Elimu ilifia Chuo Kikuu au ilizikwa chuo kikuu?

pefla

Senior Member
Jan 31, 2012
105
74
ELIMU ILIFIA CHUO KIKUU au ILIZIKWA CHUO KIKUU?
Imeandikwa na ASKOFU BAGONZA


Mzee Jenerali Ulimwengu kasema vyuo vikuu vyetu ni kama Extended High School. Anayebishi anitafute. Sababu ni nyingi kama idadi ya wajinga wetu waliosoma vyuo vikuu.

1. Tulipokuwa na Chuo Kikuu kimoja, tulifuta ujinga kwa asilimia 85. Sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 50, tuna wajinga wengi mitaani na maofisini kuliko enzi ya chuo kikuu kimoja.

2. Vyuo vilitengeneza wanasiasa na viongozi makini. Waliposhika madaraka wakapiga marufuku mijadala ya kisiasa na kijamii katika vyuo vikuu.

3. Wakati ule wanafunzi wa vyuo vikuu waliwahoji watawala, siku hizi watawala wanawahoji wanafunzi wa vyuo vikuu.

4. Vyuo vikuu vilizalisha wachambuzi na watafiti. Siku hizi vinazalisha ma-chawa na wapiga debe. Hata mbunge mwenye darasa la saba anaajiri wapiga debe kutoka chuo kikuu. Nampongeza.

5. Kuna tofauti ndogo inayotenganisha uchawa na ujinga. Wote wanazalishwa katika vyuo vikuu. Mmoja anaishi ofisini na mwingine anaishi mitaani akiunga mkono asiyoyajua.

6. Elimu ya wakati ule ilichochea uasi mtakatifu (holy rebellion). Hii ya sasa inachochea woga na utii usiomnufaisha anayetii.

Nini kilitokea?

Waliohitimu chuo kikuu walienda kuua elimu kuanzia shule za msingi. Vyuo vikuu vikageuka kuwa mhanga wa mafanikio yake. Kwa hiyo elimu ilifia chuo kikuu na kuzikwa chuo kikuu.Shule za Msingi na sekondari ni vitalu vya uzalishaji unaoenda kukuzwa chuo kikuu.

FB_IMG_1700793092472.jpg
 
Unapofika chuo kikuu unabidi kuhakikisha unajitengea Muda wa kutafuta Sana MAARIFA ikiwemo kusoma VITABU mbalimbali maana ipo wazi Elimu yetu bado ipo Nyuma SANA katika kumuibua yule aliyepo ndani yako.

Hivyo kama kijana kujitambua na kujua unahitaji nini katika Maisha yako hilo Jambo sio la serikali Wala wanasiasa ni Jambo lako mwenyewe.
 
Dah,ila Mkuu wa Chuo cha Biashara CBE naona anaendesha mijadala ya kisomi.Ila juzi kati kumwalika JK ambaye amerusha dongo Ikulu.

Namuunga mkono JK,Samia hasikilizi ushauri,Mimi mwenyewe nimeshawai kumpa ushauri wa kitaalamu kabisa juu ya namna ya kutangaza Utalii ila aliishia ku-like yeye na Waziri Mkuu wake.
 
Dah,ila Mkuu wa Chuo cha Biashara CBE naona anaendesha mijadala ya kisomi.Ila juzi kati kumwalika JK ambaye amerusha dongo Ikulu.
Namuunga mkono JK,Samia hasikilizi ushauri,Mimi mwenyewe nimeshawai kumpa ushauri wa kitaalamu kabisa juu ya namna ya kutangaza Utalii ila aliishia ku-like yeye na Waziri Mkuu wake.
Wameua elimu na kila kitu kwa upumbavu wao, lengo la CCM ni nchi iwe na wajinga wengi ili wachaje waendele kula mema ya nchi.
 
ELIMU ILIFIA CHUO KIKUU au ILIZIKWA CHUO KIKUU?
Imeandikwa na ASKOFU BAGONZA


Mzee Jenerali Ulimwengu kasema vyuo vikuu vyetu ni kama Extended High School. Anayebishi anitafute. Sababu ni nyingi kama idadi ya wajinga wetu waliosoma vyuo vikuu.

1. Tulipokuwa na Chuo Kikuu kimoja, tulifuta ujinga kwa asilimia 85. Sasa tuna vyuo vikuu zaidi ya 50, tuna wajinga wengi mitaani na maofisini kuliko enzi ya chuo kikuu kimoja.

