Bungeni: Maswali ya 'papo kwa papo' kwa Waziri Mkuu

Acheni wagongane vichwa, Januari Makamba si amesema huo ni mpango wao wa taifa wa kuondoa posho, leo waziri mkuu anajikanyaga.
 
Si ni huyu huyu alisema magari ya bei kubwa serikalini yasinunuliwe? leo anatetea posho ya kukaa? Mungu ibariki Tanzania na viongozi wake
 
wakati jana tu,Rais mstaafu wa ujerumani waliambia wawe wangalifu na malipo ya posho.
Hizo hela wanazo jilipa ni hela za misaada na mikopo toka nje.Siyo hela za kulipana posho.
Pia aliwaambia ulimwengu unafuatilia kwa kina hili swala,athari yake ni wafazili kuzuia misaada.
 
Pinda hata wewe mtoto wa mkulima? siamini ninachokisikia lakini neno moja tu amini ninakuambia siku zenu zimekwisha...!!!
 
CCM ilishakufa,imejaa upoteshaji kwa wananchi,kwa hiyo hata sishangai huyo bwana ndiyo mkuu kusema hivyo,ANGUKO LA CCM LIMETIMIA
 
huyu makunyanzi anashindwa kujenga hoja kabisaa, yaani pm unasema mkitoka nje mnakutana na wapiga kura
wenu wanawaomba? are you ok! NO. you are mentally retarded. kama ni ombaomba basi huku mitaani ndo bwerere.
na kama ni kweli wapiga kura wanawaomba, basi zitumwe moja kwa moja jimboni kwake kama zitto alivyofanya.
"PINDA DONT KID US, WE ARE NOT STUPID ENOUGH TO LISTEN TO YOU"
 
Nashanga kabisa. Chief whip wao anasema serikali imeliona hilo, likawekwa kwenye mpango wa miaka mitani ili posho hizo zifutwe. Akakubaliana na Mbowe kuwa posho hizi kwa watumishi ni tatizo, kuwa watumishi hawafanyi kazi bali kufukuzia posho. semina, warsha. makongamano nk. Akadai aliyeliona hilo kwanza siyo Zitto bali serikali. Sasa namshangaa huyu Pinda. Kweli amepinda. hajui hata yaliyomo kwenye mipango ya serikali yake.
Nani yupo sahihi, Pinda au Lukuvi? NAMLILIA EDWARD MORINGE SOKOINE.
 
Hawa jamaa wanajichanganya kama karata......huku J.Makamba,E.Bulaya n.k wakisema serikali imekusudia kupunguza posho hizo katika mpango wa maendeleo,leo msimamo wa serikali hiyohiyo kupitia kwa waziri mkuu wake unasema posho si tatizo kwani zinawasaidia wabunge...hizi ni sarakasi,huyu Pinda mtoto wa mkulima asiyelima (anayelima kwa rimoti) pale magogoni huwa anaitwa mshauri nasaha,kwa maana amezoeleka kutoa ushauri kuliko ku-act
 
Kama kweli hiyo ndio kauli ya PM basi ametutukana watanzania wote yaani kazi yetu ni kwenda kuomba misaada ya fedha kwa wabunge,wabunge wachovu ambao hawajui baya wala zuri kwa nchi yao isipokuwa posho,ubinafsi,ufisadi nk.kupitisha hoja za kijinga kwa wingi wao basi,wanaofurahia watoto wa wakulima kufukuzwa vyuo kwa kunyimwa fedha ya field tsh 10000/= wakati wao wanatanua,eti wanajiita watetezi wa wananchi,wasubiri 2015 watasema walitutetea nini sijui.Hivi wameshasahau kilichowatokea 2010, wasubiri
 
Kwa hiyo Huyu mtoto wa mkulima ana taka kutuambia kuwa watanzania tutaendelea kwa kuomba nauli kwa wabunge wetu na maafisa wa serikali? je atakubaliana na mimi kwamba kama yeye PM anabariki ombaomba ndio maana watanzania omba omba wanaongezeka mjini? Kwa nini matonya alifukuzwa Dar na Bungeni?
Ushauri.
Kama PM anaona hiyo fedha inatumika kuwapa wapiga kura wanoomba wabunge wao nauli kwanini pesa hiyo isitengwe katika ruzuku ya petrol au diesel ili kumwezesha huyu omba omba wa nauli kupata unafuu wa kulipa hiyo nauli.
omba omba ya namna hii si ya kuiongea bungeni tena ni aibu kama unampiga kura wako anakufuata bungeni kuja kuomba nauli.
 
