Indume Yene
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 2,950
- 711
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) inakusudia kuja na orodha mpya ya mafisadi kama ilivyoandikwa katika gazeti la Nipashe (Jumatatu). Tunaelewa serikali ya SISIEMU bado inajikongoja kuwashughulikia mafisadi waliowahi kutajwa na chama hicho juu ya ufisadi.
Swali, je serikali kipindi hiki imejiandaa vipi na hii orodha ya AIBU. Kwa habari zaidi soma hapo chini:-
CHADEMA waibua orodha mpya ya mafisadi
2009-01-11 16:03:15
Na Mashaka Mgeta
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeibuka na orodha mpya ya aibu, yenye majina ya watu wanaojihusisha na kashfa za ufisadi, hivyo kuhujumu uchumi na kulitia hasara Taifa.
Hatua hiyo imebainika jana, ikiwa ni siku moja kabla ya kuanza kwa kampeni ya operesheni sangara Jijini Dar es Salaam, itakayozinduliwa kesho.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Kabwe Zitto aliliambia NipasheJumapili jana kuwa, majina ya watuhumiwa hao wa ufisadi yanaendelea kushughulikiwa na chama hicho, kwa kushirikiana na vyanzo mbalimbali katika vita dhidi ya vitendo hivyo.
Hata hivyo, Zitto hakutaja majina wala nyadhifa za wahusika katika kadhia hiyo ya ufisadi, kwa madai kuwa uchunguzi wa kina unaendelea ili kupata uhakika wa kuyaweka hadharani.
``Itachukuwa muda kidogo kuwataja, kwa sababu tunaendelea na uchunguzi wa kina, ili kujiridhisha na ukweli uliopo kuhusu tuhuma zinazowakabili, ndipo tuwataje,`` alisema.
Taarifa za awali zilizolifikia gazeti hili, zilidai kuwa katika mikutano yake ya operesheni sangara Jijini Dar es Salaam, Chadema itataja majina mapya ya mafisadi, wakiwemo wamiliki wa kampuni ya Kagoda Agricultural Limited.
``Tunaendelea kuwashughulikia, hivyo hatutawataja kwa sasa, lakini huenda tukawatoa wengine pindi tutakapojiridhisha dhidi ya vitendo vya ufisadi walivyovifanya,`` alisema.
Zitto, alisema uchunguzi wa tuhuma dhidi ya majina ya mafisadi wanayoyafanyia kazi utakapokamilika, watatumia jukwaa la siasa kuwataja hadharani, na si kuwasilisha majina kwa Tume ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa (TAKUKURU).
``Sisi Chadema ni wanasiasa na TAKUKURU wanafanya kazi zao kwa mujibu wa sheria inayowangoza, hivyo tutatumia majukwaa ya siasa kuwataja na si kupeleka majina hayo TAKUKURU,`` alisema.
Kuhusu kutajwa majina ya wamiliki wa kampuni ya Kagoda, Zitto alisema kwa ufupi, ``Mkurugenzi wetu wa kampeni na uchaguzi ameshasema kupitia Alasiri (gazeti dada la Nipashe), hivyo tunasimama katika maneno yake.``
Akitoa maoni yake kuhusu Chadema kuibua orodha mpya ya mafisadi, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati, alisema hatua hiyo inapaswa kuungwa mkono kwa kuwa inasaidia jitihada za Rais Jakaya Kikwete kupambana na uovu nchini.
``Hawa Chadema wanachokifanya siyo kitu chenye maslahi kwa chama hicho, hiyo ni vita yetu sote, sasa kama wanawajua wao wawataje tu na vyombo vya dola vitafanya kazi zake,`` alisema.
Chiligati, alisema ni dhana potofu kwa chama kimoja cha siasa kuichukua ajenda ya vita ya ufisadi kama `miliki` yake, kwa kuwa athari zake zinaiathiri jamii nzima.
Mwaka jana, Chadema katika mkutano uliohudhuriwa na vyama kadhaa vya upinzani, ilitaja majina yaliyopo kwenye orodha ya aibu ya watu wanaojihusisha na vitendo vya ufisadi.
Hata hivyo, hatua hiyo iliwafanya watu waliotajwa, kujitokeza hadharani na kutaka waombwe radhi, vinginevyo wangemshtaki `kinara` wa kutaja majina hayo, Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbroad Slaa.
Licha ya karipio hilo, Dk. Slaa hakuwahi kuomba radhi, badala yake aliwataka wahusika katika kashfa hiyo, kwenda mahakamani, mahali ambapo ukweli ungejulikana.
Katika mchakato wa matukio yanayohusiana na vitendo vya ufisadi, mawaziri kadhaa walijiuzulu na baadhi ya watu waliotajwa katika kadhia hiyo, wameshafikishwa mahakamani wakituhumiwa kuhusika katika makosa mbalimbali yenye kuhujumu uchumi na kulitia hasara Taifa.