2. Vyuo vilitengeneza wanasiasa na viongozi makini. Waliposhika madaraka wakapiga marufuku mijadala ya kisiasa na kijamii katika vyuo vikuu.

3. Wakati ule wanafunzi wa vyuo vikuu waliwahoji watawala, siku hizi watawala wanawahoji wanafunzi wa vyuo vikuu.

4. Vyuo vikuu vilizalisha wachambuzi na watafiti. Siku hizi vinazalisha ma-chawa na wapiga debe. Hata mbunge mwenye darasa la saba anaajiri wapiga debe kutoka chuo kikuu. Nampongeza.

5. Kuna tofauti ndogo inayotenganisha uchawa na ujinga. Wote wanazalishwa katika vyuo vikuu. Mmoja anaishi ofisini na mwingine anaishi mitaani akiunga mkono asiyoyajua.

6. Elimu ya wakati ule ilichochea uasi mtakatifu (holy rebellion). Hii ya sasa inachochea woga na utii usiomnufaisha anayetii.

Nini kilitokea?

Waliohitimu chuo kikuu walienda kuua elimu kuanzia shule za msingi. Vyuo vikuu vikageuka kuwa mhanga wa mafanikio yake. Kwa hiyo elimu ilifia chuo kikuu na kuzikwa chuo kikuu.Shule za Msingi na sekondari ni vitalu vya uzalishaji unaoenda kukuzwa chuo kikuu.

View attachment 2822820
Cc: PASKALI mayalla choice variables Tlaatlaah
 
Mie naona tatizo lipo ktk WAZAZI.

Ndio.

Nasisitiza sana kumjenga mtoto wako wewe mwenyewe kwa kumpa maarifa au njia ya kupata maarifa. Wazazi wengi ndio hao product ya Elimu mbovu, na wengine hata Elimu hakuna. Hana uwezo wa kujua ni kipi cha kumlisha mtoto wake ili baadae awe na ujuzi flani.

Wazazi wanategemea Waalimu ndio wawaandae watt wao. Kumbe waalimu wenyewe ndio hivyo hamna kitu.

Mtoto ni kama udogo utaamua utengeneze bakuli, sahani, kikombe etc.
 
Sasa huyu anamlaumu nan ? Huyu ana point ila tatizo ni yeye na kama vile hajielewi ,tatizo lingine ana kitu kama educational ego ambayo haina maana.

Mijadala ya kisiasa ndio imekaa kichwani mwake ila hatambui katika nchi zetu sio mahali pake na ndio chanzo cha kupata viongozi wabovu...

Ukisoma hao maprofessor wengi kama yeye wamesoma elimu ya zamanu ila hakuna kitu wamefanya zaid kufanya kazi nje ya nchi...

Kama yeye na kundi la generation yake wameshindwa mpaka leo especially mtu kama Nyerere alishindwa kabisa na sera zake za kucopy na kupaste.

The man is full doubts but no single solution ...Moja kati ya wasomi wa hovyo kutokea ni hyu mzee hana cha maana wao na elimu yao wa ukoloni ndio walishinwa kuleta ukombozi ,kizazi chao za maprofessor hawana jipya na wamesoma hiyo elimu mjadala.

Badala mtu na akili zake akae chini aeleze mambo ya ubunifu ,kichwa kimejaa siasa mpaka mtu kazeeka ,kuna nchi wa hawana hizi mambo hata za kukosoa nenda Russia ,china, Korea ,iran still wapo far kiuchumi ...Instead watu wawe bussy kweny innovation yeye akili yake ni siasa tu ndio chanzo cha wezi.

Nchi zinazofanya mijadala kwa sasa kama USA wale wana haki ya kuwa na milumbano ya kisiasa kwa vile walishakuwa njema kweny uchumi miaka kiboo watu walishajikomboa tangu mwaka 1776..

Tanzania ijikomboe kwanza kweny uchumi ndio mje kweny siasa.
 
Sasa huyu anamlaumu nan ? Huyu ana point ila tatizo ni yeye na kama vile hajielewi ,tatizo lingine ana kitu kama educational ego ambayo haina maana.

Mijadala ya kisiasa ndio imekaa kichwani mwake ila hatambui katika nchi zetu sio mahali pake na ndio chanzo cha kupata viongozi wabovu...

Ukisoma hao maprofessor wengi kama yeye wamesoma elimu ya zamanu ila hakuna kitu wamefanya zaid kufanya kazi nje ya nchi...

