Elections 2010 CCM waanza kumwaga damu mkoani Mara

yani nimeona kwenye taarifa ya habari nimeshangaa sana, naomba wana jf tusifanye makosa kuwapa hawa jamaa uongozi kama wameshaanza kumwaga damu kabla ya uchaguzi je tukiwapa uongozi si ndo watatumaliza kkabisa
 
Heading ingeweza pia kuwa; "CCM yaanza kutengeneza maiti ili wawe ngazi ya kuendelea Ikulu". Hizi ni kejeli alizozitoa JK dhidi ya CHADEMA. Lakini cha kushangaza tangu JK amesema haya, matukio mengi yaliyoripotiwa ya uvunjaji wa amani na utulivu yamekuwa yakifanywa na CCM. Naona kuna sababu sasa ya Slaa kulisema hili waziwazi majukwaani kwamba CCM pamoja na kutangaza kutumia jeshi kuvunja amani sasa wameanza kuwatumia green guard kwa kazi hiyo.
 
cpati picha tukio hili lingefanywa na chadema, kinana angeongea mpaka mapovu yamtoke mdomoni. Hata ngoja tusubiri. Maana tulihakikishiwa na afande shimbo kuwa hakuna damu itakayomwagika. Ila hii iliyomwagika sio damu?.
 
Heading ingeweza pia kuwa; "CCM yaanza kutengeneza maiti ili wawe ngazi ya kuendelea Ikulu". Hizi ni kejeli alizozitoa JK dhidi ya CHADEMA. Lakini cha kushangaza tangu JK amesema haya, matukio mengi yaliyoripotiwa ya uvunjaji wa amani na utulivu yamekuwa yakifanywa na CCM. Naona kuna sababu sasa ya Slaa kulisema hili waziwazi majukwaani kwamba CCM pamoja na kutangaza kutumia jeshi kuvunja amani sasa wameanza kuwatumia green guard kwa kazi hiyo.

mkuu lukolo, nimeipenda hiyo heading yako ,.... natamani mwanahalisi au tanzania daima waitumie kwenye magazeti ya kesho.
 
Hakuna kitakachotokea kwa sababu ''we have hopeless people katika nyanja za usalama wa raia, nchi na mipaka yake na taifa kwa ujumla wake , the moment hawa watu watakapotambua kiapo chao cha kuilinda taifa la Tanzania na mwisho wanamuhusisha Mungu kuwa shahidi wao na Mungu ambaye ni kweli na kweli tupu'' we want have no more of these nonsenses happening!! kwa wakati huu utapewa kila excuse possible ili mradi wasitimize wajibu wao wa kulinda raia watanzania, wao wanachojua ni kuilinda na kuitetea ccm na matunbo yao, shame on you!!!!
lakini biblia imesema ''Tazama na kila mtu atalipwa kwa ujila wake kwa kadri ya matendo yake pana siku na wakati haki itatendeka kwa watanzania wote ''Ee Mungu ibariki na kuilinda Tanzania ''
Chagua Dr. Slaa
 