SOURCE: Nipashe
Swali, je serikali kipindi hiki imejiandaa vipi na hii orodha ya AIBU. Kwa habari zaidi soma hapo chini:-
CHADEMA waibua orodha mpya ya mafisadi
2009-01-11 16:03:15
Na Mashaka Mgeta
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeibuka na orodha mpya ya aibu, yenye majina ya watu wanaojihusisha na kashfa za ufisadi, hivyo kuhujumu uchumi na kulitia hasara Taifa.
Hatua hiyo imebainika jana, ikiwa ni siku moja kabla ya kuanza kwa kampeni ya operesheni sangara Jijini Dar es Salaam, itakayozinduliwa kesho.
Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Kabwe Zitto aliliambia NipasheJumapili jana kuwa, majina ya watuhumiwa hao wa ufisadi yanaendelea kushughulikiwa na chama hicho, kwa kushirikiana na vyanzo mbalimbali katika vita dhidi ya vitendo hivyo.
Hata hivyo, Zitto hakutaja majina wala nyadhifa za wahusika katika kadhia hiyo ya ufisadi, kwa madai kuwa uchunguzi wa kina unaendelea ili kupata uhakika wa kuyaweka hadharani.
``Itachukuwa muda kidogo kuwataja, kwa sababu tunaendelea na uchunguzi wa kina, ili kujiridhisha na ukweli uliopo kuhusu tuhuma zinazowakabili, ndipo tuwataje,`` alisema.
Taarifa za awali zilizolifikia gazeti hili, zilidai kuwa katika mikutano yake ya operesheni sangara Jijini Dar es Salaam, Chadema itataja majina mapya ya mafisadi, wakiwemo wamiliki wa kampuni ya Kagoda Agricultural Limited.
``Tunaendelea kuwashughulikia, hivyo hatutawataja kwa sasa, lakini huenda tukawatoa wengine pindi tutakapojiridhisha dhidi ya vitendo vya ufisadi walivyovifanya,`` alisema.
Zitto, alisema uchunguzi wa tuhuma dhidi ya majina ya mafisadi wanayoyafanyia kazi utakapokamilika, watatumia jukwaa la siasa kuwataja hadharani, na si kuwasilisha majina kwa Tume ya Kupambana na Kudhibiti Rushwa (TAKUKURU).
``Sisi Chadema ni wanasiasa na TAKUKURU wanafanya kazi zao kwa mujibu wa sheria inayowangoza, hivyo tutatumia majukwaa ya siasa kuwataja na si kupeleka majina hayo TAKUKURU,`` alisema.
Kuhusu kutajwa majina ya wamiliki wa kampuni ya Kagoda, Zitto alisema kwa ufupi, ``Mkurugenzi wetu wa kampeni na uchaguzi ameshasema kupitia Alasiri (gazeti dada la Nipashe), hivyo tunasimama katika maneno yake.``
Akitoa maoni yake kuhusu Chadema kuibua orodha mpya ya mafisadi, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Chiligati, alisema hatua hiyo inapaswa kuungwa mkono kwa kuwa inasaidia jitihada za Rais Jakaya Kikwete kupambana na uovu nchini.
``Hawa Chadema wanachokifanya siyo kitu chenye maslahi kwa chama hicho, hiyo ni vita yetu sote, sasa kama wanawajua wao wawataje tu na vyombo vya dola vitafanya kazi zake,`` alisema.
Chiligati, alisema ni dhana potofu kwa chama kimoja cha siasa kuichukua ajenda ya vita ya ufisadi kama `miliki` yake, kwa kuwa athari zake zinaiathiri jamii nzima.
Mwaka jana, Chadema katika mkutano uliohudhuriwa na vyama kadhaa vya upinzani, ilitaja majina yaliyopo kwenye orodha ya aibu ya watu wanaojihusisha na vitendo vya ufisadi.
Hata hivyo, hatua hiyo iliwafanya watu waliotajwa, kujitokeza hadharani na kutaka waombwe radhi, vinginevyo wangemshtaki `kinara` wa kutaja majina hayo, Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbroad Slaa.
Licha ya karipio hilo, Dk. Slaa hakuwahi kuomba radhi, badala yake aliwataka wahusika katika kashfa hiyo, kwenda mahakamani, mahali ambapo ukweli ungejulikana.
Katika mchakato wa matukio yanayohusiana na vitendo vya ufisadi, mawaziri kadhaa walijiuzulu na baadhi ya watu waliotajwa katika kadhia hiyo, wameshafikishwa mahakamani wakituhumiwa kuhusika katika makosa mbalimbali yenye kuhujumu uchumi na kulitia hasara Taifa.
SOURCE: Nipashe