Biashara ya kuingiza movie na miziki kwenye flash na simu

CONTROLA

JF-Expert Member
Sep 15, 2019
6,939
22,990
Biashara hazijawahi kuisha chini ya jua ni vile tu unavyoamua kuchukulia mambo na kujichukulia wewe upo vipi,leo nataka nimsaidie mtu mmoja mahali flani kuichambua hii biashara ili kama alikua akiwaza nini chakufanya na hapati apate pakuanzia,na kwa wanaoifanya basi waboreshe ili mwisho wa siku urudi nyumbani ukiona mafanikio ya kazi ya mikono yako.

Kwanza nataka utambue hakuna biashara yyte chini ya jua kwasasa utakayoianzisha ukawa peke yako, kwahyo ondoa yale mawazo aah biashara hii kila mtu anaifanya, kila hatua mbili mtu anaifanya,nk ukiona biashara yyte kila mtu anaifanya sio kwamba eti ni rahisi ila ni kwasababu Kuna pesa ktk hiyo biashara, sasa kama na wewe utaamua kupishana na pesa kisa kila mtu anapesa ni sawa, vizuri.

Mahitaji ya hii biashara makubwa ni

1. Meza
2. Mwamvuli
3. Computer
4. Moderm
5. Benchi
6. Radio

Yawezekana upo unatafuta kazi na una mtaji flani au huna mtaji kbisa lakini una weza kutumia computer vizuri na pia una computer,hapa yaweza kuwa laptop au desktop ilimradi ni computer yoyote ya uwezo wowote inatosha na inafaa kukurudisha nyumbani na pesa,kuliko kukaa bure.

Unaifanyaje hii biashara sasa kwa wewe unaetaka kuanza kuifanya?

Amka hapo ulipo tembea nenda huko barabarani tafuta duka la mtu ambalo lina kibaraza kwa mbele au sehemu yyte unayoweza kuweka meza yako na ukapata pakui hifadhi usiku wakati wa kuondoka,au inaweza kuwa hata kisehemu cha pub,NK mtafute muhusika muombe kukaa eneo lake na mueleze nia yako na unachotaka kukifanya na kwmba unahtaji 1.eneo lake 2. Umeme wake 3.Kuhifadhi vitu vyako wakati unafunga usiku.

Utakapopata nadhani sasa kazi itakua kwako kufata vitendea kazi vyako na kuja navyo site kuanza kazi rasmi,Hakikisha meza yako mbele umechora huduma unazotoa kisha njoo kazini tulia pale.

Watu wengi wakiskia huduma ya kuingiza movie au miziki wanadhani n lazima computer iwe na nafasi kubwa sana ya kuhifadhi miziki ya tangu enzi zileee,hapana si lazima Japo ni vizuri kama ungekua na vihifadhi data (hdd) ili kufanikisha kazi yako kwa urahisi kidogo lakini kama huna nayo sio kesi unaweza kuanza hivyo hivyo ndio mana ktk mahitaji pale juu nilisema Moderm inahitajika.

Kama una moderm yako mtu akija akakwambia naomba wimbo wa pepe kale audio unaitwa Roger mila, kazi yako ni kuingia youtube unampakulia wimbo wake unamuwekea,ukiingia youtube ukiandika pepe kale tu Yatakuja majimbo yake kibaooo Na kwakua upo na mteja shabiki wa pepe kale Akiona hizo nyimbo lazima atakwambia niwekee na huo na huo na huo.

Katika chagua chagua pale nyimbo 1 n 200 akichagua 10 = 2000 asubuhi uliweka bando lako la buku 1gb,nyimbo kumi ukizidownload za mp4 low quality lets say nyimbo ina mb 10 x 10 = 100mb kumbuka ulinunua 1GB na mteja wako wa kwanza katumia MB 100 TU ok tufanye katumia mb 200,bado una akiba ya mb 800 zinakusubiri.

Taratbu mdogo mdogo yawezekana umepata mteja anataka movie flani,amekuja anakwambia Kwakua ndio siku yako ya kwanza wala usi panik mwambie tu ukweli ndio unaanza ila kuanzia next week movie zitakuepo ila kesho naweza kukuletea hyo movie yako,kama ana nia kesho atarudi tena hakikisha umeipata movie aliyokuambia,kesho akija aikute hata kama kwa kwenda kununua mahali.

Naamini computer yako hukosi movie ambazo ulikua tu ukiangalia kwa kujifurahisha tu,sasa huyo mteja alietaka movie akakosa hakikisha haondoki bure,MPE ofa mwambie leo wakati unasubiri movie yako kesho ije leo nenda kaangalie hizi movie Muwekee movie mbili akacheki (bure kabisa).

Kesho utamuona karudi ikitokea hujaipata ile movie yake usichoke wala usisite kumuwekea movie zngine BURE KABISA (hiyo ndio adhabu yako) ila ukishampatia movie yake akija siku ingine akitaka movie Mtandike bei.

Yawezekana hiii thread usi ielewe ila tuliza akili yako ondoa hofu,amini unaweza Fanya hii biashara kama una vifaa vyote nilivyotaja hapo juuu Mfukoni uwe na akiba ya kama 100,000 tu inakutosha,hii hela unajua n ya nini? n kwasababu umeanza huna nyimbo,huna movie,huna chochote zaidi ya pc yako kwahyo hii hela itakua inakusaidia kwenda kununua vile vitu wateja watakavyokua wanakuagiza.

Ukiwa hapo kazini naamini meza yako utakua umeichora tunaunganisha mitandao ya kijamiii, tunatoa simu lock,n hata usipoingiza miziki na movie unapokaa hapo kazini piga zako mziki Atatokeea tu mmatumbi mmoja WhatsApp yake imekua outdated haelewi a wala b,Tandika hela huyo.