Kama yeye na kundi la generation yake wameshindwa mpaka leo especially mtu kama Nyerere alishindwa kabisa na sera zake za kucopy na kupaste.

The man is full doubts but no single solution ...Moja kati ya wasomi wa hovyo kutokea ni hyu mzee hana cha maana wao na elimu yao wa ukoloni ndio walishinwa kuleta ukombozi ,kizazi chao za maprofessor hawana jipya na wamesoma hiyo elimu mjadala.

Badala mtu na akili zake akae chini aeleze mambo ya ubunifu ,kichwa kimejaa siasa mpaka mtu kazeeka ,kuna nchi wa hawana hizi mambo hata za kukosoa nenda Russia ,china, Korea ,iran still wapo far kiuchumi ...Instead watu wawe bussy kweny innovation yeye akili yake ni siasa tu ndio chanzo cha wezi.

Nchi zinazofanya mijadala kwa sasa kama USA wale wana haki ya kuwa na milumbano ya kisiasa kwa vile walishakuwa njema kweny uchumi miaka kiboo watu walishajikomboa tangu mwaka 1776..

Tanzania ijikomboe kwanza kweny uchumi ndio mje kweny siasa.
Katika majadiliano jadidi huwa ndio chanzo cha kujenga hoja zenye ubunifu ndani yake. Lakini bila kujua unawaza nini ni vigumu kupata views zako. Hivyo basi tutafute jukwaa la vijana lenye maona endelevu kama wewe tujenge nchi yetu
 
Cc: PASKALI mayalla choice variables Tlaatlaah
ndio maana waswahili husema ujana maji ya moto. Utumie vizuri kuepuka majuto na maumivu moyoni baadae.

Mzee ana mawazo mazuri sana. Lakini pia kama haridhiki na mawazo na uwezo wa kujieleza na kuhoji wa vijana wanaohitimu vyuo vikuu kwasababu hakuna mijadala hilo ni tatizo lake binafsi. Lakini vijana wa sasa wana ujuzi, umahiri na uwezo mkubwa sana wa kujieleza na kuhoji mambo.

Na mimi binafsi na mpa pole sana generali kama jambo hilo linamkwaza. Mambo yanabadilika wakati wake uliisha, awape fursa vijana wajiandalie kesho yao kulingana na mazingira yao yaliopo.

Vijana wanaohitimu vyuo vikuu mbalimbali nchini. Wanaohitimu na kutoka na maarifa, ujuzi na umahiri mkubwa sana wa kadre mbalimbali na wanasonga mbele kwa furaha na mikogo kama yote ama hamuhudhuriagi graduations, wameridhika na kwakweli inaridhisha na kutia moyo sana.

Babu jenerali tunampenda na tunamuheshimu sana. Anajaribu kufundisha na kuichochea jamii ya hususani ya wasomi ujasiri wa kubeza kama ilivyo hulka yake. Umri wake umesonga kidogo ni vigumu vijana kumuunga mkono kwenye pendekezo lake. Nashukuru vijana na wasomi makini wamekua wakimpuuzia kisomi zaidi ,Mzee wetu huyu ambae tunaempenda sana asijiskie vibaya, na kwakweli wamefanikiwa pakubwa na mambo yanasonga vizuri...

Mawazo yake mazuri ikiwa yanafaa basi atathiminiwe na yatekelezwe na vyuo husika kwa wakati wana ona unafaa na kama jambo lenyewe linamanufaa.

Ana uhuru wa kutoa maoni, kukosoa, kupendekeza mambo yawe vipi ili tusonge mbele kama Taifa, ila nia yake ya ndani inafahamika vizur sana muda mrefu. Na kwahivyo hasira na ghadhabu ndani ya maoni mazuri sana ya generali ulimwengu vinafahamika sio jambo geni humu nchini.

Maoni yangu kwenye pendekezo na na maoni juu ya mijadala.

Mijadala mbalimbali ya kisiasa, kijamii na kiuchumi iendeshwe na vyama vya kisiasa, kupitia jumuiya zake mathalani jumuiya za vijana, wanawake, wazazi, chipukizi n.k ili kuwajengea vijana uwezo wa kujieleza na kuhoji, ikiwa hilo ndio tatizo kama anavyodai Mzee general ulimwengu.

Platforms za mijadala ni nyingi mno si vyuo vikuu tu.

