CHADEMA watoka tena bungeni, Mrema naye atoka!

Juzi wabunge watukufu wa CHADEMA walitoka ndani ya ukumbi wa bunge kwa sababu serikali na CCM wanataka kuburuza mchakato wa kupata katiba mpya. Mara ya kwanza wakati wa kukataa posho Mh. Shibuda aliwaponda na hakutoka nje kuungana na wenzake. Sasa ningependa kujua kama juzi naye alitoka nje, alikula pini au alikacha mapema.
Shibuda hana madhara yoyote kwa sasa yuko sawa na Dr. Augustino Mrema lolote analosema tutakuwa busy na story na sms kama jana tulivyokuwa busy wakati wale wabunge wa CCM waliosokomezewa mic wachangie kwa lazima coz hawajawai kuongea tangu bunge lianze sasa wanapewa air time ya kujichoresha mbele ya wapiga kura wao juu ya swala hili la mswada wa katiba.
 
Makamanda wanaokimbia uwanja wa vita na kwenda chooni kuzungumza.

Huo ni unafiki na upuuzi wa hali ya juu sana kwa Chama kama Chadema. Kama kweli wanajiamini kwanini wasibaki mlemle bungeni kuleta mnakasha ulio bora. Sasa kutoka kwao nje kunawasaidia nini wananchi na wakti muswada ndio hivyo tena unapita bila kipingamizi.

Nakupa pole na Chadema yako kwa koga wenu wa kuongelea barazani tena mchana kweupeeeeeeeee.

Usilete unishani usion na maana. Kama kweli wewe ni mfuatiliaji wa mijadala bungeni hapa Tanzania utakuwa unajua muswada wa mahakama ulivyokuwa na mpambano mkali sana kati ya Tundu Lissu na serikali. Serikali walitaka mamlaka ya nidhamu kwa mahakimu wlya na mikoani wew wakuu wa wilaya na mikoa. Lissu alipinga kwa hoja nzito ambazo kila mtu mwenye fikira pevu lakini mwso wa siku CCM walipitisha kama serikali ilivyotaka. Kwa hiyo, kubaki bungeni hakusaidii kama wewe unavyopotosha BALI kubaki bungeni kunawafanya wewe sehemu ya uhuni wa serikali na CCM yake.

Hatua ya Chadema ni nzuri kwa sababu wanatonesha sisi wapiga kura wao kwamba wapo upande wetu na si genge la mafisadi wanaodhani Tanzania ni mali yao na wanaweza kufanya chochote wanacotaka.
 
Hata hivyo wakipewa hizo mic badala ya kuongelea mswada uliopo mezani, wanabaki kujadili wabunge wenzao wa CDM, mipasho kama taarabu. Mimi najiuliza issue iliyoko mezani ni wabunge wa CDM au Muswada wa mchakato wa Katiba?

Kwa wabunge makini wangetumia muda huo kudadavua contents za muswada ulio mbele yao. Angalia mtu kama Rage: Mimi nashangaa hata tume ya uchaguzi kumruhusu agombee ubunge ili hali alishapatikana na hatia ya wizi, akahukumiwa kifungo jela, akatumikia miaka, kabla ya kuokoewa na msamaha wa raisi. Leo anawaita wenzake wahuni. Aibu sana watu wa Tabora. Anasema mlikuwa mnatoa mawazo ya huu muswada kupitia redio yake, ni kweli??
 
Juzi wabunge watukufu wa CHADEMA walitoka ndani ya ukumbi wa bunge kwa sababu serikali na CCM wanataka kuburuza mchakato wa kupata katiba mpya. Mara ya kwanza wakati wa kukataa posho Mh. Shibuda aliwaponda na hakutoka nje kuungana na wenzake. Sasa ningependa kujua kama juzi naye alitoka nje, alikula pini au alikacha mapema.
Alitoka na alikuwepo kwenye ile kushikana mikono kwa wabunge wote wa chadema na nccr,alikuwa akiimba kabisa.Asingetoka,ccm walivyo,wangemuweka wa kwanza kuchangia.Nadhani wazee wa chadema wamemuonya,naona tangu kikao hiki cha bunge kianze mzee ametulia.Na pia asingetoka magazeti mengi yangeandika issue hiyo.
 
