayoyaita majibu ya hoja yangu, ambayo wanayasambaza mitandaoni inaonekana chanzo chake ni myu mmoja tu, anayeitwa Ansbert Ngurumo.
1f603.png
1f603.png
1f603.png
yaani maelezo ya mtu mmoja pekee ndiyo yanayosambazwa na vijana zaidi ya 500 ktk mitandao ya kijamii. Hii inatoa tafsiri kuwa Hakuna kati yao aliyekuwa akijua chochote kuhusu mmiliki wao isipokuwa Ansbert Ngurumo aliyetambulishwa kama Classmate wa Freeman huko Uingereza
1f603.png
1f603.png
au kwa lugha nyingine ikiwa aliyoyaandika Ngurumo ni KWELI, inatoa tafsiri kuwa Ansbert Ngurumo ndiye mtu pekee aliye hai ambaye angalau amejaribu kuandika kitu kuhusu historia ya safari ya kielimu ya Freeman. Huyu mtu anapaswa kulindwa sana maana akitoweka historia ya safari ya kielimu ya kiongozi huyu inaweza kufa milele.

v) Imetajwa mara nyingi kuwa Freeman alipata Ziro ktk matokeo ya kidato cha sita
1f602.png
1f602.png
1f602.png
1f603.png
1f603.png
siku zote huwa nawashauri kuwa kabla hujakusanya karatasi la mtihani jifunze kuyasoma majibu yako yote huenda ukajikuta unarudia darasa kwa kujibu 'out of poit'. Iwapo Freeman alijiunga na hiyo wanayoiita degree ya kwanza Uingereza, swali linakuja alijiunga kwa kutumia ufaulu wa matokeo ya kidato cha nne au cha sita?? Maana form six alipata ziro, haiwezekani akatumia matokeo ya kidato cha sita, itakuwa alitumia yale ya kidato cha nne. Kama ndiyo aliweza vipi kujiunga na degree bila EQUIVALENT?? yaani diploma nk?

Kama alitumia diploma mbona kwenye majibu yao wanayoyaita ya msingi hakuna kipengele kinachoonyesha kuwa alisoma diploma kabla ya hiyo degree ??

vi) Wanasema alijiunga na masomo ya PPE, programu iliyoanzishwa kwa ajili ya watumishi wa serikalini. Sasa wakati huo Mbowe alikuwa ni mtumishi wa serikali ipi?? Au waliruhusiwa hata wasiokuwa watumishi kusoma??

vii) Niwashauri hao wanaojaribu angalu kumjibia mmiliki wao kuwa, wasisahau maswali ya msingi. Waende taratibu ili waweze kujibu yote kwa ufasaha. Alisoma wapi? Alitumia majina gani kidato cha sita?? Alisoma Mwaka Gani mpaka gani? Baba Mkwe alitumia vigezo gani kumuajiri pale Benki Kuu?

Bomu la Leo

Inasemekana kuwa kinachofanya taarifa a safari ya kielimu ya Freeman hususani ngazi ya form six haipatikani kirahisi, ni kwa sababu huenda sisi tunaitafuta taarifa hiyo kwa kutumia jina lake la Freeman. Lakini inatajwa kuwa kidato cha sita pale ihungo SURA ilikuwa ya Freeman ila jina haikuwa lake. Maana inasemekana kuwa alitumia jina la mtoto aliyefaulu, ila alipoanza kulisomea hilo jina yeye akalipa zawadi ya ziro form six. Hii ni taarifa ambayo siyo rasmi

Magoiga SN-Mwanza
 
JAMANI WANA JF MLIOPO HUMU NILIKUWA NAPENDA KUFAHAMU YA MWENYEKITI WA CHADEMA AMBAE KWA SASA NI KIONGOZI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom