Taarifa kwa Wanafunzi 238 wa Samia Scholarship 2022/2023 kupata mkopo wa Bodi ya Mikopo

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,875
Taarifa kwa wanafunzi 238 wa Samia Scholarship 2022/2023 ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8.

Leo tar.2/Novemba /2023 niliandika taarifa ya kwamba wanafunzi 238 kati ya 640 ambao wana ufadhili wa Samia Scholarship ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8 na hivyo kuambiwa wameondolewa kwenye ufadhili na kuzuiwa hata kufanya usajili vyuoni.

Taarifa ya awali hii hapa - Wanafunzi 238 wa ufadhili wa Samia Scholarship 2022/2023 hawajui hatma yao

Waziri wa Elimu Prof.Mkenda @professoradolfmkenda aliona taarifa niliyoandika na akafuatilia kujua tatizo lipo wapi ,ameahidi ya kwamba wanafunzi wote ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8 wataendelea na masomo na usajili watafanya na fedha wataendelea kulipiwa kama kawaida ila tuu kama mkopo ambao wataulipa na sio kama ufadhili 100% tena sababu wameshindwa kufikisha GPA ya 3.8 kama inavyotakiwa. Na ameahidi taarifa rasmi itatolewa na Wizara ya Elimu muda sio mrefu .

Binafsi nichukue nafasi kumshukuru Mh.Waziri wa Elimu Prof. Mkenda kwa uwajibikaji wake wa kusikia changamoto na kuzitolea majibu,ufafanuzi na utatuzi haraka. Binafsi napongeza hatua hii ni nzuri sababu itaendelea kufanya wanafunzi hao wasome zaidi kufikisha GPA 3.8 ili wapate ufadhili 100% na hata hao ambao hawatafikisha GPA 3.8 wataendelea kupewa fedha hizo kama mkopo . Hivyo ni chaguo la mwanafunzi. Nina shauri wanafunzi chaguo liwe moja tuu kusoma , kusoma,kusoma kwa bidii ili kufikisha hiyo GPA 3.8 kuendelea kupata ufadhili 100% , tofauti na hapo huo ni mkopo na utapaswa kulipwa.

Tutaendelea kufuatilia ufanisi wa Program hii na hatutasita kukosoa ,kushauri na kupendekeza kwa manufaa ya Elimu yetu na nchi yetu , popote tukiona kuna tatizo.

Ahsante sana.

=========== ============

UFAFANUZI WA BODI YA MIKOPO
Mkuu wa Mawasiliano wa HESLB, Omega Ngole amezungumza na JamiiForums na kusema “Ni kweli kuna Kundi la hao Wanafunzi ambao hawajatimiza vigezo, watahamishiwa katika mkopo wa Bodi na wataruhusiwa kufanya maombi ya mkopo kwa kuwa huwezi kupata mkopo kama hujaomba.”

Ikumbukwe kuwa sehemu ya mkataba wa Ufadhili wa Samia ni kuwa Mnufaika hatakiwi kupata chini ya ufaulu wa GPA 3.8, kinyume na hapo ataondolewa katika ufadhili na kuingizwa katika Mkopo wa HESLB.
 
Taarifa kwa wanafunzi 238 wa Samia Scholarship 2022/2023 ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8.

Leo tar.2/Novemba /2023 niliandika taarifa ya kwamba wanafunzi 238 kati ya 640 ambao wana ufadhili wa Samia Scholarship ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8 na hivyo kuambiwa wameondolewa kwenye ufadhili na kuzuiwa hata kufanya usajili vyuoni.

Waziri wa Elimu Prof.Mkenda @professoradolfmkenda aliona taarifa niliyoandika na akafuatilia kujua tatizo lipo wapi ,ameahidi ya kwamba wanafunzi wote ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8 wataendelea na masomo na usajili watafanya na fedha wataendelea kulipiwa kama kawaida ila tuu kama mkopo ambao wataulipa na sio kama ufadhili 100% tena sababu wameshindwa kufikisha GPA ya 3.8 kama inavyotakiwa. Na ameahidi taarifa rasmi itatolewa na Wizara ya Elimu muda sio mrefu .

Binafsi nichukue nafasi kumshukuru Mh.Waziri wa Elimu Prof. Mkenda kwa uwajibikaji wake wa kusikia changamoto na kuzitolea majibu,ufafanuzi na utatuzi haraka. Binafsi napongeza hatua hii ni nzuri sababu itaendelea kufanya wanafunzi hao wasome zaidi kufikisha GPA 3.8 ili wapate ufadhili 100% na hata hao ambao hawatafikisha GPA 3.8 wataendelea kupewa fedha hizo kama mkopo . Hivyo ni chaguo la mwanafunzi. Nina shauri wanafunzi chaguo liwe moja tuu kusoma , kusoma,kusoma kwa bidii ili kufikisha hiyo GPA 3.8 kuendelea kupata ufadhili 100% , tofauti na hapo huo ni mkopo na utapaswa kulipwa.

