Barabara za Juu kwa Juu kweli ni kwa ajili ya kupunguza msongamano?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
Hivi nchi ambazo zina barabara za juu kwa juu hazina msongamano wa magari? Je kuna njia nyingine rahisi ya kupunguza msongamano wa magari Jijini Dar bila kuanza ujenzi wa mabarabara ya juu kwa juu? Ni kitu gani kingine basi kilicho nyuma ya push hii ya kuwa na mabarabara ya juu kwa juu? Yawezekana ni kwa ajili ya picha (postcards) au kusema na "sisi tunazo"?
 
Juzi[wapinzani]; serikali ya CCM haitekelezi ahadi zake za ujenzi wa bara bara za juu.

janap[serikali]; Serikali ya CCM IMETANGAZA kutengwa kwa pesa za ujenzi wa barabara za juu

Leo[wapinzani]; Hatuoni umuhimu wa bara bara za juu

kweli nimeamini upinzani wa nchi masikini ni kupinga kila kitu cha chama tawala
 
Malori makubwa yanaopita barabara za Mandela na Mororgoro yana mchango mkubwa sana kuongeza foleni katika jiji hili. Njia ya haraka kupunguza foleni ki kuweka muda maalumu malori kusafiri mfano yatoke bandarini kuanzia saa tatu usiku na yaruhusiwe kuingia mjini (kutoka Kibaha) muda huo huo. Ila kufanikisha hilo kitengo cha kutoa magari bandarini kifanye kazi hadi saa sita usiku. Pia kuna umuhimu wa vitengo vya TRA pale Bandarini na kule Posta vifanye kazi angalau hadi saa sita usiku kwa ajili ya watu ku process documents.

Pia Askari traffic waache kuongoza magari sehemu zenye mataa wafanye hivyo kwa muda maalumu labda kama kuna msafara. kazi yao iwe kudhibiti wanaotanua na kutoheshimu taa. Mfumo wa kuongoza magari ulifaa wakati ule kulipokuwa na uneven distribution ya magari lakini hivi sasa magari ni mengi kila upande, hakuna barabara isiyo na foleni. Uwepo wa trafiki unasababisha foleni kwa vile wanavuta sana upande mmoja na kuacha upande mwingine. Pia huwa wanapigiwa simu za jamaa zao kuvuta magari ya upande mmoja.......
 
hawa jamaa wanakurupuka sana...huwezi kuweka barabara za juu ili kuzuia foleni kwani huko zinakopangwa kuelekea ni kufinyu mno...chukulia posta na kariakoo na mnazi mmoja zilivyobanana halafu uongeze free movement ya magari unategemea nini???
 
Msongamano unachangiwa pia na barabara kuwa na low quality. Kama kuna mashie na mabonde kila mtu anahurumua gar yake, hapo ujue kwenye lami lakini ni 20kms per hour!
Lile la ustaarabu wa kutokutanua, naona tumlaumu Nyerere manake inawezekana alitunuizia wakati anatuloga:A S-baby:
 
watanzania tumezidi unafiki sasa! hata hao waunge tunaowaamini wanatutetea walikuwanataka road za juu pia! sisi wenyewe tukiwa kwenye mabus tunasema road za juu zitatusaidia kupunguza foleni! na hichi kitu kimeanza muda mrefu! leo watu wameanza kusema watweka road za juu! tunasema wanakurupuka, mabus ya kasi ivo ivo! basi solution yake TUTEMBEENI KWA MIGUU SASA! au tusafiri kwa ungo! mana wenzetu walioendele wanatumia road za juu na mabus ya kasi kujaribu kuboresha hali ya usafiri japo wanazo zaidi kama treni za umeme nk! mana sisi hatuta maendeleo basi tutumie njia asilia sasa.
 
Research ilifanywa na iko dizaini kamili ya namna ya kupunguza msongomano dar. Tena nakumbuka ilifanywa na wajapani wakishirikiana na wataalaam wa chuo kikuu na wengineo. Na hii ni mwanzo tu wakutekeleza yaliyomo.

