Bongo movie kukosa uwakilishi mpana unaidumuza tasnia, uswahili na u-Dar ni mwingi kupitiliza.

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,641
46,283
Sababu mojawapo tasnia ya bongo movie imekuwa dumavu, mbovu na isiyofanya vizuri kwa muda wote tangu nchi ipate uhuru inaweza kuwa ni kutokana na kutawaliwa na watu/waigizaji wa pwani na kusini zaidi. Upande wa maudhui na mazingira ni hivyo hivyo pia, ni ya kipwani, Kusini na Uswahili zaidi.

Kinachotakiwa sasa ni wadau wafanye jitihada binafsi kuifanya sekta hiyo kuwa jumuishi zaidi na yenye uwakilishi mpana kwa kuhakikisha watu wa jamii nyingi tofauti zaidi kama Wahaya, Wasukuma, Wakuria, Wambulu, Wamasai, Wanyakyusa, Wasafwa, Wakinga n.k wanashiriki katika kuigiza bongo movie ili kutanua wigo wake, kuvutia watu wengi zaidi na kuongeza ubunifu na tija.

Pia wajaribu kufanyia kazi zao katika mazingira tofauti na ya Dar au pwani. Nchi kubwa kama hii ni ujuha kazi zote za bongo movie kuigizia mazingira ya ki'Dar es Salaam na Kipwani tu. Igizieni hata huko Katavi, Mbeya, Arusha, Kigoma, Mbeya, Mara, Mwanza.
 
Hawajui Kiswahili hivyo hawavutii wakiongea!
Watanzania wote wanajua Kiswahili, wanatofautiana lafudhi tu. Na hiyo ndio maana ya uwakilishi mpana na jumuishi, unakuwa na kazi za sanaa zenye watu wenye lafudhi tofauti kuzivutuia jamii husika. Tena watu halisi wa hizo jamaa, sio mndengereko anayeigiza kuongea lafudhi ya Kisukuma au Kimasai.
 
Mtoa sijui unaongea nini,maana unachowaza hakina maana. Bongo Fleva yenyewe centre yake ni Dar,watu wanafuata studio nzuri za kurekodi muziki,wanafuata directors wenye majina makubwa,wanafuata masoko, show nyingi na promotions mjini.
Bongo movie ni hivyo hivyo. MC mboneke alitoka Mbeya sasa hivi yupo Dar. Msanii ufanye sanaa yako Musoma kuna directors gani wa maana? utafanyia promotions kwenye media gani? utazindulia kazi zako Musoma kwa audience ipi?
Nadhani ulichotakiwa kushauri ni wasanii wakubwa kuwa na fikra pana zaidi,story zao zitanuke. Wafanye filamu zenye maudhui mbalimbali yanayohusu watu wa mikoani,pia wawe na bajeti ya kwenda huko mikoani kufanya shooting huko.
Sio kwamba haifanyiki inafanyika lakini sio kwa ukubwa sana.
NB. Siamini kama nimechangia kitu kuhusu Bongo Movie,ni kichefuchefu kwangu.
 
Mtoa sijui unaongea nini,maana unachowaza hakina maana. Bongo Fleva yenyewe centre yake ni Dar,watu wanafuata studio nzuri za kurekodi muziki,wanafuata directors wenye majina makubwa,wanafuata masoko, show nyingi na promotions mjini.
Bongo movie ni hivyo hivyo. MC mboneke alitoka Mbeya sasa hivi yupo Dar. Msanii ufanye sanaa yako Musoma kuna directors gani wa maana? utafanyia promotions kwenye media gani? utazindulia kazi zako Musoma kwa audience ipi?
Nadhani ulichotakiwa kushauri ni wasanii wakubwa kuwa na fikra pana zaidi,story zao zitanuke. Wafanye filamu zenye maudhui mbalimbali yanayohusu watu wa mikoani,pia wawe na bajeti ya kwenda huko mikoani kufanya shooting huko.
Sio kwamba haifanyiki inafanyika lakini sio kwa ukubwa sana.
NB. Siamini kama nimechangia kitu kuhusu Bongo Movie,ni kichefuchefu kwangu.
Nchi hii imetengenezewa mazingira ya kila kitu kufanyika Dar! Ni mentalite ya kijinga na imasikini tu! Ndo maana serkali kila kitu inarundika Dar! Hawana ubunifu wa kufanya maeneo mengine pia yawe na mwamko wa kimaendeleo!

