Leo ni siku ya pili wanafunzi wa chuo kikuu cha Muhimbili (IHAS) hawajaingia madarasani au wodini kufundishwa kwa kile kinachodaiwa kuwa chuo hakina chakula kwa ajili ya wanafunzi. Chuo kilifunguliwa jana Jumatatu lakini hakuna kusoma kwa wasababu hakuna chakula.
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ndiyo yenye wajibu wa kutoa fedha kwa ajili ya chakula. Mkurugenzi wa IHAS alifika Wizarani (MoHSW) jana na haijafahamika mara moja aliambiwa nini ila hakuna matumaini kwa sasa, Wizara haina fedha.
Uongozi wa chuo unakwepa hata kukutana na wanafunzi na hakuna kinachoelezwa. Wanafunzi hao wanaosoma kozi mbalimbali za afya, kama uuguzi, ufamasia, elimu ya mionzi, sayansi ya baabara n.k hawajui nini cha kufanya huku wanaoishi jijini Dar wakirudi majumbani.
Hali si shwari kwa baadhi yao hasa wanaotoka nje ya Dar kwani wanaishi kwa kuwaomba wenzao wanaishi jijini au angalau wenye vijipesa kuwasaidia kupata chakula.
Waziri na Naibu Waziri wake, sijui wanalipi la kutueleza kwa sasa.
Taarifa hizi zinatoka ndani ya chuo hicho kwa wanafunzi wenyewe na baadhi ya viongozi wa chuo kwa sharti lakutotajwa majina au nyadhifa zao wenye uchungu na mateso wanayopata wanafunzi pamoja na kuzorotehwa kwa elimu nchini.
Binafsi niombe muhimili wa nne wa Taifa yaani Waandishi wa habari kufika chuoni hapo Muhimbi Institute ya Allied Sciences (IHAS) kudodosa na kuwapatia watanzania habari hizi.
Inaniuma sana...
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ndiyo yenye wajibu wa kutoa fedha kwa ajili ya chakula. Mkurugenzi wa IHAS alifika Wizarani (MoHSW) jana na haijafahamika mara moja aliambiwa nini ila hakuna matumaini kwa sasa, Wizara haina fedha.
Uongozi wa chuo unakwepa hata kukutana na wanafunzi na hakuna kinachoelezwa. Wanafunzi hao wanaosoma kozi mbalimbali za afya, kama uuguzi, ufamasia, elimu ya mionzi, sayansi ya baabara n.k hawajui nini cha kufanya huku wanaoishi jijini Dar wakirudi majumbani.
Hali si shwari kwa baadhi yao hasa wanaotoka nje ya Dar kwani wanaishi kwa kuwaomba wenzao wanaishi jijini au angalau wenye vijipesa kuwasaidia kupata chakula.
Waziri na Naibu Waziri wake, sijui wanalipi la kutueleza kwa sasa.
Taarifa hizi zinatoka ndani ya chuo hicho kwa wanafunzi wenyewe na baadhi ya viongozi wa chuo kwa sharti lakutotajwa majina au nyadhifa zao wenye uchungu na mateso wanayopata wanafunzi pamoja na kuzorotehwa kwa elimu nchini.
Binafsi niombe muhimili wa nne wa Taifa yaani Waandishi wa habari kufika chuoni hapo Muhimbi Institute ya Allied Sciences (IHAS) kudodosa na kuwapatia watanzania habari hizi.
Inaniuma sana...