Tutaendelea kufuatilia ufanisi wa Program hii na hatutasita kukosoa ,kushauri na kupendekeza kwa manufaa ya Elimu yetu na nchi yetu , popote tukiona kuna tatizo.

Ahsante sana.
Kazi nzuri kijana mzalendo
 
Walipata ufadhili Kwa sababu ya kufaulu vizuri, Sasa kwanini uwaekee masharti ya g.p.a 3.8 , serikali ya CCM ni ya kihuni, hii ni zawadi ya kufaulu form six vizuri, haikutakiwa masharti ilimradi wamefaulu
 
Taarifa kwa wanafunzi 238 wa Samia Scholarship 2022/2023 ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8.

Leo tar.2/Novemba /2023 niliandika taarifa ya kwamba wanafunzi 238 kati ya 640 ambao wana ufadhili wa Samia Scholarship ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8 na hivyo kuambiwa wameondolewa kwenye ufadhili na kuzuiwa hata kufanya usajili vyuoni.

Taarifa ya awali hii hapa - Wanafunzi 238 wa ufadhili wa Samia Scholarship 2022/2023 hawajui hatma yao

Waziri wa Elimu Prof.Mkenda @professoradolfmkenda aliona taarifa niliyoandika na akafuatilia kujua tatizo lipo wapi ,ameahidi ya kwamba wanafunzi wote ambao wamepata chini ya GPA ya 3.8 wataendelea na masomo na usajili watafanya na fedha wataendelea kulipiwa kama kawaida ila tuu kama mkopo ambao wataulipa na sio kama ufadhili 100% tena sababu wameshindwa kufikisha GPA ya 3.8 kama inavyotakiwa. Na ameahidi taarifa rasmi itatolewa na Wizara ya Elimu muda sio mrefu .

Binafsi nichukue nafasi kumshukuru Mh.Waziri wa Elimu Prof. Mkenda kwa uwajibikaji wake wa kusikia changamoto na kuzitolea majibu,ufafanuzi na utatuzi haraka. Binafsi napongeza hatua hii ni nzuri sababu itaendelea kufanya wanafunzi hao wasome zaidi kufikisha GPA 3.8 ili wapate ufadhili 100% na hata hao ambao hawatafikisha GPA 3.8 wataendelea kupewa fedha hizo kama mkopo . Hivyo ni chaguo la mwanafunzi. Nina shauri wanafunzi chaguo liwe moja tuu kusoma , kusoma,kusoma kwa bidii ili kufikisha hiyo GPA 3.8 kuendelea kupata ufadhili 100% , tofauti na hapo huo ni mkopo na utapaswa kulipwa.

Tutaendelea kufuatilia ufanisi wa Program hii na hatutasita kukosoa ,kushauri na kupendekeza kwa manufaa ya Elimu yetu na nchi yetu , popote tukiona kuna tatizo.

Ahsante sana.

=========== ============

UFAFANUZI WA BODI YA MIKOPO
Mkuu wa Mawasiliano wa HESLB, Omega Ngole amezungumza na JamiiForums na kusema “Ni kweli kuna Kundi la hao Wanafunzi ambao hawajatimiza vigezo, watahamishiwa katika mkopo wa Bodi na wataruhusiwa kufanya maombi ya mkopo kwa kuwa huwezi kupata mkopo kama hujaomba.”

Ikumbukwe kuwa sehemu ya mkataba wa Ufadhili wa Samia ni kuwa Mnufaika hatakiwi kupata chini ya ufaulu wa GPA 3.8, kinyume na hapo ataondolewa katika ufadhili na kuingizwa katika Mkopo wa HESLB.
Kigezo hiki ni hatari sana, kinaweza kuchochea rushwa ya ngono. Ufadhili uendelee kwa kila mwanafunzi aliyefaulu mwaka. Kumbuka sekondari na chuo ni vitu viwili tofauti. Maisha ya chuo kikuu yanaweza kusababisha mwanafunzi kuyumba hasa mwaka wa kwanza.
 
