malimwengu
Member
- Aug 29, 2011
- 21
- 12
Hivi karibuni Bodi ya Mikopo ya wanafunzi (HESLB) imetoa majina ya wadaiwa sugu ambao hawajaanza kukatwa kile kinachoitwa 'mikopo yao' kwa mujibu wa sheria ya bodi ya mikopo kifungu cha 9 ya mwaka 2004. Wanaodaiwa wengi ni wale waliomaliza chuo kati ya mwaka 1994 mpaka 2005.
Katika majina bodi ambayo imeyatoa kuna majina ya watu ambao wao walipata ufadhili wa serikali, wapo waliopata ufadhili wa mashirika tofauti mfano ule wa mpango maalum wa wanawake ambao hawajafikia kiwango kwa wakati ule ambao waliitwa pre entry.
Kipindi hicho waliofaulu tu nfio walipewa scholarship na serikali na waliitwa Government sponsored students an wengi walipata division one na two tu.
Sasa leo iweje watu ambao hawakukopeshwa na bodi majina yao yatoke kama wadaiwa? Huu ni udhalilishaji ambao kama kuna baadhi ya watu wataamua kwenda mahakamani kudai fidia, serikali itaingia hasara kubwa kuliko ile ya richmond. Hatua za haraka zichukuliwe kabla hili halijawa janga la kitaifa. wanasheria tunaomba msaada wenu katika hili tuweze kuepuka hasara hii
Katika majina bodi ambayo imeyatoa kuna majina ya watu ambao wao walipata ufadhili wa serikali, wapo waliopata ufadhili wa mashirika tofauti mfano ule wa mpango maalum wa wanawake ambao hawajafikia kiwango kwa wakati ule ambao waliitwa pre entry.
Kipindi hicho waliofaulu tu nfio walipewa scholarship na serikali na waliitwa Government sponsored students an wengi walipata division one na two tu.
Sasa leo iweje watu ambao hawakukopeshwa na bodi majina yao yatoke kama wadaiwa? Huu ni udhalilishaji ambao kama kuna baadhi ya watu wataamua kwenda mahakamani kudai fidia, serikali itaingia hasara kubwa kuliko ile ya richmond. Hatua za haraka zichukuliwe kabla hili halijawa janga la kitaifa. wanasheria tunaomba msaada wenu katika hili tuweze kuepuka hasara hii