Biashara ya salon za kiume na kike

viti viwili 1.2M, Kitanda cha msg 0.6M, Vioo na kufix 0.1M, shaving mashines nzuri mbili 0.3M, Hair bowl mpya ya kisasa 0.7M, consumables and towels weka 0.1M. milioni tatu imeishia hapo ila ukiwa na 5M kwa saluni ya kiume unaanza vizuri sana. cc Cutie M

Shukurani mkuu kwa taarifa, wapi naweza pata viti 2 kwa 1.2M maana pale fire kiti kimoja wanaanzia 1M.
 
Last edited by a moderator:
Hii kazi ni nzuri sana, inalipa vema sana. Cha muhimu ni usimamizi madhubuti. Ni nzuri sana ukifungua mahali karibu nawe, atleast ndani ya wiki uwepo hapo golini hata mara tatu. Vijana wasimamizi na vinyozi hukosa uaminifu pindi boss anapokuwa nao mbali.
 
Hii kazi ni nzuri sana, inalipa vema sana. Cha muhimu ni usimamizi madhubuti. Ni nzuri sana ukifungua mahali karibu nawe, atleast ndani ya wiki uwepo hapo golini hata mara tatu. Vijana wasimamizi na vinyozi hukosa uaminifu pindi boss anapokuwa nao mbali.

Muda muafaka ukiwadia huu ushauri nitauzingatia.
 
Jaman mwenye kujua Hesabu ya saluni kulingana na bei ya kunyolea inakuwaje? Mfano bei ya kunyolea ni 1,500 2,000 au 3,000 hapo makusanyo yanapaswa kuwa shilingi ngapi kwa siku au kwa week??
 
Mkuu Shark's Style inategemeana na ubora wa salon na eneo ilipo, kama ya kawaida tu range ya elfu 60 hadi 80 kwa kiti, kama ya kiwango kizuri wanaweza kulipa h?ta laki1 kwa wiki kwa kila kiti.
 
Jaman mwenye kujua Hesabu ya saluni kulingana na bei ya kunyolea inakuwaje? Mfano bei ya kunyolea ni 1,500 2,000 au 3,000 hapo makusanyo yanapaswa kuwa shilingi ngapi kwa siku au kwa week??

hiyo haitabiriki mkuu mana siku hazifanani? sema ndo una angalia nasehemu yenyewe sasa kama ni ya watu wengi sana unakubaliana hesabu kamili?
 
Nimeupenda sana huu Uzi maana Mimi mwenyewe mjasiriamali na Nina plan ya kufungua Barber shop next year. So wenye uzoefu endeleeni kutoa darasa
 
Wakuu hapo juu wamechangia vizuri sana tu,ila kuna vitu hawajaviainisha wazi sana.
Karibia frames zote zinazopangishwa unakuta hazikidhi vigezo kwa salon,inabidi uingize gharama zako tena sio kidogo,kama milango,rangi,tiles nk,na wahuni wengine wanakutwanga umeme wa ku-share

Hapo bado kodi ya Frame,ambapo be zake zinafahamika,labda iwe uswahili saana,na si chini ya 100,000 hata huko uswazi,sasa ukijongea centers za eneo ulipo ndio kabisaa.

Na Salon yenye chumba cha massage lazima iwe na frame kubwa au uchukua frames mbili,siku hizi watu wanajenga frame ndogo sana kimaslahi zaidi,sasa hapo lazima ziwe mbili.
Suala jingine ni kuangalia na viti vya kuanza navyo,kwanza lamzima uwe na malengo ya kufikia angalau viti vinne.Ila anza na viwili kwanza,then utaangalia muelekeo wa kazi yako.
 
Wakuu hapo juu wamechangia vizuri sana tu,ila kuna vitu hawajaviainisha wazi sana.
Karibia frames zote zinazopangishwa unakuta hazikidhi vigezo kwa salon,inabidi uingize gharama zako tena sio kidogo,kama milango,rangi,tiles nk,na wahuni wengine wanakutwanga umeme wa ku-share

Hapo bado kodi ya Frame,ambapo be zake zinafahamika,labda iwe uswahili saana,na si chini ya 100,000 hata huko uswazi,sasa ukijongea centers za eneo ulipo ndio kabisaa.