Walipata ufadhili Kwa sababu ya kufaulu vizuri, Sasa kwanini uwaekee masharti ya g.p.a 3.8 , serikali ya CCM ni ya kihuni, hii ni zawadi ya kufaulu form six vizuri, haikutakiwa masharti ilimradi wamefaulu
Serikali ilikuwa inatafuta vijana wenye akili nyingi ikitegemea baadaye iwaajiri serikali nafasi nyeti kumbe wote hao 238 wezi wa mitihani tu shule walisoma au walibahatisha tu mwenye akili kubwa anakuwa consistent haibadiliki kama kinyonga

Na hao waliobaki waambieni wakaze Buti mwaka wa Pili wakifeli out scholarship ya mama Samia wasahau
 
Baada ya kuisoma hii nikakumbuka maisha yangu ya chuo

Mwaka wa kwanza kutokana na ugeni wa kozi ya sheria nilipata GPA ya 3.6
Ila mwaka wa pili baada ya kuzoea nikapata GPA ya 4.6 nimekuja kumaliza chuo na overall ya 4 point kazaa

Huu ni mfano ulio hai.. hichi kigezo cha 3.8 ni kigumu hasa mfumo wetu wa elimu ulivyo ambao haukuandai kwa ajili ya kuspecialize kitu fulani
 
Kigezo hiki ni hatari sana, kinaweza kuchochea rushwa ya ngono. Ufadhili uendelee kwa kila mwanafunzi aliyefaulu mwaka. Kumbuka sekondari na chuo ni vitu viwili tofauti. Maisha ya chuo kikuu yanaweza kusababisha mwanafunzi kuyumba hasa mwaka wa kwanza.
Maisha ya chuo marahisi sna ukipiga shule. Mtihani unatoka vile ulivyofundishwa mhadhiri akitoa tofauti mnkg rufaa.
A level kuna upuuzi mwingi wa walimu kutofundisha wakati mtihani upo pale pale.
Sasa mtu kashindwa kuwa consistent afanyweje?
Vigezo na masharti vizingatiwe
 
Baada ya kuisoma hii nikakumbuka maisha yangu ya chuo

Mwaka wa kwanza kutokana na ugeni wa kozi ya sheria nilipata GPA ya 3.6
Ila mwaka wa pili baada ya kuzoea nikapata GPA ya 4.6 nimekuja kumaliza chuo na overall ya 4 point kazaa

Huu ni mfano ulio hai.. hichi kigezo cha 3.8 ni kigumu hasa mfumo wetu wa elimu ulivyo ambao haukuandai kwa ajili ya kuspecialize kitu fulani
Itategemea mtu na mtu sababu Kuna ambao huo mwaka wa kwanza tu wanapiga 4 and above.
Na mfadhili ndiye anatoa masharti usipofikia out.
 
Hapo ni mwendo wa kuomba vyuo vya praiveti tu,vyuo vya serikali,baadhi kufikisha GPA ya 3.8 ni wachache wanaofikisha.
 
Maisha ya chuo marahisi sna ukipiga shule. Mtihani unatoka vile ulivyofundishwa mhadhiri akitoa tofauti mnkg rufaa.
A level kuna upuuzi mwingi wa walimu kutofundisha wakati mtihani upo pale pale.
Sasa mtu kashindwa kuwa consistent afanyweje?
Vigezo na masharti vizingatiwe
Ukifika chuo unazika division one yako getini la sivyo utashangaa mtu ulikuwa unamuona wa kawaida A level lakin chuo anakimbiza
 
Baada ya kuisoma hii nikakumbuka maisha yangu ya chuo

Mwaka wa kwanza kutokana na ugeni wa kozi ya sheria nilipata GPA ya 3.6
Ila mwaka wa pili baada ya kuzoea nikapata GPA ya 4.6 nimekuja kumaliza chuo na overall ya 4 point kazaa

Huu ni mfano ulio hai.. hichi kigezo cha 3.8 ni kigumu hasa mfumo wetu wa elimu ulivyo ambao haukuandai kwa ajili ya kuspecialize kitu fulani
Hao waliobaki waliopata 3.8 kwenda juu wao ni wenyeji chuo kikuu? Ndio waliojenga chuo kikuu?
 
Serikali ilikuwa inatafuta vijana wenye akili nyingi ikitegemea baadaye iwaajiri serikali nafasi nyeti kumbe wote hao 238 wezi wa mitihani tu shule walisoma au walibahatisha tu mwenye akili kubwa anakuwa consistent haibadiliki kama kinyonga

Na hao waliobaki waambieni wakaze Buti mwaka wa Pili wakifeli out scholarship ya mama Samia wasahau
We una elimu gani babuu mbona unajifanya jiziazi
 
Kama waliandikishwa kwenye MKATABA.. na waliambiwa.. wakafanya MASIKHARA huko CHUONI wakaendekeza UZINZI na ULEVI..

Walimwe tu.. hata kuwapa Mkopo huko Helsb ni kupoteza hela ambazo hazitarudi.
 
Back
Top Bottom