CCM wamejiaibisha kwa tukio hili. Kama Reginald Mengi alivyokuwa anasema sasa hivi kwamba ''watu wakitaka kumbambikia madawa ya kulevya mtoto wake,hiyo haiwezi kuitwa 'rushwa,hiyo ni zaidi ya rushwa'' Kwa wale wanaosoma Biblia unaweza kulifananisha na ile hadithi katika Biblia ambapo kashfa inatokea katika kabila la Benjamin,mwanamke mmoja anauawa kikatili,halafu watu wote wa Israel wanapelekeana habari wanaulizana maswala,kama unyama huo unaruhusiwa,mwisho wake,makabila yale yote mengine yanakwenda kupigana na kabila la Benjamin.
Sijasoma Biblia siku nyingi,in fact,miaka kumi na tatu sijasoma Biblia. Zamani nilikuwa nasoma sana Biblia,kwa sababu,among other things,nilikuwa sijaigundua CNN. [Hili swala la kutosoma Bibila kwa siku nyingi linaweza kuwa kesi dhidi yangu.]
Kwa kifupi,ninalosema ni kwamba this kind of incident is very serious,linaweza kuleta sympathy vote kwa Dr.Slaa,mtu ambaye,I had already written him off. Lakini CCM wakifanya namna hii,na watu
wote Tanzania wakilijadili,haya ni mambo ambayo yanaweza kuiletea matatizo CCM.
Nilikuwa Butiama wakati ule wa Kampeni ya Ubunge,by election,baada ya kufariki Chacha Wangwe,na CCM walikuwa wanakuja kutua na Helicopter yao,halafu sijui ikatokea nini,nadhani wakatoa amri watu wakatwekatwe mapanga huko chini ili helikopta iweze kutua.
Halafu utaona huko Mara wapinzani wamekuwa very successful,jambo ambalo usingetegemea kutokea kwa sababu ule ndio Mkoa wa Mwalimu Nyerere. Inaonyesha wanaona ishara,wanapokuwa kule kwamba CCM hii ya leo haimwakilishi Mwalimu Nyerere.
Kwa sababu nimeona watu kadhaa walikuwa wanaulizwa maswali hapa na Mlimani TV kuhusu Uchaguzi,na wapo kina mama pale Kinondoni walikuwa wanasema CCM imeongoza Nchi kwa utulivu,na sasa pia inaongoza kwa utulivu;CCM ndio imetulea siku zote;CCM ni toka enzi za mababu,babu yangu aliichagua CCM,baba yangu aliichagua CCM, kwa hiyo na mimi pia nitaichagua CCM. Hayo ni maneno yenye mantiki. Lakini kwa nini watu wa Mara wanaikana CCM? Na huyo mgombea anayefanyiwa fujo hapo ni Vicent Nyerere,mtoto wa Josephata Nyerere,mdogo wake Mwalimu, ambaye anagombea Ubunge kwa tiketi ya Chadema,ndipo zilipotokea hizo vurugu za watu kukatwa mapanga.
Haya mambo hayakubaliki. Inafanya mimi nifikirie kwamba yoyote akichaguliwa kuwa Rais ni sawa tu,kama ni Lipumba au Dr, Slaa,au Mziray au Kikwete. Siyo lazima Kikwete achaguliwe kuwa Rais. Hakuna maafa yatalifika Taifa kama Rais asipokuwa wa CCM.
Lakini hata kama nikienda a step further na kusema kwamba sitaki Kikwete achaguliwe kuwa Rais,sidhani kama Watanzania wanachagua Rais kwa kufuata kauli yangu. Lakin ndio hivyo,mimi napinga Kikwete kuchaguliwa Rais,kwa sababu sasa naona gloves zi

 
WATU watano wanashikiliwa na jeshi la Polisi mjini hapa kwa tuhuma za kuhusika katika tukio lililotokea jana(juzi) ambapo watu wanaosadakiwa kuwa ni wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi CCM na viongozi wa chama hicho kuhusika katika kuwakata na kitu chenye ncha kali wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kile kilichodaiwa kuwa wananchi hao kutoonyesha ushirikiano na chama hicho tawala.

Wakiongea kwa tabu baada ya kufanyiwa unyama huo katika hospital ya mkoa wa Mara majeruhi hao walisema kuwa kitendo hicho kimetokea jana jioni baada ya mkutano wa kampeni wa cha CHADEMA katika kata ya Buhare.

Sele Mwita(27) ambaye ni mmoja wa wahusika waliojeruhuiwa katika shambulio hilo alisema kuwa wakati anatoka kwenye kampeni za CHADEMA alikutana na kundi la watu wakiwa wamevalia bendera na skafu za CCM huku wakisema kuwa huyu naye anahusika.

‘Mimi wakati natoka kwenye mkutano nilikutana na vijana wakiwa na mapanga huku wakiwa wamevaa vitambaa vya CCM wakiongozwa na Kapul na kuanza kusema huyu naye ni wa CHADEMA na kuanza kunikata ndipo nikaanza kukimbia" alisema Sele

Naye Pambano Malima(30) mkazi wa Kigera ambaye mkasa huo ulianzia kwakwe alisema kuwa alikutana na kundi hilo la vijana wakati anapeleka pikipiki na kuanza kumshambulia kwa kumkata mapanga

Walisema kuwa vitendo hivyo vyote vinatokea huku viongozi wa Chama cha Mapinduzi mjini hapa wakiwa wanahusika kwa ukaribu,ambapo mmoja wa kiongozi wa tawi katika kata ya Kigera Kapul Charles alikamatwa kwa kuhusika na tukio la kwanza la kuwakata vijana wawili mapanga .

