Abdul-Aziz Carter
Member
- Sep 27, 2023
- 7
- 23
Naitwa Abdul-Aziz Ally Carter mwanafunzi wa mwaka wa 3 chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM), nasomea historia na sayansi ya siasa,
Namba yangu ya usajili 2021-04-01016.
UDSM tunafundishwa kwa namna 2, lectures za Darasani na seminar presentation,
Kwenye seminar presentation ndiyo sehemu pekee ya ufundishaji ambayo wanafunzi tunaruhusiwa kutoa mawazo, kuuliza maswali na kutetea hoja zetu.
Kuna baadhi ya seminar leaders kutoka department ya utawala wa umma na sayansi ya siasa na department ya historia hawatutendei haki katika seminar presentation,
Tunapouliza maswali,kujenga na kutetea hoja zetu tunapokea majibu ya udhalilishaji na kukatisha tamaa mfano muongo, huna hoja nk pasina kuuliza chanzo cha taarifa tulichotumia au kuturekebisha kwa njia ya kistaarabu,
Na hivyo kutufanya baadhi ya wanafunzi kushindwa kuuliza maswali, Kuhoji au kutetea hoja kwa hofu ya kukosolewa na seminar leaders ,
Hili tatizo limekuwa sugu na hatuoni dalili za hao seminar leaders kubadilika hasa katika hizo department 2 nilizozitaja hapo juu,
Tunashindwa kutoa taarifa kwa mamlaka kwa kuwa kama seminar leader hatochukuliwa hatua tatizo linabaki kwa mwanafunzi maana seminar presentation zina alama 15 na seminar leader ndiyo mwenye maamuzi ya kukupa ngapi kati ya hizo,
Baadhi ya wanafunzi tunajifunza vyema kupitia mijadala, kuuliza maswali ,Kuhoji na kudadisi mambo lakini baadhi ya seminar leaders kutoka kwenye hizo department wanatunyima haki yetu ya kujifunza kwa kauli zao za kukatisha tamaa.
Naomba tusaidie kusambaza ujumbe wetu ,ufike wizara ya elimu ili kero hii itatuliwe.
Ahsante
Namba yangu ya usajili 2021-04-01016.
UDSM tunafundishwa kwa namna 2, lectures za Darasani na seminar presentation,
Kwenye seminar presentation ndiyo sehemu pekee ya ufundishaji ambayo wanafunzi tunaruhusiwa kutoa mawazo, kuuliza maswali na kutetea hoja zetu.
Kuna baadhi ya seminar leaders kutoka department ya utawala wa umma na sayansi ya siasa na department ya historia hawatutendei haki katika seminar presentation,
Tunapouliza maswali,kujenga na kutetea hoja zetu tunapokea majibu ya udhalilishaji na kukatisha tamaa mfano muongo, huna hoja nk pasina kuuliza chanzo cha taarifa tulichotumia au kuturekebisha kwa njia ya kistaarabu,
Na hivyo kutufanya baadhi ya wanafunzi kushindwa kuuliza maswali, Kuhoji au kutetea hoja kwa hofu ya kukosolewa na seminar leaders ,
Hili tatizo limekuwa sugu na hatuoni dalili za hao seminar leaders kubadilika hasa katika hizo department 2 nilizozitaja hapo juu,
Tunashindwa kutoa taarifa kwa mamlaka kwa kuwa kama seminar leader hatochukuliwa hatua tatizo linabaki kwa mwanafunzi maana seminar presentation zina alama 15 na seminar leader ndiyo mwenye maamuzi ya kukupa ngapi kati ya hizo,
Baadhi ya wanafunzi tunajifunza vyema kupitia mijadala, kuuliza maswali ,Kuhoji na kudadisi mambo lakini baadhi ya seminar leaders kutoka kwenye hizo department wanatunyima haki yetu ya kujifunza kwa kauli zao za kukatisha tamaa.
Naomba tusaidie kusambaza ujumbe wetu ,ufike wizara ya elimu ili kero hii itatuliwe.
Ahsante