Bunge lasema halijapokea barua ya Nyalandu kujiuzulu, lamvua ubunge kutokana na CCM kumfukuza uanachama

Hiyo your take hiyo ndiyo umevuruga mambo kabisa;

Hata hivyo;

Amebipu wenzake wamempigia; sasa historia itasomeka kuwa CCM ndio imemmwaga Nyalandu kutokana na makando kando yake na sio yeye kukiacha chama.
 
Hata hivyo, Mhedhimiwa Spika amepokea barua toka kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi ya tarehe 30 Oktoba, 2017 akimuarifu kwamba kwa muda sasa Chama hicho kilishaanza kumchukulia hatua za kiudhibiti na kinidhamu dhidi ya vitendo na kauli zake zisizoridhisha kinyume na misingi, falsafa na itikadi ya Chama cha Mapinduzi.

Hivyo, Chama cha Mapinduzi kuanzia tarehe ya barua yao kimemjulisha Mheeshimiwa Spika kuwa Ndugu Lazaro Nyalandu amepoteza sifa za Uanachama wa Chama cha Mapinduzi, na hivyo kupoteza nafasi zote za uongozi wa ndani wa Chama hicho na Ubunge kwa mujibu wa Ibara ya 13 ya Chama hicho.

Mheshimiwa Spika, angependa kuwaarifu Watanzania kwamba kwa barua hiyo toka mamlaka halali ndani ya Chama cha Mapinduzi ambacho Ndugu Lazaro Nyalandu alipata Ubunge kupitia Chama hicho na kwa mujibu wa Ibara ya 71 (1)(f) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotamka kwamba:

“Mbunge atakoma kuwa Mbunge na ataacha kiti chake cha Ubunge iwapo litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo: (f) Iwapo Mbunge ataacha kuwa Mwanachama cha chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au alipoteuliwa kuwa Mbunge.”

Hivyo, Ndugu Lazaro Nyalandu si Mbunge tena na hatua stahiki za kuiarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi zinaendelea kuchukuliwa.

Screen-Shot-2017-11-01-at-3.19.21-PM-950x704.png
Screen-Shot-2017-11-01-at-3.20.17-PM-950x559.png
 
Juzi Polepole alisema "....kuhama kwa Nyalandu sio jambo geni.....ni afya ya siasa..." Polepole says Nyalandu is insignificant

...na kisha akasema tena "....namshangaa Nyalandu kuhama CCM chenye itikadi ya Ujamaa na kwenda CHADEMA kisicho na itikadi...."

Spika Ndugai anadhalilisha Bunge na kiti cha u-Spika, Ofisi ya Bunge imekuwa kama Tawi la Wakereketwa wa CCM Kizota. Wabunge mwajibisheni huyo ili msizidi kudhalilika.
 
Amebipu wenzake wamempigia; sasa historia itasomeka kuwa CCM ndio imemmwaga Nyalandu kutokana na makando kando yake na sio yeye kukiacha chama.
hahahaha..yapi hayo..haya yaliyokuwa highlighted hapa..kwamba CCM ilikuwa inachukizwa na kauli zake...na kumbe sio ufisadi wake...hahahhahahaahah...akili zenu hakuna aiseee

upload_2017-11-1_15-49-29.png
 
View attachment 621949 Moja ya habari kubwa za sasa hivi nchini Tanzania ni Lazaro Nyalandu ambae juzi ametangaza kujiuzulu nafasi zake zote ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM pamoja na Ubunge wa Singida Kaskazini.

Baadae Spika Ndugai alihojiwa na vyombo vya habari na kusema kwamba pamoja na kusikia taarifa za kujiuzulu kwa Nyalandu kwenye vyombo vya habari, yeye bado hajapokea barua ya kujiuzulu kwa Mbunge huyo.

Sasa leo imetoka taarifa kutoka Ofisi ya Bunge Dodoma ikiwa imeandikwa kama inavyosomeka hapa chini....

Ofisi ya Spika ingependa kuwaarifu Watanzania wote kwamba mpaka sasa haijapokea barua toka kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini (CCM) Ndugu Lazaro Nyalandu ambayo amekuwa akiarifu kwamba amemwandikia Mheshimiwa Spika kumtaarifu kujiuzulu kwake.

Hata hivyo, Mhedhimiwa Spika amepokea barua toka kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi ya tarehe 30 Oktoba, 2017 akimuarifu kwamba kwa muda sasa Chama hicho kilishaanza kumchukulia hatua za kiudhibiti na kinidhamu dhidi ya vitendo na kauli zake zisizoridhisha kinyume na misingi, falsafa na itikadi ya Chama cha Mapinduzi.

Hivyo, Chama cha Mapinduzi kuanzia tarehe ya barua yao kimemjulisha Mheeshimiwa Spika kuwa Ndugu Lazaro Nyalandu amepoteza sifa za Uanachama wa Chama cha Mapinduzi, na hivyo kupoteza nafasi zote za uongozi wa ndani wa Chama hicho na Ubunge kwa mujibu wa Ibara ya 13 ya Chama hicho.

Mheshimiwa Spika, angependa kuwaarifu Watanzania kwamba kwa barua hiyo toka mamlaka halali ndani ya Chama cha Mapinduzi ambacho Ndugu Lazaro Nyalandu alipata Ubunge kupitia Chama hicho na kwa mujibu wa Ibara ya 71 (1)(f) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotamka kwamba:

“Mbunge atakoma kuwa Mbunge na ataacha kiti chake cha Ubunge iwapo litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo: (f) Iwapo Mbunge ataacha kuwa Mwanachama cha chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au alipoteuliwa kuwa Mbunge.”

Hivyo, Ndugu Lazaro Nyalandu si Mbunge tena na hatua stahiki za kuiarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi zinaendelea kuchukuliwa.

My Verdict,
Spika jana alisema hajapokea Barua ya Nyalandu lakini hakuzungumzia kabisa kuhusu Barua kutoka CCM. Leo Ofisi yake inaibuka na kudai kuna barua kutoka kwa Katibu wa CCM iliyokuja Mapema kuliko ya Nyalandu. Hapa nadhani kuna kitu hakiko sawa.
1509540659454.jpg
yetu macho
 
Duh, inaelekea imewauma kweli kusikia kuwa Jamaa kajitoa CCM ................!!

Wameamua kutwist taarifa ili kwenye kumbu kumbu zao ionekane kuwa hakujiuzulu bali amefukuzwa!!
 
Hapa hata mtu asiye na akili atakwambia huu ni utoto..

Nimekumbuka kipindi unamtamkia mchumba wako kwamba umemuacha, analalamika,analia halafu baada ya siku mbili kuisha anakutumia ujumbe mfupi anakutaarifu hata yeye pia alishafikiria kukuacha muda mrefu sana!

Kwa lugha nyepesi hiki ni kichekesho tena cha kuvunja mbavu!

Hongera Lazaro Nyalandu, umewashika sawasawa!
 
Back
Top Bottom