Upande wa sanaa kusema kweli watu wengi wanaigiza movie zenye maudhui ya ukisasa na ufeki mwing!
Mtu anaigiza yuko shamba bado anaonekana kavaa wigi,kope feki na makeup na hali ya juu!

Pia uigizaji usioendana na uhalisia wa maisha ya watazamaji wengi! Mfano maigizo mengi yanakuwa na uswahili mwingi sana wa kipwani na yako mengi na hakuna uhalisia wa maisha ya jamii zingine!
 
Sababu mojawapo tasnia ya bongo movie imekuwa dumavu, mbovu na isiyofanya vizuri kwa muda wote tangu nchi ipate uhuru inaweza kuwa ni kutokana na kutawaliwa na watu/waigizaji wa pwani na kusini zaidi. Upande wa maudhui na mazingira ni hivyo hivyo pia, ni ya kipwani, Kusini na Uswahili zaidi.

Kinachotakiwa sasa ni wadau wafanye jitihada binafsi kuifanya sekta hiyo kuwa jumuishi zaidi na yenye uwakilishi mpana kwa kuhakikisha watu wa jamii nyingi tofauti zaidi kama Wahaya, Wasukuma, Wakuria, Wambulu, Wamasai, Wanyakyusa, Wasafwa, Wakinga n.k wanashiriki katika kuigiza bongo movie ili kutanua wigo wake, kuvutia watu wengi zaidi na kuongeza ubunifu na tija.

Pia wajaribu kufanyia kazi zao katika mazingira tofauti na ya Dar au pwani. Nchi kubwa kama hii ni ujuha kazi zote za bongo movie kuigizia mazingira ya ki'Dar es Salaam na Kipwani tu. Igizieni hata huko Katavi, Mbeya, Arusha, Kigoma, Mbeya, Mara, Mwanza.
bado una muda wa kuwafuatilia? Hata House Girls nao walisha acha, saaa kama Beki tatu walisha acha kufuafilia Bongo move, wewe utakuwa wa ajabu sana kuwafuatilia
 
Sababu mojawapo tasnia ya bongo movie imekuwa dumavu, mbovu na isiyofanya vizuri kwa muda wote tangu nchi ipate uhuru inaweza kuwa ni kutokana na kutawaliwa na watu/waigizaji wa pwani na kusini zaidi. Upande wa maudhui na mazingira ni hivyo hivyo pia, ni ya kipwani, Kusini na Uswahili zaidi.

Kinachotakiwa sasa ni wadau wafanye jitihada binafsi kuifanya sekta hiyo kuwa jumuishi zaidi na yenye uwakilishi mpana kwa kuhakikisha watu wa jamii nyingi tofauti zaidi kama Wahaya, Wasukuma, Wakuria, Wambulu, Wamasai, Wanyakyusa, Wasafwa, Wakinga n.k wanashiriki katika kuigiza bongo movie ili kutanua wigo wake, kuvutia watu wengi zaidi na kuongeza ubunifu na tija.

Pia wajaribu kufanyia kazi zao katika mazingira tofauti na ya Dar au pwani. Nchi kubwa kama hii ni ujuha kazi zote za bongo movie kuigizia mazingira ya ki'Dar es Salaam na Kipwani tu. Igizieni hata huko Katavi, Mbeya, Arusha, Kigoma, Mbeya, Mara, Mwanza.
Mkuu weka pesa u produce yako uwe mfano wa kuigwa.
 
Mkuu weka pesa u produce yako uwe mfano wa kuigwa.
Kumbe wewe ni mpuuzi! hutaki kukosolewa na unajua kila kitu. Sasa huyo mdau hapo anashauri vizuri tayari wewe unamuona hana maana na kuonesha dharau wakati watu tunategemeana kwenye kila idara maishani1
Ubishoo mwingi na upumbavu mwingi kichwani! Mnafanya tasinia kijiwe cha ngono badala ya kuelimisha na kuburudisha jamii1
 
bado una muda wa kuwafuatilia? Hata House Girls nao walisha acha, saaa kama Beki tatu walisha acha kufuafilia Bongo move, wewe utakuwa wa ajabu sana kuwafuatilia
Wakati nasafari kwenye bus nitaanza kuwaambia makondakta wasiwe wanaweka bongo movies ili nisiwafuatilie.
 
