Bulembo: Polepole ni Unyasi kaletwa CCM na kokoro, V8 ameijulia CCM, Bashiru alitoka CUF. Nataka Mdahalo na Polepole

sambulugu

JF-Expert Member
Jun 1, 2021
3,942
7,406
Maneno ya Bulembo!

Polepole ni unyasi mkavu ni mdogo sana Mangula ashughulike naye.

Bulembo anataka mdahalo na Polepole na yuko tayari kulipia ukumbi.

Bashiru wa CUF hakutakiwa kuwa pale maana hajakulia katika chama cha mapinduzi! Sasa najiuliza kumbe chama cha mapinduzi ili uwe kwenye kundi la mwenye chama unatakiwa uwe umekulia humo!

Inaonekana pia suala la kinana na makamba ni kubwa hawa wazee ndo CCM yenyewe!

Paramagamba Kabudi aliharibu mahusiano ya kimataifa na Rais Samia sio sawa na Magufuli!

Hayo ni mambo ya Bulembo! Mmoja ya wenye COmbi.

Ombi! Vijana ambao Baba zenu sio wenye chama mwisho wenu 2025!

======

20211212_185750.jpg

Sitaki kumjibu Polepole, kwenye CCM ni mchanga, ni sawa sawa na mtoto wa darasa la kwanza anajibiwa na wa chuo kikuu. Polepole ni sawa na unyasi mkavu. Siku Polepole anaingia kwenye chama kujitangaza, alipewa nguo za CCM na Nape Nnauye- Abdallah Bulembo

Najiuliza Mzee Philip Mangula yupo wapi kwa hili linaloendelea kwa Polepole? Kama aliweza kuwahoji makatibu wakuu Wazee Makamba na Kinana, ameshindwa nini kwa Polepole? Naamini, Polepole analo jambo na ukitaka kufanya jambo, usiseme nishikeni nisipigane, wewe pigana tu- Bulembo

Polepole hawezi kuwa mzuri kwa Magufuli kuliko mimi. Nimekaa na Magufuli siku 90 kwenye kampeni za uchaguzi. Nimebadilishana naye nguo wakati wa kampeni. Polepole anampenda Magufuli kwa kuwa alimpa zawadi ya nafasi- Abdallah Bulembo

Lengo la Polepole ni kumkatisha tamaa Rais Samia. Hawezi ni mdogo sana. Rais Samia aachwe, namjua anaweza. Nimekaa naye namjua. Aachwe afanye kazi, lakini wakija vijana wenzenu na shule ya uongozi, huwezi kuifanya ukiwa mbunge, subiri umalize ubunge. Hivi unasema lipi?- Bulembo

Magufuli alituwekea Profesa Kabudi mambo ya nje akavuruga mahusiano yote ya kimataifa. Mama Samia kaingia amemteua Balozi Liberata Mulamula, leo Mama Samia amehutubia mikutano huko UN. Mambo ya kimataifa nchi zinaingiliana- Abdallah Bulembo

"Tuliwaheshimu Polepole na mwenzake kutoka CUF anaitwa Bashiru kwa sababu tu aliyewateuwa tulikuwa tunamheshimu, Magufuli alimteuwa Bashiru Kutoka Cuf kuja kutuhoji kuhusu mali za chama nikamgomea kunihoji nikamwambia yeye sio mwana CCM" Abdallah Bulembo

ZAIDI SOMA;

Dar es Salaam. Mwenyekiti mstaafu wa jumuiya ya wazazi ya CCM, Abdallah Bulembo amemtaka mbunge wa kuteuliwa, Humphrey Polepole amwache Rais Samia Suluhu Hassan atekeleze majukumu yake.

Ametoa kauli hiyo leo Jumapili Desemba 12,2021 katika mkutano wake na waandishi wa habari akimjibu Polepole kuhusu lawama alizotoa dhidi ya Samia ambaye ni mwenyekiti wa CCM.

Bulembo amemuomba makamu mwenyekiti wa chama hicho bara, Philip Mangula kumuhoji Polepole kama alivyowahoji makatibu wakuu wa zamani, Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba ambao sauti zao zilivuja wakikosoa viongozi na mwenendo wa chama hicho tawala, akitaka Polepole naye aitwe kamati ya maadili.

Huku akisisitiza kuwa anakemea suala hilo kama mwanachama wa kawaida na hajatumwa na mtu amesema, “kama Polepole anataka kutoka atoke atuachie CCM maana ana wenzake wanaomshawishi kuanzisha chama chao, asitapetape na kuongea mambo ambayo hayaeleweki.”

"Hawa kina Polepole waliojificha hawatusumbui ndani ya CCM kwa mujibu wa kanuni na katiba ya chama kama mwanachama anaenda tofauti kuna onyo, kufungiwa au kufukuzwa uanachama.”

Bulembo amesema anamfahamu Polepole tangu mwaka 2012 alipoteuliwa na rais mstaafu Jakaya Kikwete kuwa mjumbe wa iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba.

"Siyo kwamba ndani ya CCM tulifurahia uteuzi wake wa ukatibu mwenezi Taifa bali tuliheshimu mamlaka ya aliyekuwa mwenyekiti Taifa hayati John Magufuli bali. Hamjali Samia na kimsingi hawezi kumpangia rais cha kufanya, yeye ni nani,”amesema Bulembo
 
Hahahaaaa....... huyu Bulembo alikuwa kampeni meneja wa Magufuli 2015.

Akapewa ubunge yeye na mwanawe Halima.

Zitto Kabwe akaingilia kati akaoa yule bint!
Hahahah mda mwingine akina Bulembo wanasumbuliwa na udini pamoja na ujinga! Yaani anajidai alikuwa anampenda Magufuli kwani kutembea na Magufuli kama kampeni maneja ndo kuwa naupendo nae? Yaani ukimsikiliza ndo utajua kiwango chake cha ujinga!
 
Back
Top Bottom