Kucheleweshwa kwa malipo ya Boom kwa baadhi ya Wanafunzi wa UDSM tatizo liko wapi?

Sep 27, 2023
7
23
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliofanya mitihani ya supplementary na special hawajapata stahiki zao.

Hii ni wiki ya tano (5) sasa hii, sawa na mwezi 1 na wiki 1, Wanafunzi wamekuwa wakiishi katika mazingira magumu kutokana na changamoto za kiuchumi zilizo sababishwa na kucheleweshwa kwa pesa hizo.

Ukiingia kwenye mfumo wa mkopo (Account ya chuo ya ARIS3) inaonekana tayari Bodi ya Mikopo imeshaweka tayari location, wanafanya hivyo ili ionekane Mwanafunzi yupo chuo, kinachoonekana hakijafanyiwa kazi ni chuo chenyewe kutokamilisha mchakato ama wa kutuma majibu au majina.

Changamoto hii hasa imewakuta Wanafunzi wa Mwaka wa Pili na Watatu.

Daraja letu sisi ni Serikali ya Wanafunzi, tunachofanya tunaenda kuzungumza nao kisha wao ndio wanaotakiwa kuzungumza na uongozi wa chuo.

Tunaziomba mamlaka husika kufanya uchunguzi juu ya jambo hili na kuwasaidia wanafunzi hawa kupata stahiki zao.
aa2b268b-e8ba-4eb0-9614-f5165667ae0a.jpeg

====
====
1705994550299.png
 
Wanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM), waliofanya mitihani ya suplimentary na special hawajapata stahiki zao,
Hii ni wiki ya tano (5), sawa na mwezi 1 na wiki 1 wanafunzi wanaishi katika mazingira magumu kutokana na changamoto za kiuchumi zilizo sababishwa na kucheleweshwa kwa pesa hizo,
Tunaziomba mamlaka husika kufanya uchunguzi juu ya jambo hili na kuwasaidia wanafunzi Hawa kupata stahiki zao.
Bint yangu yupi kundi hili aiseee
 
Siyo udsm pekee kuna vyuo vingine vingi tu vimechelewesha matokeo ya wanafunzi na hivyo kupelekea wanafunzi hao kukosa stahiki zao mapema.

Ukienda kule katani naskia kuna baadhi ya program wanafunzi wote hawajapelekewa matokeo yao bodi regardless alikuwa ana supp au hana.

Maisha ya chuo ni magumu sana.
Muwafikirie vijana wetu kabla madudu yenu hayajaanza kutolewa kwa mitandao.

Tunatoa siku tatu vijana hao wawe wamepata stahiki zao la si hivyo.
Tunaanika madudu yenu waziwazi kama mange kimambi.
 
Kweli wanafunzi wana changamoto kubwa. Kumbuka kusoma na yaingie mwanafunzi anatakiwa kichwa kimetulia sio anafikiri mlo au kodi.
Wahusika kuweni makini na huruma
 
Ni uzembe pia kutokufaulu mapema hadi kusubiri sup
SWALI.
Mkuu kuna wengine walipata matatizo wakati wa mitihani mwezi wa saba hivo wakaomba special exams, je nawao ni wazembe?
CHANGAMOTO.
upande wangu naona shida imeanza baada ya chuo kubadilisha ratiba ya sup and special exams na kiuweka October mwisho yaani ni wiki moja tu kabla ya kufungua.
Kitu hiki kinapelekea chuo kuchelewa kutuma matokeo bodi ya mikopo na hatimae kucheleweshwa kwa allocation za mwaka husika kwa wanafunzi waliokuwa na special and sup.
PENDEKEZO.
Chuo kiweke utaratibu ambao utawawezesha wanafunzi kufanya mitihani hiyo mapema refer to udom
 
Back
Top Bottom