Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Haya ndiyo mambo. Tumekuwa tukisikia tu kuwa baadhi ya viongozi wa Upinzani pamoja na wanasheria watamfungulia mashitaka fisadi BWM kama hatafunguliwa mashitaka na serikali. Imekuwa ni lonolongo tu. Hayo mashitaka yamefikia wapi??? Fisadiz wanantakiwa kusogezwa lupango wanakostahili.
Wamekwisha fungua mashtaka kwenye mahakama ya wananchi na sisi wenye uchungu tayari tunasikiliza kesi. Tunazidi kuwaomba wenye ushahidi wazidi kujitokeza na kwa hakika tutawahukumu. Wengine wao wameanza kutumikia kifungo cha wananchi hapa hapa - kwa kuogopa hata kujitokeza kuwasalimia wanannchi. Kwa hivi sasa kesi za nyani hatuwezi kuzifikisha kwenye mahakama za ngedere.