Mbali na tukio hilo ambalo limetokea jana usiku lakini leo asubuhi katika kata ya Nyakato mjini hapa wafuasi wengine wawili wa chama cha CHADEMA walivamiwa ndani na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa cha cha Mapinduzi wakisema kuwa washushe bendera zao za CHADEMA ambazo wameziweka katika nyumba zao.

Akiongea na waandishi wa habari mjini hapa leo kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mara kamishina msaidizi ACP Robert Boaz alikiri kutokea kwa tukio hilo katika eneo hilo la Kigera Migombani.

Alisema kuwa watu waliojeruhiwa walikatwa na vitu vyenye ncha kali baada ya vurugu kutokea ambapo katika eneo hilo kulikuwa na mkutano wa CCM katika nyumba ya Mkono Salima ambaye kamanda Boaz alishindwa kuthibitisha kama alikuwa balozi au la katika hatua hiyo aliongeza kuwa baada kikao hicho ndipo ulizuka ugomvi huo kati ya vijana waliokuwa ndani na waliokuwa katika maeneo yale.

Yaliyotabiliwa na Mnajimu wa JWTZ yametimia.
Kwa yaliyotoea musoma, nimeamini kuwa mnajimu alikuwa mkweli. Ni kweli aliona kuwa CCM watamwaga damu, na kweli wamefanya hivyo. Na bado wataimwaga zaidi. Chama Cha mapinduzi, kinatakiwa kufutwa kabisa. Kimekosa sifa za kuitwa chama cha siasa kwa kuanzisha jeshi na kusababisha umwagaji wa damu.
 
Kwa kweli inasikitisha,kama hatua madhubuti hazitachukuliwa kuwawajibisha waliohusika kutoa maelekezo hayo mpaka waliyoyatekeleza,basi kutakuwepo na visasi na hakuna mtu atakaye kubali kudhuriwa wakati wahusika wanapeta.Ngoja tuone itakuwaje..
 
Kama kweli ni hivyo shimbo akautangazie umma tena ni hatua gani watachukua kuzuia umwagaji wa damu kama unavyoripotiwa huko Mara, au labda kwake yeye kumwagika damu ni mpaka asikie watu 200 wamekufa...???
 
wanatoa kafara watanzania .. matatizo ya kuamini sana waganga na nguvu za giza za bagamoyo.
 
MODS mbona nashindwa kuelewa nia yenu. Nini kilichowavutia zaidi na heading ya kichochezi na kuacha hii ambayo ipo balanced? Ethics sio lazima ziendelezwe na magazeti na TVs tu. Hata mitandao kama hii inaweza kuonyesha njia ya kuepuka headlines za kichochezi na kukumbatia zile za kistaarabu and responsible. Ni kwa faida ya taifa hilihili mnalopigania kulikomboa. Hakuna ukombozi wa kweli katika lindi la chuki. Historia imeporve hivyo jamani.
"Mapambano ya CCM na CHADEMA mkoani Mara yasababisha damu kumwagika?"
 
MODS mbona nashindwa kuelewa nia yenu. Nini kilichowavutia zaidi na heading ya kichochezi na kuacha hii ambayo ipo balanced? Ethics sio lazima ziendelezwe na magazeti na TVs tu. Hata mitandao kama hii inaweza kuonyesha njia ya kuepuka headlines za kichochezi na kukumbatia zile za kistaarabu and responsible. Ni kwa faida ya taifa hilihili mnalopigania kulikomboa. Hakuna ukombozi wa kweli katika lindi la chuki. Historia imeporve hivyo jamani.
"Mapambano ya CCM na CHADEMA mkoani Mara yasababisha damu kumwagika?"

Omar, soma stori yote. Hakuna kinachosema kuwa chadema na ccm wamepigana. Stori inasema kuwa wanaccm wamewashambulia wanachadema na kuwacharanga mapanga. Polisi wanawashikiria viongozi wa ccm. Kwa nini unataka kuweka 'balance' isiyokuwepo?

Na kama wakiweka kuwa mapambano ni kati ya chadema na ccm, wewe kama mwanaccm unafaidika nini na hilo?
 
Ndugu zangu watanzania,

Nimepokea kwa maskitiko mauaji yaliyotokea Musoma kwa kuwahusisha wanachama wa CCM. Kama mtanzania mwenye uchungu na nchi hii, nimejiuliza kwanini nchi hii inatawaliwa kihuni? Damu inayomwagwa na CCM nani atailipa?