Kwako Tindo
 
Sasa huyu anamlaumu nan ? Huyu ana point ila tatizo ni yeye na kama vile hajielewi ,tatizo lingine ana kitu kama educational ego ambayo haina maana.

Mijadala ya kisiasa ndio imekaa kichwani mwake ila hatambui katika nchi zetu sio mahali pake na ndio chanzo cha kupata viongozi wabovu...

Ukisoma hao maprofessor wengi kama yeye wamesoma elimu ya zamanu ila hakuna kitu wamefanya zaid kufanya kazi nje ya nchi...

Kama yeye na kundi la generation yake wameshindwa mpaka leo especially mtu kama Nyerere alishindwa kabisa na sera zake za kucopy na kupaste.

The man is full doubts but no single solution ...Moja kati ya wasomi wa hovyo kutokea ni hyu mzee hana cha maana wao na elimu yao wa ukoloni ndio walishinwa kuleta ukombozi ,kizazi chao za maprofessor hawana jipya na wamesoma hiyo elimu mjadala.

Badala mtu na akili zake akae chini aeleze mambo ya ubunifu ,kichwa kimejaa siasa mpaka mtu kazeeka ,kuna nchi wa hawana hizi mambo hata za kukosoa nenda Russia ,china, Korea ,iran still wapo far kiuchumi ...Instead watu wawe bussy kweny innovation yeye akili yake ni siasa tu ndio chanzo cha wezi.

Nchi zinazofanya mijadala kwa sasa kama USA wale wana haki ya kuwa na milumbano ya kisiasa kwa vile walishakuwa njema kweny uchumi miaka kiboo watu walishajikomboa tangu mwaka 1776..

Tanzania ijikomboe kwanza kweny uchumi ndio mje kweny siasa.
Huwezi kuitenga siasa na uchumi,
USA walijikomboa kwanza kisiasa kutoka Uingereza ndio wakajenga uchumi walio nao sasa.
 
ndio maana waswahili husema ujana maji ya moto. Utumie vizuri kuepuka majuto na maumivu moyoni baadae.

Mzee ana mawazo mazuri sana. Lakini pia kama haridhiki na mawazo na uwezo wa kujieleza na kuhoji wa vijana wanaohitimu vyuo vikuu kwasababu hakuna mijadala hilo ni tatizo lake binafsi. Lakini vijana wa sasa wana ujuzi, umahiri na uwezo mkubwa sana wa kujieleza na kuhoji mambo.

Na mimi binafsi na mpa pole sana generali kama jambo hilo linamkwaza. Mambo yanabadilika wakati wake uliisha, awape fursa vijana wajiandalie kesho yao kulingana na mazingira yao yaliopo.

Vijana wanaohitimu vyuo vikuu mbalimbali nchini. Wanaohitimu na kutoka na maarifa, ujuzi na umahiri mkubwa sana wa kadre mbalimbali na wanasonga mbele kwa furaha na mikogo kama yote ama hamuhudhuriagi graduations, wameridhika na kwakweli inaridhisha na kutia moyo sana.

Babu jenerali tunampenda na tunamuheshimu sana. Anajaribu kufundisha na kuichochea jamii ya hususani ya wasomi ujasiri wa kubeza kama ilivyo hulka yake. Umri wake umesonga kidogo ni vigumu vijana kumuunga mkono kwenye pendekezo lake. Nashukuru vijana na wasomi makini wamekua wakimpuuzia kisomi zaidi ,Mzee wetu huyu ambae tunaempenda sana asijiskie vibaya, na kwakweli wamefanikiwa pakubwa na mambo yanasonga vizuri...

Mawazo yake mazuri ikiwa yanafaa basi atathiminiwe na yatekelezwe na vyuo husika kwa wakati wana ona unafaa na kama jambo lenyewe linamanufaa.

Ana uhuru wa kutoa maoni, kukosoa, kupendekeza mambo yawe vipi ili tusonge mbele kama Taifa, ila nia yake ya ndani inafahamika vizur sana muda mrefu. Na kwahivyo hasira na ghadhabu ndani ya maoni mazuri sana ya generali ulimwengu vinafahamika sio jambo geni humu nchini.

Maoni yangu kwenye pendekezo na na maoni juu ya mijadala.

Mijadala mbalimbali ya kisiasa, kijamii na kiuchumi iendeshwe na vyama vya kisiasa, kupitia jumuiya zake mathalani jumuiya za vijana, wanawake, wazazi, chipukizi n.k ili kuwajengea vijana uwezo wa kujieleza na kuhoji, ikiwa hilo ndio tatizo kama anavyodai Mzee general ulimwengu.

