nickname
JF-Expert Member
- Dec 20, 2009
- 544
- 147
WATU watano wanashikiliwa na jeshi la Polisi mjini hapa kwa tuhuma za kuhusika katika tukio lililotokea jana(juzi) ambapo watu wanaosadakiwa kuwa ni wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi CCM na viongozi wa chama hicho kuhusika katika kuwakata na kitu chenye ncha kali wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kile kilichodaiwa kuwa wananchi hao kutoonyesha ushirikiano na chama hicho tawala.
Wakiongea kwa tabu baada ya kufanyiwa unyama huo katika hospital ya mkoa wa Mara majeruhi hao walisema kuwa kitendo hicho kimetokea jana jioni baada ya mkutano wa kampeni wa cha CHADEMA katika kata ya Buhare.
Sele Mwita(27) ambaye ni mmoja wa wahusika waliojeruhuiwa katika shambulio hilo alisema kuwa wakati anatoka kwenye kampeni za CHADEMA alikutana na kundi la watu wakiwa wamevalia bendera na skafu za CCM huku wakisema kuwa huyu naye anahusika.
Mimi wakati natoka kwenye mkutano nilikutana na vijana wakiwa na mapanga huku wakiwa wamevaa vitambaa vya CCM wakiongozwa na Kapul na kuanza kusema huyu naye ni wa CHADEMA na kuanza kunikata ndipo nikaanza kukimbia alisema Sele
Naye Pambano Malima(30) mkazi wa Kigera ambaye mkasa huo ulianzia kwakwe alisema kuwa alikutana na kundi hilo la vijana wakati anapeleka pikipiki na kuanza kumshambulia kwa kumkata mapanga
Walisema kuwa vitendo hivyo vyote vinatokea huku viongozi wa Chama cha Mapinduzi mjini hapa wakiwa wanahusika kwa ukaribu,ambapo mmoja wa kiongozi wa tawi katika kata ya Kigera Kapul Charles alikamatwa kwa kuhusika na tukio la kwanza la kuwakata vijana wawili mapanga .
Mbali na tukio hilo ambalo limetokea jana usiku lakini leo asubuhi katika kata ya Nyakato mjini hapa wafuasi wengine wawili wa chama cha CHADEMA walivamiwa ndani na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa cha cha Mapinduzi wakisema kuwa washushe bendera zao za CHADEMA ambazo wameziweka katika nyumba zao.
Akiongea na waandishi wa habari mjini hapa leo kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mara kamishina msaidizi ACP Robert Boaz alikiri kutokea kwa tukio hilo katika eneo hilo la Kigera Migombani.
Alisema kuwa watu waliojeruhiwa walikatwa na vitu vyenye ncha kali baada ya vurugu kutokea ambapo katika eneo hilo kulikuwa na mkutano wa CCM katika nyumba ya Mkono Salima ambaye kamanda Boaz alishindwa kuthibitisha kama alikuwa balozi au la katika hatua hiyo aliongeza kuwa baada kikao hicho ndipo ulizuka ugomvi huo kati ya vijana waliokuwa ndani na waliokuwa katika maeneo yale.
Wakiongea kwa tabu baada ya kufanyiwa unyama huo katika hospital ya mkoa wa Mara majeruhi hao walisema kuwa kitendo hicho kimetokea jana jioni baada ya mkutano wa kampeni wa cha CHADEMA katika kata ya Buhare.
Sele Mwita(27) ambaye ni mmoja wa wahusika waliojeruhuiwa katika shambulio hilo alisema kuwa wakati anatoka kwenye kampeni za CHADEMA alikutana na kundi la watu wakiwa wamevalia bendera na skafu za CCM huku wakisema kuwa huyu naye anahusika.
Mimi wakati natoka kwenye mkutano nilikutana na vijana wakiwa na mapanga huku wakiwa wamevaa vitambaa vya CCM wakiongozwa na Kapul na kuanza kusema huyu naye ni wa CHADEMA na kuanza kunikata ndipo nikaanza kukimbia alisema Sele
Naye Pambano Malima(30) mkazi wa Kigera ambaye mkasa huo ulianzia kwakwe alisema kuwa alikutana na kundi hilo la vijana wakati anapeleka pikipiki na kuanza kumshambulia kwa kumkata mapanga
Walisema kuwa vitendo hivyo vyote vinatokea huku viongozi wa Chama cha Mapinduzi mjini hapa wakiwa wanahusika kwa ukaribu,ambapo mmoja wa kiongozi wa tawi katika kata ya Kigera Kapul Charles alikamatwa kwa kuhusika na tukio la kwanza la kuwakata vijana wawili mapanga .
Mbali na tukio hilo ambalo limetokea jana usiku lakini leo asubuhi katika kata ya Nyakato mjini hapa wafuasi wengine wawili wa chama cha CHADEMA walivamiwa ndani na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa cha cha Mapinduzi wakisema kuwa washushe bendera zao za CHADEMA ambazo wameziweka katika nyumba zao.
Akiongea na waandishi wa habari mjini hapa leo kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mara kamishina msaidizi ACP Robert Boaz alikiri kutokea kwa tukio hilo katika eneo hilo la Kigera Migombani.
Alisema kuwa watu waliojeruhiwa walikatwa na vitu vyenye ncha kali baada ya vurugu kutokea ambapo katika eneo hilo kulikuwa na mkutano wa CCM katika nyumba ya Mkono Salima ambaye kamanda Boaz alishindwa kuthibitisha kama alikuwa balozi au la katika hatua hiyo aliongeza kuwa baada kikao hicho ndipo ulizuka ugomvi huo kati ya vijana waliokuwa ndani na waliokuwa katika maeneo yale.