Swali kubwa zaidi ni kuwa kama CCM wameweza kuanzisha jeshi (Green Guard) na matunda ya jeshi hilo tumeisha yaona, Umwagaji wa damu Musoma na bado watafanya hivyo nchi nzima.
  1. Je bado CCM wana haki ya kuendelea kuwepo?
  2. Je nini kinazuia Msajili wa vyama vya siasa kukifuta mara moja chama hiki kwa sababu kimekiuka sheria ya kukianzisha kwa kuanzisha jeshi?
  3. Je ni sababu zipi zinazowazuia jeshi la polisi kukichukulia hatua chama hicho (CCM) kwa makosa hayo?
Maoni yenu ni muhimu. kama itaonekana ni makala nzuri, waandishi wa makala, waichukue na kuichapisha kwa ajili ya kuwafikia wengi.
 
MODS mbona nashindwa kuelewa nia yenu. Nini kilichowavutia zaidi na heading ya kichochezi na kuacha hii ambayo ipo balanced? Ethics sio lazima ziendelezwe na magazeti na TVs tu. Hata mitandao kama hii inaweza kuonyesha njia ya kuepuka headlines za kichochezi na kukumbatia zile za kistaarabu and responsible. Ni kwa faida ya taifa hilihili mnalopigania kulikomboa. Hakuna ukombozi wa kweli katika lindi la chuki. Historia imeporve hivyo jamani.
"Mapambano ya CCM na CHADEMA mkoani Mara yasababisha damu kumwagika?"

Na wewe Omari bana, balanced wapi? Kwa mfano, mtu akibaka mkeo, utasema yalikuwa mapambano kati ya mke wako na mbakaji au mbakaji kabaka?
 
Omar, soma stori yote. Hakuna kinachosema kuwa chadema na ccm wamepigana. Stori inasema kuwa wanaccm wamewashambulia wanachadema na kuwacharanga mapanga. Polisi wanawashikiria viongozi wa ccm. Kwa nini unataka kuweka 'balance' isiyokuwepo? Na kama wakiweka kuwa mapambano ni kati ya chadema na ccm, wewe kama mwanaccm unafaidika nini na hilo?

Hivi wewe kwa akili yako ni kuwa kila mtu anayejaribu kutumia sauti ya rationality dhidi ya huu ushabiki pofu mnaoendeleza hapa jamiiforum basi ni lazima atakuwa CCM? Hivi ukishweka heading kama hiyo unadhani ndio itasaidia huo ukombozi wako unaoupigia chepuo hapa. Its just sowing the seeds of selfdestructions ambayo in the end ni wote watakaoathirika .....

Kuna mtu aliniambia kuwa she wish that she will be around to see atleast opposition parties, by actions and intent behave like a government in waiting and not just another opportunist in waiting... I feel sorry for she will never see that in years as all signs shows that insensitivity and irrationality is central to our opposition political psych...

If you want to be trusted with our destiny u should try to behave like some people who deserve that.......
 
Hivi wewe kwa akili yako ni kuwa kila mtu anayejaribu kutumia sauti ya rationality dhidi ya huu ushabiki pofu mnaoendeleza hapa jamiiforum basi ni lazima atakuwa CCM? Hivi ukishweka heading kama hiyo unadhani ndio itasaidia huo ukombozi wako unaoupigia chepuo hapa. Its just sowing the seeds of selfdestructions ambayo in the end ni wote watakaoathirika .....

Wewe ni mtetezi na shabiki wa Kikwete na chama lake la mafisadi. hii sio siri Omar.

Kuna mtu aliniambia kuwa she wish that she will be around to see atleast opposition parties, by actions and intent behave like a government in waiting and not just another opportunist in waiting... I feel sorry for she will never see that in years as all signs shows that insensitivity and irrationality is central to our opposition political psych...

The "she" unayemuongelea hapo ni mama Salma Kikwete?

If you want to be trusted with our destiny u should try to behave like some people who deserve that.......

Bwa ha ha ha ... huu ni ushauri toka kwa mwanaccm!.... Umeanza lini kuwatakia wema wapinzani?
 
Sisi tukifuta oct 31, bado kitabaki ni chama cha upinzani lakini kikifutwa, itakuwa ni fundisho kwa vyama vingine vyenye nia kama hiyo
 
Back
Top Bottom