Pitia pitia mitandao utaupata huo utafiti, niliusoma kwenye mtandao lakini sikuweka kumbukumbu ni muda mrefu.

Barabara za juu zinapunguza sana msongamano, hilo halina ubishi.
 
Jamani mimi siipend ccm mpaka basi yaani. Lakini kuna vitu siwezi kupinga japokuwa nahisi hawatatekeleza as longo longo ndo zao.

Katika kuzurura zurura duniani fly overs works a lot kwenye kupunguza foleni na kiukweli dar es salaam ni mj mdogo sana dunian na hauna magari ya kutisha sema miundo mbinu tu hakuna, kwa dar es salaam wakizijenga za kawaida tu kama za malaysia au india yaan folen hakuna kabisa, haina haja ya kuzichanganya sana hewan kama nchi zilizoendelea sana maana utajiri huo hatuna. ila ziwe fly over imara zile ambazo unapanda mlima kubadilisha njia kama upo tambarare. Sema wasi wasi wangu kwa madereva wa kitanzania na lesen za kununua tra itakuwa balaa.

Jamani kabla hatujapinga kitu inabidi tutembee kidogo tuone wenzetu wanafanyaje as kwenye flyovers mataa ya barabaran yanakuwa sehem chache na mara nyingi zinawekwa sehem zenye makutano na zinasaidia sana kusema kweli.

Kiukweli dar es salaam hakuna magari mengi ukilinganisha na majiji mengi dunian. Asia and europe kuna magari yaan kama utitiri but dar gar hata likikugonga kesho unaweza kukutana nalo tena as magar idad ndogo sana
 
Hivi nchi ambazo zina barabara za juu kwa juu hazina msongamano wa magari? Je kuna njia nyingine rahisi ya kupunguza msongamano wa magari Jijini Dar bila kuanza ujenzi wa mabarabara ya juu kwa juu? Ni kitu gani kingine basi kilicho nyuma ya push hii ya kuwa na mabarabara ya juu kwa juu? Yawezekana ni kwa ajili ya picha (postcards) au kusema na "sisi tunazo"?

Mzee Mwanakijiji,

Marehemu Nyerere aliwahi kusema Watanzania mazuzu. Magufuli ni mbunifu wa Dili za ulaji CCM in the last days of Mkapa alikuja na hoja ya kuuza Nyumba za serikali. Leo kaanzisha au kafanikiwa kupitisha bajeti pamoja na mambo Mengineyo kujenga flyovers Tazara na Ubungo.

Hakuna Mbunge aliyemwuliza time frame japo Mbatia alimwelezea triangle ya project. Of course MagUfuli akiwa Kama Mwalimu wa Chemistry hakuelewa swali. Na watu wa Tanroads na Wizara wakauchuna. Angepaswa awaonyeshe Wabunge of course 90% ni wababaishaji including wa upinzani.

My take : it is going to take miaka mingi and come 2015 hakuna kitakachofanyika. This requires a feasibility study, design tendering, compensation etc, etc, sijaona umakini wa Wizara au mkemia akitueleza itachukua muda gani mpaka tuwe na the first flyover . The Dar rapid transport was incepted almost 10 years ago Leo hii bado wanaanza kujenga kiajabu and for sure it's not going to work cut my neck!

Pesa zitaliwa tu kwani sijui bila coordinated structural design and having on ground scientific flow wanaishia kusema pesa hazitoshi . If you use elimu ya darasa la kwanza chanzo cha foleni Dar is associated with kufa kwa reli zote ambazo zingeweza kupunguza trucks. Hata uamuzi wa kuweka one central bus stand for a city with over 5 million people it's crazy .

Nakubaliana partially na Mch. Msigwa akili ndogondogo kusimamia akili kubwa. Asubuhi all vehicles and bodaboda including gutas move towards Ubungo likewise jioni huna haja ya kuwa na degree kuona kwamba it's not going to work.

