VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mimi si mwanachama wa CHADEMA. Ni mwanachama wa CCM tangu miaka ya 80 nilipohitimu Chuo Kikuu. Tangu kumaliza utumishi wangu ndani ya Serikali na chama, nimebakia kuwa mwanachama mtiifu wa chama changu-nikishirikishwa mipango mbalimbali ya kichama na kiserikali katika kushauri na kuitekeleza kupitia vijana wetu chamani. Nimekuwa wakati wote mfuata utaratibu na kuwa na nidhamu kwa CCM yangu ingawa huusema ukweli.
Chama ni kikubwa kuliko mtu au watu fulani. Hakuna awaye yeyote, mwanachama wa CCM au chama kingine cha siasa, ambaye ni mkubwa kuliko chama. Mtu huwa na nguvu ya kuongea na kutenda kupitia chama, nje ya chama chake mtu huyo si kitu. Katika muktadha huo, kila mwanachama wa chama huulinda UANACHAMA wake kwa nguvu kubwa. Huulinda kwa kuwa na nidhamu-hata iliyochanganyika na woga; hekima, utii na busara. Masikio huwa hayakizidi kichwa!
Nikiwa huku Kigoma, nimefuatilia Mkutano wa Baraza Kuu la CHADEMA uliofanyika Mlimani City huko Dar es Salaam. Nilizifuatilia ajenda zake lakini kubwa ni kuwahusu akina-Halima Mdee na wenzake 18. Baraza Kuu limeridhia kufukuzwa kwao uanachama wa CHADEMA na Kamati Kuu ya chama hicho. Yaani, Baraza Kuu limetupilia mbali rufaa za yeyote kati yao ambaye alipinga uamuzi wa Kamati Kuu. Sasa wamefukuzwa na Mamlaka ya juu kabisa ya CHADEMA.
Kama mwanasiasa mbobevu na mpenda demokrasia, uamuzi juu ya akina Halima Mdee NIMEUFURAHIA na NAUPONGEZA. Sababu yangu ni ujumbe unaobebwa na uamuzi huo: nidhamu kwanza, umaarufu baadaye. Wahusika walipaswa kujishusha kabla ya jana. Kusimama katika ubatili na kuutetea kumewaponza. Sasa wamevuna walichopanda. Watetezi wao Serikalini na Bungeni hawapo na hawawezi kuwasaidia tena. Heshima na nidhamu ni vitu vya bure. Hakuna mkubwa kuliko chama chake!
Nawashauri CHADEMA, siku watakayopeleka taarifa ya kufukuzwa uanachama kwa akina Halima Mdee, walifanye jambo hilo mubashara. Hatutaki tena kumsikia Spika au Katibu wa Bunge akikana kupokea barua ya CHADEMA. Hatutaki kuona tena jambo hili linaendelea. Taarifa ipelekwe Bungeni; Spika awaondoe akina Halima Mdee Bungeni halafu CHADEMA waamue kupeleka Wabunge wengine wa viti maalum au la.
Royal Tour!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Ujiji, Kigoma)
Chama ni kikubwa kuliko mtu au watu fulani. Hakuna awaye yeyote, mwanachama wa CCM au chama kingine cha siasa, ambaye ni mkubwa kuliko chama. Mtu huwa na nguvu ya kuongea na kutenda kupitia chama, nje ya chama chake mtu huyo si kitu. Katika muktadha huo, kila mwanachama wa chama huulinda UANACHAMA wake kwa nguvu kubwa. Huulinda kwa kuwa na nidhamu-hata iliyochanganyika na woga; hekima, utii na busara. Masikio huwa hayakizidi kichwa!
Nikiwa huku Kigoma, nimefuatilia Mkutano wa Baraza Kuu la CHADEMA uliofanyika Mlimani City huko Dar es Salaam. Nilizifuatilia ajenda zake lakini kubwa ni kuwahusu akina-Halima Mdee na wenzake 18. Baraza Kuu limeridhia kufukuzwa kwao uanachama wa CHADEMA na Kamati Kuu ya chama hicho. Yaani, Baraza Kuu limetupilia mbali rufaa za yeyote kati yao ambaye alipinga uamuzi wa Kamati Kuu. Sasa wamefukuzwa na Mamlaka ya juu kabisa ya CHADEMA.
Kama mwanasiasa mbobevu na mpenda demokrasia, uamuzi juu ya akina Halima Mdee NIMEUFURAHIA na NAUPONGEZA. Sababu yangu ni ujumbe unaobebwa na uamuzi huo: nidhamu kwanza, umaarufu baadaye. Wahusika walipaswa kujishusha kabla ya jana. Kusimama katika ubatili na kuutetea kumewaponza. Sasa wamevuna walichopanda. Watetezi wao Serikalini na Bungeni hawapo na hawawezi kuwasaidia tena. Heshima na nidhamu ni vitu vya bure. Hakuna mkubwa kuliko chama chake!
Nawashauri CHADEMA, siku watakayopeleka taarifa ya kufukuzwa uanachama kwa akina Halima Mdee, walifanye jambo hilo mubashara. Hatutaki tena kumsikia Spika au Katibu wa Bunge akikana kupokea barua ya CHADEMA. Hatutaki kuona tena jambo hili linaendelea. Taarifa ipelekwe Bungeni; Spika awaondoe akina Halima Mdee Bungeni halafu CHADEMA waamue kupeleka Wabunge wengine wa viti maalum au la.
Royal Tour!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Ujiji, Kigoma)