Heading ingeweza pia kuwa; "CCM yaanza kutengeneza maiti ili wawe ngazi ya kuendelea Ikulu". Hizi ni kejeli alizozitoa JK dhidi ya CHADEMA. Lakini cha kushangaza tangu JK amesema haya, matukio mengi yaliyoripotiwa ya uvunjaji wa amani na utulivu yamekuwa yakifanywa na CCM. Naona kuna sababu sasa ya Slaa kulisema hili waziwazi majukwaani kwamba CCM pamoja na kutangaza kutumia jeshi kuvunja amani sasa wameanza kuwatumia green guard kwa kazi hiyo.
WATU watano wanashikiliwa na jeshi la Polisi mjini hapa kwa tuhuma za kuhusika katika tukio lililotokea jana(juzi) ambapo watu wanaosadakiwa kuwa ni wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi CCM na viongozi wa chama hicho kuhusika katika kuwakata na kitu chenye ncha kali wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kile kilichodaiwa kuwa wananchi hao kutoonyesha ushirikiano na chama hicho tawala.
Wakiongea kwa tabu baada ya kufanyiwa unyama huo katika hospital ya mkoa wa Mara majeruhi hao walisema kuwa kitendo hicho kimetokea jana jioni baada ya mkutano wa kampeni wa cha CHADEMA katika kata ya Buhare.
Sele Mwita(27) ambaye ni mmoja wa wahusika waliojeruhuiwa katika shambulio hilo alisema kuwa wakati anatoka kwenye kampeni za CHADEMA alikutana na kundi la watu wakiwa wamevalia bendera na skafu za CCM huku wakisema kuwa huyu naye anahusika.
‘Mimi wakati natoka kwenye mkutano nilikutana na vijana wakiwa na mapanga huku wakiwa wamevaa vitambaa vya CCM wakiongozwa na Kapul na kuanza kusema huyu naye ni wa CHADEMA na kuanza kunikata ndipo nikaanza kukimbia" alisema Sele
Naye Pambano Malima(30) mkazi wa Kigera ambaye mkasa huo ulianzia kwakwe alisema kuwa alikutana na kundi hilo la vijana wakati anapeleka pikipiki na kuanza kumshambulia kwa kumkata mapanga
Walisema kuwa vitendo hivyo vyote vinatokea huku viongozi wa Chama cha Mapinduzi mjini hapa wakiwa wanahusika kwa ukaribu,ambapo mmoja wa kiongozi wa tawi katika kata ya Kigera Kapul Charles alikamatwa kwa kuhusika na tukio la kwanza la kuwakata vijana wawili mapanga .
Mbali na tukio hilo ambalo limetokea jana usiku lakini leo asubuhi katika kata ya Nyakato mjini hapa wafuasi wengine wawili wa chama cha CHADEMA walivamiwa ndani na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa cha cha Mapinduzi wakisema kuwa washushe bendera zao za CHADEMA ambazo wameziweka katika nyumba zao.
Akiongea na waandishi wa habari mjini hapa leo kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mara kamishina msaidizi ACP Robert Boaz alikiri kutokea kwa tukio hilo katika eneo hilo la Kigera Migombani.
Alisema kuwa watu waliojeruhiwa walikatwa na vitu vyenye ncha kali baada ya vurugu kutokea ambapo katika eneo hilo kulikuwa na mkutano wa CCM katika nyumba ya Mkono Salima ambaye kamanda Boaz alishindwa kuthibitisha kama alikuwa balozi au la katika hatua hiyo aliongeza kuwa baada kikao hicho ndipo ulizuka ugomvi huo kati ya vijana waliokuwa ndani na waliokuwa katika maeneo yale.
MODS mbona nashindwa kuelewa nia yenu. Nini kilichowavutia zaidi na heading ya kichochezi na kuacha hii ambayo ipo balanced? Ethics sio lazima ziendelezwe na magazeti na TVs tu. Hata mitandao kama hii inaweza kuonyesha njia ya kuepuka headlines za kichochezi na kukumbatia zile za kistaarabu and responsible. Ni kwa faida ya taifa hilihili mnalopigania kulikomboa. Hakuna ukombozi wa kweli katika lindi la chuki. Historia imeporve hivyo jamani.
"Mapambano ya CCM na CHADEMA mkoani Mara yasababisha damu kumwagika?"
MODS mbona nashindwa kuelewa nia yenu. Nini kilichowavutia zaidi na heading ya kichochezi na kuacha hii ambayo ipo balanced? Ethics sio lazima ziendelezwe na magazeti na TVs tu. Hata mitandao kama hii inaweza kuonyesha njia ya kuepuka headlines za kichochezi na kukumbatia zile za kistaarabu and responsible. Ni kwa faida ya taifa hilihili mnalopigania kulikomboa. Hakuna ukombozi wa kweli katika lindi la chuki. Historia imeporve hivyo jamani.
"Mapambano ya CCM na CHADEMA mkoani Mara yasababisha damu kumwagika?"
Omar, soma stori yote. Hakuna kinachosema kuwa chadema na ccm wamepigana. Stori inasema kuwa wanaccm wamewashambulia wanachadema na kuwacharanga mapanga. Polisi wanawashikiria viongozi wa ccm. Kwa nini unataka kuweka 'balance' isiyokuwepo? Na kama wakiweka kuwa mapambano ni kati ya chadema na ccm, wewe kama mwanaccm unafaidika nini na hilo?
Hivi wewe kwa akili yako ni kuwa kila mtu anayejaribu kutumia sauti ya rationality dhidi ya huu ushabiki pofu mnaoendeleza hapa jamiiforum basi ni lazima atakuwa CCM? Hivi ukishweka heading kama hiyo unadhani ndio itasaidia huo ukombozi wako unaoupigia chepuo hapa. Its just sowing the seeds of selfdestructions ambayo in the end ni wote watakaoathirika .....
Kuna mtu aliniambia kuwa she wish that she will be around to see atleast opposition parties, by actions and intent behave like a government in waiting and not just another opportunist in waiting... I feel sorry for she will never see that in years as all signs shows that insensitivity and irrationality is central to our opposition political psych...
If you want to be trusted with our destiny u should try to behave like some people who deserve that.......