Na Salon yenye chumba cha massage lazima iwe na frame kubwa au uchukua frames mbili,siku hizi watu wanajenga frame ndogo sana kimaslahi zaidi,sasa hapo lazima ziwe mbili.
Suala jingine ni kuangalia na viti vya kuanza navyo,kwanza lamzima uwe na malengo ya kufikia angalau viti vinne.Ila anza na viwili kwanza,then utaangalia muelekeo wa kazi yako.



Shukurani mkuu Zanzibar Spices kwa ufafanuzi mzuri sana. Nimefanya utafiti kidogo gharama ya vifaa vya kuanzia haiko mbali sana na mchango wa Husninyo. Pia bei ya fremu inafahamika kutegemeana na site ya ilipo salon. Nikuombe uzoefu wako kwenye hilo la ukarabati wa chumba kimoja kuwa katika average standard kwa kuanzia inaweza cost kiasi gani na pia mfumo bora wa kukusanya na kusimamia mapato kwa mmiliki ambaye hayupo pale full time.
 
Last edited by a moderator:
Kuweni serious mtoa mada asije kupiga hesabu zisizo msaidia,kwa Berbershop yenye kumuingizia pesa hawezi shuka mtaji wa 10M,trust me..kiti kimoja tu ni 1M,yamkini aanze kwa uchache wa viti viwili vya kunyolea,kimoja cha scrub na cha kuoshea,hapo tu ni 4Million,hajaipamba kwa maana ya viyoo na muonekano wa kuvutia watu,kumlipa mtu atakaeitengeneza,kulipa pango la nyumba pia.kiufupi mtaji wa Berbershop hata iwe ndogo lakini inahitaji mtu ajipange,ila ni biashara nzuri sana iwapo utaipatia mitaa mizuri na vinyozi wako wawe wazuri ktk kazi na wasikimbiekimbie ovyo,hua wanapenda kulubunika mtu akifungua berbershop akawapa mshahara kidogo unazidi na wa kwako wanahama na kukimbia na wateja wao wote.hyo ni changamoto ila kama office iko vzr inajiuza yenyewe.kwa hyo mtoa mada uchekeche mwenyewe kulingana na mtaji wako
 
Shukurani mkuu Zanzibar Spices kwa ufafanuzi mzuri sana. Nimefanya utafiti kidogo gharama ya vifaa vya kuanzia haiko mbali sana na mchango wa Husninyo. Pia bei ya fremu inafahamika kutegemeana na site ya ilipo salon. Nikuombe uzoefu wako kwenye hilo la ukarabati wa chumba kimoja kuwa katika average standard kwa kuanzia inaweza cost kiasi gani na pia mfumo bora wa kukusanya na kusimamia mapato kwa mmiliki ambaye hayupo pale full time.
Hapo red siku hizi mnapangiana hesabu kwa kiti, kiti kimoja kizae elf 10 na kuendelea inategemea na location.
 
Safi sana vijana wenzangu kwa huu Uzi. Maana tuache majungu ya huyu kafanya vile hayana maana cha msingi tuwezeshane njia za kupata kipato tuepukane na njaa na umasikini. Naunga hoja kwa mtoa mada imekuja wakati mwafaka tukiwa tunaandaa strategic plan ya MWAKA 2016
 
;). It pay well
 

Attachments

  • 1453198409255.jpg
    1453198409255.jpg
    24.1 KB · Views: 188
Wanabodi nimeamua kijiajiri nataka niingie katika biashara ya saloon za kiume na mgahawa naomba kwa wenye uzoefu wa mambo Haya mnishauri kijana wenu
Asante nitakuwa online kuhubiri ushauri na mawazo yenu wataalamu
 
Back
Top Bottom