Wakati umekaa hapo atatokea mzembe mmoja katia simu Lock kashau pattern au password akikupa simu mwambie bei yakutoa ni 25k akikupa mwambie aifate baada ya nusu saa, akiondoka akikupa mgongo Kimbia kwa fundi simu mpe 5000 au 10000 atakutolea simu hiyo lock kisha unarudi kazini kwako, mteja akirudi badae anakuta simu yake ipo tayari.

Ukiwa hapo hapo kazini utapata hela ambazo hutojua zimetokea wapi Hapa ndipo ule msemo unaosema mtembea bure si sawa na mkaa bure utagundua maana yake, Amini nakwambia wapo watu wanapenda kuona vijana tukijibidiisha kutafuta maisha,mtu wa namna hiyo akikuona Haoni shda kuja kukwambia muwekeee nyimbo 5 halafu akakuachia 5000, si kwamba ana pesa ila atakwambia kakupa kwasababu anaona juhudi zako.

Usikae bure Amka hiyo PC yako n kitendea kazi kikubwa sana kama hujui, Hii biashara kwa makadirio ya chiini day 1 unaweza ondoka home na 5000,day 2 ukaondoka na zaidi kadri siku zinavyoenda hii biashara income itakua ikipanda,usiikatie tamaaa na usiache kujiongeza unapokua hapo kazini, ile watu wanasema huyu jamaa ni mjanja mjanja Hakikisha hiyo ndio sifa yako nambari 1,usiwajali wewe piga kazi.

Kwa wenye mitaji sasa,yawezekana unaitamani hii biashara kuifanya na umeidhamiria

Mahitaji ni hayo hayo juu lakini sasa wewe itakubidi uwe na Frem au kibanda chako
Computer yako isiwe na HDD chini ya 1TB

Uwe atleast una mzigo wa baadhi ya nyimbo na movie za aina zote ambazo unaweza pata kwa wanaofanya hii biashara unaenda unamuomba atakwambia gharama zake mta bargain mwsho atakupa mzigo wwake utakuja kazini kwako kuanza kazi.

Wewe mwenye mtaji utakua tofauti na yule kule juu atleast wewe uhakika wa vi 10k kwa mwanzoni utakua unao,lakini biashara ikikolea Kuingiza vi 50k ni jambo la kugusa tu kama unamsukuma mlevi.

Usiwasikilize watu wanaosema eti siku hizi watu wana download nyimbo,siku hizi watu wanapata kila kitu mtandaoni ni kweli ndio ila wapo na lipo kundi kubwa sana la watu wasiojua kudownload nyimbo na fahamu si kila nyimbo n rahisi kuipata mtandaoni,swala la kudownload nyimbo/movie si kila mtu mwenye uelewa nalo.

Ndio mana movie za kifilipino watu hawana nyingi,si kwamba hazipo mtandaoni zipo kibao ila uliza n wangapi wanajua site zakudownload phillipines movies? au movie za ki turuki, nk si rahisi kwahyo usiogope et utakosa wateja,Utapata wateja na ktk biashara nzuri kwa wanachuo za kutaftia mitaji nahisi hii n nambari 1 lakini kama una mtaji na unataka ifanya hii biashara mtaji mzito mzito (mitaji mizito mnaielewa wajuba) ukiamua ifanya hii biashara ya movies na miziki,kuingiza 200k to 300k per day ni swala la kugusa tu kama unamsukuma mlevi.

Usidharau kazi,heshimu kila unaemuona anatafuta riziki yake mahali popote.Huijui kesho yako.
 
Be blessed boss. Ulizaliwa bongo kwa makusudi, mtanzania siyo mwepesi kutoa codes kama unavyofanyaga. Huwa napitaga kwenye vibanda vyao kule kuuliza maswali mawili matatu, majamaa wanaanza uswahili mwingi, huwa nawachora tu.
Sidhani kama ni Mtanzania huyu. Hata kama ni mtanzania basi atakuwa ametembea tembea huko duniani na ana exposure kubwa; na roho njema. Mtu anaweza kusoma uzi huu akaufanyia kazi akaanza na baada ya muda akapiga hatua na kujikomboa. Hii ni sadaka
 
Sidhani kama ni Mtanzania huyu. Hata kama ni Mtanzania basi atakuwa ametembea tembea huko duniani na ana exposure kubwa; na roho njema. Mtu anaweza kusoma uzi huu akaufanyia kazi akaanza na baada ya muda akapiga hatua na kujikomboa. Hii ni sadaka
Kweli kabisa mkuu. Huyu jamaa ukifuatilia nyuzi zake kadhaa na ukawa mtu wa kuzifanyia kazi kwa moyo kweli, lazima utapiga hatua.
 
Vijana wa ktz tuna mawazo mazuri sna tatizo letu n mambo mawil tu yanatufanya tusisonge mbele

1 UTHUBUTU
Kijana ana mawazo ila uthubutu wa kuanza Jambo n tatzo atajivuta vuta had fursa inampita

2 AIBU

Hapa biashara ndogondogo hawataki kisa fulan ataniona na digrii yangu bado wanamindset za vyuon wakat mtaan gemu ndyo hili halitak mzaha

3 MTAJI

Ndio Chaka tulilojifichia vijana ooh tuwekeze mtaj umetupatia? Lakn anahonga ana simu kal ambayo n mtaj tosha

Tubadilike vijana mleta mada kaleta mawazo Kama haya yasiyohtaj mtaj mkubwa ni wakat wa kiamka

#SHTUKA KIJANA TOKA USINGIZINI
 
Kwenye biashara yako unaingiza za kutafsiriwa au za kizungu

Ntk tufanye kitu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom