armanisankara
JF-Expert Member
- Jul 15, 2011
- 283
- 49
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewataka wananchi kukipa madaraka ya kuongoza nchi kwa miaka mitano, ili kuwaondolea umasikini kwa kutumia rasilimali zilizopo ambazo zimekuwa zikifujwa na baadhi ya mafisadi walioko ndani ya serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Chadema imesema ili kufanikisha hilo, hivi sasa kimeanza kuwaunganisha Watanzania wote katika kupigania haki na kuwaondolea hofu ambayo imejazwa na watawala kwa muda mrefu huku mhimili wa mahakama ukianza kutumika vibaya.
Akizungumza katika mikutano ya Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) inayoendelea katika vijiji mbalimbali mkoani Morogoro, Mwenyekiti wa taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema kuwa vuguvugu la mabadiliko linaloendeshwa na chama hicho kwa kuzunguka nchi nzima ni mapambano ya ukombozi wa watu wanyonge na masikini ambayo ni mapinduzi ya tabaka la watu masikini, wakulima na wafanyakazi.
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, alisema kuwa operesheni ya M4C ambayo kwa Mkoa wa Mororgoro itafika katika kata 180, majimbo 10, vijiji 585 na vitongoji 3,122 vya mkoa huu, ni sehemu ya mkakati wa Chadema wa kuendelea kujijenga na kujikita kwa watu nchi nzima hasa maeneo ya vijijini, ambapo moja ya kazi kubwa katika operesheni hiyo ni kuendelea kuwatia ujasiri Watanzania, kuwaunganisha na kuwaondolea hofu Watanzania ambayo wamejazwa kwa muda mrefu na watawala ili waweze kupigania haki zao.
Tumeanzia na mkoa wenu wa Morogoro, baada ya hapa makamanda tutaitafuta Iringa, tutakwenda Dodoma, kisha tutapiga Manyara, tutamalizia na Singida," alisema Mbowe (pichani) na kuongeza:
"Tutapumzika siku chache kisha awamu ya pili itaanza na tumeamua kutetea sauti za watu wasiokuwa na sauti, kwani Watanzania zaidi ya asilimia 95 ni masikini wasiokuwa na haki na rasilimali zao za nchi."
Alisema kuwa mbali na vuguvugu hilo la mabadiliko kutumika kuwaunganisha Watanzania wote kudai mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutawala katika nchi yao, alisema chama hicho kinataka mchakato huo umilikiwe na wananchi wao wenyewe, ndiyo maana Chadema kimeanza mpango wa kuchangisha fedha.
"Hivi unakwenda kuandaa mabadiliko makubwa katika nchi hii ndiyo maana tunataka mchakato huu wa vuguvugu hili umilikiwe na wananchi wenyewe. Hivi ndivyo walivyofanya akina Mwalimu Nyerere na wenzake wakati Tanu ilipokuwa ikipigania uhuru wa nchi hii, tofauti na wakati huu ambapo siasa imefanywa kuwa biashara badala ya kuwatumikia watu na kutengeneza fursa ya maendeleo ya watu," aliongeza Mbowe.
Mbowe alisema: "Sasa tumefikia mahali pabaya, mnaona wenyewe Mahakama inavyoanza kutumika vibaya kulinda udhalimu wa CCM, wanajaribu kuzuia nguvu ya mabadiliko kwa kutumia Mahakama, wanataka kuzuia ‘Proletarian Revolution' kwa kutumia mahakama, tunawaambia hawawezi, huwezi kuzuia madai ya madaktari, walimu, wakulima, wafugaji na watu wengine wa tabaka la chini na kati kwa kutumia mahakama. Haiwezekani, tumefika hapa kwa sababu ya utawala mbovu wa CCM ambayo imeshaonyesha dalili zote za kushindwa kuongoza."
Jana viongozi wa Chadema walianza ziara yao ya kuhutubia katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Morogoro Vijijini.
CHANZO: NIPASHE
Chadema imesema ili kufanikisha hilo, hivi sasa kimeanza kuwaunganisha Watanzania wote katika kupigania haki na kuwaondolea hofu ambayo imejazwa na watawala kwa muda mrefu huku mhimili wa mahakama ukianza kutumika vibaya.
Akizungumza katika mikutano ya Operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) inayoendelea katika vijiji mbalimbali mkoani Morogoro, Mwenyekiti wa taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema kuwa vuguvugu la mabadiliko linaloendeshwa na chama hicho kwa kuzunguka nchi nzima ni mapambano ya ukombozi wa watu wanyonge na masikini ambayo ni mapinduzi ya tabaka la watu masikini, wakulima na wafanyakazi.
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, alisema kuwa operesheni ya M4C ambayo kwa Mkoa wa Mororgoro itafika katika kata 180, majimbo 10, vijiji 585 na vitongoji 3,122 vya mkoa huu, ni sehemu ya mkakati wa Chadema wa kuendelea kujijenga na kujikita kwa watu nchi nzima hasa maeneo ya vijijini, ambapo moja ya kazi kubwa katika operesheni hiyo ni kuendelea kuwatia ujasiri Watanzania, kuwaunganisha na kuwaondolea hofu Watanzania ambayo wamejazwa kwa muda mrefu na watawala ili waweze kupigania haki zao.
Tumeanzia na mkoa wenu wa Morogoro, baada ya hapa makamanda tutaitafuta Iringa, tutakwenda Dodoma, kisha tutapiga Manyara, tutamalizia na Singida," alisema Mbowe (pichani) na kuongeza:
"Tutapumzika siku chache kisha awamu ya pili itaanza na tumeamua kutetea sauti za watu wasiokuwa na sauti, kwani Watanzania zaidi ya asilimia 95 ni masikini wasiokuwa na haki na rasilimali zao za nchi."
Alisema kuwa mbali na vuguvugu hilo la mabadiliko kutumika kuwaunganisha Watanzania wote kudai mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutawala katika nchi yao, alisema chama hicho kinataka mchakato huo umilikiwe na wananchi wao wenyewe, ndiyo maana Chadema kimeanza mpango wa kuchangisha fedha.
"Hivi unakwenda kuandaa mabadiliko makubwa katika nchi hii ndiyo maana tunataka mchakato huu wa vuguvugu hili umilikiwe na wananchi wenyewe. Hivi ndivyo walivyofanya akina Mwalimu Nyerere na wenzake wakati Tanu ilipokuwa ikipigania uhuru wa nchi hii, tofauti na wakati huu ambapo siasa imefanywa kuwa biashara badala ya kuwatumikia watu na kutengeneza fursa ya maendeleo ya watu," aliongeza Mbowe.
Mbowe alisema: "Sasa tumefikia mahali pabaya, mnaona wenyewe Mahakama inavyoanza kutumika vibaya kulinda udhalimu wa CCM, wanajaribu kuzuia nguvu ya mabadiliko kwa kutumia Mahakama, wanataka kuzuia ‘Proletarian Revolution' kwa kutumia mahakama, tunawaambia hawawezi, huwezi kuzuia madai ya madaktari, walimu, wakulima, wafugaji na watu wengine wa tabaka la chini na kati kwa kutumia mahakama. Haiwezekani, tumefika hapa kwa sababu ya utawala mbovu wa CCM ambayo imeshaonyesha dalili zote za kushindwa kuongoza."
Jana viongozi wa Chadema walianza ziara yao ya kuhutubia katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Morogoro Vijijini.
CHANZO: NIPASHE