Gazeti la Nipashe limeripoti kilio kuhusu mikopo ya Elimu ya Juu kutoka Bodi ya Mikopo

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Nipashee.jpg

UFAFANUZI WA BODI YA MIKOPO: MKOPO UNATEGEMEA NA UHITAJI WA MUOMBAJI KWA ALIVYOOMBA

Mkuu wa Mawasiliano wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Tanzania (HESLB), Omega Ngole anafafanua:

“Upangaji wa viwango vya mikopo kwa Wanafunzi wanufaika unatokana na uhitaji wa muombaji kulingana na nyaraka alizowasilisha HESLB wakati wa maombi yake, mfano muombaji akisema ana ulemavu, yatima, historia yake kimasomo n.k inaweza kuchangia kiwango anachotakiwa kukipata.

“Hali hiyo inafanya viwango vitofautiane, kuna makundi yanayopewa kipaumbele mfano yatima, wenye ulemavu au waliofanya vizuri zaidi katika mitihani n.k

"Hao wanaolalamika wanatakiwa kujua kiwango cha mkopo kinatokana na nyaraka zao wenyewe.

"Kiwango cha mkopo hakiwezi kulingana kwa kila Mwanafunzi na ndio maana kila mmoja anaingiziwa fedha kwenye akaunti yake binafsi, hilo ni suala la mtu mmoja mmoja kulingana na mahitaji na ndio maana wapo ambao wamepata mkopo kwa kiwango cha 100%."

Pia soma:
-TAHLISO wanapaswa kusimama na kupigania haki za Wanafunzi kuhusu Mikopo
- Matokeo ya mikopo ya elimu ya juu 2023/2024 na changamoto zake
 
Serikali inachofanya ni kutaka kuharibu elimu ya vijana wa taifa hili, haiwezekani vijana wamejitahidi kusoma hadi ngazi ya kidato cha sita na kufaulu kwenda vyuo vikuu halafu wakwame hapo kisha mikopo.

Kama watu wachache wanaweza kufisadi trilioni 30, hao vijana wanahitaji pesa nyingi kiasi gani hadi wabaguliwe kupewa hiyo wanayoita mikopo!​
 
TAHLISO hiyo ni taasisi tanzu ya CCM,hakuna wa kuwapigania Wanafunzi humo.Wanafunzi wapambane wenyewe.
Siku Ile hao TAHLISO wamekutana na Rais,wakamuomba awaongezee hela ya kujikimu,Mama akawaambia atawapa 10000, yakatoka yana shingilia kama Mazuzu.Sasa gharama za maisha zilivyo juu 10000 ni Hela gani!??

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Mikopo waliyotoa ni kama vile hawataki Hawa vijana waendelee na elimu. Kuna mwingine alifaulu kwao Wana maisha ya shida mpaka sasa hareport chuo kwa sababu ya ada
 
Mpaka akili zikae sawa,tuache kushangilia CCM, samia, na kenge wengine wa CCM, Kuna vijana waliandsmana kumshangilia makonda! Mpaka unajiuliza, Hawa wana ubongo vichwani au USAA! We upo kitaa, apeche aloloo! Unafaidika nini na CCM, pesa za mikopo zinaenda kulipa wake wa viongozi mishahara!
 
TAHLISO ni janga kubwa Sana wapo kwa ajili ya kupiga mapambiao na kuweka status za ccm tu ,wanatumika kiccm na sio kupazasauti za wanyonge fikiria mwanafunzi alipa ada 1300000 lakini bodi wanamlipia 230000 upuuzi lakini hao TAHLISO WAKO WANATANUA MIDOMO MAMA ANAUPIGA MWINGI
 
Back
Top Bottom