Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 9,661
- 14,719
Wana JF
kuna member siku za nyuma alishawahi kuleta thread inayohusu kipindi cha Skonga kinachoonyeshwa EATV (Channel 5) ni kipindi kinachofurahisha, elimisha na kuchangamsha sana
naweza nikasema na mimi nimelazimika kuja na thread ambayo inaweza ikawa imefanana na member mwanzangu.
Jana nilikuwa naangalia kipindi cha Skonga, muendesha kipindi Allan
akamuuliza swali mwanafunzi mmoja wa kike ni kitu gani anachopendelea? mwanafunzi akajibu kuangalia Movies
akaulizwa swali jingine ni movie gani inayozungumzia Maisha ya Idd Amini Dikteta aliyewahi kutawala Nchi ya Uganda, Mwanafunzi akajibu MISUKOSUKO"(MISUKOSUKO ni movie ya Kibongo), Presenter akabaki kinywa wazi akamuuliza nani kacheza Badi" kwa waliokiangalia kipindi walijionea mengi. (jina sahihi la movie ni THE LAST KING OF SCOTLAND)
lakini lengo langu ni hapo kwa huyo mwanafunzi kusema ni Mpenzi wa Movies halafu Movie zenyewe za Kibongo,
wadau naomba tusaidiane kwa hili hivi Movie za kibongo zinamsaidiaje au zinamwelimishaje Kijana wa Kitanzania katika Dunia ya sasa??
hivi hata kama ni wewe unaweza ukasimama mbele za watu tena kwenye television kama Channel 5 na kusema ni shabiki wa Bongo Movies???
yawezekana jibu likawa ndio/hapana!
Movies za kibongo zina maudhui gani katika ulimwengu wa kisasa?
ni zinamjenga vipi kijana ambae anajiandaa kuwa mtu mzima?
Asanteni!!!
kuna member siku za nyuma alishawahi kuleta thread inayohusu kipindi cha Skonga kinachoonyeshwa EATV (Channel 5) ni kipindi kinachofurahisha, elimisha na kuchangamsha sana
naweza nikasema na mimi nimelazimika kuja na thread ambayo inaweza ikawa imefanana na member mwanzangu.
Jana nilikuwa naangalia kipindi cha Skonga, muendesha kipindi Allan
akamuuliza swali mwanafunzi mmoja wa kike ni kitu gani anachopendelea? mwanafunzi akajibu kuangalia Movies
akaulizwa swali jingine ni movie gani inayozungumzia Maisha ya Idd Amini Dikteta aliyewahi kutawala Nchi ya Uganda, Mwanafunzi akajibu MISUKOSUKO"(MISUKOSUKO ni movie ya Kibongo), Presenter akabaki kinywa wazi akamuuliza nani kacheza Badi" kwa waliokiangalia kipindi walijionea mengi. (jina sahihi la movie ni THE LAST KING OF SCOTLAND)
lakini lengo langu ni hapo kwa huyo mwanafunzi kusema ni Mpenzi wa Movies halafu Movie zenyewe za Kibongo,
wadau naomba tusaidiane kwa hili hivi Movie za kibongo zinamsaidiaje au zinamwelimishaje Kijana wa Kitanzania katika Dunia ya sasa??
hivi hata kama ni wewe unaweza ukasimama mbele za watu tena kwenye television kama Channel 5 na kusema ni shabiki wa Bongo Movies???
yawezekana jibu likawa ndio/hapana!
Movies za kibongo zina maudhui gani katika ulimwengu wa kisasa?
ni zinamjenga vipi kijana ambae anajiandaa kuwa mtu mzima?
Asanteni!!!