Mi nadhani kama moja ya lengo la posho ni kuwagawia wapiga kura, basi uanzishwe utaratibu wa ruzuku kwa wananchi. Kila mwezi wasio na kipato wepewe mgawo hata 50,000, ili kuondoa kero kwa waheshimiwa wabunge kuombwa pesa na wapiga kura wao, na pia kupunguza/ ama kuondoa kabisa posho zinazoingia mkono wa kulia na kutokea kushoto, kumbe ziko intended kwa mpga kura ombaomba.
 
Pinda atatafuta watu wa kumpigia chapuo ili agombee urais 2015......wana ccm saaizi wote mtazamo wao ni 2015 na sijui km kuna kiongozi yeyote wa ccm atatumikia mwananchi zaidi ya kujiandaa kwa ndumba km yale majini ya sheikh yahaya yaliyopkuwa yanamlinda kikwete na upuuzi mwingine,....................nchi sasa inakaribia kupasuka na mikono ya ccm ni mikono isiyosalama hata kidogo...................
tuiogope ccm km ukoma kwani viongozi wa ccm wote ni wanafiki
 
Kweli hii nchi yetu inazidi kujidhihirisha kuwa inaongozwa na VIHIYO WATUPU! Rais kihiyo,Spika kihiyo,PM kihiyo,IGP kihiyo,Mwanasheria Mkuu kihiyo,Jaji Mkuu kihiyo,Mawaziri vihiyo,Ma-DC/RC vihiyo n.k.

Sikutegemea PM wa Taifa maskini la Tanzania ambalo wananchi wake wanaishi chini ya Dola 1 kwa siku(chini Tshs.1500)!
Sikuamini masikio yangu nilipomsikiliza PM Kayanza Pinda akitetea ulaji wa Posho na Ulaji wa Wabunge wa CCM wa Tshs.150,000/= kwa siku!!!!
Je,hivi ni kweli huyu PM ndiye anayejitambulisha kama MTOTO WA MKULIMA????No,hawezi kuwa mtoto wa mkulima halafu atetea upuuzi huu!

Utetezi wake wa Posho ya 150,000/=kwa siku kwa kila Mbunge umejaa porojo,kebehi na longolongo tupu! Hivi ni nani aliyewaambia Wabunge kuwasaidia Wapiga kura wao au ndugu zao kwa fedha ya posho ya Seating Allowance????Hivi ni wabunge wangapi wanaogawa posho yao kila siku kwa wapiga kura wao wanaokuja pale mjengoni? Maana Pinda kadai kuwa ukitoka kwenye Ukumbi wa Bunge unakutana na mtu anakwambia mzee naomba unisaidie nauli nimeishiwa!!!!!! Huyu mtu(ndugu/mpiga kura anaishiwa nauli alikuwa anatoka wapi???
Ninachojua hawa Wabunge kuna fedha ya Mfuko wa Jimbo wanayolipwa kwa mwezi. Je,kwanini wasitumie hiyo kutatua kero na shida ndogo ndogo za ndugu au wapiga kura wao????

Mimi niseme tu kwamba CCM hawana hoja,Waziri Mkuu Pinda hana hoja! Wanachochotetea hapa ni WIZI,UFISADI NA UFUJAJI WA PESA ZA WALIPA KODI WA TANZANIA!