Tukiendelea kuwaachia wanasiasa seriou engineering solutions hatutoki hapa tulipo. Huwezi waambia madiwani who are mixed grill kusimamia ujenzi kwa local governments , yaani wawasimamie wahandisi this is a joke of the 21st century.

I have lost faith in weak ccm strategies. Kuna mpumbavu anakimbilia kuchukua eneo la mbuga ya Selous kuchimba Uranium??

Just ask them dhahabu ambayo ina bei nzuri na friendly imeshindwa kututoa mbona DRC hiyo Uranium haijawatoa au Zambia. Kagasheki is another fool uranium is radioactive it has huge catasrophic ecological impact. Nawashauri to stop learn from the Russians walichowafanyia wafungwa wao, just three years in the mines and you are a dead body!

Sorry nimetoka nje ya mada ya flyovers I just wanted to show you how damned is Dhaifu and his henchmen!
 
Nadhani watu hamtaki kuangalia ukweli uliofichika. Mahali pote duniani ambapo Highways zimeweza kupunguza msongangamano zimeenda sambamba na uboreshwaji wa feeder roads na barabara nyingine.. mfumo mzima wa barabara unafanya kazi as a single unit. Kutengeneza mabarabara ya juu kwa juu wala siyo shida sana lakini itajikuta inatengeneza dreadlocks mpya kabisa ama wakati wa kuelekea kwenye hizo freeways au wakati wa kutoka. Mfumo wa kuingia na kutoka kwenye highways ni sehemu nzima ya kupunguza msongamano. Matumizi ya traffic lights ni njia nzuri zaidi ya kupunguza msongamano - kama watu watazitii..
 
Nadhani watu hamtaki kuangalia ukweli uliofichika. Mahali pote duniani ambapo Highways zimeweza kupunguza msongangamano zimeenda sambamba na uboreshwaji wa feeder roads na barabara nyingine.. mfumo mzima wa barabara unafanya kazi as a single unit. Kutengeneza mabarabara ya juu kwa juu wala siyo shida sana lakini itajikuta inatengeneza dreadlocks mpya kabisa ama wakati wa kuelekea kwenye hizo freeways au wakati wa kutoka. Mfumo wa kuingia na kutoka kwenye highways ni sehemu nzima ya kupunguza msongamano. Matumizi ya traffic lights ni njia nzuri zaidi ya kupunguza msongamano - kama watu watazitii..

Hujaiona Dar toka lini? na hujamsikia Magufuli leo akichambuwa hizo feeder roads? au ni lazima uponde kila mafanikio kwa usongo tu?
 
Watu huwa hawakurupuki tu, haya mambo yamefanyiwa utafiti zamani, ushahidi:

Traffic Congestion cause of concern

Concentrations of particulate matter are much higher near the Tazara Intersection than at other sites nearby. (Source: 2008 Presentation on Dar es Salaam Transport Policy and System DevelopmentMaster Plan Preliminary Feasibility Study, funded by the Japanese International Cooperation Agency)
 
watanzania tumezidi unafiki sasa! hata hao waunge tunaowaamini wanatutetea walikuwanataka road za juu pia! sisi wenyewe tukiwa kwenye mabus tunasema road za juu zitatusaidia kupunguza foleni! na hichi kitu kimeanza muda mrefu! leo watu wameanza kusema watweka road za juu! tunasema wanakurupuka, mabus ya kasi ivo ivo! basi solution yake TUTEMBEENI KWA MIGUU SASA! au tusafiri kwa ungo! mana wenzetu walioendele wanatumia road za juu na mabus ya kasi kujaribu kuboresha hali ya usafiri japo wanazo zaidi kama treni za umeme nk! mana sisi hatuta maendeleo basi tutumie njia asilia sasa.

Hawajakurupuka, utafiti wa kina umefanyika. Na si barabara za juu tu zinazokuja ni pamoja na mabasi ya kwenda kasi (ikimaanishwa kuwa yatakuwa na lane yao tu na hayataoingiliana na lane za magari mengine) ujenzi umeshaanza. Pantoni za kubeba watu kwa wingi kutoka bagamoyo na zikiwa na vituo vinane tofauti. Barabara za juu. Kupanuliwa baadhi ya barabara (Ali Hassan Mwinyi imeshaanza kutoka kawe mpa juu huko. Feeder road ya Mbezi Goba imeshaanza kuwa designed. Train za abiria za mjini kutka ubungo mpaka posta kuanza kabla ya mwisho wa mwaka.

Magufuli anasema, barabara hazina siasa, wa chadema anapita humo hata maandamano anafanya humo akimaliza anakwenda kulala.
 
Hawajakurupuka, utafiti wa kina umefanyika. Na si barabara za juu tu zinazokuja ni pamoja na mabasi ya kwenda kasi (ikimaanishwa kuwa yatakuwa na lane yao tu na hayataoingiliana na lane za magari mengine) ujenzi umeshaanza. Pantoni za kubeba watu kwa wingi kutoka bagamoyo na zikiwa na vituo vinane tofauti. Barabara za juu. Kupanuliwa baadhi ya barabara (Ali Hassan Mwinyi imeshaanza kutoka kawe mpa juu huko. Feeder road ya Mbezi Goba imeshaanza kuwa designed. Train za abiria za mjini kutka ubungo mpaka posta kuanza kabla ya mwisho wa mwaka.

Magufuli anasema, barabara hazina siasa, wa chadema anapita humo hata maandamano anafanya humo akimaliza anakwenda kulala.

Zomba

Sijui Kama unaweza kuona the large picture. Barabara unazoziita Rapid tayari kuna road humps kibao? Unazungumzia speed gani? Kuna a lot of pedestrian crosses on all roads utaziondoa na huku watoto wa skuli wanomba matuta day in day out?
the distance from Magomeni up to Kinondoni junction na Ali Hasan Mwinyi is about 3km utakimbia speed gani au kutoka Shekilango kwenye kituo Hadi Magomeni also 3km utakimbia speed gani and the pedetrian crosses plus bumps, huu ndio uzumbukuku?

My friend in Dar you need another think tank hii ya ccm and it's **** achana nayo ni mawazo mgando!
Sioni Kama kuna kitakachofanyika bila kuwa na under ground roads and a lot of circle lines and this require a lot of redesign including kuhamisha na kufidia watu. You need more high rise parking lots. Go around the world and see what is happening?

If you still want people to park on the streets just forget. Kama interim solution you have to introduce city entrance fees for personal cars as high as 10,000/= per day and to do this you have to improve the size and quality of commuter buses ambayo they should be allowed minimum five minutes time for picking passengers amongst others. Haya mawazo ya kutumia na Bajaji it's a failed system iliyoshindikana Nigeria walikoanzia!,,
 
2 be honest kuna njia nyingi na bora zaidi za kupunguza foleni! hizo fly-overs ni either ubishoo wa Jk au ile kuuonyesha umma kuwa wanaweza "kufanya" mambo/kutimiza ahadi au itakuwa ni kauli mbiu ya kuombea kura 2015! kama ilivokuwa MACHINGA COMPLEX 2010! Lakini pia inaweza kuwa ni UJINGA WAO! Yaani mawazo yao yameishia hapo na ndio yalivo!!
 
No research,wanakurupuka tuu kishamba shamba

Barabara za mitaa na nyingine za kuunganisha na barabara kuu ambazo zingepunguza msongamano ndio ingekuwa suluhisho. Wazungu kwao walifikia hatua hiyo baada ya kuona hakuna uwezekano mwingine, sisi jiji lina barabara kuu 10 halafu tunataka bridge and ramps wapi na wapi! Kwa ajili ya show sawa, vinginevyo ni kuongeza kero zaidi.
 
Back
Top Bottom