Nakumbuka Kuna muigizaji mmoja kutoka huku Africa alikuwa na mpango.wa kutenheneza movie hivyo aka amua kwenda kwa anord Schwarzenegger kuomba ushauri

Mwihizaji huyo aka muuliza anornd kwamba nifanyeje ili movie yangu itazamwe dunia mzima? Anord alimjibu hivi

Ukitaka movie yako itazamwe dunia mzima Basi unapaswa kuhakikisha movie yako inakuwa imesheheni maeneo mbalimbali ya dunia

mf Singapore, south Africa,Beijing, New York,hongkong, Jerusalem, nk hakikisha zina kuwepo kwenye movie yako

lakini pia vivutio.mbali mbali vya dunia Kama piramid za misri, Everest mountains,Kilimanjaro,na zile water bodies Kama Indian ocean,pasific, nk hakikisha vina kueopo pia

Mkuu ni nadra kuona milima,ng'ombe,tembo,fisi,chui,kiboko au mamba kwenye movie zetu za kibongo. Si rahisi kuona miji Kama mwanza,kigoma,tabora, Zanzibar,kwenye movie zetu

Si rahisi kuona mashamba ya mipunga,mahindi,katani,chai migomba kwa mwonekano.wa kitarii kwenye movie zetu

Kwahiyo Nina ungana na wewe katika Hilo mkuu tuna paswa kubadirika ili kuikuuza Sanaa yetu🙏🙏🙏
 
Ukitaka kuamini nchi yetu bado ni yakishamba ndio vitu kama hizi kla ktu Dar, lkn hatuna haja yakiwalaumu Bongo Movie badla yake tuilaumu gvt inayowekeza nguvu Dsm kulko mikoa mingne
 
Nakumbuka Kuna muigizaji mmoja kutoka huku Africa alikuwa na mpango.wa kutenheneza movie hivyo aka amua kwenda kwa anord Schwarzenegger kuomba ushauri

Mwihizaji huyo aka muuliza anornd kwamba nifanyeje ili movie yangu itazamwe dunia mzima? Anord alimjibu hivi

Ukitaka movie yako itazamwe dunia mzima Basi unapaswa kuhakikisha movie yako inakuwa imesheheni maeneo mbalimbali ya dunia

mf Singapore, south Africa,Beijing, New York,hongkong, Jerusalem, nk hakikisha zina kuwepo kwenye movie yako

lakini pia vivutio.mbali mbali vya dunia Kama piramid za misri, Everest mountains,Kilimanjaro,na zile water bodies Kama Indian ocean,pasific, nk hakikisha vina kueopo pia

Mkuu ni nadra kuona milima,ng'ombe,tembo,fisi,chui,kiboko au mamba kwenye movie zetu za kibongo. Si rahisi kuona miji Kama mwanza,kigoma,tabora, Zanzibar,kwenye movie zetu

Si rahisi kuona mashamba ya mipunga,mahindi,katani,chai migomba kwa mwonekano.wa kitarii kwenye movie zetu

Kwahiyo Nina ungana na wewe katika Hilo mkuu tuna paswa kubadirika ili kuikuuza Sanaa yetu🙏🙏🙏
Umenena sisi watazamaji tunataka tuone zaidi ya story iliyopo...nadhani bajeti ni ndogo,vifaa vichache na duni na wataalamu wa kunasa matukio ni wachache.
Naamini waigizaji makini wapo ila vikwazo ni hivyo hapo juu.
 
NAONA MOJA YA SBB YA KUSHINDWA KUINUKA KWA HIYO SANAA NI
UKOSEFU WA MGAWANYO WA KAZI, MAJUKUMU NA UKOSEFU WA UTAFITI.
MTU MMOJA NAWEZA KUWA NDIO:

  • MTUNZI
  • MUONGOZAJI/DIRECTOR
  • MZALISHAJI/PRODUCER
  • SOUND PRODUCER
  • PRINCIPAL CAST
  • EDITOR
  • MUSIC EDITOR
  • CAMERA AND LIGHTING
  • MAPAMBO NA UREMBO
  • LOCATION MANAGER
  • TRANSPORT OFFICER
  • MWEKA HAZINA!
 
Back
Top Bottom