Platforms za mijadala ni nyingi mno si vyuo vikuu tu.

Kwako Tindo
Typical chawa post 😂
 
ndio maana waswahili husema ujana maji ya moto. Utumie vizuri kuepuka majuto na maumivu moyoni baadae.

Mzee ana mawazo mazuri sana. Lakini pia kama haridhiki na mawazo na uwezo wa kujieleza na kuhoji wa vijana wanaohitimu vyuo vikuu kwasababu hakuna mijadala hilo ni tatizo lake binafsi. Lakini vijana wa sasa wana ujuzi, umahiri na uwezo mkubwa sana wa kujieleza na kuhoji mambo.

Na mimi binafsi na mpa pole sana generali kama jambo hilo linamkwaza. Mambo yanabadilika wakati wake uliisha, awape fursa vijana wajiandalie kesho yao kulingana na mazingira yao yaliopo.

Vijana wanaohitimu vyuo vikuu mbalimbali nchini. Wanaohitimu na kutoka na maarifa, ujuzi na umahiri mkubwa sana wa kadre mbalimbali na wanasonga mbele kwa furaha na mikogo kama yote ama hamuhudhuriagi graduations, wameridhika na kwakweli inaridhisha na kutia moyo sana.

Babu jenerali tunampenda na tunamuheshimu sana. Anajaribu kufundisha na kuichochea jamii ya hususani ya wasomi ujasiri wa kubeza kama ilivyo hulka yake. Umri wake umesonga kidogo ni vigumu vijana kumuunga mkono kwenye pendekezo lake. Nashukuru vijana na wasomi makini wamekua wakimpuuzia kisomi zaidi ,Mzee wetu huyu ambae tunaempenda sana asijiskie vibaya, na kwakweli wamefanikiwa pakubwa na mambo yanasonga vizuri...

Mawazo yake mazuri ikiwa yanafaa basi atathiminiwe na yatekelezwe na vyuo husika kwa wakati wana ona unafaa na kama jambo lenyewe linamanufaa.

Ana uhuru wa kutoa maoni, kukosoa, kupendekeza mambo yawe vipi ili tusonge mbele kama Taifa, ila nia yake ya ndani inafahamika vizur sana muda mrefu. Na kwahivyo hasira na ghadhabu ndani ya maoni mazuri sana ya generali ulimwengu vinafahamika sio jambo geni humu nchini.

Maoni yangu kwenye pendekezo na na maoni juu ya mijadala.

Mijadala mbalimbali ya kisiasa, kijamii na kiuchumi iendeshwe na vyama vya kisiasa, kupitia jumuiya zake mathalani jumuiya za vijana, wanawake, wazazi, chipukizi n.k ili kuwajengea vijana uwezo wa kujieleza na kuhoji, ikiwa hilo ndio tatizo kama anavyodai Mzee general ulimwengu.

Platforms za mijadala ni nyingi mno si vyuo vikuu tu.

Kwako Tindo
Unategemea mijadala yenye tija kutoka UVccm? Utangoja sana.
Ccm ina strategy ya kuwapumbaza vijana kwa kuwakoleza na muziki na mpira wa miguu ili wapumbae hivyo kuwatumia kirahisi kuendelea kutawala!!
Mbinu kama hizo Wabeligiji walizitumia huko Congo kwa kuwapumbaza wananchi kwa muziki na starehe huku wao wakichota maliasili za nchi.
 
Unapofika chuo kikuu unabidi kuhakikisha unajitengea Muda wa kutafuta Sana MAARIFA ikiwemo kusoma VITABU mbalimbali maana ipo wazi Elimu yetu bado ipo Nyuma SANA katika kumuibua yule aliyepo ndani yako.

Hivyo kama kijana kujitambua na kujua unahitaji nini katika Maisha yako hilo Jambo sio la serikali Wala wanasiasa ni Jambo lako mwenyewe.
Ni nani aliyehalalisha na kuhimiza matumizi ya vitini (handouts) badala ya vitabu vyuoni?! Ni mwanafunzi au utawala?! Utawala wa Chuo usiohimiza wanafunzi kutumia vitabu kama rejea, mwanafunzi atapata wapi guts ya kutafuta maarifa nje ya vitini ambapo ndo mitihani inatokea humohumo? Tatizo ni kubwa, siyo kama ulivyoshauri hapo juu.
 
Back
Top Bottom