mie nadhani jukwaa la katiba waongoze mchakato wa kuandaa katiba mpya, kisha upelekwe bungeni...ukajadiliwe na kupitishwa!
Jukwaa la katiba liongoze mjadala na bunge la katiba ndilo lipitishe. Yaani bunge la katiba huundwa na wananchi bila kufuata vyama, bali wananchi wote kwa makundi yao huwakilishwa. Bunge hilo litakuwa na wawakilishi wa dini zote, asasi za kiraia, kila wilaya, na kila mkoa, kila chama cha siasa, taasisi za elimu kama vyuo vikuu, watoto, walemavu nk. Unajua katiba inawagusa wote, hivyo kupitisha katiba kwa kutumia bunge lililoundwa kwa misingi ya vyama vya siasa ni kuwanyima uwakilishi mamilioni ya waTZ ambao hawako kwenye vyama vya siasa. Kumbuka waliopiga kura ni kama 6m out of over 19m waliotakiwa na out of over 45m tanzanians.
 
Mrema katoka siamini! labda alikuwa kalala anamwaga maudenda kushtuka anakuta watu wanatoka akafikiri bunge limeahirishwa. Mrema sio mpinzani anaganga njaa.

Mama kubwa umenivunja mbavu na comments zako ila kuna ukweli kuhusu Mrema.
 
CHADEMA tuliwatuma bungeni kufanya kazi ya wananchi na ndicho wanchaofanya. Sasa hivi c wakati wa kubuluzwabuluzwa lazima washike adabu kama walizoea ni kipindi hicho cha nyuma

kazi mliyowatuma wakifika mjengoni wasaini mahudhurio wachukue posho alafu watoke nje, wakirudi mtaani wahamasishe vurugu, ...
 
Jamani huyu mama wa kwetu anayeongea sasa hv bungeni mshenzi tu badala ya kujadili mambo ya msingi anagusa issue za watu kuingia kwenye bunge na ndugu ccm wangapi wameingia na vimada zao eti mbunge wa nkenge siwezi kumpa kura mshenzi tu eti bunge litunge sheria ya kuzuia maandamano alafu eti mchungaji sijui anachunga nini???hata haki za binadam hazijui wanawaza kula tu!!!!!
 
post yako sijaielewa wewe ulieianzisha afadhali nimeambulia taarifa kutoka kwa wadu wengine zenye kufurahisha,hasa hii ya mabalozi kuwepo mjengoni japo sina hakika hao wakalimani wao watakuwa wamewaeleza cha ukwelii?au CCM wamewawahi na kuwakatia takrima ili wawadanganye mabalozi?
 
Huyu Hassan Zungu anasema etii yaliyosemwa na Mhe, Lissu kuhusu Zanzibar wakati wa mjadala wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba hayajawafurahisha wabunge wenzake wa CDM...inawezekana haya??
 
MAKINDA ETI ALIIAMBIA KAMATI ya bunge katiba na sheria HAIWEZI ZUNGUKA KTK KANDA 10 KUKUSANYA MAONI KWA KUWA YEYE YUPO SAFARINI INDIA KUWAANGALIA WAGONJWA AKINA MWANDOSYA!source bbcnews!bi koroboto unanisikitisha sana kwa akili finyu
 
MAKINDA ETI ALIIAMBIA KAMATI ya bunge katiba na sheria HAIWEZI ZUNGUKA KTK KANDA 10 KUKUSANYA MAONI KWA KUWA YEYE YUPO SAFARINI INDIA KUWAANGALIA WAGONJWA AKINA MWANDOSYA!source bbcnews!bi koroboto unanisikitisha sana kwa akili finyu
mkuu, kama vp ungekitemea mate usoni. Kinakera hiki!
 
Jamani vp shibuda hivi alitoka naye?mana huyu jamaa akili zake anazijua mwenyewe
 
Mrema katoka siamini! labda alikuwa kalala anamwaga maudenda kushtuka anakuta watu wanatoka akafikiri bunge limeahirishwa. Mrema sio mpinzani anaganga njaa.

Ugonjwa wa kisukari hulazimisha mtu kwenda kujisaidia mara kwa mara, it was just a coincidence
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom