Chanzo cha ukahaba na uzinzi

Danp36

JF-Expert Member
Jul 31, 2010
2,097
920
Hivi karibuni kumezuka na fasheni ya kuvaa nguo za kuacha wazi matiti kwa asilimia 75 yanaonekana mpaka kwa kinamama na makanisani hii inawafundisha nini watoto na ata ambao hawamjui mungu kwa kusingizia mungu anaangalia moyo?ukweli ni kwamba mungu anakaa patakatifu na alisema kilichopo ndani yamtu ndicho kionekanacho nje na vivyo kuvaa nusu uchi inaonesha kuna tamaa zinazowafuata watu mpaka makanisani,vilevile kwa wanao amini biblia imesema wanawake wavae mavazi yakujistili je wanao vaa mavazi nusu uchi kanisani na ata nje ya kanisa wanafuata maandiko yapi? kwa sababu niwana dini zote mbili zinatukataza.naomba mchango wako labda kuna cha kujitetea ninyi karibu kwa mchango wako.
 
Inawezekana wanawake wa Kikristo hawajafundishwa maadili mazuri. Sisi wenzenu, wanawake wa kiislamu huwa hawavai nguo fupi misikitini. Labda hampo serious kusimamia sheria za imani yenu.
 
Mtindo wa kuacha wazi matiti kwa kuyaonesha asilimia 75 je ni fashen au uzinzi?
 
Mtindo wa kuacha wazi matiti kwa kuyaonesha asilimia 75 je ni fashen au uzinzi?

kila mtu aliyetokana na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake;
wala hawezi wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu ametokana na Mungu;
naamu katika hili wana wa Mungu ni dhahiri, na wa shetani nao. Mtu yeyote asiyetenda haki
hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
 
Inawezekana wanawake wa Kikristo hawajafundishwa maadili mazuri. Sisi wenzenu, wanawake wa kiislamu huwa hawavai nguo fupi misikitini. Labda hampo serious kusimamia sheria za imani yenu.

.
Upo sawa kimaadili ila umepungungukiwa na jambo moja tu nalo ndio msingi mkuu wa yeyote anaetaka kuurithi ufalme wa Mungu. Mkabizi Bwana Yesu maisha yako, ili kumruhusu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako. NB Bwana! Hapo inamaanisha 'mwenye enzi yote yaani Yehova Mungu'
 
Mtindo wa kuacha wazi matiti kwa kuyaonesha asilimia 75 je ni fashen au uzinzi?

.
Mke huyaacha wazi asilimia mia kwa mmewe, na pia kwa mwanae anapomnyonyesha. Huo siyo uzinzi hata kidogo.
 
.......Hiyo ni fashion tu, vumilia kidogo itapita kama inakukwaza........sio uzinzi huo hata wanawake wenye ndoa zao wanaitinga.
 
Inawezekana wanawake wa Kikristo hawajafundishwa maadili mazuri. Sisi wenzenu, wanawake wa kiislamu huwa hawavai nguo fupi misikitini. Labda hampo serious kusimamia sheria za imani yenu.

ni sawa mkuu,
lakini bahati mbaya ni kwamba Mungu hakubinafisisha amri zake ama kuweka mtu wa kuzisimamia, bali kufundisha,
kwa kuwa mbinguni kila ataenda kama alivyo kuja, na wala mama hatachukua dhambi ya bintiye wala baba
hatachukua dhambi ya kijana wake wala mtoto hatachukua dhambi ya mamaye, kwa sababu hiyo
NENO likasema si wote wanitao Bwana Bwana watakaoingia mbinguni ni kwa sababu ya uwepo wa hao
wenye kufurahisha roho zao kwa kuiridhisha miili yao, unaweza ukasimamia sana sheria za imani kimwili lakini
watu wakavaa hijabu kweupe misikitini, lakini gizani ni mafirauni tu, maana hata wanaojitoa mhanga na kuua
watu wasiyo na hatia wanatii sana sharia za misikitini, sasa hapo sijui vipi
ene wei Mungu ndiyo anayeju yaliyo sirini mwa moyo wa mwanadamu
 
mzee we nenda kanisani na usali kwani ndicho kilichokupekeka huko na hivyo acha kuangalia wanawake wamevaa nini
 
ni sawa mkuu,
lakini bahati mbaya ni kwamba Mungu hakubinafisisha amri zake ama kuweka mtu wa kuzisimamia, bali kufundisha,
kwa kuwa mbinguni kila ataenda kama alivyo kuja, na wala mama hatachukua dhambi ya bintiye wala baba
hatachukua dhambi ya kijana wake wala mtoto hatachukua dhambi ya mamaye, kwa sababu hiyo
NENO likasema si wote wanitao Bwana Bwana watakaoingia mbinguni ni kwa sababu ya uwepo wa hao
wenye kufurahisha roho zao kwa kuiridhisha miili yao, unaweza ukasimamia sana sheria za imani kimwili lakini
watu wakavaa hijabu kweupe misikitini, lakini gizani ni mafirauni tu, maana hata wanaojitoa mhanga na kuua
watu wasiyo na hatia wanatii sana sharia za misikitini, sasa hapo sijui vipi
ene wei Mungu ndiyo anayeju yaliyo sirini mwa moyo wa mwanadamu