Mimi naweza kusema kwa ujasiri kabisa kuwa hii pesa ni katika zile wanazoziita TAKRIMA. Kwamba hii pesa CCM wanaing'ang'ania KWA AJILI YA KUENDELEA KUWAHONGA WAPIGA KURA ili uchaguzi unaofuata baada ya miaka 5 waweze tena kupewa ulaji. NAAMIMI KABISA KAMA MBUNGE NI BAHIRI HII PESA YA VIKAO AKIDUNDULIZA KWA VIKAO VYOTE VYA BUNGE KATIKA MIAKA 5 ATAKUWA MILIONEA!

Kwa hiyo pesa hii ya Seating Allowance wanayoing'ang'ania CCM ndiyo pesa ITAKAYONUNUA KURA KWA HONGO ILI KUWARUDISHA HAWA WABUNGE WA CHAMA CHA MAFISADI/MAGAMBA-CCM kwa kila chaguzi zinapofanyika.


Nawasilisha.

hili mi toka siku aliyolia bungeni nili conclude kuwa hili ni ***** tu!!!so sishangai kwa maupupu anayoyoongea ...
 
Nashanga kabisa. Chief whip wao anasema serikali imeliona hilo, likawekwa kwenye mpango wa miaka mitani ili posho hizo zifutwe. Akakubaliana na Mbowe kuwa posho hizi kwa watumishi ni tatizo, kuwa watumishi hawafanyi kazi bali kufukuzia posho. semina, warsha. makongamano nk. Akadai aliyeliona hilo kwanza siyo Zitto bali serikali. Sasa namshangaa huyu Pinda. Kweli amepinda. hajui hata yaliyomo kwenye mipango ya serikali yake.
Nani yupo sahihi, Pinda au Lukuvi? NAMLILIA EDWARD MORINGE SOKOINE.

Mizengo Kayanza Pinda ni waziri mwoga kabisa ambaye Tanzania haijawahi kuwa naye. Amebakia kuwa mlalamishi, mtu ambaye hawezi kutoa kauli yoyote na akaisimamia. Kiongozi yeyote mzuri, katika nafasi yeyote, ni yule ambaye anaweza kufanya maamuzi magumu kwaajili ya faida ya jamii inayoiongoza.

Unfortunately Pinda will go without leaving footprints behind. A responsible leader fights very hard to leave marks in his/her followers' hearts.

Ni bahati mbaya zaidi kwa JK, maana yeye mwenyewe ni kiongozi asiye jasiri wala asiyeweza kusimamia chochote halafu ana msaidizi aliye kama yeye mwenyewe.
 
jamani ni kweli pinda katetea posho kwa kusema eti ukitoka nje ya ukumbi wa bunge unaombwa hela na wananchi!!!!???
kama ni kweli basi hatuna waziri mkuu hapa tz. So shame to justify something like unnecessary allowances using simple and childish language like that.
 
Mimi nahisi kashinikizwa ahakikishe anatetea hizo posho zibaki.
Kinachooneka lengo la mpango wa maendeleo ni kuondoa posho za watumishi wengine na siyo za wabunge. PM lazima ajibu swali watumishi wasio hudhuria vikao watapata aina gani ya posho kupunguza ukali wa maisha au kuwasaidia ndugu zao wanao waomba? Vinginevyo wasio hudhuria vikao wasifanye kazi, tuwaachie wakuu wa idara wazifanye wakiwa kwenye vikao ili wapate posho
 
Kuna wabunge hawamisi kikao na hawachangii chochote kazi ni kuvizia posho,na wabunge wengi hawalipi kodi kwenye vibiashara vyao!
 
Sijawahi kushiriki maandamano yoyote ila kwa hili niko tayari kushiriki maandamano na kupinga wabunge na watumishi kulipwa haya mamilion
 
Pinda lazima awatetee wabunge kwani kumbuka:
  1. Ndiyo walio muapprove baada ya uteuzi wa rais kwa kumpigia kura i.e. anatetea wapiga kura wake (Wabunge)
  2. Wanaweza kupiga kura ya kutokuwa na imani naye (analinda chakula/ajira ya uwaziri mkuu)
Hivyo Mh. Pinda anachokifanya ni unafiki, ila anafahamu ukweli, na hizo ndizo siasa za bongo kwa sasa!!
 
Back
Top Bottom