Ni kweli kila mtu atauchukua mzigo wake lakini sio kweli kuwa wazazi hawatolipwa kwa uzembe wa kutowaelekeza watoto wao maadili na sio kweli kuwa wachungaji hawatokuwa na fungu kwa kutofanyakazi zao za kuwaongoza waumini.
Angalau umekubali kuwa Waislamu hawafanyi watakavyo wakiwa msikitini na hufanya pale wanapokuwa gizani lakini mwenye kuposti post hii amekerwa zaidi na tabia ya kulidharau kanisa na iwapo wewe unakubali hivyo eti kwa kuwa Waislamu hujiripuwa kwa mabomu basi una kasoro hapo.
Kumbuka tu waliotengeneza nuklia na kuitumia (Hiroshima) si Waislamu bali ni wa dini nyengine
 
Hivi karibuni kumezuka na fasheni ya kuvaa nguo za kuacha wazi matiti kwa asilimia 75 yanaonekana mpaka kwa kinamama na makanisani hii inawafundisha nini watoto na ata ambao hawamjui mungu kwa kusingizia mungu anaangalia moyo?ukweli ni kwamba mungu anakaa patakatifu na alisema kilichopo ndani yamtu ndicho kionekanacho nje na vivyo kuvaa nusu uchi inaonesha kuna tamaa zinazowafuata watu mpaka makanisani,vilevile kwa wanao amini biblia imesema wanawake wavae mavazi yakujistili je wanao vaa mavazi nusu uchi kanisani na ata nje ya kanisa wanafuata maandiko yapi? kwa sababu niwana dini zote mbili zinatukataza.naomba mchango wako labda kuna cha kujitetea ninyi karibu kwa mchango wako.

Kweli ndugu Danp36,

Quran karimu inatwambia hivi,

Waambie Waumini wanaume wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao. Hili ni takaso bora kwao. Hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za wanayo yafanya. (Quran 24:30)

Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe uzuri wao isipo kuwa unao dhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, au wana wa kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenzao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, au wafwasi wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo yaliyo khusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajuulikane mapambo waliyo yaficha. Na tubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa.
(Quran 24:31)

Na waozeni wajane miongoni mwenu na wema katika watumwa wenu na wajakazi wenu. Wakiwa mafakiri Mwenyezi Mungu atawatajirisha kwa fadhila yake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa Mwenye kujua. (Quran 24:32)

Na wajizuilie na machafu wale wasio pata cha kuolea, mpaka Mwenyezi Mungu awatajirishe kwa fadhila yake. Na wanao taka kuandikiwa uhuru katika wale ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki, basi waandikieni kama mkiona wema kwao. Na wapeni katika mali ya Mwenyezi Mungu aliyo kupeni. Wala msiwashurutishe vijakazi vyenu kufanya zina kwa ajili ya kutafuta pato la maisha ya dunia, ilhali wao wanataka kujihishimu. Na atakaye walazimisha basi Mwenyezi Mungu baada ya kulazimishwa kwao huko, atawasamehe, kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu. (Quran 24:33)

Na kwa yakini tumekuteremshieni Ishara zilizo wazi na mifano kutokana na walio tangulia kabla yenu na mawaidha kwa wachamngu. (Quran 24:34)

Mwenyezi Mungu ni Nuru ya Mbingu na Ardhi. Mfano wa Nuru yake ni kama shubaka lenye kuwekwa ndani yake taa. Taa ile imo katika tungi. Tungi lile ni kama nyota inayo meremeta, inayo washwa kwa mafuta yanayo toka katika mti ulio barikiwa, mzaituni. Si wa mashariki wala magharibi. Yanakaribia mafuta yake kung'aa wenyewe ingawa moto haujayagusa - Nuru juu ya Nuru. Mwenyezi Mungu humwongoa kwenye Nuru yake amtakaye. Na Mwenyezi Mungu huwapigia watu mifano. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua kila kitu. (Quran 24:35)
 
mzee we nenda kanisani na usali kwani ndicho kilichokupekeka huko na hivyo acha kuangalia wanawake wamevaa nini

Aah no! Niende vp ili nisione wanawake wamevaa nini? Je nifumbe macho? Dini ya kweli ina nidhamu ya kila jambo. Na kama nidhamu hizo zinavunjwa ndani ya majumba ya ibada basi hakuna sehemu zitakapotekelezwa. Itakuwa ni sawa na punda kumbebesha mzigo wa vitabu.
 
Baba Enock hongera kwa kuleta topic hii. Kweli mmomonyoko wa maadili unachangiwa na wanawake wenyewe wakiwasaidia mabinti zao. Kuacha matiti nje ni utamaduni usio wetu waafrika. Wachungaji makanisani mkemee kwa nguvu zote kwani liko madhabahuni penu.
 
Back
Top Bottom